advert

http://

Sunday, 6 October 2013

HAWA KWELI WANASTAILI KUWA MABINGWA DUNIANI.WAMEWEKA REKODI DUNIA NZIMA.




Jionee Mwenyewe hapa Chini Picha na Video za Watu wa Ajabu Duniani.


MWANAMKE MWENYE ULIMI MKUBWA DUNIANI


MWANAMKE MWENYE KUCHA NDEFU ZAIDI DUNIANI


MWANAMKE MWENYE UWEZO WA KUJIKUNJA ZAIDI DUNIANI


TAZAMA VIDEO HII UJICHEKEE MWENYEWE.



 Mama wa staa wa filamu za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, Lucresia Karugila kwa mara ya kwanza amemfungukia marehemu Steven Kanumba aliyefariki dunia Aprili 7, 2012. Mahojiano hayo yamefanywa hivi karibuni na gazeti la Risasi linalotolewa na kampuni ya GPL
Katika mahojiano rasmi na Risasi jijini Dar, Mama Lulu aliweka wazi kila kitu kuhusu madai mbalimbali ya yeye na mama Kanumba,Lulu na marehemu Kanumba.

Mambo yaliyoelekezwa ayajibu mwanamama huyo ni pamoja na madai kwamba alishapokea barua ya posa ya Kanumba kutaka kumuoa Lulu, yeye na mama Kanumba kugombana hivi karibuni na Lulu kumjali zaidi mama Kanumba kuliko yeye.


Awali, mwanamke huyo alisema miongoni mwa watu waliofiwa na Kanumba yeye yupo mstari wa mbele kwani uchungu alioupata siku ya tukio mpaka leo haujamtoka.


Mahojiano kamili yalikuwa kama ifuatavyo:
Risasi: Mama kuna madai kadhaa ambayo ni vyema uyajibu.
Mama Lulu: (Kwa ukali kidogo) maswali gani? Mimi sitaki waandishi, nilishasema! Kama ni kuhusu Lulu muulizeni mwenyewe.
Ilibidi waandishi watumie kazi ya ziada ili mama huyo aweze kuzungumza.
Risasi: Ni mambo ya kawaida tu mama, wewe ndiyo unafaa kujibu, tafadhali tusikilize.
Mama Lulu: Haya, ulizeni.

ALIUJUA UHUSIANO WA KANUMBA NA LULU?
Risasi: Kuna madai kwamba uliujua uhusiano wa kimapenzi kati ya Lulu na Kanumba,  lakini mama Kanumba alikuwa hajui kinachoendelea, ni kweli?


Mama Lulu: Kwanza katika maisha yangu hakuna siku niliyowahi kupata mshtuko kama niliposikia Kanumba amefariki dunia na mwanangu Lulu kahusishwa na kifo kile, nilishtuka sana.


“Ilikuwa mara yangu ya kwanza kujua kumbe Kanumba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanangu Lulu, lakini kabla ya hapo sikuwa najua lolote.


ALIMKABIDHI LULU KWA KANUMBA?
“Ninachoweza kukiweka wazi ni kwamba, nilikutana na Kanumba nikamkabidhi mwanangu kwa moyo mweupe amlee kisanii kwa sababu nilijua anaweza, kumbe na wao wakaanzisha uhusiano huo kwa siri.


KWA NINI ALIMKABIDHI LULU KWA KANUMBA?
 “Mimi na Kanumba tulikuwa tumezoeana sana. Alinipa heshima zote kama mama yake na alikuwa kijana mwenye aibu kwangu kutokana na heshima, haikuwa rahisi kuangaliana machoni na ndiyo maana niliamua kumpa Lulu amkuze kisanii.


ALIPOKEA BARUA YA POSA YA KANUMBA?
“Si kweli, sijawahi kuona wala kupokea barua ya posa ya Kanumba kumchumbia Lulu.


KAMA KANUMBA ANGETAKA KUMUOA LULU?
“Lakini nataka kusema kwamba kama Kanumba angekuwa hai na angetaka kumuoa Lulu ningefurahi sana kwani naamini mpaka sasa wangekuwa wamepata mtoto mzuri na sisi wazazi tukaitwa bibi.”


MADAI YA KUGOMBANA NA MAMA KANUMBA?
Risasi: Kuna madai kwamba wewe na mama Kanumba kwa sasa ni paka na panya, na sababu kubwa ni Lulu kumjali zaidi mwanamke huyo kuliko wewe, ni kweli habari hizi?


Mama Lulu: Mimi na mama Kanumba hatuwezi kugombana hata siku moja. Kwanza Lulu nimempa jukumu kwamba kwa sababu wote ni mama zake, akinunua nyama kilo tano kwa ajili yangu na kwa mama Kanumba apeleke tano.


“Akinunua vocha ya elfu tano kwangu na mama Kanumba amtumie kama hiyohiyo. Kwa hiyo hakuna ugomvi.”


Risasi: Je, Lulu akimzidishia mama Kanumba wewe hutajisikia vibaya?


Mama Lulu: Siwezi kujisikia vibaya ingawa mimi kwa sababu naishi naye ni lazima nitapata zaidi, lakini akimsaidia naona ni sawa tu.

ALIKUWA AKIMUOGOPA MAMA KANUMBA?
Mwandishi: Ilikuwaje ukakutana na mama Kanumba kwa mara ya kwanza?
Mama Lulu: Lulu ndiye aliyekuwa akinishawishi kila mara niende nikaonane na mama Kanumba ingawa wakati mwanangu yuko jela kiukweli nilikuwa namuogopa sana.


“Unajua yule aliyepotea (Kanumba) ni mtoto kama wangu, lakini alipotoka tulikwenda nyumbani kwake na tunamshukuru alitupokea vizuri. Awali kabla ya kifo cha Kanumba sikuwahi kufahamiana naye.


Risasi: Ukiambiwa uongee na Watanzania utataka kuwaambia nini?


Mama Lulu: Cha kuwaambia ni kwamba, mimi na mama Kanumba si marafiki bali ni mtu na dada yake.
 

Nawaomba wawaombee mama Kanumba na Lulu mwenyewe ili waendelee kupatana na kufanya kazi za sanaa pamoja kama walivyoanza.

Risasi: Tunashukuru sana mama.
Mama Lulu: Karibuni sana, mimi huwa naogopa sana magazeti, sipendi sana kuongea na waandishi wa habari.


KUMBUKUMBU YA LULU
Katika mahojiano na kipindi cha Take One kinachorushwa na Clouds TV, Lulu alisema:''Katika maisha yangu sitakaa nimsahau Kanumba kwa sababu alikuwa ni zaidi ya mpenzi. Kamwe sitamsahau''



source:GPL.


Mwanasheria mmoja wa Illinois ambaye alipatikana na hatia ya kufanya ngono na mwanaume mmoja kwa malipo ya Dola za Marekani 100 anamshitaki aliyekuwa wakili wake wa utetezi na mawakili wengine wawili kwa madai ya kusambaza picha zake za utupu.


Reema Bajaj, mwenye miaka 27, anasema wakili wake wa zamani Timothy Johnson, mwendesha mashitaka wa zamani Calvin Campbell, na mwanasheria aliyeorodheshwa kwenye hati ya mashitaka kama 'John Doe' walitoa hadharani picha zake za siri sambamba na taarifa kumhusu yeye.

Sasa wateja, wazee wa mahakama, na majaji wote wameshayaona makabrasha hayo ya kuaibisha, Bajaj anasema. Ana 'hasira mno, huzuni, aibu, na fedheha,' kwa mujibu wa hati yake ya mashitaka, ambayo ilisambazwa katika mtandao na gazeti la Illinois la the Daily Chronicle.


Johnson na Campbell, ambao sasa wana changamoto yao pamoja, hawakujibu simu mara moja walipotakiwa kutoa maoni yao kuhusu hati hiyo ya mashitaka.



Bajaj alipatikana na hatia ya ukahaba wakati wa majira ya joto. Alipigwa faini ya Dola za Marekani 2,500 na kutakiwa kufanya kazi za kujitolea kwa jamii masaa 50.

Polisi walimkamata Bajaj mnamo Juni 2011, wakisema wamegundua baruapepe kati yake na mwanaume ambaye alimlipa kwa ajili ya kufanya naye ngono kama sehemu ya uchunguzi kwenye kesi isiyohusiana, imeripotiwa. Alitiwa hatiani kwa makosa matatu ya ukahaba, lakini mawili yalitupiliwa mbali.

Polisi walisema hakukuwa na uhusiano wowote kati ya ukahaba wake na wateja wa kampuni yake ya uwakili. Katika hati yake ya mashitaka aliyowasilisha Jumatatu, Bajaj alisema anahofia picha hizo na maelezo kwamba zilidaiwa kusambazwa baada ya kukamatwa kwake zinaweza kuathiri biashara ya kampuni yake.

Alikuwa na changamoto yake binafsi, kwa mujibu wa ripoti mbalimbali za habari. Tovuti ya kampuni yake ya uwakili kwa sasa haifanyi kazi.

Kabla ya kushitakiwa kwa ukahaba, Bajaj alijitolea muda wake katika Ofisi ya Utetezi wa Jamii Boone County, iliripoti Rockford Register baada ya kukamatwa kwake.


Pengine huwa unajiuliza kwamba kwanini mzungu akivaa bikini na kutembea ufukweni mwa bahari hakuna anae shituka wala kupiga kelele, lakini binti wa ki afrika akivaa bikini na kutembea ufukweni au kupiga picha utasikia maneno mengi ya kumsifia, au kumsema kwamba yuko uchi. 


Ajabu ni kwamba wale wale wanaompigia kelele binti wa kiafrika ndio wasioshituka wamuonapo binti wa kizungu. Je, unajua kinachosababisha utata huu?


Tatizo sio utamaduni, mila au mazoea. Ukweli ni kwamba wanaume wengi wa kiafrika huvutika zaidi wanapomuona binti wa kibantu kuliko mzungu. 


Hali hii inasababishwa na mazoea ya wanaume wengi wa ki afrika kuwa na mahusiano (sex) na wasichana wa kwao (wabantu) na hivyo kuufanya ubongo kuvutika zaidi na rangi au maumbile ya aina fulani. 

Ndio maana mwanaume anaejenga uhusiano na msichana mwembamba, si ajabu akatafuta msichana mwingine mwenye umbile linalofanana na hilo endapo kama ataachana na huyo aliyenae. 

Ukweli huu unaungwa mkono na wanasayansi walioendesha uchunguzi maalum kutaka kujua vikolombwezo vinavyo mvutia mwanamume.
Mamia ya wanaume waliofanyiwa uchunguzi wa picha za ubongo walionesha kupata msisimko zaidi  katika hypothalamus (sehemu ya ubongo inayoshughulika na mahusiano/sex) kila walipo oneshwa picha za mwanamke wa asili yake hasa kama muhusika hajapata kuwa na uhusiano na mpenzi wa rangi au asili nyingine.

 Hata hivyo tofauti ilijitokeza kwa wanaume waliooa wanawake wa asili/rangi tofauti. Hata hivyo wanasayansi hao walikubali pia kwamba sura na umbile la mwanamke lilisaidia kuongeza msisimko kwa namna tofauti....


Linah, staa wa muziki Bongo ambaye hivi karibuni kumekuwa na maneno mengi ambayo yamezungumziwa juu yake kuhusiana na swala zima la mahusiano ya kimapenzi, huku akihusishwa na skendo za kukubali kuhongwa na pia kuendeleza mahusiano na msanii mwenzake Amini ambaye alikwishatangaza kuachana naye, ameamua kutolea ufafanuzi swala hili ili kuwaweka mashabiki wake sawa.


Linah amekanusha vikali swala zima la yeye kuhongwa, vilevile kuhusiana na mahusiano ya kwake ya kimapenzi amesema kuwa kwa sasa ana mpenzi wake ambaye hayuko tayari kumuweka wazi katika vyombo vya habari, na katika hali hii hawezi kusema kitu chochote ambacho kitamuumiza yeye ama mahusiano yake.

Lina amesema kuwa yeye na Amini walikiss katika jukwaa ili kuleta  uhalisia na burudani tu na haimaanishi kwa namna yoyote kama wana uhusiano na yeye kama msichana hawezi kujivunjia heshima yake kwa kuhongwa.
Posted: 05 Oct 2013 11:25 AM PDT

Shilole amefichua kuwa, role model wake katika muziki kwa sasa ni nyota Lady Gaga ambaye kitu kikubwa alichojifunza kutoka kwake ni kujiachia pindi anapokuwa jukwaani, na kuwaridhisha wale ambao wametoa pesa zao ili kushuhudia burudani kutoka kwake.


Shilole pia amewataka mashabiki wake kukaa tayari na kolabo ambayo aliwaahidi kuwa atafanya na mwanamuziki Jennifer Lopez ambayo anatarajia kuikamilisha mwisho wa mwaka huu atakapokwenda tena ziarani Marekani.


Mazoezi yana umuhimu mkubwa kwa maisha yako endapo utaweza kuyafanya kwa jinsi ipasavyo. Kujua muda wa kula na kitu cha kula kunaweza kukusaidia kupata matokeo tofauti katika ufanyaji wako wa mazoezi.

Wanasayansi wanasema kuwa ulaji na mazoezi ni vitu vinavyoenda bega kwa bega. Ni vizuri kuelewa chakula unachokula kinaathiri vipi mazoezi yako.

Baada ya kugundua hilo wataalamu hao waliona si vibaya ikiwa watakuja na mwongozo utakaowasaidia wafanyaji mazoezi kupata matokeo mazuri kwenye programu zao.

Unachotakiwa kuelewa  ni kwamba muda wako wa kufanya mazoezi 
unaendana na kiasi cha chakula na maji ulichopata.  Hii inawahusu hasa wale wanaotaka kupunguza uzito kwa kutumia mazoezi.

Watu walio katika kundi hili, wamekuwa wakiharibu maana nzima ya mazoezi kwani badala ya kula chakula kinachoweza kuwaongezea nishati katika ufanyaji wa mazoezi, wengi wao huamini kuwa kwa kuacha kula wanaweza kufanikiwa zaidi.

Mara nyingi kitendo cha kaacha kula na kuendelea na mazoezi huchangia kwa kiasi kikubwa kumfanya mtu husika akose nguvu na badala yake kudhoofika na hatimaye hushindwa kufanya mazoezi.

Mambo muhimu ya kuzingatia unapotaka kufanya mazoezi:

1.   -Pata kifungua kinywa sahihi kiafya
Ikiwa unafanya mazoezi asubuhi, unashauriwa kuamka mapema na kupata kifungua kinywa saa mbili kabla ya kuanza mazoezi. Kwani kwa wakati huo nishati yote uliyopata kwenye chakula cha usiku,      itakuwa imetumika usiku hivyo hadi kufikia muda huo, utakuwa una kiwango kidogo sana cha nishati na sukari katika damu pia itakuwa chini.

Ikiwa hutakula kabla ya kufanya mazoezi utajisikia mchovu. Ikiwa utaamua kula kabla ya mazoezi unashauriwa kula chakula chepesi kama vile juisi au hata matunda pamoja na maji ya kutosha. Unashauriwa kula chakula kitakachosaidia kukuongezea sukari katika damu.
Ikiwa wewe si mlaji wa asubuhi sana, jaribu kunywa hata juisi tu kabla ya kufanya mazoezi. Pia ikiwa utaweza kupata kikombe cha kahawa itakuwa ni sawa tu.

2.   -Zingatia kiasi cha chakula
Epuka kula chakula kizito kabla ya kuanza mazoezi kwani kwa kufanya hivyo unaweza kujiweka kwenye hatari ya kuongezeka zaidi badala ya kupungua au kuimarisha mwili wako.
Pia, kula kiasi kidogo cha chakula. Ikiwa utakula chakula kingi unaweza kusikia uvivu kufanya mazoezi na hivyo kuishia kupumzika badala ya kuchangamka kufanya mazoezi.


3.   -Vitafunwa vyenye virutubisho kiafya ni bora zaidi.
Unaposema kula kitafunwa haimaanishi kuwa kila kitafunwa ni sahihi, hapa unapaswa uwepo wa virutubisho muhimu katika kitafunwa husika. Wataalamu wa afya wanashauri ulaji wa matunda zaidi katika hili.
Matunda yanaweza kumweka mfanyaji mazoezi bila kumchosha hata kama atakuwa amekula kiasi kikubwa tofauti na vyakula vingine.

Ikiwa utaweza kupata mlo unaoendana na mazoezi yako, ni wazi kuwa  mazoezi yako yatakuwa yenye tija, kwani utaweza kuona tofauti.




Zitto-KabweBy ZItto Kabwe:
Napenda kuujulisha umma kwamba jana Ijumaa tarehe 4 Oktoba, 2013 nimewasilisha kwa Katibu wa Bunge muswada binafsi Bungeni kufuta Sheria ya Magazeti ya mwaka 1976.
Changamoto iliyopo ni Sheria mbadala ya vyombo vya habari baada ya Sheria ya sasa kufutwa. Hata hivyo wadau wa habari kama Baraza la Habari Tanzania wameshafanyia kazi suala hili kwa muda mrefu sana na wana mawazo kuhusu sheria mbadala. 

Nimejulishwa kuwa muswada wa sheria mpya ya habari tayari upo. Kwa hiyo katika mchakato wa kujadili muswada binafsi wa kufuta sheria ya magazeti ya mwaka 1976 mabadiliko yanaweza kufanywa ili kutunga sheria mpya.

Hatua ya kwanza ni kuifuta sheria hii kandamizi ambayo kiukweli tumechukua muda mrefu sana na baada ya madhara makubwa kufikia hatua ya muswada wa kuifuta.

Nimeamua kutumia njia za kawaida za kuwasilisha muswada na kuepuka njia ya dharura ili kujenga mazingira ya wadau wa habari kushiriki vya kutosha katika mabadiliko yanayotakiwa. 

Njia ya dharura ni ya haraka lakini huziba fursa za kupata maoni ya wadau ambao kimsingi ndio wenye sheria yenyewe haswa. Hivyo nimepeleka muswada jana ili uchapwe kwenye gazeti la Serikali (GN) kwa mujibu wa kanuni za Bunge, kisha usomwe kwa mara ya kwanza, uende kwa wadau kwa mjadala na marekebisho na kisha kusomwa kwa mara ya pili na kupitishwa na Bunge.

Ikumbukwe kuwa juhudi za kufuta sheria hii ni juhudi za wadau wa tasnia ya habari na ni juhudi walizofanya kwa muda mrefu sana. Mimi kama Mbunge ninawasilisha tu kwa sababu taratibu zetu za kuandika sheria zinataka ama Serikali, Kamati ya Bunge au Mbunge kuwasilisha muswada.

Kwa muda mrefu tumewaangusha wana habari kwa kutosukuma vya kutosha mabadiliko waliyokuwa wanayapigania. Hata hivyo, kuna msemo wa kihindi ‘asubuhi huanza pale unapoamka’. Sasa tuchukue hatua za kufuta sheria hii kandamizi.
Zitto Kabwe,Mb
Kigoma Kaskazini

Ilikuwa siku ya kawaida kama siku zingine msichana wa miaka 18 aliyejulikana kwa jina Chekwube Mbaka alitumwa sokoni kununua mahitaji ya chakula cha jioni katika mtaa mmoja huko Naigeria....lakini njiani alikutana na vijana wanane ambao walimbaka wote mpaka kupoteza maisha yake.


Polisi wamewashikilia vijana wawili kwa kutuhumiwa kuhusika na tukio hilo ....inasemekana vijana hao ni watengeneza majeneza wa eneo hilo.

 Jana ilikuwa ni zamu ya tamasha la fiesta Mjini Tanga.....Kama kawaida yake mwanadada Shilole hakosi vituko ....Safiri hii aliwapa nafasi mashabiki wawili kucheza nae jukwaani huku yeye akiimba .




Source:Udaku Specially Blog

Rihanna amejikuta kikaangoni tena wiki hii baada ya mashabiki wake kumshambulia kutokana na video yake mpya ya wimbo ‘Pour It Up’ wakisema ni chafu na ina matusi mno.


Mamia walitumia mitandao ya kijamii kumponda mrembo huyo kwamba ‘hana hata haya’ kutoa video chafu kama hiyo. 

ITAZAME HAPA CHINI!!

Mtu mmoja aliejulikana kwa jina la Burhan Islam(fundi wa gari) amenusurika kifo baada ya gari alilokuwa akisafiria aina ya Fuso kugonga lori lingine nae kubanwa na bodi na kuokolewa baada ya
jitihada zilizofanywa na baadhi ya Abiria waliokuwa wakisafiri katika barabara kuu ya Dar es salamu kwenda Mtwara na Lindi.
Gari hilo lenye namba za usajiri T 56ANQ lililokuwa likiendeshwa na Kunja Mshamu limepata ajali hiyo leo katika kijiji cha Mkwajuni wilayani Lindi baada ya kutaka kulipita gari lenye namba za usajili T 402 AJG Scania lililokuwa likiendeshwa na Amos Chadenyile na kushuhudiwa jitihada zilizokuwa zinafanywa kuokoa maisha ya kijana huo.Majeruhi huyo baada ya kuokolewa katika ajali hiyo alikimbizwa katika kituo cha afya kitomanga kwa huduma ya kwanza kabla ya kupelekwa katika hospital ya Mkoa wa Lindi kwa Uchunguzi zaidi
Katika ajali hiyo iliyousisha malori hayo hakuna majeruhi mwingine
aliepata jeraha huku gari hiyo ya Fuso likiwa limeharibika sana





IPO HIVI!!

WAKATI ulilalamika kuwa umelala njaa kwa siku mbili.
WAPO wenzako wanalalamika kuwa hawajapata mtoto mwaka wa tisa sasa.

WAKATI unaombaomba mtaani ilimradi upate pesa ya kujikimu kwa siku moja tu.
WAPO wengine wamelala vitandani wakimwomba Mungu muujiza tu aweze kumponya baba yao ambaye ni kila kitu katika familia.

WAKATI unalalamika kuwa mafua yanakusumbua na unachukia kuzaliwa,
WAPO wengine hiyo pua ya kuwa na mafua hawana. Iling’oka katika ajali ya treni. Na bado wanaishi.

WAKATI unamshangaa mkurugenzi mwenye suti kushindwa kumsaidia ombaomba mtaani.
YEYE anaumia kichwa kila mtu anamtazama yeye katika ukoo wake, kila mtu anamwomba yeye…..

WAKATI unalilia hadi kukufuru kisa una mgonjwa hospitali.
WAPO wenzetu walipoteza ukoo mzima katika vita vya wenyewe kwa wenyewe!!

WAKATI ukiona aibu kurudia nguo uliyoivaa jana.
WAPO wenzetu wanatamani walau kupata magunia wajivike miili yao.

WAKATI unapanga mipango ya kuwadanganya wasichana wanne na wote uwe nao katika mapenzi
KUNA wengine mamia kwa maelefu walifanikiwa na sasa ni wagonjwa vitandani wanatamani muda ungerudi nyuma wawe waaminifu.

WAKATI unatafuta mwanaume tajiri nd’o akuone.
NA YEYE anatafuta wasichana masikini awachezee kisha awaache.

WAKATI unamwita mtoto wako wa kumzaa ‘mbwa’ ama fisi.
WAPO wanaolala na midoli kitandani wakitamani kupata mtoto walau mmoja tu!!!

WAKATI unayasoma maandishi haya.
WENZAKO ndo wanakwapuliwa uhai dakika hii…..

**WEWE ni nani hadi uwe hai mpaka dakika hii!!!
JIGEUZE kuwa ombaomba, mwombe Mungu kila wakati na ukumbuke kumshukuru kwa zawadi ya uhai akupatiayo kila kukicha!!!

Ukiguswa na habari hii Ruksa kushare!!

Photo: Eti jamani unahisi hiki anachokitenda huyu mama ni sahihi?

9
Ndege iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu ambaye alikuwa gavana wa Nigeria, imepata ajali na baadhi ya abiria kufariki na wengine kukimbizwa hospitali.


Baadhi ya abiria hao walikuwa wanasindikiza mwili huo kwa ajili ya maziko lakini safari iliingia hitirafu.Ajali hiyo ilitokea baada ya injini kufeli ndege ikiwa hewani muda mfupi baada ya kupaa kwenye airport moja huko Nigeria. Ndege ilikuwa na watu 20 na watu watano ndiyo wamejeruhiwa na kukimbizwa hospitali 
1

HAKIKA ni mateso, tena makubwa. Mtoto Selemani Rajabu mwenye umri wa miaka 17, mkazi wa Ukonga kwa Guta, jijini Dar yuko katika mateso makali baada ya mguu wake mmoja kuvimba mithili ya tairi la gari kiasi kwamba hawezi kufanya jambo lolote zaidi ya kujiburuza tu.


 kijana huyo amesema kwamba anakumbuka amezaliwa akiwa na ulemavu kidogo chini ya nyayo za miguu yake ambazo zilikuwa nene kiasi cha kumfanya ashindwe kutembea na badala yake akawa ni mtu wa kutambaa tu.


Alisema wakati huo alikuwa akiishi na wazazi wake wote wawili, lakini baadaye wazazi hao walitengana na kumfanya aishi na mama yake huko Pugu Kajiungeni. Kutokana na uwezo duni wa mama yake, alimpeleka hospitali mara moja tu, licha ya mguu wake kuendelea kuvimba kila siku.


“Nakumbuka mama yangu aliwahi kunipeleka hospitali mara moja tu nilipokuwa mdogo, lakini sikumbuki kama aliwahi kunipeleka tena,” alisema Selemani akiwa na sura ya kukata tamaa.


Alisema tangu wakati huo, mguu wake uliendelea kuvimba siku hadi siku mpaka akashindwa hata kutambaa kama mwanzo na sasa akalazimika kujiburuza licha ya uzito mkubwa wa mguu wake kutokana na kuongezeka kwa uvimbe.


Kutokana na hali hiyo kuzidi kuwa mbaya, alisema mwaka jana mama yake alimpeleka Hospitali ya CCBRT ambako baada ya madaktari kumuangalia walisema mguu wake hauna maji ambayo wangeweza kuyanyonya ili kuyatumia kupata vipimo na kujua tatizo linalomsumbua.


Hata hivyo, kwa bahati mbaya, mama yake mzazi alifariki na kumlazimu baba yake kwenda kumchukua na kumpeleka kwa bibi yake huko Manzese.


Hali ya bibi haikuwa nzuri kiafya, hivyo baba alinichukua tena na kuishi naye kwake nikiwa na mama wa kambo,” alisema Selemani. 


Mtoto huyo analalamika kuwa anatamani hata mguu wake huo ukatwe kutokana na adha anayoipata kwani anakosa raha kama watoto wengine wanaotoka nje wenyewe tofauti na yeye anayetolewa kwa kuburuzwa na watu zaidi ya wawili.


“Siku zote  kunapokucha najiona kama sina thamani, natamani hata mguu huu ukatwe, siwezi kufanya kitu chochote, natamani kuwa kama watoto wenzangu,” alisema.


Licha ya adha hiyo, Selemani alisema kingine kinachomuumiza ni kufanya haja zote  sehemu alipokaa na hivyo kutoa wito kwa wasamaria, akiwemo Rais Jakaya Kikwete kumsaidia ili aweze kupata matibabu.


Kwa wenye nia ya kumsaidia mtoto Selamani, kwa matibabu au chakula, wanaombwa kuwasiliana na chumba cha habari kwa simu namba 0713 612 533. 

Harufu ya rushwa! Safu ya ulinzi katika maduka ya biashara ya Mlimani City, Dar kwenye geti la kuingilia na lile la kutokea, inadaiwa kutawaliwa na rushwa ambapo walinzi wamenaswa ‘laivu’ wakipokea ‘mlungula’.


Kwa mujibu wa walalamikaji, walinzi hao wanadaiwa kujiwekea utaratibu usiyo rasmi chini ya kampuni ya ulinzi wa eneo hilo iliyotajwa kwa jina la Omega Nitro Risk Solutions ya jijini Dar ambapo ‘vijana’ wake wanatuhumiwa kutoza watu faini ya shilingi elfu kumi kwa gari ambalo mhusika wake amepoteza kadi ya kuingia na kutoka. 


Madai hayo yalikwenda mbele zaidi ikielezwa kuwa kumekuwa hakuna utaratibu mahususi kwenye ishu hiyo kwani baadhi ya walinzi kila mmoja hujiamulia kuchukua fedha bila mhusika kupewa risiti ya malipo.


“Kuna tatizo kwenye safu ya ulinzi, huwa tunatozwa faini shilingi elfu kumi ukipoteza kadi,” alisema mmoja wa walalamikaji hao.


Baada ya malalamiko kutua kwenye kitengo chetu cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM), kazi ilianza ambapo kikosi kazi kilifanya doria kwa siku kadhaa na kufanikiwa kunasa laivu hatua kwa hatua, tukio la walinzi hao wakilamba ‘kitu kidogo’.


Tukio hilo lilijiri hivi karibuni katika geti la Mlimani City la upande wa Barabara ya Sam Nujoma ambapo walinzi hao walizuia gari la jamaa aliyekuwa amepoteza kadi na kuchukua rushwa.


Katika hali ya kushangaza au njaa, tofauti na kiasi cha shilingi elfu kumi kilichotajwa awali, walinzi hao walikubali kumpunguzia jamaa huyo hadi elfu tano bila kujua kwamba walikuwa wakirekodiwa hatua kwa hatua.


Baada ya kujikusanyia ushahidi wa kutosha, OFM ilizungumza na bosi wao ambaye ni Senior Inspector wa Omega Nitro Risk Solutions, Leo John Masuka juu ya vitendo hivyo ambapo mbali na kuonesha kushangazwa na habari hizo, pia alianika kila kitu jinsi wanavyofanya kazi.

“Nashangaa kama kuna tatizo kama hilo kwani  tumesitisha kuwatoza faini wanaopoteza kadi, nitafanya uchunguzi ili kuwabaini watu hao ambao wanaharibu sura ya kampuni.


Katika hali hiyo kwa kipindi hiki cha tishio la ugaidi ni rahisi kwa magaidi kutoa rushwa kisha kuingia na kufanya utekaji kama walivyofanya nchini Kenya kwenye maduka ya Westgate.


GPL.

Ajali mbaya  nyingine  imetokea  jana usiku katika mlima Kitonga wilaya ya Kilolo mkoani Iringa katika barabara  kuu ya Dar es Salaam -Iringa . 

Katika  ajali  hiyo  watu  wawili wamekufa papo hapo huku wa wawili  wakijeruhiwa  vibaya baada ya malori mawili kugongana  uso kwa uso . 
Ajali  hiyo imetokea  mida ya saa 12.50 jioni ya  jana  ikiwa ni dakika takribani 30  baada ya ajali ya basi la JM kupinduka eneo  la Mazome  wilaya ya Kilolo. 


waliopoteza maisha katika ajali  hiyo ambayo chanzo ni dereva  wa lori la IT lililokuwa  likisafirishwa kwenda nchi  za  kusini mwa Tanzania aliyekuwa akitaka  kulipita gari la mbele mlimani na katika kona kali . 


Hata  hivyo  dereva  wa  lori  hilo IT aliyetambuliwa kwa jina la Gody  amevunjika mguu  wake ambao umetoka  na  dereva  na utingo la fuso wamekufa papo hapo  huku mwanamke  aliyekuwa katika lori IT akisalimika 


Thursday, 3 October 2013

MTOTO WA MIAKA 13 AJIFUNGUA MTOTO WA MIEZI 6 SEBULENI BILA KUJIJUA.

MSICHANA aliyejitambulisha kwa jina la Salma Hemedi (13) mwanafunzi wa Shule ya Msingi Ubungo Plaza, Dar amejifungua  maiti ya kichanga cha miezi 6 bila mwenyewe kujijua.
Tukio hilo lilitokea Septemba 25, mwaka huu maeneo ya Ubungo National Housing jijini Dar ambapo asubuhi ya siku hiyo, Salma alilalamikia maumivu ya tumbo lake kiasi cha mama yake aliyejitambulisha kwa jina la Rahma Shabani kwenda kuomba msaada wa kitabibu.

Mwanamke huyo alieleza kwamba baada ya kurudi ndani alikomuacha mwanaye, alimkuta akiwa amejifungua kichanga sebuleni, kitu ambacho hakukitarajia kwa kuwa alizoea kumnunulia vifaa vya kujisitiri wakati wa hedhi kila alipomlalamikia maumivu ya tumbo akijua yupo kwenye siku zake.

Akiwa na manesi walioongozana naye, walimsaidia Salma huku kila mtu akiwa amepigwa na butwaa kwa kilichotokea kwani hakuna aliyekuwa anajua kama Salma alikuwa na ujauzito.

Akiongea na waandishi wetu, Salma alisema alipewa ujauzito na mwanaume aliyemtaja kwa jina la John Vicent ambaye alikuwa mtoto wa mwenye nyumba wao wa zamani.

Salma alisema kuwa John alikuwa akimshawishi kila mara kufanya mapenzi japo alimkatalia kwa kuwa alijua akifanya kitendo hicho atapata mimba.

Salma alizidi kutiririka kuwa John alikuwa akimpa dawa alizodai ni za kuzuia ujauzito.

Baada ya kupata taarifa hizo mama wa Salma pamoja na ndugu zake walitoa taarifa Kituo cha Polisi Urafiki ambapo walifungua jalada la mashtaka lenye namba RB, URP/RB/7316/2013 KUBAKA na kupewa PF3 kwa ajili ya matibabu na uthibitisho wa daktari.

Walimu wa shule anayosoma Salma, walipigwa na butwaa baada ya kupata taarifa hizo na kueleza kwamba hawakuwa na taarifa kwamba denti huyo alikuwa mjamzito.

ZAIDI ya wanafunzi 50 waliochaguliwa kujiunga  katika vyuo vikuu mbalimbali nchini kwa mwaka huu, jana waliandamana kwenda Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kwa lengo la kukutana na Waziri Shukuru Kawambwa, baada ya kukosa mikopo.

Wakizungumza na mwandishi wetu, wanafunzi hao walisema zaidi ya wanafunzi 200  wenye sifa za kupewa mikopo ya elimu na Bodi ya Mikopo (HELBS), wamenyimwa bila maelezo.

Walisema kuwa tangu mwisho wa wiki wamekuwa wakihangaika kujua sababu za kutopewa mikopo kutoka katika bodi hiyo bila mafanikio.

Mwanafunzi Ayoub Suleiman aliyechaguliwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), alisema kuwa wameamua kumfuata Waziri Kawambwa ili wajue ni kwa nini hawajapewa mikopo hiyo.

Alisema majibu ya wanafunzi walioomba mikopo hiyo yalitoka Septemba 27 mwaka huu, miongoni mwao hawakuwepo kwa maelezo kuwa bajeti imekwisha.

“Waliotupa majibu haya ni wafanyakazi wa mapokezi na walinzi pale bodi ya mikopo, sio wahusika wenyewe kwa kuwa kila tulipoomba kukutana na mkurugenzi, hatukupata nafasi hiyo,” alisema Suleiman.

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Godwin Uledi, alisema kuwa juzi waliwashuhudia baadhi ya wazazi wakiwa na suti  na magari ya kifahari wakifika kwenye ofisi za bodi hiyo na watoto wao, na kuingia moja kwa moja kuonana na watendaji, walipotoka walikuwa wakitabasamu, hali iliyoonyesha kuwa wamefanikiwa.

Alisema, wanataka wapewe sababu kwa nini hawajapewa mikopo ilhali wenzao wenye vigezo kama vyao wamepata?

“Taasisi ya vyuo vikuu nchini ‘TCU’ ilitoa mwongozo kuwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu wakiomba vitivo vya elimu, uhandisi, udaktari, kilimo na sayansi watapata kipaumbele katika mikopo, hivyo nasi tulifuata mwongozo huo ili tupewe mikopo lakini hatujafanikiwa.

“Isingekuwa tunahitaji mikopo hii tungeomba katika maeneo mengine ambayo tulikuwa tukikidhi vigezo. Tumeomba katika vitivo hivi ili tupate mikopo,” alisema.

Kwa upande wake mwanafunzi aliyechaguliwa katika Chuo Kikuu cha Mt. Augustine, Revocatus Baltazary, alisema kuwa wamefungua chuo tokea Septemba 18, lakini ameshindwa kuripoti kutokana na wazazi wake kuwa na kipato cha chini.

“Sasa sina hata kianzio cha kwendea huko, kwa kuwa wazazi wangu hawana uwezo nitakwendaje?,” alihoji.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Ntambi Bunyazu, alisema kuwa wizara imewasiliana na bodi ya mikopo, kwamba wanafunzi hao warudi kule wakapewe maelezo zaidi kwa kuwa kila mmoja ana tatizo lake.

Hadi mwandishi wetu  anaondoka katika maeneo hayo, wanafunzi hao waliambiwa waorodheshe tena majina ili wizara iyapeleke HELBS, baada ya wiki moja watakuwa wamepata majibu.

Jitihada za kumtafuta Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa HELBS, Cosmas Mwaisobya, kwa ajili ya ufafanuzi wa suala hilo, ziligonga mwamba baada ya simu yake ya kiganjani kuita kwa muda mrefu bila majibu

Leo nimekabidhi madawati 120 Kata ya Manzese kwa shule tatu za msingi fedha kutoka katika mfuko wa jimbo. Bado kuna upungufu wa madawati 570 ambapo dawati moja linagharimu Tsh. 80,000 hadi 100,000.


Binafsi nachangia asilimia 20 ya kila mshahara wangu kuboresha Elimu ndani ya Jimbo la Ubungo!

Ungana nami tuboreshe elimu na kuimarisha pia maabara kwa kuchangia kupitia MPesa 350350.

Pamoja Tunaweza.

Waswahili husema, ‘nyumba ni choo’, wakiwa na maana kuwa nyumba haiwezi kuwa kamili bila kuwa na huduma hiyo ya choo.


Hata hivyo, pamoja na umuhimu wa choo, lakini si kila nyumba iliyo na choo au hata zile ambazo zina huduma hiyo, basi vyoo ni vibovu, havina hadhi. Zipo aina mbalimbali za vyoo kwa matumizi ya binadamu katika maisha yake ya kawaida.


Vyoo vina matumizi mengi ingawa bado watu wengi hasa katika nchi maskini na zinazoendelea ikiwamo Tanzania wanatumia choo cha kuchuchumaa wakati wa kujisaidia, lakini mijini na katika nchi zilizoendelea, wao hutumia vyoo vya kukaa.

Nyumba nyingi mijini na ofisi mbalimbali zinazojengwa hivi sasa, huwekewa vyoo vya kukaa. Hata zile za zamani zinakarabatiwa na kubadilishwa kwa kuwekewa hivi ambavyo vinaonekana vya ‘kisasa’.
Mgunduzi wa vyoo vya aina hii, Thomas Crapper anasema kwa mtazamo wake aliona kukaa wakati wa kujisaidia ni utambulisho wa ustaarabu na maendeleo.


Hata hivyo, madaktari wanapingana naye wakisema kujisaidia katika vyoo vya kukaa kuna madhara kiafya kwa kuwa mkao huo unaweza kuleta matokeo mbalimbali ndani ya mwili.


Utafiti uliofanywa na mtandao wa ‘naturesplatform’ umegundua kuwa matumizi ya choo cha kukaa huweza kusababisha matatizo mbalimbali ikiwemo kansa ya utumbo mkubwa.


Mtaalamu wetu wa afya wa gazeti la MWANANCHI, Samwel Shita anasema, madhara ya vyoo vya kukaa ni makubwa kwani wakati mwingine yanaweza kuwa chanzo cha saratani ya utumbo mkubwa kutokana na haja kubwa kubaki kwa muda mrefu katika utumbo huo.


Shita anasema mtu anapojisaidia haja kubwa katika choo cha kuchuchumaa, kinasaidia haja yote kutoka kwa sababu ya msukumo unaosababishwa na mkao huo.


“Unapokaa unakuwa umekaa katika choo mwili unakuwa umelegea, hivyo inabidi utumie nguvu kubwa kujikamua kutoa haja, tofauti na unapochuchumaa,” anasema Shita na kuongeza:
“Matatizo huanza hapo, unapojisaidia ukiwa umekaa na kulazimisha kujikamua unaweza kusababisha vimishipa vidogo katika utumbo mpana sehemu ya haja kubwa ya ndani na ya nje kuvimba na maumivu makali husababishwa na ugonjwa unaojulikana kama ‘hemorrhoid,” anasema.


Anasema ‘hemorrhoid’ ni ugonjwa ambao pia huitwa bawasiri. Mgonjwa hupata uvimbe katika njia ya haja kubwa na hivyo kupata maumivu wakati wa kujisaidia na haja yake mara nyingine huambatana na damu.


Aidha, anasema vyoo hivi pia vinaweza kuwa chanzo cha magonjwa yanayotokana na shambukizi katika utumbo mpana, kitaalamu ‘Inflammatory Bowel Disease’.


“Kila binadamu anapaswa kujisaidia na kuhakikisha haja yote imetoka na kwisha kabisa, inapobakia inaweza kusababisha maambukizi katika utumbo mpana kwa kuwa ule ni uchafu wenye mchanganyiko wa vitu vingi,” anasema Shita.


“Haja kubwa inapokuwa tayari imeshajitengeneza inapaswa kutoka yote, kama itabaki kipindi kirefu inaweza pia kuleta uambukizi katika utumbo mkubwa na hata katika kidole tumbo,” anasema Shita.


“Uchafu huu si tu unaweza kusababisha maambukizi, lakini pia unaweza kuwa chanzo cha saratani ya utumbo mkubwa. Wote tunajua kuwa mkusanyiko wa sumu mbalimbali mwilini unakuweka katika hatari ya kupata saratani, hivyo tatizo hili lisipotafutiwa ufumbuzi mapema linaweza kufikia huku,” anasema Shita.


Daktari Berko Sikirov kutoka Misri ambaye alifanyia utafiti matumizi ya vyoo vya kukaa anasema kuwa iwapo mtu ana tatizo la vivimbe vya ‘hemorrhoid’ linaweza kumalizika iwapo ataacha kutumia vyoo vya kukaa.


Hata hivyo, anasisitiza kuwa tatizo hili linaweza kwisha kama litakuwa katika hatua za awali. Kwa wenye tatizo lililokomaa watalazimika kufuata matibabu kulingana na ukubwa wake.


Dk Sikirov anaongeza kuwa mbali na kupata vivimbe, pia mgonjwa anaweza kupata tatizo la kutokupata choo kwa muda mrefu.


Anabainisha kuwa kitendo cha haja kutoka kidogo na nyingine kubakia husababisha kuganda katika ukuta wa utumbo na zoezi hilo huendelea mpaka kuwa tatizo sugu.


“Haja kubwa huganda katika kuta za utumbo, hali hii huifanya haja izunguke kwa muda mrefu na ndiyo tatizo hili huanzia hapa,” anasema na kuongeza:
“Unapojisaidia ukiwa umekaa, ile njia ya haja kubwa huwa kama imejifunga, inabidi utumie nguvu nyingi sasa ukiwa na tatizo hili la kukosa haja kubwa huifanya itoke kwa uchache zaidi,” anasema Dk Sikirov.


Aidha, anasema kupata haja kubwa mara kwa mara ni muhimu kwa kuwa usipoitoa maana yake inazungusha sumu katika damu jambo ambalo ni hatari kwa afya.


Anaongeza kuwa kutopata haja kubwa ni kichocheo chenye uwezo mkubwa wa kusababisha saratani ya utumbo mkubwa na uambukizi katika kidole tumbo.


Tafsiri ya kitabibu inasema hali ya kukosa haja kubwa ni pale mtu anaposhindwa kuipata angalau mara tatu kwa wiki. Hata hivyo, ili ujue afya yako ni njema unapaswa kuwa unapata haja kubwa angalau mara moja kila siku.
Daktari Denis Burkitt aliwahi kuandika kitabu cha maelekezo ya chakula ili kuepuka ugonjwa wa saratani. Katika kitabu hicho alieleza namna ambavyo watu wanaweza kujikinga na saratani za aina mbalimbali.


Akizungumzia saratani ya utumbo mpana pamoja na kuelezea vyakula na aina ya maisha, pia aliwaasa watu kutumia choo cha kukaa ili kujiepusha na tatizo hilo.


Anaeleza kuwa kwa Marekani pekee, watu zaidi ya 150,000 hufa kila mwaka kutokana na ugonjwa wa saratani ya utumbo mkubwa.


Mtaalamu wa Ngozi katika Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya na Tiba Muhimbili (MUHAS), Profesa Kisali Pallangyo anasema matumizi ya vyoo hivyo yanaweza kuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ya ngozi. Profesa Pallangyo anasema ni rahisi kuambukizwa magonjwa ya ngono na ngozi kwa urahisi pale unapotumia vyoo vya kukaa tofauti na vile vya kuchuchumaa.


Aidha, anayataja magonjwa yanayoweza kuwambukizwa kwa kutumia vyoo vya kukaa kuwa ni kaswende, harara, mba, kisonono, upele na mengine.


“Mtu mwenye magonjwa ya ngozi au ya ngono, anaweza kuyaacha katika ‘sink’ anapolikalia, hivyo ni rahisi kwa mtu mwingine ‘kuyachukua’ mara atakapokaa wakati wa kujisaidia,” anasema Prof Pallangyo.


Anasema vyoo hivi ni hatari kwa afya hasa pale vinapotumika katika jumuiya na kuongeza kuwa ni bora kutumia vile vya kukaa ili kujikinga na magonjwa.
Source: MWANANCHI


Kwa jina unaweza muita Leilani Franco  ana urahia wa nchi mbili (Uingereza / Philippines) alisafiri katika nafasi backbend umbali wa 20m  katika muda wa 10.05 dk katika  tamasha la Royal Hall mjini London Uingereza, tarehe 11 Machi 2013. Backbend binadamu ambaye ana uwezo wa kutembealea mikono na miguu kwa umbali mrefu.


Pia kama inavyothaniwa kwa kawaida Mtu anaweza tumia mikono kwa kulia chakula na kufanya shughuli nyingine, lakini kwa mwanamke huyu imekuwa ni tofauti kabisa, Mwamake huyu ana uwezo wa kutumia miguu yake  katika shughuli zake binafsi kama Kula na kadhalika.....
Hatimaye, Leilani pia anashikilia rekodi ya Dunia kutokana na uwezo wake katika kuuzungusha  Mwili wake. 




TAZAMA MAAJABU YA HUYU MREMBO KATIKA VIDEO!!
Anasema yeye mwenyewe binafsi katika kazi zake za ujasiriamali mtaji wake ameupata kwa kuhongwa na mpenzi wake akachanganya na fedha yake na maisha yanakwenda.


Anafafanua kuwa siku zote mpenzi wako hawezi kuacha kukuhonga kwakuwa kwenye mapenzi kusaidiana ni lazima,kwahiyo haoni ajabu yoyote mtu kuhongwa.

"Kusema ukweli mimi mwenyewe boy friend wangu kanisaidia sana na bado anaendelea kunisaidia,mimi sijali mtu aseme lolote analotaka lakini kama nahongwa for benefit sina tatizo na hilo"alisema Linah.

Ameongeza kuwa tatizo watu wamekuwa wana maneno maneno sana na kufuatilia ya watu badala ya kufanya mambo yao lakini ili mradi mambo yake yanakwenda safi hajali lolote anatazama maisha yake zaidi.

 Mwanalizombe Studios Ni Recording Lebel Inayomilikiwa na Rapper Profesa Jay, Studio ipo msasani na Ameamua kuipa Jina la Mwanalizomba kwasababu Jay Ni mtu wa Ruvuma na Mwanalizombe maana yake ni Mwana Ruvuma na kufanya hivyo ameonyesha mapenzi ya mkoa wake wa Ruvuma. Producer kwenye studio hii ni Duke Touchez.


 Profesa ameshindwa kusema amewekeza kiasi gani cha fedha kwenye studio hio ila fahamu kuwa vifaa vilinunuliwa kwa wakati tofauti na ni vifaa vya hali ya juu sana.



Rapper Prezzo wa Kenya aliyehusishwa hivi karibuni na msako wa polici baada ya kusemekana alirushiana risasi na askari, Prezzo amejitokeza na kuweka mambo wazi kuhusu issue hizo na nini hasa kilitokea siku hio na kuhakikisha jina lake linasafishwa. Prezzo ni moja ya rappers wenye aka ya Bad Boy so sio issue mpya kusikia story kama hizi.



Sasa Bwana Jackson Makini aka Prezzo ana habari mpya kwa shabiki wake kuhusu muziki wake. Kaa tayari kwa ngoma mpya kutoka kwa Prezzo Itaitwa " 7 Am" na itatoka siku yoyote mwezi huu. Star huyu kwa sasa bado anatamba na wimbo wake wa ‘Celebration Of Life’aliyomshirikisha Chess .

Rita Paulsen aka Madam Rita wa Bongo Star Search na Walter Chilambo tayari wameshazijibu Salamu za Nay wa Mitego na jana ilikuwa zamu ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe .

Kwake mbunge huyo, Nay ni msanii wa pili wa Hip Hop anayemkubali zaidi Tanzania baada ya Roma na kwamba anakiheshimu kile alichokisema kwenye wimbo huo kwakuwa ni kazi ya sanaa.

Tazama tweets hizi.



CarolNdosi @CarolNdosi
I wonder if @zittokabwe  ever listens to hip hop..local or international..



@CarolNdosi: I wonder if @zittokabwe ever listens to hip hop..local or international..” I do. Roma is my favourite followed by Ney
@zittokabwe @CarolNdosi surprising, after everything Nay Wamitego said in his new truck Salam zao ft Neiba Hon: Zitto still ranks him his n2


@SadiqAbdallah @CarolNdosi Ney amefanya sanaa. Nachukua maneno yake kama changamoto. Ni kazi ya Sanaa ninayoithamini sana.


 Leo tar 2|10 STARBOY was born... el presidente Diamond Platinumz beibb... ikisemekana Penny na Diamond wameachana lakini Penny alivunja ukimya baada ya kupost huo ujumbe on Instagram.

Pichani juu ni taswira mbalimbali za muonekano mpya wa Video Queen wa Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ ambaye kwa sasa yupo uraiani baada ya kufutiwa mashitaka yaliyokuwa yakimkabili ya kukamatwa na madawa ya kulevya aina ya crystal methamphetamine yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8, Julai 5, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg, Afrika Kusini.


MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), jana alitikisa Jiji la Arusha baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kumfutia kesi ya uchochezi iliyokuwa ikimkabili.


Lema alidaiwa kutoa kauli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo alienda kwenye Chuo cha Uhasibu Arusha kama anaenda kwenye sherehe za kuaga mtoto wa kike “send off”.
  
Uamuzi huo ulitolewa jana na Hakimu Mkazi, Devota Msofe baada ya wakili wa serikali, Eliananyi Njiro, kutumia kifungu cha 20 kifungu kidogo cha 1 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai kuliondoa shauri hilo ambalo lilikuwa lianze kusikilizwa kwa siku mbili mfululizo. Upande wa serikali ulipanga kuleta mashahidi tisa.
  
Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliofurika mahakamani hapo kusikiliza mwenendo wa kesi hiyo waliupokea uamuzi huo kwa shangwe kubwa.
  
Akizungumza nje ya mahakama mara baada ya uamuzi huo, Lema alisema kuwa alikuwa anajua shauri hilo ni la kutengenezwa ndiyo maana mashahidi wengi walikuwa ni polisi.
  
“Ni kama nimeshinda kesi, na Mungu ameendelea kutupigania, na tutaendelea kupambana kutafuta haki bila hofu maana miili yetu na nafsi zetu zimeishapoteza maumivu kwa sababu ya mateso yaliyojaa uongo na hila.
“Tutaendelea na kelele zetu za kupigania haki bila kurudi nyuma huku uvumilivu ukiwa nguzo yetu kubwa,” alisema Lema.
  
Hata hivyo, alikiri kutamka kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mulongo alienda Chuo cha Uhasibu kama anaeenda kwenye “send-off” kwani yeye ndiye alimpigia simu akimtaka afike kusikiliza kero za wanachuo, lakini hakulipa uzito unaostahili suala hilo hasa ikizingatiwa kuwa pale kuna mwanachuo alikuwa amepoteza maisha.
  
Lema alisema kuwa wanaweza kuwa wamemfutia kesi hiyo ili kesho wamfungulie nyingine jambo alilodai kuwa yuko tayari kwani anaelewa kuwa lengo ni kutaka kumuogopesha ili aache kuwatetea wananchi kitu alichodai kuwa hawatafanikiwa kwani tayari ana ganzi mwilini mwake, hivyo haogopi kufa, kesi wala kufungwa.
  
Kwa upande wake wakili wa Lema, Method Kimomogoro alisema kuwa ni vema kama serikali ingeamua kutumia busara ya kuona hakuna kesi toka awali, hivyo wasingefungua kabisa shauri hilo lililopoteza muda wa mahakama na mteja wake, kwani hata maelezo ya kesi yalionyesha dhahiri hakukuwa na kosa la uchochezi.
  
Alisema kuwa sheria inaruhusu kumfurahia, kumkejeli au kumzomea mtu, ndiyo maana hata bungeni wanaonekana waheshimiwa wakizomeana na kurushiana vijembe, na akadai hata kauli iliyodaiwa kutolewa na Lema dhidi ya mkuu wa mkoa ilikuwa kijembe tu.
  
Kimomogoro alilitaka Jeshi la Polisi kutenda kazi zao kwa mujibu wa sheria, huku akiwataka warudi kwenye hoja ya msingi na wawaeleze wananchi endapo wameshawakamata waliohusika na mauaji ya mwanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha.
  
Awali, ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mnamo Aprili 24, mwaka huu, mshtakiwa Lema akiwa eneo la Freedom Square ndani ya Chuo cha Uhasibu, alitoa maneno ya uchochezi yaliyosababisha uvunjifu wa amani.
  
Maneno hayo yanayodaiwa kutamkwa ni kinyume na kifungu cha 390 sura ya 35 cha sheria ya kanuni ya adhabu, marejeo ya mwaka 2002 .
  
“RC anakuja (Chuo cha Uhasibu) kama anaenda kwenye send-off, hajui chuo kilipo wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hicho... (RC) Ameshindwa hata kuwapa (wanafunzi) pole kwa kufiwa na amesema hawezi kuongea na wanafunzi wasio na nidhamu.” Yalinukuliwa baadhi ya maneno yaliyodaiwa kuwa yalitamkwa na Lema.
  
Kauli hizo zinadaiwa zilipandisha hasira za wanafunzi ambao walianza kumrushia mawe na chupa Mkuu wa Mkoa, Mulongo alipokuwa akiwahutubia kuhusiana na tukio la kifo cha mwanafunzi, Henry Koga kilichotokea Aprili 23, mwaka huu.

Kwa miaka mingi Coca cola imekuwa ni bidhaa namba moja yenye ubora wa kimataifa lakini mwaka huu Bidhaa Apple ikiwemo simu za Iphone imechukua namba moja kwa kuwa ni bidhaa boraDuniani.


Namba mbili imechukuliwa na Google kwa bidhaa zake mbali mbali...Namba tatu ndio imechukua Coca Cola


From New York Times 
Apple is the new most valuable brand in the world, according to a closely followed annual report. The report, to be released next Monday, is from Interbrand, a corporate identity and brand consulting company owned by the Omnicom Group that has been compiling what it calls the Best Global Brands report since 2000. The previous No. 1 brand, Coca-Cola, fell to No. 3.
Not only has Apple replaced Coca-Cola as first among the 100 most valuable brands based on criteria that include financial performance, this is the first time that the soft drink known for slogans like “It’s the real thing” has not been No. 1.