advert

http://

Sunday 15 December 2013

Mama Mlemavu Akionyesha UPENDO kwa Mwanae.


Upendo wa Mama.

Wakazi wa eneo la Likoni, Mombasa nchini Kenya walipatwa na mshangao mkubwa mara baada ya mbuzi mmoja kujifungua mtoto mwenye sura inayofanana na binadamu.

Tukio hilo lilifanya shughuli mbalimbali kwenye kijiji hicho kusimama huku wakazi wa eneo hilo wakiwa wanastaajabu juu ya tukio hilo la ajabu.
 
Tazama video ya tukio hilo hapo chini....
 

Lulu
Muigizaji wa filamu nchini Elizabeth Michael aka Lulu, amesema kuwa hatamani tena kutumia simu ya mkononi kwakuwa anasumbuliwa mno na watu wasiokuwa na mambo ya msingi huku akitamani irudi enzi ya kutumiana barua.


Akiongea na paparazi wetu jana,Lulu alisema kuwa kero hiyo humfanya atamani kurudi katika enzi za kale za kuwasilia kwa kutumiana barua kwa njia ya posta.

“Nadhani sihitaji simu ya mkononi kwa sasa, mwenye shida na mimi atanitumia barua. Sijui, hata sijielewi nikasimame wapi, maana hata nikibadili nambari ya simu inasambaa kwa kasi sana,”alisema.

Lulu alibainisha kuwa kwa siku hupigiwa simu zisizokuwa na idadi na zisizo na faida kwake, lakini akakiri kwamba idadi kubwa ya watu wanaompigia simu ni mashabiki wake.

“Ninapigiwa simu nyingi kwa siku ambazo ni kero kwangu, nafurahi sana ninapopigiwa simu na shabiki wangu, lakini wapo wanaopiga simu kutaka mambo ya ajabu. 

Sawa ni wengi wao ni mashabiki wangu, lakini simu kwangu ni kero kubwa ingawa ni msaada mkubwa pia kwangu ni sehemu ya kitendea kazi.”
Posted: 14 Dec 2013 04:07 PM PST
http://www.theclicktz.com/
Mwanafunzi wa chuo kimoja alimwagiwa mafuta ya moto na rafiki yake kipenzi baada ya kumkuta na boyfriend wake wakifanya mapenzi.


Ilikuwa ni siku ya ijumaa Nasra alipokuwa akitoka darasani na kurejea hostel alipokea sms ikisema "Nenda kwa Rafiki yako kipenzi Naima kuna Bonge la Surprize, tafadhali usikose nenda sasa hivi" Nasra aliamua kuchukua pikipiki hadi kwa rafiki yake alipofika tu alikuta viatu vya boyfriend yake nje, akashtuka kwanza kwani sio kawaida ya jamaa huyo kwenda kwa Naima bila ya kuwa na Nasra, Nasra alijaribu sana kugonga lakini hakufunguliwa, na baadae aliamua kupiga simu zote mbili ya rafiki yake na ya boyfriend wake pia zote zikaita tu bila kupokelewa, Alikaa pale nje hadi majira ya saa sita usiku, ambapo alishajua kunakitu kinaendelea. Muda ulivyozidi kwenda  Nasra alitoka na kwenda kuchukua marafiki zake wengine wawili, aliporudi alikuta bado hawajatoka ndani.

Mpaka majira ya saa saba hivi usiku, Nasra akiwa amebeba mafuta ya moto kwenye chupa ya chai yeye na marafiki zake walivunja mlango na kuwakuta wawili hao ndani wakiwa katika hali ya uoga jamaa alifanikiwa kukimbia na kumuacha Naima chumbani ambapo Nasra alifungua chupa ya chai na kumwagia mafuta hayo ya moto rafiki yake huyo msaliti.
Nasra alikamatwa baadae na kufikishwa kituo cha polisi ambayo alihojiwa na kusema kwamba, alikuwa akipata tetesi na uvumi kwamba mchumba ake anatembea na rafiki yake kwa siku nyingi hivyo alikuwa anatafuta tu uthibitisho, na ameupata baada ya kuatilia kwa muda mrefu. 

 Exclusive: Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mjini, Jackson Msome aelezea mapokezi ya Mshindi wa EBSS 2013 na washiriki waliofika top 5 Musoma, yanatarajiwa kuweka historia (Audio)

Mshindi wa EBSS 2013 Emmanuel Msuya ameandaliwa mapokezi ya kiserikali leo, Musoma mjini ambapo ndipo makazi yake.

Mkuu wa wilaya ya Musoma Mjini, mheshimiwa Jackson Msome amesema wamemuandalia mapokezi mazuri kwa kuwa ushindi wake umeleta heshima kubwa katika mji huo.
“Kwanza ni mkazi wetu, ni mkazi wa mji wa Musoma. Sisi tukiwa kama wenzie na viongozi wake, kwanza tunayo fahari kwa ushindi wake. Lakini la pili tulimsapoti sana na tulimuomba sana Mungu amsaidie katika jitihada zake hizo. Ushindi wake huo unaleta heshima kwake, kwa wilaya yetu, kwa mkoa wetu, kwa kanda yetu na Tanzania kwa ujumla. Kwa hiyo tuna kila sababu ya kufurahi pamoja naye.” Mheshimiwa Msome aliiambia tovuti ya Times Fm.
Mheshimiwa Msome, ameelezea pia faida/changamoto waliyoipata vijana wa Musoma wenye vipaji kutokana na ushindi wa Emmanuel Msuya.
“Hii ni changamoto kwa vijana, kwamba vijana wapo na wana vipaji mbalimbali. Kinachotakiwa ni kutambua fursa zilizopo na hivyo kuzitumia kujitokeza kukuza vipaji vyao, na kwa kweli ni sehemu ya ajira kwa vijana wetu.”
Naye mratibu wa mapokezi hayo ambaye ni mdau wa muziki mjini musoma maarufu kwa jina la Kayombo, amesema kuwa mapokezi hayo yatakuwa ya kihistoria kwa mtu wa kawaida ambaye sio kiongozi wa nchi, na kwamba kutakuwa na misafara ya pikipiki na magari. Ameongeza kuwa kesho (December 15) washiriki waliombatana na Msuya watatumbuiza katika ukumbi wa Bwalo la Polisi.
Akiongea na Times Fm wakati akiwa uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam, Emmanuel Msuya amesema yuko na timu ya washiriki waliofika Top 5 ya shindano hilo pamoja na mama yake mzazi na wanaelekea Mwanza.
Amesema wanategemea kuingia Musoma majira ya saa kumi na moja jioni.
Emmanuel Msuya alitangazwa kuwa mshindi wa EBSS 2013, November 30 na kuwa mmiliki wa shilingi Million 50 zilizokuwa zinashindaniwa. 

No comments: