advert

http://

Monday 13 April 2015

Nigeria:APC yatwaa majimbo19 kati ya 29


 mwenzako
Nigeria:APC yatwaa majimbo19 kati ya 29
Chama cha rais mteule wa Nigeria APC, kimesajili ushindi mkubwa wa majimbo 19 kati ya 29 katika matokeo ya hivi punde yaliyotangazwa na tume huru ya uchaguzi INEC.
Awali INEC ilikuwa imethibitisha kuwa chama cha rais mteule The All Progressives Congress (APC) kilikuwa kimetwaa miji mikuu ya Lagos Kaduna na na Katsina.
Matokeo haya ya hivi punde ni dhihirisho kuwa raia wa Nigeria walipigia Kura kiongozi wa upinzani Jenerali mtaafu Muhammadu Buhari.
Ushindi huo ni dhidirisho ya kuwa chama kinachoondoka madarakani cha Rais Goodluck Jonathan PDP kimepata kichapo chake kikubwa zaidi tangu kukamilika kwa utawala wa kijeshi mwaka wa 1999.
APC, kimeshinda majimbo makuu ya Lagos kaduna na Katsina katika uchaguzi mkuu wa Nigeria
Jenerali mstaafu Muhammadu Buhari anatarajiwa kuapishwa rasmi kama rais wa taifa hilo lenye uchumi mkubwa zaidi barani Afrika mwishoni mwa mwezi Mei.
Mwandishi wa BBC aliyeko Abuja Bashir Saad Abdullahi anasema kuwa chama cha jenerali mstaafu Muhammadu Buhari The All Progressives Congress (APC)
Kilihifadhi jimbo la Lagos mbali na kutwaa majimbo zaidi ya Kaduna naKatsina.
Ushindi huu wa majimbo zaidi unaiongezea pondo serikali mpya haswa baada ya kutwaa ushindi mkubwa dhidi ya Rais Goodluck Jonathan.
Matokeo kamili ya kura za majimbo 39 na magavana 29 unatarajiwa kutolewa baadaye.
Jenerali mstaafu Muhammadu Buhari anatarajiwa kuapishwa rasmi mwishoni mwa mwezi Mei.
Magavana 29 wa Nigeria wanaushawishi mkubwa kutokana na uwezo wao mkubwa wa kiuchumi
Lagos
Uchaguzi huu wa majimbo umeendeleza dhana ya kuwa APC itazoa maeneo wakilishi mengi kufuatia ushindi wa wa kihistoria wa jenerali mstaafu Muhammadu Buhari.
Siku ya jumapili, tume huru ya uchaguzi nchini humo (Inec) ilitangaza rasmi kuwa chama cha Jenerali mtaafu Buhari APC ilikuwa imetwaa jimbo la Lagos mbali na kushinda ugavana wa majimbo ya Kaduna na Katsina majimbo
ambayo yaliongozwa na kudhaniwa kuwa ni ngome ya PDP
Chama cha PDP hata hivyo kilihifadhi jimbo la Rivers
Kwa wadadisi wengi utawala wa Jenerali mstaafu Buhari utakuwa utawala wa kwanza kutawala nchi na vilevile mji mkuu wa kiuchumi nchini humo wa Lagos tangu kumalizika kwa utawala wa kiimla mwaka wa 1999.
Vilevile hii ndio itakayokuwa mara ya kwanza kwa chama ambacho sio PDP kuwahi kuiongoza majimbo ya Kaskazini mwa taifa hilo.
Uongozi wa majimbo 36 unaumuhimu mkubwa haswa kiuchumi kwani magavana wengi katika maeneo yenye utajiri mkubwa wa mafuta huwa wana makadirio ya bajeti makubwa hata zaidi ya mataifa mengine ya Magharibi mwa Afrika.
Chama cha PDP hata hivyo kilihifadhi jimbo la River

Hatimaye waliombaka Liz wahukumiwa Kenya

Mshirikishe mwenzako
Hatimaye haki imetendeka baada ya watu watatu waliombaka msichana mdogo Liz kuhukumiwa kifungo cha mika 15 jela nchini Kenya
Mahakama moja mjini Busia, imewahukumu washukiwa watatu vifungo vya kati ya miaka saba na kumi na tano gerezani,baada ya kuwapata na hatia ya kumbaka na kumjeruhi msichana mmoja, aliyefahamika kama Liz.
Liz inasemekana alishambuliwa na vijana hao na kubakwa wakati alipokuwa akirejea nyumbani kutoka kwa mazishi ya babu yake katika eneo la Busia Magharibi mwa Kenya.
Tukio hilo lilizua mjadala mkali nchini Kenya huku wanaharakati wa kijamii wakishinikiza serikai kuwachukulia washukiwa hao hatua kali.
Watatu hao walikuwa wamehukumiwa ''kufyeka nyasi katika kituo cha polisi'' na kuachiliwa huru.
Hata hivyo msichana huyo alikuwa amepooza kiwiliwili chake kuanzia kiunoni kufuatia kutupwa katika shimo ilikuficha ushahidi alipata
msaada baada ya wanaharakati wa kupigania haki za kibiniadamu kuishinikiza polisi kuchukua hatua dhidi ya polisi waliotoa hukumu hiyo nyepesi dhidi ya watu hao watatu.
Mamake Liz ameiambia BBC kuwa hatimaye haki imetendeka.
Mamake Liz ameiambia BBC kuwa hatimaye haki imetendeka.
Watatu hao sasa wamepatikana na hatia ya kumjeruhi Liz na kuhukumiwa kifungo cha miaka 7 Jela.
They were also found guilty of causing bodily harm and sentenced to 7 years in prison.
Harakati za kumtafutia haki msichana huyo ziligonga vichwa vya habari mwaka uliopita watu zaidi ya miklioni 2
kote duniani walipotia sahihi kampeini ya kumlazimisha Inspekta mkuu wa Polisi
kuwachukulia hatua watatu hao ambao walikuwa wamedaiwa kuwahonga maafisa polisi huko Busia Magharibi mwa Kenya.
CHANZO: BBCSWAHILI.COM

Sunday 12 April 2015

Ubalozi wa K Kusini washambuliwa Libya


Libya
Watu wasiojulikana wameushambulia ubalozi wa Korea Kusini kwenye mji mkuu wa Libya Tripoli ambapo walinzi wawili wa ubalozi huo waliuawa.
Wizara ya mashauri ya kigeni nchini Korea Kusini imesema kua watu hao walifyatua risasi wakilenga ubalozi huo wakiwa ndani ya gari.
Hakuna raia yeyote wa Korea Kusini aliyeripotiwa kujeruhiwa wakati wa shambulizi hilo.
CHANZO.BBCSWAHILI.

Tuesday 12 August 2014

Ndugu Watano Watembea kwa Miguu na Mikono...




FAMILIA moja ya Uturuki inawapasua kichwa wanasayansi, kutokana na wanandugu watano kutokuwa na uwezo wa kutembea kama binadamu, na badala yake wanatembea mithili ya wanyama, wakitumia miguu na mikono.
 
Hata hivyo, katika uchunguzi wao wa awali, wanasayansi hao wameeleza kuwa, hali iliyowakumba wanandugu hao haina uhusiano na mabadiliko ya binadamu, kwamba wanaanza kurudi katika zama za mwanzo ambako inaelezwa walitembea kwa miguu minne, wengine wakisema walianza kuwa nyani.
 
Ndugu hao watano ambao ni kaka na madada, wakiwa na umri wa miaka 16 hadi 34 kutoka kijiji cha Jimbo la Hatay, kusini mwa Uturuki, walianza kufuatiliwa na wanasayansi mwaka 2005 baada ya kugundulika na watu kutoka nje ya kijiji chao.
 
Wanatembea kwa mtindo wa kutambaa kama dubu kwa mikono na wanaweza kusimama tu kwa muda mfupi, kwa magoti yao.
 
Utafiti wa hivi karibuni ulifanywa na wanasayansi, Shapiro, Whitney Cole, Scott Robinson na Karen Adolph, wote wa Chuo Kikuu cha New York, Jessica Young wa Chuo Kikuu cha Tiba cha Northeast Ohio na David Raichlen, wa Chuo Kikuu cha Arizona.
 
“Lakini hawa hawana uhusiano na mgeuko wa binadamu kwamba baada ya kupitia hatua kadhaa za mabadiliko, sasa wanarudi katika hatua za awali, hilo halipo,” mmoja wa wanasayansi hao amenukuliwa akisema.
 
Nadharia za awali zilidai familia ya Ulas ilikuwa ikitembea kama nyani, na kupendekeza kuwa huenda ni hatua ya kurudi nyuma kwa mabadiliko ya binadamu.
 
Lakini sasa, wanasayansi wa Kimarekani wamethibitisha kwa kusema wanandugu hao wanakabiliwa na kasoro isiyoonekana na hutokea mara chache.
 
Katika ripoti iliyochapishwa na PLOS One, watafiti walisema familia hiyo wanatembea kwa namna tofauti kama nyani, ambao wakitembea huweka mikono upande mmoja na miguu upande mwingine wakijirudiarudia.
 
Walidai kutembea kwa wanandugu hao ni matokeo ya hali ya kurithi ambayo husababisha uwiano wa akili kutatizika.
 
“Nilikuwa na hamu ya kuweka rekodi sawa, kwa kuwa haya madai ya asili na sababu ya kutembea kama mnyama wa miguu minne imechapishwa mara kwa mara, bila kuwepo uchambuzi wa kwa nini wanatembea hivyo, na watafiti ambao si wataalamu wa namna mamalia wa hali ya juu wanavyotembea,” Mtafiti Kiongozi Liza Shapiro wa Chuo Kikuu cha Texas alilieleza gazeti la The Washington Post.
 “Tumeonesha wanyama wa miguu minne wanavyofanana na mtu mzima mwenye afya njema ambaye ameambiwa atembee kwa miguu minne wakati wa kufanya majaribio."
 
Mwaka 2005, watafiti wa Uingereza walikubali katika utafiti tofauti kuwa utembeaji wa ndugu hao unatofautiana na baadhi ya mamalia wengine, ikizingatiwa wenyewe hubeba uzito wao wote kwenye viganja vya mkono na kifundo cha mkono na sio kiungio.
 
Hata hivyo, Mtaalamu wa Bayolojia wa Uturuki, Uner Tan awali alidai wanandugu hao, ambao pia wanaonekana kuwa wameathirika kwenye ubongo wanakabiliwa na hali inayoitwa Uner Tan Syndrome.
 
Alisema watu wanaokabiliwa na hali hiyo hutembea kwa miguu minne na mara nyingine huzungumza kama wanyama na huwa na mtindio wa ubongo.
 
“Ghafla nimegundua wanatembea kwa mtindo kama nyani kama walivyokuwa wahenga wetu… nilikuwa wa kwanza kupendekeza kuwa kuna uwezekano wa hali ya binadamu kugeuka na kurudi enzi za zamani za ubinadamu,” alisema.
 
Wandugu hao ambao wazazi wao wanatembea kawaida, mara ya kwanza walirushwa mwaka 2006 kwenye dokumentari ya BBC2, dokumentari hiyo ikiitwa The Family That Walks On All Fours.
 
Wakati mabinti wawili na mtoto mmoja wa kiume wamekuwa wakitembelea mikono miwili na miguu miwili, mtoto mwingine wa kiume na kike mara nyingine huweza kutembea wakiwa wamenyooka sawa, ingawa si kwa muda mrefu.
 
Profesa Nicholas Humphrey, ambaye aliitembelea familia hiyo mara mbili wakati wa dokumentari hiyo, alisema,“inashangaza kama mfano wa kitu cha ajabu cha maendeleo ya binadamu. Lakini kinachovutia ni jinsia wanavyoweza kuishi katika ulimwengu wa kisasa.”
 
Alisema alifikiri familia hiyo imerudi katika silika ya mfumo wa tabia iliyojikita ndani sana kwenye ubongo, lakini aliachwa wakati wa mageuko.
 
“Sidhani kama walitakiwa kuwa wanyama wanaotembelea miguu minne kutokana na jeni zao, lakini mfumo wa utengenezaji jeni zao zinawaruhusu kuwa hivyo,” alisema.
 
Wanandugu hao watano ambao wana kaka na dada zao wengine 14 ambao hawajaathirika na hali hiyo, hutumia muda mwingi kukaa nje ya nyumba yao ya familia iliyoko kijijini. Hata hivyo, mmoja wao hutembea kijijini, kuchanganyika na kuzungumza na watu.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe, Fulgence Ngonyani na dereva wake, Nuaka Seme wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Njombe ya Kibena baada ya kupata ajali ya gari iliyomuua mlinzi wa kamanda huyo, usiku wa kuamkia jana, eneo la kiwanda cha miwati (TANWAT).
 
Ngonyani akizungumza hospitalini hapo, alisema ilitokea kati ya saa tatu na saa nne usiku katika barabara ya Makambako -Njombe. Alimtaja mlinzi wake aliyekufa ajalini kuwa ni Konstebo George Stephano Matiko (24).
  
Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe ASP Fulgence Ngonyani.

Naye dereva Nuaka, alisema akiwa anaendesha gari la Polisi lenye namba za usajili PT 2058 alivaana na lori ambalo dereva wake aliendesha akiwa katikati ya barabara na baada ya kumwashia taa zote, alijaribu kuhamia upande wake lakini hakufanikiwa kunusuru ajali baada ya kukwanguana.
 
“Mara baada ya kukwanguliwa tulilikwepa lori tukaigonga nguzo ya umeme na hapo hapo mwenzetu akafa na tunashukuru sana wafanyakazi wa kampuni ya Tanwat ambao waliwahi kuja kutusaidia... na lile lori hatukuweza kuchukua namba zake na liliendelea na safari.”
 H580 Pc George  Enzi za uhai wake.

                                                   SOURCE: BABA MZAZI

Monday 30 June 2014

Chui apanda boti na kumshambulia mvuvi akiwa na watoto wake.


Chui apanda boti na kumshambulia mvuvi akiwa na watoto wake
Imeripotiwa kuwa chui mwenye hasira na njaa aliingia majini na kupanda boti ya mvuvi aliyetajwa kwa jina la Shushil Manjhi huko Kolkata, India na kuondoka nae.

Taarifa zilizoripotiwa na vituo vya nchini India vinaeleza kuwa, mvuvi huyo alikuwa na watototo wake wawili (wa kike na wakiume) wakijaribu kutafuta kitoweo karibu na hifadhi ya taifa ya Sunderbans yenye wanyama wakali.
Mwanae wa kiume, Jyotish alieleza kwa njia ya simu kuwa chui huyo alirukia boti na kumkamata baba yake shingoni kwa upande wa nyuma na kuanza kumburuza akiondoka nae akielekea msituni.
“Alimrukia baba yangu kwa haraka mgogoni na kung’ata kwa nguvu kabla hajatokomea nae msituni.” Alieleza.
Mtoto huyo anaeleza kuwa baada ya chui huyo kumkamata baba yake, yeye na mdogo wake walijaribu kumpiga na fimbo na visu walivyokuwa navyo lakini hakuweza kumuachia.
Tukio hilo linatoa picha ya maisha duni ya wananchi masikini wa eneo hilo ambao licha ya kuwa na hatari kubwa ya kuuawa na wanyama wakali, hali ngumu ya maisha huwasukuma kuingia msituni kusaka kitoweo au chochote licha ya kwamba ni kinyume cha sheria kufanya uvuvi katika eneo la hifadhi ya wanyama.
Inaelezwa kuwa samaki wanaopatikana katika hifadhi hiyo hunuliwa kwa pesa nyingi katika miji ya jirani na vijiviji vya eneo hilo.

BOFYA HAPA UWACHEKI HAWA JAMAA KATIKA VIDEO, NI SHETTA FT DIAMOND, ILA NI FEKI SIO WENYEWE REAL https://www.youtube.com/watch?v=bRDoVEh9eh8


M 2 THE P AKIWA NA SWAHIBA WAKE NGWEAR KIPINDI HICHO
BOFYA HAPA KUINJOI SHOW YAKE  https://www.youtube.com/watch?v=WRtmRKzL5Zw&feature=em-subs_digest

Msichana aliyemuua mama yake kwa kumchoma visu mara 151 akwepa jela
 Taarifa kutoka Colorado, Marekani zinaeleza kuwa Msichana mwenye umri wa miaka 19, anaefahamika kwa jina la Isabella Yun-Mi Guzman ambaye alimchoma mama yake visu mara 151 ameachiwa huru.

 Mahakama imemuachia huru Isabella baada ya kubaini kuwa ni mgonjwa wa akili na kwamba wakati anatekeleza tukio hilo hakuwa katika hali ya kawaida kiakili hivyo kwa mujibu wa sheria hana hatia.
 Mahakama imeamuru msichana huyo kupelekwa katika hospitali ya wagonjwa wenye matatizo ya akili kwa ajili ya kupata matibabu badala ya kumpeleka jela.
 Kwa mujibu wa ripoti zilizofikishwa mahakamani hapo na polisi, Issabella alimchoma mama yake visu mara 151 (Mara 35 usoni, mara 51 shingoni, na mara 65 katika sehemu nyingine za mwili.
 Msichana huyo amepelekwa  Colorado Mental Health Institute.   



Millard Ayo (Mtangazaji machachari wa Clouds Fm) ameibuka kidedea kwa kunyakua tuzo mbili,
hivyo vikiwa ni vipengele vyote alivyoshindanishwa. Kilele cha Tuzo hizo kilikuwa ni Ijumaa hii
katika Serena Hotel, Dar es Salaam.

Kumbuka tu kwamba hivi majuzi nilikujuza kwamba Wema alikuwa mstari wa mbele kuwashawishi mashabiki kumpigia kura Millard Ayo, unaweza kujikumbusha hapa http://www.babamzazi.com/2014/06/millard-ayo-na-wema-sepetu-mhhh.html Je hatuwezi kusema Wema amechangia kwa kiasi kikubwa kushinda kwa Millard? Maana Wema ana fans wengi sana, na kama fans wake wote wamemuunga mkono kwa kutekeleza kile achowaomba nazani hilo halikuwa la kutowezekana. Picha kati ya waili hawa ikiendelea, basi ww.babamzazi.com itaendelea kuwajuza.

Tuzo alizonyakua Millard ni ya MTANGAZAJI WA REDIO
ANAYEPENDWA na KIPINDI CHA REDIO KINACHOPENDWA (Ambacho ni AMPLIFAYA)

Hongreara sana  Millard Ayo kwa kunyakua Tuzo mbili

Washindi wengine katika vipengele mbalimbali ni kama ifuatavyo:

1 na 2 = MILLARD AYO

3.MTANGAZAJI WA RUNINGA ANAYEPENDWA = Salim Kikeke – BBC Swahili

4. KIPINDI CHA RUNINGA KINACHOPENDWA= Mkasi – EATV

5. MWANAMICHEZO ANAYEPENDWA=Juma Kaseja – Yanga

6. MUONGOZAJI WA VIDEO ZA MUZIKI ZINAZOPENDWA =Nisher

7. VIDEO YA MUZIKI INAYOPENDWA YA MWANAMUZIKI WA KIUME=My Number – Diamond

8. VIDEO YA MUZIKI INAYOPENDWA YA MWANAMUZIKI WA KIKE= Yahaya – Lady Jaydee

09. MUIGIZAJI WA KIUME KWENYE FILAMU ANAYEPENDWA= King Majuto

10. MUIGIZAJI WA KIKE KWENYE FILAMU ANAYEPENDWA =Elizabeth ‘Lulu’ Michael

11. FILAMU INAYOPENDWA =Ndoa Yangu



     SOURCE:D'JARO ARUNGU

Saturday 28 June 2014

Canada wamefungisha ndoa 115 za jinsia moja kwa wakati mmoja.



wedding2
Wapenzi wa muda mrefu Richard Laslett na Collin Gunther ambao wamedumu kwenye mahusiano kwa muda wa miaka 37 wamepata nafasi ya kuwa moja kati ya wapenzi wa jinsia moja 115 waliofungishwa ndoa kwa wakati mmoja mjini Toronto, Canada.

weddind
Ndoa hizo zimefungwa kwa pamoja na kuwakutanisha wapenzi wa jinsia moja kutoka maeneo mbalimbali duniani kusherekea nguvu ya mapenzi yao.
Meya wa Toronto Norm Kelly amesema wanandoa hao wamekutana na kufurahia hatua hiyo muhimu ya kufunga pingu za maisha.
wedding3 
Takribani nchi 15 duniani sasa zimeruhusu mapenzi ya jinsia moja .
lesbian

ChargingCables22
Mamlaka nchini Australia imetoa tahadhari dhidi ya matumizi ya charger aina ya USB feki au zilizo chini ya viwango huku zikiwa zimechomekwa kwenye umeme baada ya mwanamke mmoja kufariki dunia wakati akitumia charger ya aina hiyo kucharge simu yake iliyokuwa imechomekwa kwenye kompyuta yake ndogo.

Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 28 alikutwa amevaa headphones masikioni akiwa na kompyuta yake mikononi huku akiwa na majeraha ya kuungua kifuani na masikioni nyumbani kwake huko Gosford, Kaskazini mwa Sydney.
ChargingCables
Polisi nchini humo bado wanafanya uchunguzi kujua mazingira ya kifo hicho lakini kitengo cha biashara kilichofuatilia suala hilo kimetahadharisha kuwa charger za simu zilizo chini ya viwango ni moja ya sababu kubwa.
Mwanamke huyo ambaye ripoti zinadai kuwa anatokea nchini Ufilipino na baadae kuwa raia wa Australia alivaa headphones zilizokuwa zimechomekwa kwenye kompyuta ndogo iliyokuwa imechomekwa kwenye socket ya umeme.
Eminem alizuiwa kuperform Uingereza kwa kuwa nyimbo zake zina matusi

 Ripoti zilizoandikwa na gazeti la The Daily Mirror zinaeleza kuwa lugha ya matusi kwenye nyimbo za Eminem ndio chanzo cha yeye kukataliwa kufanya show kwenye eneo la Hyde Park, Uingereza.

 Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mmiliki wa Hyde Park, Linda Lennon ameeleza kuwa aliamua kutompa nafasi Eminem kuperform katika eneo hilo kwa kuhofia ujumbe wa nyimbo zke na lugha anayotumia ingewaudhi wateja wake.
 Ofisi ya Mayor wa jiji la London, Boris Johnson imeeleza kuwa haikuhusishwa kabisa katika uamuzi wa kumzuia Eminem kuperform katika Hyde Park. Walifafanua kuwa hawakufahamu Eminem ni nani na hawakuwa na uwezo wa kuingilia maamuzi ya Wamiliki wa eneo hilo.
 Eminen alitarajiwa kuperform katika Hyde Park June 3 kabla hajazuiwa.
Lupita Nyong

 Lupita Nyong’o anazidi kuwaongezea wakenya nafasi ya kutajwa kwenye tuzo za Oscar hata kama sio katika kupata tuzo tu baada ya kuongezwa kuwa kati ya watu 271 wanaounda Academy ya tuzo za Oscar mwaka huu.
Muigizaji huyo wa 12 Years A Slave, ambaye ni mshindi wa tuzo ya Oscar ya mwaka jana kama muigizaji bora wa kike msaidizi, anaungana na wasanii wengine waliong’ara mwaka jana katika tasnia ya filamu pamoja na mwanamuziki Pharrell Williams kama members wapya wa Academy hiyo.
 Wasanii wengine wenye umri mdogo watakaoungana na Lupita ni pamoja na Josh Hutcherson, Michael Fassbender, Ben Foster, Sally Hawakins, Julia Lousi-Dreyfus, Chris Rock na Jason Statham.
 Rais wa Oscar Academy, Cheryl Boone Isaac ameeleza kuwa Academy ya mwaka huu itawahusisha watu ambao wana vipaji zaidi na wabunifu katika masuala ya fulamu.
 “Mchango wao katika filamu umewaburudisha hadhira kote duniani, na tunajivunia kuwakaribisha kwenye Academy.” Aliseam Cheryl Boone.

Uingereza warejea nyumbani kama yatima, mashabiki wagoma kujitokeza uwanja wa ndege
Mashabiki wa soka nchini Uingereza wamegoma kuilaki timu yao wakati ilipowasili jijini Manchester, ikitokea nchini Brazil ambapo ilikuwa ikishiriki fainali za kombe la dunia za mwaka 2014.

 Wakati kikosi cha Uingereza kikiwasili kwenye uwanja wa ndege wa Manchester, palionekana kimya, kama mashabiki wa soka walikuwa hawajui kinachoendelea mara baada ya timu yao kushindwa kufurukuta kwenye michezo ya kundi la nne ambalo liliijumuisha timu ya Italia, Uruguay pamoja na Costa Rica.
 Hata hivyo wachezaji wa timu ya taifa ya Uingereza walionekana kutokuwa na furaha licha ya kurejea nyumbani salama, ambapo kila mmoja alionekana anashuka kutoka kwenye ndege akiwa na begi pamoja na mfuko mweupe ambao unahisiwa huenda ikiwa ni zawadi za familia zao.
 Kitendo cha mashabiki wa Uingereza kuilaki timu yao huko Manchester Airport, kimekuwa ni tofauti kubwa kilichoonekana katika nchi nyingine zilizoshindwa kuendelea katika fainali za kombe la dunia, ambapo imeonekana mashabiki wa nchi hizo kama Hispania wakijitokeza uwanja wa ndege na kuonyesha upendo dhidi ya wachezaji wao.

Mwanariadha mwenye ujauzito wa miezi nane akimbia mita 800 kwa dakika 2

 Alysia Montano, mwanariadha wa kike na mshiriki wa Olympic aliyewahi kushinda mara tano mashindano ya riadha ya Marekani ambaye hivi sasa anaujauzito wa miezi 8, bado anashiriki riadha na hali aliyonayo.

 Alysia amewashangaza wengi baada ya kukimbia umbali wa mita 800 kwa dakika 2 na sekunde 32 huko California, jana (June 26), ikiwa amechelewa sekunde 35 tu ya uwezo wake wakati akiwa hana ujauzito.
 Mwaka 2010, mwanamke huyo akiwa katika hali nzuri alikimbia mita 800 kwa dakika 1 na sekunde 57.
 Mwanariadha huyo ameeleza kuwa yeye anajisikia vizuri kukimbia umbali huo akiwa na ujauzito na kwamba amekuwa akifanya hivyo katika kipindi chote cha ujauzito na ameruhusiwa na daktari.
 “I've been running throughout my pregnancy and I felt really, really good during the whole process.” Alisema baada ya kumaliza kukimbia.
Diego Maradona awachokonoa FIFA, avaa nguo inayounga mkono utovu wa nidhamu

 Gwiji wa soka nchini Argentina Diego Armando Maradona ameushangaza ulimwengu wa soka baada ya kuonekana amevaa flana yenye maandishi yanayomuunga mkono mshambuliaji kutoka nchini Uruguy Luis Suarez ambaye ameanza kutumikia adhabu ya kufungiwa.
Maradona alionekana amevalia flana hiyo alipokuwa kwenye kipindi cha televishani usiku wa kuamkia hii leo huko nchini Brazil, ambapo maandishi hayo yalisomeka “Luisito, estamos con vos” yakimaanisha tupo pamoja na wewe.
 Hatua hiyo Maradona kuvaa flana yenye maandishi ya kumuunga mkono Luis Suares inadhihirisha ni vipi mchezaji huyo wa zamani wa Argentina hakubaliani na maamuzi ya FIFA.
 
 Mbali na kuhisiwa hivyo pia mashabiki wa soka duniani kote wameanza kubaini huenda watu wa Amerika ya kusini wakawa kitu kimoja katika harakati za kupingana na maamuzi ya FIFA ambayo yamenza kutafsiriwa kama kutaka kuwabeba baadhi ya wachezaji kwenye fainali za kombe la dunia zinazoendelea nchini Brazil.
 
 Hata hivyo hii si mara ya kwanza kwa Luis Suarez kuungwa mkono baada ya kuonyesha vitendo vya utovu wa nidhamu anapokuwa uwnajani, kwani kama itakumbukwa vyema mwaka 2011, wakati alipokabiliwa na sakata la kumtolewa maneno ya kibaguzi beki wa pembeni wa Man Utd Patrice Evra, wachezaji wenzake wa klabu ya Liverpool walivaa flana zilizokuwa na maandishi yalionyesha kuwa wapo pamoja na mshambuliaji huyo.
 Wachezaji wa Liverpool walivaa flana hizo kwa pamoja wakati wakijiandaa na mchezo wa ligi ya nchini humo dhidi ya Wigan katika msimu wa mwaka 2010-11.

Uvutaji Shisha wapigwa marufuku Kenya, hubeba dawa za kulevya
 Kenya imepiga marufuku uvutaji wa Shisha (Sheesha) kwa ladha 19 baada ya kugundua kuwa zinabeba madawa ya kulevya kama heroin, bangi na cocaine.

 Amri hiyo imetangazwa jana na kuongezewa uthibisho na chombo kinachoshughulikia kampeni ya kupambana na matumizi ya dawa za kulevya, NACADA (National Campaign Against Drug Abuse) ambacho kilieleza kuwa kimefanyia majaribia ladha 100 za Sheesha wakiwa na ofisi ya wizara ya afya na wamegundua kuwa aina hizo 19 hubeba madawa ya kulevya.
 Kati ya ladha zilizopigwa marufu ni Al Fakher strawberry flavor, Al Fakher orange flavor, Al Fakher two apples with mint flavour, Al Fakher vanilla flavour, Al Fakher two appeals flavor, Al Fakher guava flavor, Al Fakher orange with mint flavor, Al Fakher orange flavor na 

nyingine.



          SOURCE:DJARO ARUNGU