advert

http://

Saturday, 12 October 2013

DIWANI WA CHADEMA ATUHUMIWA WIZI WA MILIONI 10 ZA KITANZANIA MKOANI KILIMANJARO.




WATU tisa akiwemo Diwani wa Kata ya Old Moshi Magharibi, Elisaria Mosha (Chadema) wametiwa mbaroni wakituhumiwa kupokea fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia mradi wa umeme mkoani Kilimanjaro.


Hatua hiyo imechukuliwa baada ya Makamu wa Rais Dk Mohamed Gharib Bilal, kufanya ziara mkoani Kilimanjaro na kuagiza watu waliofanya hivyo wakamatwe mara moja.

AKIZUNGUMZA na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz alisema diwani huyo anatuhumiwa kujipatia Sh milioni 9.6 kwa njia ya udanganyifu. 

Wengine wanaoshikiliwa ni Zakayo Kimathi (52) mkazi wa Mandaka, anayedaiwa kupokea Sh milioni 10.3, Oforo Kimambo (56) mkazi wa Mandaka anayedaiwa kupokea Sh milioni 29. 

Wengine wanaotuhumiwa kupokea malipo hayo kwa njia ya udanganyifu ni Daud Mallya (69) mkazi wa Chekereni aliyepokea Sh milioni 8.6, Richard Mlaki (69) mkazi wa Kiboroloni alipokea Sh milioni 18.6 na Focus Herman (88) mkazi wa Kilototoni aliyepokea Sh milioni 36. 

Boaz alisema kwa sasa watuhumiwa watatu hawajapatikana. Alieleza kuwa pamoja na watuhumiwa hao, polisi imemkamata Mwenyekiti wa Kijiji cha Mandaka Monono, Hassan Nduva (41) na Ofisa Mtendaji wa kijiji hicho, Vendelini Shayo (58) kwa kuhusika kufanikisha malipo hayo. 

Dk Bilal alitoa agizo hilo mapema wiki hii wakati akizindua vituo vya kupozea na kusambaza umeme maeneo ya Kiyungi, YMCA na Makuyuni. 


Alipokea taarifa kwa Mkuu wa Mkoa kuwapo kwa wananchi ambao hawakulipwa fidia zao, kutokana na kuwapo watu waliotumia ujanja wa kupokea fedha hizo, Sh milioni 169.2. 

“Halmashauri ya Moshi Vijijini ndio ilikuwa wakala wa malipo hayo na ndio iliyofanya tathmini kwa kushirikiana na watendaji wa vijiji, ambapo wao walipeleka tathmini hiyo kwa Shirika la Umeme (Tanesco), ambalo lilitoa fedha hizo hivyo Tanesco hawahusiki,” alisema,” alisema Boaz. 

  Habari leo.

One week after the first episode of
the talent search show Tusker
Project Fame Season 6 went on air
from the academy in Nairobi, there
have been twists and turns in
events.

The Beat has reliably learnt that
organisers at the academy have
dropped Tanzanian judge, musician
Zahir Ali Zorro from the panel of
judges.

Details of the fallout are still sketchy
but word from Zahir Zorro’s camp
has it that it was an amicable
understanding between both
parties.

Speaking to The Beat , the veteran
musician said he had chosen to leave
the show in order to concentrate on
his personal musical engagements
back at home.

“After the show in Nairobi last week
it dawned on me that the responsibility was heavy and I
couldn’t handle both the academy
duties and my other engagements at
home satisfactorily,” he said.

Zahir Zorro’s appointment to the
judges’ panel was greeted with
cheers of hope as many thought he
would take the contest to a different
level after replacing producer
Hermes Bariki.

He was to work with Juliana
Kanyomozi who filled the Ugandan
spot and as agreed, controversial Ian
Mbugua filled the Kenyan spot.
But as the posts on the TPF website
announced that the vastly experienced musician had joined the
panel, discord was brewing.
Though there has not been any
official communication from
Endermol and East Africa Breweries,
sources privy to the academy cite his
laid back display at the inauguration
as the potential cause.

In his trademark bling-bling and
suit, Zorro barely said anything
during the blockbuster show that
ushered in 25 contestants. “He was a
bit uncomfortable with the
surroundings and looked not at ease
with the other judges who were
enjoying themselves throughout the
show,” said the source.

But in an interview with The Beat,
Zorro cited generation gap as the
reason for his mysterious exit from
the regional show. In hi own words:
“They will have to appoint a more
youthful person to take over from
me.”

This leaves some unanswered
questions whether it was the age
gap that left the singer in the cold.


Source:The Beat pull-out magazine,of The Citizen Newspaper,Tanzania

Binti wa Darasa la sita katika Shule ya Msingi Kilimani iliyopo Kipunguni, Dar mwenye umri wa miaka 12 (jina tunalihifadhi kwa sababu za kimaadili) amejikuta akishindwa kuendelea na masomo baada ya kupewa ujauzito na kijana wa mtaani aliyejulikana kwa jina moja la Roja.


Akizungumza kwa huzuni mama wa mtoto huyo, Aziza Mohammed alisema kuwa mwishoni mwa mwezi uliopita ndiyo aligundua kuwa binti yake huyo ni mjamzito na ilikuwa ni baada ya kukataa kwenda shule huku akitapika mara kwa mara.
Mama huyo alisema, baada ya kuona ilibainika kuwa ana mimba, wakanipa taarifalili hizo  aliamua kwenda kununua kifaa cha kupimia mimba lakini mwanaye huyo alikimbilia kwa mama yake mdogo, Temeke ambako waligundua kuwa ni mjamzito.
 “Alipofika kwa mama yake mdogo, nikawaomba wamlete kisha tukampeleka hospitali ambako tulithibitishiwa na daktari kuwa kweli ana ujauzito wa miezi mitano,” alisema mama huyo na kuongeza:
“Nilimbana aniambie mwenye mzigo huo ambapo alimtaja kijana aitwaye Roja. Akaniambia kijana huyo ambaye ni jirani yetu amekuwa akimbaka na kumtishia kumuua ikiwa atasema.
“Kwa maelezo hayo ilibidi tumtaarifu mjumbe wa mtaa wa Kipunguni B, Bakari Issa ambaye tulikwenda naye kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi cha Stakishari na kufungua jalada la kesi lenye namba STK/RB/18639/2013 KUMPA
 MWANAFUNZI MIMBA
“Jamani naomba taasisi husika zinisaidie kwa sababu baada ya kutoa ripoti polisi nimekuwa nikuzungushwa tu...mtuhumiwa hakamatwi.”
 SIMULIZI YA KUSIKITISHA
Binti aliyepata dhahama hiyo alipata kuzungumza na Ijumaa ambapo alisimulia simulizi ya kusikitisha sana ikionesha jinsi mchezo mzima ulivyokuwa.
Alisema: “Wadogo zake Roja ndiyo walikuwa marafiki zangu...Roja alikuwa akiwatumia wao kuniita kila siku jioni na nilipoenda alikuwa akinifungia chumbani kwake na kunilazimisha kufanya naye mapenzi huku akinitishia kuwa nikisema ataniua.
“Pamoja na vitisho hivyo alikuwa akinipa shilingi elfu tatu hivyo nikawa naogopa kumwambia mama na nilipogundua nina mimba nilimtuma wifi yangu (dada wa Roja) akamwambie lakini akakataa na kusema mimba siyo ya ndugu yake, mimi sijawahi kufanya mapenzi na mwanaume mwingine zaidi yake,” alisema binti huyo.
 KUTOKA IJUMAA
Tukio hili linaumiza na kusikitisha. Ni wito wetu kwa taasisi husika kufuatilia sakata hili na kumsaidia binti huyu ambaye ndoto zake zimezimwa ghafla akiwa bado mdogo.

Aidha, ni vyema wazazi wakawa makini katika kufuatilia nyendo za watoto wao kabla mambo mabaya hayajawakuta
KOCHA Mkuu wa timu ya Yanga, Ernest Brandts, amesema kuifunga Simba katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom itakayochezwa Oktoba 20 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, ni kazi rahisi.


Brandts amewatoa hofu viongozi na mashabiki wa Yanga, huku akitamba kupata ushindi dhidi ya mahasimu wao Simba. 

Akizungumza na RAI jana, Brandts alisema Simba hawamtishi kwa kuwa ana kikosi bora ambacho kina kila sababu ya kushinda mechi hiyo.

Alisema amekuwa akiifuatilia Simba mara nyingi inapocheza mechi na hakuna ushindani ambao umekuwa ukionyeshwa na wachezaji wa timu hiyo, licha ya kupata ushindi katika mechi zake.

“Simba hawana kiwango kikubwa, wanabebwa na mabao ambayo kwa bahati wamekuwa wakifunga, kikosi changu mimi ni bora, wachezaji wangu wana nguvu za kutosha na uwezo zaidi kuhakikisha tunashinda,” alisema.


Yanga tayari imewasili Bukoba kwa ajili ya mechi yao dhidi ya Kagera Sugar itakayochezwa kesho kwenye Uwanja wa Kaitaba.


Source:Rai.

KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa ameikumbuka timu yake ya zamani ya Azam FC baada ya kuonekana akiwa kwenye Uwanja wa Chamazi Complex nje ya jiji la Dar es Salaam.

Ngassa, ambaye awali aliuzwa na Yanga kwenda Azam FC kwa kitita cha pauni milioni 98, miaka mitatu iliyopita kabla ya kurudi msimu huu, juzi alitua kwenye Uwanja wa Chamazi na kushuhudia mechi ya Ligi Kuu Bara kati ya wenyeji na Mgambo Shooting.


Ngassa aliyeondoka Azam FC kwa mgogoro huku timu hiyo ikimpeleka Simba, alikuwa kivutio na wengi walianza kuonyeshana alipokuwa amekaa jukwaani.


Baada ya kufika uwanjani hapo, moja kwa moja Ngassa alikwenda kukaa alipokuwa amekaa mshambuliaji wa Azam FC, Gaudence Mwaikimba waliyewahi kukipiga pamoja Jangwani.


Mara baada ya mechi hiyo, kiungo huyo aliyerudi kwa kasi katika Klabu ya Yanga, kwa kuifungia bao moja mpaka sasa, alisalimiana na baadhi ya wachezaji wa timu hiyo na kuondoka zake.


Ngassa alipoulizwa sababu za kwenda uwanjani hapo alisema kwa ufupi: “Nimekuja kutembea tu.”

Tayari Ngassa yupo mjini Bukoba kwa ajili ya mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya wenyeji Kagera Sugar, kesho.
GPL


Mbali ya karipio hilo, Waziri Mkuu amewataka viongozi wengine wa Serikali, kuepuka mfumo usio shirikishi katika uamuzi wao kwa kuwa unasababisha migogoro ndani ya jamii na usumbufu kwa Serikali.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana juu ya mgomo wa wasafirishaji wa mizigo na abiria ulioanza Oktoba 5, mwaka huu, Pinda alisema Serikali imeamua kurejesha kwa muda wa mwezi mmoja asilimia tano ya uzito wa mizigo uliozidi kwenye mizani.


Alisema hatua zilizochukuliwa na Dk. Magufuli kufuta vifungu vilivyokuwa vikiruhusu asilimia tano zilifuata sheria, lakini tatizo lililojitokeza ni kutoshirikisha pande zinazohusika ili kushauriana na kupata uamuzi wa pamoja.

Alisema mbali ya kutoshirikisha pande hizo, uamuzi wa Dk. Magufuli ulikuwa wa ghafla kwa wasafirishaji kitendo ambacho kimewapa wakati mgumu wa utekelezaji, kwa sababu wafanyabiashara walikuwa wameingia mikataba na wateja wao.

“Chimbuko la mgogoro huu, ni tangazo la Dk. Magufuli alilotoa Oktoba mosi, mwaka huu la kuondoa ofa ya asilimia ya uzito uliozidi, baada ya uamuzi huo wadau wa usafirishaji wa malori na mabasi waliingia kwenye mgomo na kulalamikia hatua hiyo.

“Kutokana na mgogoro huu, nililazimika kukutana na Dk. Magufuli, baadhi ya mawaziri wa wizara zenye uhusiano na masuala haya, wanasheria na wataalamu wa masuala ya usafiri na uchumi.

“Kilichoongeza mgogoro ni tafsiri ya vifungu vya sheria na kwenye kanuni ya 7 (2) na 7(3) ambacho kinaeleza wasafirishaji wa magari yenye uzito uliozidi, lakini upo ndani ya asilimia tano ya uzito unaokubaliwa kisheria, wanatakiwa kupunguza mzigo, kupinga na iwapo watashindwa kutekeleza, watatakiwa kulipia mara nne ya tozo za kawaida.

“Sasa suala la asilimia tano, lilitokana na ombi la wadau wa usafirishaji kwa aliyekuwa waziri wa Ujenzi miaka ya nyuma na halikuwa sheria kamili, ndio maana limeondolewa baada ya kuonekana linatumiwa vibaya.


“Nakubaliana na Dk. Magufuli, wapo baadhi ya wasafirishaji ni wakorofi na hawataki kufuata sheria…ndio maana walifanya mazoea ingawa wapo wengine wazuri na hao nawapongeza sana kutii sheria.


Mtanzania.

MTAYARISHAJI mahiri wa muziki wa Kizazi kipya, anayemiliki studio za ya B Hits, Hermes Bariki ‘Hermy B’ ameteuliwa kuwa Jaji wa shindano la kusaka vipaji vya kuimba Afrika Mashariki la Tusker Project Fame.


Mkali huyo anayemiliki studio za B Hits, ataiwakilisha Tanzania na kwa kuungana na majaji wengine jijini Nairobi, nchini Kenya akichukua nafasi ya Zahir Zorro aliyekuwa Jaji katika shughuli ya kusimamia usaili wa shindano hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Meneja wa bia ya Tusker, Sialouise Shayo, alisema katika kuelekea awamu ya kwanza ya shindano hilo msimu huu wa sita, wamejipanga kuhakikisha Watanzania wanahusishwa kikamilifu.

“Kama tunavyomkaribisha Jaji mpya Hermy B ambaye amekuwa katika kinyang’nyiro hiki cha Tusker Project Fame kwa muda mrefu, tunatumia fursa hii kuwatangazia Watanzania kuwa tumejifunza mengi kupitia kwa Zorro,” alisema.

Katika shindano hilo, Tanzania inawakilishwa na Angela Karashani, Elisha Simon, Mgeni Kalinga na Ussa Dubart.

Kwa upande wake, Hermy B aliishukuru Tusker kwa kumchagua kuwa Jaji katika shindano hilo kwa mara ya sita pamoja na Zahir Zorro.


Mshindi wa Tusker Project Fame atajinyakulia Sh 100, 000, 000 na mkataba wa kurekodi utakaogharimu Sh 200, 000, 000.

Thursday, 10 October 2013

WEMA SEPETU NA DIAMOND PLATNUMZ MAMBO MAZITO.PENZI LIKO PALEPALE.



Baada ya habari kuenea kuwa Diamond PLatnumz amerudiana na Wema walipokuwa Malaysia katika moja ya show zake na Platnumz kukanusha habari hiyo kupitia website yake, hatimaye BK imepata picha nyingi za Diamond na C.E.O wa Endless Fame Wema Sepetu wakiwa kwenye pozi tofauti tofauti za kimahaba nchini humo.

Baadhi ya picha hizo, moja inawaonesha Diamond na Wema wakiwa wamevaa Mapajama (nguo za kulalia) sehemu kama hotelini hivi na nyingine ikimuonesha Diamond akim-kiss Wema wakiwa kitaa. Lakini Diamond ni real boyfriend wa Penny…

Nimepata shida kidogo kuamini hii habari na picha coz nimeitoa kwenye blog ingine ikanibidi nichimbe kidogo ili nione kama ni kweli manake nilihisi hizo picha ni za zamani wakiwa na wema....nimetafuta picha ingine ya diamond ambayo alipiga juzi juzi wakati haya maneno yakiongelewa na kuziowanisha ..na nimegundua mtindo wa nywele ni ule ule kwa picha zote ona hii picha chini alafu fananisha na picha za juu....Au ndio wanacheza Movie??

Picha akiwa na Penny baada ya kutoka Malaysia....

Rapper Nay Wa Mitego amesema amekuwa akisumbuliwa mno na maafisa usalama pamoja na vyombo mbalimbali vya habari wanaomdhania kuwa anajihusisha na biashara ya madaya ya kulevya kitu ambacho amekuwa akikanusha kwamba sio kweli.


Nay amesema anasikitishwa kupokea taarifa zinazodai kuwa anajihusisha na biashara hiyo haramu, kitu ambacho hakifanyi kwakuwa anategemea shughuli zake za muziki zinazomlipa vizuri.

“Watu wamekuwa wakishangaa sifanyi show hata mwaka mzima lakini maisha yanaenda namiliki gari ndio maana wanaongea mengi huku media na maafisa usalama wananichunguza kila siku,” alisema Nay.

Pia msanii huyo wa Salam Zao, amesema yupo kwenye maongezi na kampuni ya simu ili imfanye kama balozi wake.


“Nasubiria mambo yangu yaende poa, nimeingia mkataba wa kuwa balozi wa mtandao wa simu hapa nchini bado muda wake kuuweka wazi kwasababu tupo kwenye makubaliano zaidi na pia ikifika muda nataka kuanika vyanzo vyangu vyote vya mapato, ” alisema

Ikiwa ni wiki chache toka kesi ya Agnes Gerald a.k.a Masogange ya kutuhumiwa kusafirisha dawa za kulevya kuisha kwa kulipa faini nchini Afrika Kusini na kuwa mtu huru, hatimaye juzi Jumanne amerejea nyumbani Tanzania.


Kupitia Instagram juzi Agnes alipost picha (hapo juu) akiwa uwanja wa ndege na kuandika “am cmng homeeeeeeeee”.

Mwishoni mwa mwezi uliopita (September) mrembo huyo aliachiwa huru pamoja na mdogo wake Melissa Edward ambaye mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg, Afrika Kusini ilimuachia huru baada ya kukosa ushahidi wa kumtia hatiani.

Kama tunakumbuka vizuri mwaka 2010 Puff Daddy alishawahi kusema kuwa analaumu maisha yake ya utotoni hakupata malezi ya Baba ndio maana mpaka sasa hana mpango wa kuwa na mke sababu anaogopa kuwa kama Baba yake,hivi karibuni kaongea mapya kuhusu ndoa.


Rapper Na mfanya biashara mkubwa Marekani Puff Daddy maarufu sasa kama  Pdd amesema hana mpango wa kufunga ndoa siku za karibuni kwani anaamini kuwa watu wengi hutumia muda mwingi kuboresha ndoa badala ya kuwa na maisha yenye furaha na mtu anaye mpenda.

Pdd anaendela kusema kuwa mpaka sasa hajapata sababu za kuwa na mke ila anapenda sana watoto wake na familia yake na Bado Yupo yupo.

Fahamu kuwa Puff Daddy kwa sasa ana mahusiano ya muda mrefu na msanii wa Rnb Cassie ambaye yupo chini ya lebel yake Ya Bad Boys Entertainment

 Klabu ya Sunderland ya Egland imemteua Kocha wa zamani wa Brighton, Gus Poyet kuwa kocha mpya wa klabu hiyo kwa mkataba wa miaka miwili.
Klabu hiyo ambayo inajulikana kama "The Black Cats " inashikilia mkia katika ligi kuu ya Premier na ilimuondosha kazini Paolo Di Canio mnamo mwezi wa September baada ya kushikilia nafasi hiyo kwa mechi 13 tu.
"nina hamu ya kuwathibitishia uwezo wangu mashabiki--ninataka wawe na imani kwa sababu tunahitaji kushikamana " Poyet, mwenye umri wa miaka 45, ameiambia wavuti wa klabu hiyo.
Ataungana na wasaidizi wake za zamani wa Brighton, Mauricio Taricco na Charlie Oatway.
"Nadhani msingi wa mafanikio yangu katika mechi za nyumbani Brighton ni uhusiano wangu na mashabiki, --na naweza kuona hali hiyo hiyo hapa ,"aliongeza Poyet, ambaye alipigwa kalamu na Brighton mnamo mwezi wa Juni.
"ni changamoto kubwa lakini inanipa motisha na nashukuru kwa kupata fursa hii ya kuongoza katika ligi kuu"
Poyet ambaye ni mchezaji wa zamani wa taifa wa timu ya Uruguay atakua meneja wa sita wa Sunderland katika kipindi cha miaka mitano.
Kocha msaidizi wa Sunderland Kevin Ball amekua akishikilia uongozi wa klabu hiyo tangu Di Canio afutwe kazi kutokana na malalamiko ya wachezaji.

 Mke wa rapper Wiz Khalifa, Amber Rose amekata mtindo mpya wa nywele na kuwapa mashabiki nafasi ya kutoa maoni yao kuhusu mtindo huu kwenye instagram yake. Mtindo huu ameuita Zig Zag. 


 

 Daniel amekuwa kinyozi wa Bale toka siku ya kwanza ameanza kuichezea Tottenham.Jamaa ni kinyozi anaye aminika sana na mastaa wa soka nchini Uingereza kwa ujuzi na ubunifu wake wa mitindo tofauti ya nywele. 


Pia anauwezo wa kusikiliza na kufanya anacho taka mteja wake bila tatizo.
Picha Zingine Zipo Hapa 
Daniel Akiwa na Mchezaji Wa Man Untd Rooney.
Daniel Akiwa na Mchezaji Wa Man Untd Rio Ferdinand.
Hapa Daniel alikuwa amemaliza kumnyoa Mario Balotelli
Ashley Young
Jermain Defoe

Rais wa Cameroon Paul Biya amemshawishi mshambuliajhi Samuel Eto'o kufikiria kwa mara nyingine juu ya maamuzi yake ya kustaafu soka la kimataifa.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Cameroon na klabu ya  Chelsea alikutana na wawakilishi wa Rais Biya jijini Yaounde wakijadili juu ya hatima ya baadaye ya mshambuliaji huyo.

Baada ya kukutana hatimaye Eto'o, amekubali kurejea kuitumikia tena Cameroon. 
Sasa anatarajiwa kusafiri kuelekea Ufaransa kujiunga na kikosi cha timu hiyo ambacho kinajiandaa kwa ajili ya mchezo wa hatua ya mwisho kusaka tiketi ya kufuzu kombe la dunia wakikabiliwa na mchezo dhidi ya Tunisia.

Eto'o mwenye umri wa miaka 32 hapo kabla aliwaambia wachezaji wenzake kuwa hana nia ya kuendelea kuitumikia Cameroon kauli ambayo aliitoa baada ya mchezo dhidi ya Libya ambao walishinda na kusonga mbele katika hatua ya mwisho ya mtono.
 
Licha ya taarifa za kujiondoa kikosini, bado kocha wa kikosi hicho Volker Finke ameendelea kumtaja mchezaji huyo katika kikosi chake kitakacho vaana na Tunisia kwani alikuwa bado hajawasilisha taarifa rasmi ya tangazo lake hilo.
Eto'o amekuwa hana mahusinao mazuri na mamlaka ya soka ya nchi yake tangu huko nyuma ambapo akiwa nahodha aliongoza mgomo wa kudai posho kiasi hata kuvuruga mchezo wa kirafiki dhidi ya Algeria mwaka 2011.
Tukio hilo lilipelekea kufungiwa kwa michezo 15 kabla ya adhabu hiyo kupunguzwa na kuwa miezi minane.
Hii si mara ya kwanza kwa Rais Biya kukatisha majaribio ya kustaafu kwa wachezaji, kwani aliwahi kufanya hivyo kwa Roger Milla ambaye alirejea dimbani katika fainali za kombe la dunia mwaka 1990 nchini Italia.

Baada ya miaka 12 ya kuwa Boy Friend Na Girl Friend na kupata mtoto moja wa kiume mwenye umri wa miaka mitano sasa, inasemekana rapper Fabolous amejipanga kwa ndoa.


Hii ni baada ya mpenzi wake wa muda mrefu Emily B kuonyesha pete yake ya uchumba aliyovalishwa na rapper huyo.

Msanii wa kike kutoka Tanzania mwenye uwezo mkubwa wa kufanya muziki  wowote 'Shaa' ametia wino kwenye mkataba wa miezi sita na Saidi Fella kupitia Mkubwa Na Wanawe.
Saidi Fella amesema leo  kuwa mkataba huu ni wa muda mfupi na watafanya kazi tofauti na Shaa sababu anauwezo mkubwa wa kuimba na kufundisha muziki.

Saidi Fella amesema wamefanya mazungumzo na Aliyekuwa manager wa Shaa 'Master J' na wamekubaliana kuwa atafanya kazi na mkubwa na wanawe kwa misingi yao na baraka zote wamepewa.

Bab Tale amekuwa akifanya kazi na Shaa kwa muda sasa na kuhamia kwa Said Fella kutaka msaidi zaidi Shaa kuteka soko la nyumbani zaidi. Shaa amekuwa moja ya  wasanii Kutoka Tanzania mwenye mashabiki wengi nje ya nchi yake.

Awali Shaa aliwahi kufanya kasimamiwa na  Ay Na Master J. I Hope hizi ngoma mbili kutoka kwa Shaa zitatisha sana hapa Tanzania, Moja amefanya na At na Nyingine Na Rapper Shetta.

Shaa amesema haya ni maamuzi mazuri na yataongeza sana mashabiki wa muziki wake Nyumbani.
Star wa Basketball Wives LA Malaysia Pargo amegundua njia nyingine nzuri ya kumbana mume au mke wako. Hii itasaidi zaidi wale wana ndoa wanaopenda kuvua pete wakati wana saliti ndoa zao.
Pete hii unayoiva kwenye kidole chako cha ndoa inabakiza neno MARRIED Kwenye kidole chako so ata ukitoa bado unaye mdanganya atajua tu kuwa upo kwenye ndoa.

Malaysia amesema wanaume husema wanapenda kuvua pete wakiwa Kwenye mazoezi 'Gym' na muda mwingine wana sahau kuzirudishia kidoleni.

Malaysia amesema tayari ametengeneza Pete moja kwa ajili ya mume wake na ndio hio kwenye picha.

Waombolezaji walikua wamejaa katika msiba wa mpiga misele (drifter or spinner) maarufu Bongani Makhubo (40) jijini Pretoria, Afrika Kusini.

Baada ya mazishi, wapiga misele wenzie wakaanza kupiga misele na magari yao kama kumtolea heshima marehemu, huku wahudhuriaji wakishangilia.

Ghafla binti huyu akavua chupi yake na kuipunga hewani huku akidansi katikati ya magari yanayozunguka kupiga misele


Baadhi ya waombolezaji walikerwa na kitendo hicho lakini cha ajabu wengi walimuacha aendelee na walikua wakishangilia

Wimbo huu hapa chini nloikuta leo youtube na tayari  imetazamwa na Watu zaidi ya elf 50 ni kituko kwa sababu Diamond hawezi kamwe kumshirikisha Tanzanite wakati wana Bonge La Bif.


Tanzanite ndo yule msanii alokopy wimbo wa Diamond uitwao Tatizo kwetu Mbagala na kuiita Uchawi naWanga.

Tangia hapo Diamond alimchukia mno huyo mtoto.Sasa huu wimbo eti wamefanya Pamoja.Inaitwa MAPENZI-DIAMOND FT TANZANITE.Tetesi ni kwamba Tanzanite aliipata juu kwa juu huu wimbo na kuamua kuingia studio na kuweka mashairi zake.Ni ngoma ambayo ilikuwa bado haijakamilika na Diamond hakutaka kuitoa kwa sasa.Tanzanite akamzidi ujanja!!

TAZAMA MWENYEWE HAPA CHINI UJIONEE VITUKO.



Mauaji ya kikatili yanayodaiwa kufanywa na Kikundi cha Chinjachinja dhidi ya vikongwe, yamezidi kuutikisa Mkoa wa Geita baada ya kikongwe mwingine, kuuawa kwa kukatwa kwa mapanga akiwa nyumbani kwake.


Marehemu huyo ametajwa kuwa ni, Maua Ikoti(60) mkazi wa Kasang'hwa, wilayani Geita .

Mauaji hayo yamekuja huku takwimu zikionyesha kuwa  vikongwe watatu, wameuawa na kikundi hicho katika kipindi cha wiki nne zilizopita.

Baadhi ya watu wanahusisha maujai hayo  na imani za kishirikina.

Tukio la mauaji hayo lilitokea saa 6 usiku wa kuamkia juzi  baada ya wauaji  kuvamia familia hiyo na kisha kuingia ndani ya chumba alimokuwa amekala kikongwe huyo.

Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kasang'hwa, Maganiko Ndiomali, alisema wauaji walimkata kwa mapanga kikongwe huyo kichwani,mikono na kwenye matiti.

Alisema pamoja na mayowe yaliyopigwa na watoto wa marehemu ili kuomba msaada, juhudi za wananchi kuwasaka wauaji hazikuzaa matunda.

Kuna madai kuwa kikundi kinachohusishwa na mauaji hayo kimekuwa kikodiwa na baadhi ya watu ili kulipiza kisasi baada ya kufiwa na ndugu zao wakiamini kwamba wamerogwa.

Kikundi hicho kinadaiwa kuhusika na mauaji ya kikatili dhidi ya Mondesta Nchambi (53) mkazi wa kitongoji cha Isabilo wilayani Chato kwa kumchinja mithili ya kuku.


Kamanda wa polisi mkoani Geita,Leonard Paulo alithibitisha kuwepo kwa matukio hayo lakini alisema hadi sasa hakuna mtu au watu waliokamatwa wakihusishwa na mauaji hayo.



Source-Mwananchi
MAKOMANDOO sita wa Jeshi la Marekani, wakiwamo wawili walioshiriki kumuua Kiongozi wa Al Qaeda, Osama bin Laden, wamefanikiwa kumuua kinara wa kundi la Al Shabaab anayedaiwa kupanga mashambulizi ya kigaidi katika jengo la biashara la Westgate mjini Nairobi nchini Kenya mwezi uliopita na kusababisha vifo vya watu 68 na wengine zaidi ya 175 kujeruhiwa.


Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, John Kerry, aliyeko ziarani nchini Indonesia, aliwaambia waandishi wa habari jana, kuwa gaidi huyo aliuawa wakati wa mapambano kati yake na makomandoo hao. Hata hivyo, hakumtaja jina.

John Kerry alisema “Jumamosi iliyopita, makamandoo hao wa Marekani, walishambulia nyumba ya kiongozi huyo mjini Barawe, Somalia. Mashambulizi yaliyofanywa na wanajeshi wa kikosi maalumu cha Marekani nchini Libya na Somalia, yanaonyesha dhamira ya Serikali ya Marekani kuwasaka magaidi.”

Alisema kwamba, taarifa za kiintelijensia, zinaonyesha kinara huyo ambaye alikuwa mshirika mkuu wa Kundi la Al-Shabaab, alihusika moja kwa moja katika shambulio la kigaidi katika jumba la maduka la Westgate.

Kerry alisema kwamba, baada ya kumaliza kazi hiyo, wanajeshi hao waliondoka mjini Barawe na kurudi Marekani.


Ni katika operesheni hii ambapo pia makomandoo wa Marekani walimkamata kiongozi wa Kundi la Al-Qaeda, Anas al Libi katika mji mkuu wa Libya, Tripoli. Anas al-Liby, anahusishwa na matukio mengi makubwa yakiwamo ya kuwavizia watu wenye asili ya Marekani kuwakamata na kuwafanyia vitendo vya kinyama

HATIMAYE Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Zitto Kabwe, ameweka wazi mshahara wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Zitto ameutaja mshahara huo wa Pinda anayejitambulisha kama ‘mtoto wa mkulima’ juzi mjini Mpanda na jana wilayani Sikonge wakati akihutubia mikutano ya hadhara katika ziara ya Kanda ya Magharibi kwa ajili ya ujenzi wa chama.

Alisema Pinda anapokea jumla ya sh milioni 26, ambazo ni kiasi kikubwa kulinganisha na uchumi wa nchi.

Akichanganua alisema Pinda anapokea sh mil. 11.2 kama mbunge, sh mil. 8 kwa nafasi ya waziri na kiasi kinachosalia kufikia sh mil. 26 kwa nafasi yake ya uwaziri mkuu.

Alisema sababu hiyo ya mishahara mikubwa isiyokatwa kodi ndiyo huwafanya viongozi wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwa wakali pale vyombo vya habari vinapotaka kuwafahamisha wananchi namna watumishi wao wanavyojilipa.

“Nimeanza na mshahara wa waziri mkuu pia siku zijazo nitataja na wa rais, kwa kuwa amesaini makubaliano na Serikali ya Marekani kuendesha nchi kwa uwazi, na moja ya uwazi ni kwa muajiri kujua kiasi anachomlipa mwajiriwa wake,” alisema Zitto.

Hatua ya Zitto imekuja baada ya kuwapo mvutano mkubwa kuhusiana na kile kinachodaiwa ‘usiri’ wa mishahara ya watumishi wa umma, wakati ni haki ya walipa kodi kujua kile wanachowalipa walioomba kuwaongoza.

Kodi ya laini za simu

Akizungumzia sakata la kodi katika laini za simu, Zitto alisema CCM ina ajenda ya kisiasa kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2015.

Alisema serikali baada ya kubaini watu wengi wanapeana taarifa kwa njia ya ujumbe mfupi, hususan katika masuala ya kisiasa, wakaona njia sahihi ya kudhibiti ni kuwatoza kodi ya laini ili kupunguza hatari ya mawasiliano hayo kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao.

“Sikuwepo bungeni wakati wabunge wa CCM wanapitisha kadhia hiyo ya kuwanyonya wananchi, wenzangu wakaniambai tukasema hapana, kwa maana tuliona hii leo kuna Watanzania wengi wasio na uwezo wa kuhudumia simu kwa kiasi cha sh 1,000 kwa mwezi,” alisema Zitto.

Akijibu maswali ya wananchi mjini Mpanda waliotaka kujua sababu ya kupunguza makali bungeni, Zitto alisema hakuna makali yaliyopungua bali ni mitazamo ya watu.

Alisema kwa kushirikiana na wabunge wenzake wa upinzani wamekuwa wakisimamia hoja zenye manufaa kwa wananachi huku wabunge wanaojipambanua kuwa majasiri kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakiwaunga mkono wazi wazi.

Akiwa  wilayani Sikonge, Zitto alisema Watanzania hawawezi kujivunia uhuru huku mama zao, watoto wao na wazee wao wakiwa hawana uhakika wa kupata huduma bora ya afya, elimu na maji safi.

Alisema kwa sasa Tanzania ni taifa moja lililogawanyika katika nchi mbili za wenye fedha na wasio na fedha.


Alisema nchi ya wenye fedha, fam