advert

http://

Monday 16 December 2013

MWALIMU AFA KIMIUJIZA.



Mwalimu Gloria Tarimo ‘Ticha Gloria’ (29) aliyekuwa akifundisha katika Shule ya Mbezi High School ya jijini Dar, amefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha
huku baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wakidai kifo chake ni cha kimiujiza.
Ticha Gloria ambaye alikuwa akikaimu nafasi ya mwalimu mkuu wa shule hiyo, alifariki dunia Desemba 6, mwaka huu katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar huku wengi wakihisi kuna mkono wa mtu nyuma ya kifo hicho.
                                                      Marehemu Glory A Tarimo enzi za uhai wake.
USHIRIKINA WAHUSISHWA
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa ndugu wa marehemu aliyeomba hifadhi ya jina lake kwa kuwa si msemaji wa familia alisema, kifo cha Ticha Gloria kinahusishwa na ushirikina kwa kuwa kabla ya mauti kumfika alikumbana na mambo mengi ya ajabu.
“Ni kifo cha ajabu kwa kweli na kimemshangaza kila mmoja wetu. Nakumbuka ilikuwa Juni, mwaka huu ambapo alienda kazini na alipofika kwenye mlango wa ofisi yake alikuta nazi imevunjwa.
“Licha ya kushangazwa na uwepo wa nazi hiyo, aliiruka kisha akaingia ofisini kwake. Kuanzia hapo alianza kuumwa mguu, kuna wakati akawa anahisi unawaka moto. Tulimpeleka Hospitali ya Muhimbili, akapatiwa matibabu na akapata nafuu,” alisema ndugu huyo.

AKUTA NJIWA KWENYE KITI OFISINI
Ndugu huyo alizidi kueleza kwa masikitiko kuwa, baada ya tukio hilo la kukuta nazi imevunjwa kwenye mlango wa ofisi yake, mambo hayakuishia hapo kwani hivi karibuni alipoingia ofisini kwake alikuta Njiwa kwenye kiti chake.
“Alipiga kelele sana, walimu na wanafunzi wake wakaja  kushuhudia huku kila mmoja akishangaa na kuogopa kumtoa njiwa yule kwenye kiti.
“Mwalimu mmoja aliyefahamikwa kwa jina la Fadhili ndiye aliyemuondoa njiwa yule. Bila kujua kuwa roho yake inasakwa, Gloria akakaa kwenye kile kiti na kuendelea na shughuli zake,” alisema ndugu huyo na kuongeza:
“Haikuchukua muda mrefu akahisi kama anachomwa na kitu chenye ncha kali kwenye makalio yake huku kichwa kikimuuma sana. Walimu wenzake walimchukua na kumrudisha hospitalini.”

AANZA KUZIONA SIKU ZAKE MFULULIZO
 Ilielezwa kuwa, baada ya mwalimu Gloria kufikishwa hospitalini, hali ilizidi kuwa mbaya na akaanza kutokwa na damu ya hedhi mabongemabonge huku damu nyingine ikitokea puani.
Ndugu wa Marehemu.
“Hali ilikuwa hivyo, akawa anateseka sana huku wakati mwingine akilalamikia baadhi ya walimu wenzake kuwa ndiyo wanaotaka kumtoa roho.
“Kuna siku alimuita daktari aliyekuwa akimhudumia na kumwambia anamshukuru kwa kujitahidi kuokoa uhai wake lakini anaamini hatapona kwani anajua kuna walimu wamedhamiria kumuua ili wakalie kiti cha ualimu mkuu, baada ya hapo alikata roho,” alisema ndugu huyo ambaye ndiye aliyekuwa akiwasiliana na marehemu mara kwa mara.

WALIMU WANASEMAJE?
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, baadhi ya walimu wa shule hiyo walisema wamesikitishwa sana na kifo cha Ticha Gloria, wakasema licha ya kwamba kila kifo kinapangwa na Mungu lakini hiki cha mwenzao kimeacha utata.
“Kwa kweli kifo cha Gloria kimenifanya niamini kuwa Mungu yupo lakini pia ushirikina upo. Amekufa kifo cha kimiujiza sana, mambo yaliyomtokea kabla ya kufariki dunia yanaashiria kabisa kuna mkono wa mtu,” alisema mwalimu mmoja wa kike aliyeomba hifadhi ya jina lake.
MSIKIE MWENYE SHULE
Mkurugenzi wa shule hiyo aliyefahamika kwa jina la Said Mgude alielezea masikitiko yake juu ya kifo cha mwalimu Gloria kwa kuwa alikuwa mchapakazi sana ila akataka watu wasihusishe kifo hicho na mambo ya kishirikina.
“Kila mmoja lazima aumie kwa kifo cha Gloria, lakini nawasihi watu wamuamini Mungu na waachane na dhana za kishirikina. Shule yangu ni taasisi kubwa sana, minazi ipo mingi hivyo kama alikuta nazi imevujwa mlangoni inawezekana ilianguka tu na kupasuka.
“Kuhusu Njiwa hapa Dar es Salaam siyo jambo la ajabu kwa sababu wapo wengi sana, mimi siwezi kukubaliana na mambo hayo ya kishirikina na hakuna kitu kama hicho,” alisema.
Mwili  wa mwalimu Gloria uliagwa Desemba 10, mwaka huu katika Kanisa Katoliki Mbezi Mwisho jijini Dar na baadaye ulisafirishwa kwenda  Moshi Rombo mkoani Kilimanjaro na kuzikwa siku iliyofuata ya Desemba 11.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amin.

Stori: Gladness Mallya, Nyemo Chilongani na Haruni Sanchawa.

Stori: Mayasa Mariwata na Chande Abdallah

JAMANI jamani! Dunia imefika pabaya zaidi, Mungu asaidie. Mwanamke mkazi wa Chalinze,
Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga, inauma sana kwa kweli!
  Mwanamke mkazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga.

Tukio hilo la kutisha lilijiri usiku wa Desemba 7, mwaka huu…
Stori: Mayasa Mariwata na Chande Abdallah
JAMANI jamani! Dunia imefika pabaya zaidi, Mungu asaidie. Mwanamke mkazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga, inauma sana kwa kweli!
  Mwanamke mkazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga.
Tukio hilo la kutisha lilijiri usiku wa Desemba 7, mwaka huu Chalinze Kwamwarabu ambapo mwanamke huyo alikwenda kujumuika na ndugu na majirani katika mkesha wa ngoma ya kuwatoa wari siku ya Jumapili.
                                                              Eneo la tukio Chalinze Kwamwarabu.
Mkasa huu unasimuliwa kwa majonzi mazito na mdogo wa marehemu ambaye alikuwa mshehereshaji wa shughuli hiyo ‘MC’, Siwema Rashid.
Alisema: “Mpaka sasa tunashindwa kuelewa kilichotokea maana siku ya tukio tulikuwa naye kwenye ngoma usiku. Alikuwa mchangamfu sana, aliifanya shughuli ipendeze.
“Ilipofika saa nane usiku baadhi ya watu walianza kulala, sasa sijui yeye ilikuwaje mpaka hali hiyo ikamfika maana hao watu walichomfanyia wametuachia historia kubwa sana.
“Walimbaka wakaona haitoshi wakamwingiza chupa ya soda sehemu ya siri ya mbele halafu wakamwingiza chupa ya bia sehemu ya siri ya nyuma.
“Ili kuzidi kutimiza unyama wao, waliondoka na kumwacha kama alivyozaliwa, inauma sana halafu matukio ya hivyo yamekithiri sana.”
Aliongeza: “Marehemu ametuachia jukumu la malezi kwa watoto wake wawili, Sikudhani Juma (18) na Ally Juma (12).”
Naye mtoto mkubwa wa marehemu, Sikudhani akisimulia kifo cha mama yake, alisema: “Nasikitika sikuweza kuuona mwili wa mama hata pale watu walipojazana na kumshangaa.

“Hata polisi na mganga mkuu wa mkoa walipofika kumchomoa zile chupa sikutaka kusogea kabisa, naamini Mungu atawaonesha jambo hao watu hapahapa duniani.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Yurichi Mtei akizungumzia ukatili huo alisema: “Taarifa za tukio hilo bado hazijafika kwangu kutokana na majukumu mengine ya kikazi, isipokuwa nalifanyia kazi kuhakikisha watuhumiwa wanakamatwa.”
Tukio hilo lilifunguliwa jalada kwenye Kituo cha Polisi Chalinze kwa nambaCH/RB/3767/2013 MAUAJI.
Mpaka kifo chake, mwanamke huyo alikuwa akiishi na mwanaume mmoja (jina halikupatikana mara moja lakini si aliyezaa naye watoto hao wawili). Alizikwa Jumapili iliyofuata, Chalinze.
Mungu ailaze pema peponi roho yake. Amina.

source:GPL

Sunday 15 December 2013

Mama Mlemavu Akionyesha UPENDO kwa Mwanae.


Upendo wa Mama.

Wakazi wa eneo la Likoni, Mombasa nchini Kenya walipatwa na mshangao mkubwa mara baada ya mbuzi mmoja kujifungua mtoto mwenye sura inayofanana na binadamu.

Tukio hilo lilifanya shughuli mbalimbali kwenye kijiji hicho kusimama huku wakazi wa eneo hilo wakiwa wanastaajabu juu ya tukio hilo la ajabu.
 
Tazama video ya tukio hilo hapo chini....
 

Lulu
Muigizaji wa filamu nchini Elizabeth Michael aka Lulu, amesema kuwa hatamani tena kutumia simu ya mkononi kwakuwa anasumbuliwa mno na watu wasiokuwa na mambo ya msingi huku akitamani irudi enzi ya kutumiana barua.


Akiongea na paparazi wetu jana,Lulu alisema kuwa kero hiyo humfanya atamani kurudi katika enzi za kale za kuwasilia kwa kutumiana barua kwa njia ya posta.

“Nadhani sihitaji simu ya mkononi kwa sasa, mwenye shida na mimi atanitumia barua. Sijui, hata sijielewi nikasimame wapi, maana hata nikibadili nambari ya simu inasambaa kwa kasi sana,”alisema.

Lulu alibainisha kuwa kwa siku hupigiwa simu zisizokuwa na idadi na zisizo na faida kwake, lakini akakiri kwamba idadi kubwa ya watu wanaompigia simu ni mashabiki wake.

“Ninapigiwa simu nyingi kwa siku ambazo ni kero kwangu, nafurahi sana ninapopigiwa simu na shabiki wangu, lakini wapo wanaopiga simu kutaka mambo ya ajabu. 

Sawa ni wengi wao ni mashabiki wangu, lakini simu kwangu ni kero kubwa ingawa ni msaada mkubwa pia kwangu ni sehemu ya kitendea kazi.”
Posted: 14 Dec 2013 04:07 PM PST
http://www.theclicktz.com/
Mwanafunzi wa chuo kimoja alimwagiwa mafuta ya moto na rafiki yake kipenzi baada ya kumkuta na boyfriend wake wakifanya mapenzi.


Ilikuwa ni siku ya ijumaa Nasra alipokuwa akitoka darasani na kurejea hostel alipokea sms ikisema "Nenda kwa Rafiki yako kipenzi Naima kuna Bonge la Surprize, tafadhali usikose nenda sasa hivi" Nasra aliamua kuchukua pikipiki hadi kwa rafiki yake alipofika tu alikuta viatu vya boyfriend yake nje, akashtuka kwanza kwani sio kawaida ya jamaa huyo kwenda kwa Naima bila ya kuwa na Nasra, Nasra alijaribu sana kugonga lakini hakufunguliwa, na baadae aliamua kupiga simu zote mbili ya rafiki yake na ya boyfriend wake pia zote zikaita tu bila kupokelewa, Alikaa pale nje hadi majira ya saa sita usiku, ambapo alishajua kunakitu kinaendelea. Muda ulivyozidi kwenda  Nasra alitoka na kwenda kuchukua marafiki zake wengine wawili, aliporudi alikuta bado hawajatoka ndani.

Mpaka majira ya saa saba hivi usiku, Nasra akiwa amebeba mafuta ya moto kwenye chupa ya chai yeye na marafiki zake walivunja mlango na kuwakuta wawili hao ndani wakiwa katika hali ya uoga jamaa alifanikiwa kukimbia na kumuacha Naima chumbani ambapo Nasra alifungua chupa ya chai na kumwagia mafuta hayo ya moto rafiki yake huyo msaliti.
Nasra alikamatwa baadae na kufikishwa kituo cha polisi ambayo alihojiwa na kusema kwamba, alikuwa akipata tetesi na uvumi kwamba mchumba ake anatembea na rafiki yake kwa siku nyingi hivyo alikuwa anatafuta tu uthibitisho, na ameupata baada ya kuatilia kwa muda mrefu. 

 Exclusive: Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mjini, Jackson Msome aelezea mapokezi ya Mshindi wa EBSS 2013 na washiriki waliofika top 5 Musoma, yanatarajiwa kuweka historia (Audio)

Mshindi wa EBSS 2013 Emmanuel Msuya ameandaliwa mapokezi ya kiserikali leo, Musoma mjini ambapo ndipo makazi yake.

Mkuu wa wilaya ya Musoma Mjini, mheshimiwa Jackson Msome amesema wamemuandalia mapokezi mazuri kwa kuwa ushindi wake umeleta heshima kubwa katika mji huo.
“Kwanza ni mkazi wetu, ni mkazi wa mji wa Musoma. Sisi tukiwa kama wenzie na viongozi wake, kwanza tunayo fahari kwa ushindi wake. Lakini la pili tulimsapoti sana na tulimuomba sana Mungu amsaidie katika jitihada zake hizo. Ushindi wake huo unaleta heshima kwake, kwa wilaya yetu, kwa mkoa wetu, kwa kanda yetu na Tanzania kwa ujumla. Kwa hiyo tuna kila sababu ya kufurahi pamoja naye.” Mheshimiwa Msome aliiambia tovuti ya Times Fm.
Mheshimiwa Msome, ameelezea pia faida/changamoto waliyoipata vijana wa Musoma wenye vipaji kutokana na ushindi wa Emmanuel Msuya.
“Hii ni changamoto kwa vijana, kwamba vijana wapo na wana vipaji mbalimbali. Kinachotakiwa ni kutambua fursa zilizopo na hivyo kuzitumia kujitokeza kukuza vipaji vyao, na kwa kweli ni sehemu ya ajira kwa vijana wetu.”
Naye mratibu wa mapokezi hayo ambaye ni mdau wa muziki mjini musoma maarufu kwa jina la Kayombo, amesema kuwa mapokezi hayo yatakuwa ya kihistoria kwa mtu wa kawaida ambaye sio kiongozi wa nchi, na kwamba kutakuwa na misafara ya pikipiki na magari. Ameongeza kuwa kesho (December 15) washiriki waliombatana na Msuya watatumbuiza katika ukumbi wa Bwalo la Polisi.
Akiongea na Times Fm wakati akiwa uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam, Emmanuel Msuya amesema yuko na timu ya washiriki waliofika Top 5 ya shindano hilo pamoja na mama yake mzazi na wanaelekea Mwanza.
Amesema wanategemea kuingia Musoma majira ya saa kumi na moja jioni.
Emmanuel Msuya alitangazwa kuwa mshindi wa EBSS 2013, November 30 na kuwa mmiliki wa shilingi Million 50 zilizokuwa zinashindaniwa. 

MWANAMKE MMOJA AMWAGIWA MAJI YA MOTO NA MWANAMKE MWENZIE KISA WIVU WA KIMAPENZI.


Bi. Neema Teti aliyemwagiwa maji ya moto mwili mzima, kwa kudaiwa kuwa na uhusiano na mume wa mtu. 


Muuguzi wa zamu Bi. Neema Bayo akimfunika majeruhi Bi. Neema Teti aliyemwagiwa maji ya moto mwili mzima, kwa kudaiwa kuwa na uhusiano na mume wa mtu.  

Bi. Neema Teti aliyemwagiwa maji ya moto mwili mzima, kwa kudaiwa kuwa na uhusiano na mume wa mtu.

Na Gadiola Emanuel -Arusha

Mwanamke mmoja mkazi wa Mbuguni Arusha,Bi. Neema Teti amejeruhiwa vibaya kwa kumwagiwa maji ya moto katika sehemu mbalimbali za mwili wake katika kisa kinachodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi. Tukio hilo limetokea baada ya mtekelezaji wa kitendo hicho Mama Tatu Msuya ambaye ni jirani yake akidaiwa kumtuhumu majeruhi huyo kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mume wake.
Katika wodi ya wagonjwa majeruhi hosipitali ya Mkoa wa Arusha Mount Meru alikolazwa,Neema ameelezea tukio hilo kuwa limetokea juma lililopita baada ya kuitikia mwito wa jirani yake Tatu Msuya uliomtaka afike nyumbani kwake kwaajili ya kumsaidia uangalizi wa familia yake kutokana na kuhitajika msibani na ndipo alipomjeruhi vibaya kwa kumwagia maji ya moto.Neema Teti-Majeruhi
Muuguzi wa zamu katika hospitali ya Mount Meru,Neema Bayo amesema majeruhi huyo aliletwa hospitalini hapo akiwa katika hali mbaya lakini hali yake imezidi kuimarika baada ya kupatiwa matibabu na jopo la madaktari hospitalini hapo. Nae Muuguzi wa wodi ya majeruhi mount Meru Hospitali Bi.Neema Bayo amesema matukio kama hayo yakizidi kushamiri katika maeneo mbalimbali
nchini,bado inaelezwa kuwako kwa ugumu wa kutoa taarifa katika vyombo vya sheria kutokana na wahusika kuwaficha wahalifu mara wanapotoka hospitalini
Afisa wa dawati la jinsia mkoa wa Arusha Maria Maswa akizungumza wakati alipotembelea waathirika wa matukio ya unyanyasaji wa kijinsia katika hospitali ya mount Meru,amesema yanapotokea matukio hayo,walengwa wamekuwa wagumu kutoa ushirikiano kwa madai ya kumaliza swala hilo kinyumbani hatua inayochochea ukuaji wa matatizo hayo.Maria Maswa-Afisa Dawati la Jinsia Mkoa wa Arusha Bi. Maria Maswa alisema "Kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi Mkoani Arusha limeeleza kuwa linaendelea na msako dhidi ya Mama Tatu Msuya anayedaiwa kutekeleza kitendo hicho; pia aliongeza kuwa jumla ya kesi 507 zimeripotiwa kati kipindi cha mwezi november 2012 mpaka sasa. 
Picha zote na Gadiola Emanuel wa Wazalendo 25 Blog.

Rihanna aandika historia nyingine kubwa kimuzikiRihanna amefanikiwa kuandika historia nyingine kimuziki kufuatia wimbo alioshirikishwa Eminem, Monster kuwa wimbo wake 13 kukamata nafasi ya kwanza kwenye chart za Billboard.
Akiwa na nyimbo 13 zilizokamata nafasi ya kwanza, amewazidi Madonna, Stevie Wonder na Whitney Houston na amefungana na hayati Michael Jackson.
Wanaoongoza kwa kuwa na nyimbo nyingi zilizoshika nafasi ya kwanza ni the Beatles walioingiza nyimbo 20 na kufuatiwa na Mariah Carey mwenye nyimbo 18.

Video: Mkalimani feki wa viziwi kwenye kumbukumbu ya Mandela ajitetea, asema aliona malaika wakiingia uwanjani akachanganyikiwaMkalimani anayeshutumiwa kwa kudanganya alama za viziwi wakati akitafsiri hotuba za viongozi mbalimbali wa dunia akiwemo Rais Barack Obama wa Marekani kwenye hafla ya kumbukumbu ya Nelson Mandela, Alhamis hii amesema alikuwa akiona malaika wakiingia kwenye uwanja huo wa mpira wa FNB na kwamba amekuwa akisumbuliwa na tatizo la akili.
Thamsanqa Jantjie amehojiwa na shirika la habari la The Associated Press aliloliambia kwamba mauzauza hayo yalianza alipokuwa akitafsiri na kwamba alijaribu kutopanic kwasababu polisi wenye silaha walikuwa karibu yake.
“Kilichotokea siku hiyo, niliona malaika wakiingia uwanjani. Nilianza kugundua kuwa tatizo lilikuwa hapa. Na tatizo, sijui shambulio la tatizo hili, litakujaje. Wakati mwingine huwa nakua katili sehemu hizo. Huwa naona vitu vinavyonifukuza,” alisema Jantjie.
“Nilikuwa kwenye wakati mgumu sana,” aliongeza. Na kumbuka watu hao, Rais na kila mtu, walikuwa na silaha, kulikuwa na polisi wenye silaha pembeni yangu. Ningeanza kupanick ningezusha tatizo. Nilitakiwa kukabiliana nalo ili nisiiabishe nchi yangu.”
Aliongeza kuwa aliwahi kulazwa hospitali ya wagonjwa wa akili kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Serikali ya Afrika Kusini imekiri kuwa kulifanyika makosa katika kumchukua Jantjie kwa kazi hiyo.
Naibu waziri wa Wanawake, Watoto na Walemavu, Hendrietta Bogopane-Zulu alisema maafisa wa serikali wamejaribu kufuatilia kampuni iliyompa kazi Thamsanqa Jantjie lakini wamiliki wa kampuni hiyo wameingia mitini.
Aliwaomba radhi watu wote wenye ulemavu wa kusikia na kusema kuwa uchunguzi unafanyika kubaini ni vipi Jantjie alikuwa amechukuliwa kufanya kazi hiyo.
Aliongeza kuwa kampuni hiyo ilitoa huduma chini ya kiwango na kwamba ujira waliomlipa mkalimani huyo kilikuwa kidogo mno. Mkalimani huyo alilipwa dola 85 tu.
AP waliomuonesha Jantjie video inayomuonesha akitafsiri kwenye hafla hiyo na kusema hakumbuki  chochote.
“I don't remember any of this at all.

Surprise: Beyonce aachia album mpya kwa kushtukizaWeekend hii, Beyonce ameachia album yake ya 5, iliyopewa jina lake mwenyewe na inapatikana itunes pekee yake.

Katika album hiyo, Beyonce amewashirikisha wakali akiwemo mumewe, Jay Z, Drake, Frank Ocean na mwanae Blue Ivy.
Hiyo ni album yake ya kwanza tangu mwaka 2011 alioachia albam yake ya nne, "4".
Beyonce ina jumla ya nyimbo 14. Cha kuvutia ni kuwa kila wimbo kwenye albam hiyo ina video yake ambayo nayo inapatikana iTunes.
Hizi ni nyimbo zilizopo kwenye "Beyonce":
1. Pretty Hurts
2. Haunted
3. Drunk In Love (feat. Jay Z)
4. Blow
5. No Angel
6. Partition
7. Jealous
8. Rocket
9. Mine (feat. Drake)
10. XO
11. Flawless (feat. Chimamanda Ngozi Adiche)
12. Superpower (feat. Frank Ocean)
13. Heaven
14. Blue (feat. Blue Ivy) 

Label ya Baby Madaha, Candy n Candy yakumbwa na mgogoro, polisi waingilia katiMigogoro kwenye label ya Kenya inayomsimamia Baby Madaha imeonesha kutengeneza makazi ya milele kila anaposainishwa msanii mpya. Ikumbukwe kuwa wasanii wa zamani wa label hiyo walianza kulalamika kuwa CEO wa label hiyo, Joe Kariuki alikuwa akimpendelea mno Baby Madaha na kuwaacha wao wakisaga miguu tu.
Na sasa baada ya kusainishwa msanii mpya wa Nigeria, Lil Gee na kuachia wimbo mpya na kisha kutaka afanyiwe video, vijana wa zamani wameanza kulalamika tena.
Mmoja wao ni Dazlah Kiduche, aka ‘Dazlah’ ambaye hiyo haijamuingia kichwani kwakuwa anashangaa iweje mgeni apate video wakati yeye aliyeanza kuachia wimbo wake “Bangereba” akiwa hana video bado. Wasanii hao walijikuta wakiingia kwenye ugomvi mkubwa uliofanya hadi polisi waitwe kwenye ofisi hizo kusuluhisha mambo.
Chanzo kilichoongoea na mtandao wa Niaje wa Kenya kimesema kuwa CEO Joe Kariuki bado hajaamua video ya nani ianze kutoka.

Rich Mavoko atolewa machozi na Mama Sharo anayedai kudhulumiwa haki za mwanaeMuimbaji wa Roho Yangu, Rich Mavoko amemtembelea mama mzazi wa marehemu Sharo Milionea huko wilayani Muheza Tanga.

Mavoko ameshare picha akiwa na mama mzazi wa msanii huyo aliyefariki November mwaka jana inayoonesha akiwa kwenye simanzi zito kutokana na alichokuwa akisimuliwa na mama huyo.
"Muda mwingine wasanii tunahitaji tukumbuke wenzetu walio tangulia tena kwa kuwa enzi ata kwa kuwatembelea ndugu zake coz kuna vitu vinauma sana ukielezewa hapa alikuwa ana nielezea sharo baada ya kufa haki zake nyingi hajui zipo zinaenda wapi na mambo mengi yanayo muhusu marehem sharo kiukweli ili niuma... pole sana mama angu binadamu ndivyo walivyo,” ameandika Mavoko.

Watu 41 akiwemo waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa wanusurika kifo baada ya ndege waliyopanda kupasuka matairi
Abiria 37 na wafanyakazi 4 wa ndege ya Precision Air wamenusurika kifo baada ya ndege waliyokuwa wamepanda kupasuka matairi wakati ikitua katika uwanja wa ndege wa Arusha leo majira ya mchana.

Waziri mkuu mstaafu ambaye ni mbunge wa Monduli, Edward Lowassa alikuwa miongoni mwa abiria wa ndege hiyo waliokuwa wakisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Arusha.  
Shirika la ndege la Precision Air limetoa tamko rasmi kwa umma, ambapo limeeleza kuwa watu wote waliokuwa kwenye ndege hiyo wako salama.

Ivo Mapunda kuichezea rasmi Klabu ya Simba

Baada ya uongozi wa Klabu ya Gor Mahia ya Kenya kuweka wazi mpango wa kumuongeza mkataba mlinda mlango wao shujaa wa kupangua michomo ya penalti, Ivo Mapunda, uongozi wa klabu ya Simba nao umesema umeshafanya mipango ya kumsainisha mkataba nyota huyo.

Uongozi wa mabingwa wa Ligi Ku ya Kenya -- Gor Mahia ulikaririwa juzi ukieleza kuwa utambakisha kipa Mapunda kwa gharama yoyote.

Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, ambaye alikuwa nchini Kenya juzi, ameiambia NIPASHE kuwa Mapunda alitarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili kuwatumikia 'Wanamsimbazi', na kwamba tayari ameshatanguliziwa shilingi million 15.

"Tayari tulishamkabidhi mke wake shilingi milioni 15 jijini Dar es Salaam jana (Jumatano) kabla ya kuja huku (Nairobi)," alisema Mtawala.

Katibu Mkuu huyo alisema wamelazimika kuja jijini hapa kumsajili baada ya kusikia kuwa klabu yake ya Gor Mahia ina mpango wa kumwongeza mkataba mpya.

Kipa huyo amejipatia umaarufu nchini hapa kwa ushujaa wake wa kupangua mikwaju ya penalti. Katika mchezo wa jana wa Kombe la Chalenji kutafuta mshindi wa tatu kati ya Zambia (Chipolopolo) na Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), Mapunda alidaka penalti mbili kati ya nane ambazo mabingwa hao wa zamani wa Afrika -- Chipolopolo walipiga.

Kutua kwa Mapunda Simba kutaisaidia timu hiyo iliyopo katika mgogoro mkali wa uongozi kwani kuanzia msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, hakuna timu itakayoruhusiwa kuwa na kipa wa kigeni ili kukidhi matakwa ya Azimio la Bagamoyo.
Source:Nipashe

Tuesday 10 December 2013

Hakuna mahali pa kukanyaga’ msibani kwa Mandela

.

Makazi ya Rais wa Kwanza mzalendo wa Afrika Kusini yaliyopo katika Mtaa wa Laa namba 12,
Houghton ambako ndiko alikokuwa hadi alipokutwa na mauti, ni kama hapaingiliki kutokana na wingi wa watu, magari na vyombo vya habari kutoka sehemu mbalimbali duniani ambavyo vimeweka kambi katika eneo hilo, usiku na mchana kufuatilia safari ya mwisho ya kiongozi huyo. 
Anga la mtaa huo na sehemu za jirani, limehanikizwa na sauti nyingi za nyimbo zikiongozwa na Wimbo wa Taifa wa Afrika Kusini ‘Nkosi Sikeleli Afrika’ (Mungu Ibariki Afrika), ukifuatiwa kwa zamu na nyimbo za kidini na zile za asili ambazo zinasifu ushujaa wa Mandela.
Katika lango la kuingia kwenye makazi hayo ya Mandela, kuna maombolezo ya aina yake kwani yameambatana na kitu ambacho kwa macho kinaonekana kama shamrashamra kwa nyimbo za sifa na kufurahia kile Waafrika Kusini wanachokiita kazi nzuri ya kutukuka ya Mandela aliyoifanya katika umri wa miaka 95 ya uhai wake.
Mwandishi wetui alitembelea makazi hayo ya Mandela jana na kushuhudia umati mkubwa wa watu wakifika nje ya nyumba yake kwa ajili ya kuomboleza; wakiweka mashada ya maua, mishumaa na kadi zenye ujumbe wa pole kwa familia yake. 
Miongoni mwa waliokuwapo katika eneo hilo ni Mtanzania, Christer Mwageni na watoto wake; Sabina na Faraja.
Mwageni alisema: “Kwa jinsi hali ilivyo, huwezi kukwepa kuwa mwombolezaji, mimi na wanangu tulikuja hapa kutembea tu kwa siku tatu hivi lakini tumejikuta tukishiriki msiba na hata kama tungekuwa hatutaki kushiriki, uhalisia unatulazimisha”.
“Kweli tuna mengi ya kujifunza, inaonekana msiba huu wa Mzee Mandela umewaunganisha zaidi Waafrika Kusini, maana wote bila kujali rangi wala kingine chochote, wanaonekana kuomboleza kwa dhati kutoka mioyoni kabisa.”
Katika eneo hilo la Houghton, ulinzi umeimarishwa na polisi wako kila kona na wamekuwa wakiwaelekeza waombolezaji na watu wengine njia sahihi za kufuata hadi kuyafikia makazi ya Mzee Mandela kutoka na barabara nyingi za kuingia katika eneo kufungwa na nyingine kugeuzwa maegesho ya magari ya waombolezaji.
Kwa ujumla, pilikapilika ni nyingi, lakini katika lango kuu la kuingia makazi ya Mandela, ulinzi ni mkubwa na hakuna anayeruhusiwa kulikaribia isipokuwa wanafamilia, vingozi wa Serikali na watu wengine wenye shughuli maalumu.

Soweto, Mandela Square
Hali kama hiyo ipo katika makazi yake ya zamani Mtaa wa Vilakazi Na: 8115, Orlando Magharibi, Soweto ambako kuna pilikapilika nyingi zinazoyahusisha makundi ya watu kutoka ndani na nje ya Afrika Kusini.
Mandela aliishi katika Mtaa wa Vilakazi kabla ya kukamatwa na kuwekwa kizuizini na alirejea katika nyumba hiyo miaka 27 baadaye alipoachiwa huru na kuishi humo kwa siku kumi na moja kabla ya kuhamia katika nyumba ya aliyekuwa mkewe, Winnie Mandela katika eneo hilohilo la Soweto.
Kama ilivyo Houngton, katika eneo hilo pia ulinzi umeimarishwa na baadhi ya njia zimefungwa kutokana na wingi wa watu na magari. Vyombo vya habari kutoka kila pembe ya dunia navyo vipo vikiendelea kufuatilia maombolezo hayo.
Katika nyumba ya Soweto ambayo sasa ni makumbusho ya Mzee Mandela, idadi kubwa ya watu wanafurika kujifunza historia ya kiongozi huyo na nje vipo vikundi vinavyoimba nyimbo za maombolezo na kumsifu Mandela kwa ushujaa wake.
Eneo la tatu ni Mandela Square lililopo katika Jiji la Sandton, Johannesburg ambako kuna sanamu kubwa ya kiongozi huyo yenye urefu wa mita sita kwenda juu, likimwonyesha katika hali ya kucheza muziki. Iliwekwa katika eneo hilo, Machi 31, 2004.
Katika eneo hilo, pia ulinzi umeimarishwa na askari wanalazimika kusimamia jinsi watu wanaovyoingia na kutoka. Watu wamekuwa wakisimama katika msitari mrefu kupata fursa ya kupiga picha katika sanamu hiyo yenye uzito wa tani mbili na nusu (kilo 2,500).
Pembezoni mwa sanamu hiyo, kama ilivyo Houghton na Malakazi, limetengwa eneo maalumu kwa ajili ya watu wanaoomboleza kuweka maua, nembo, nyaraka na mishumaa.
Maombolezo ya kifo cha Mandela yanaingia katika siku ya nne leo na yataendelea hadi Jumapili ijayo ya Desemba 15 wakati kiongozi huyo atakapozikwa kijijini kwake Qunu, Mthatha Mkoa wa Eastern Cape.


MADAM, Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ amesema anakumbuka vitu vitatu muhimu alivyokuwa akifanyiwa na marehemu baba yake, Abraham Sepetu.
 

Akizungumza na paparazi wetu, Wema alitaja matukio hayo ambayo ni kuona simu ya baba yake ikimpigia katika simu yake, jinsi alivyokuwa akimbembeleza na kubwa zaidi ni uwepo wake pia 
kwa jumla.
 
Wema (katikati) akiwa na mama yake pamoja na marehemu baba yake enzi za uhai wake.

“Maisha yangu yote nitakumbuka vitu vitatu ninavyovikosa baada ya kifo cha baba yangu, kwanza uwepo wake, kuona simu yake pindi anipigiapo, na alivyokuwa akinibembeleza. Nitamkumbuka sana baba yangu,” alisema Wema.

Huddah Monroe
Uhasama mkali unaozidi kuchemka kati ya rapa mbishi CMB Prezzo na 'msocialite’ Huddah Monroe wameamua kuanikana wazi na kuzitoa siri zao za ndani kwenye mtandao.


Tatizo nzima lilianza pale Huddah alipomkashifu Prezzo kwenye akaunti yake ya Instagram akimtaja kuwa mtu aliyeishiwa na anayependa kudekezwa sana.
Kama kawaida yake 'king wa maBling’ alijibu mpigo kwa kumwita Huddah kiruka njia asiyejielewa na ambaye yupo tayari kutumiwa na kila mtu.
Kipusa huyo naye hakuchoka kumjibu akisema kwamba kheri kuwa kiruka njia kuliko kuwa mtu wa kutegemea mamake hata katika umri mkubwa kama wake Prezzo
Majibizano yalizidi kuwa makali huku wawili hao wakitupiana cheche zaidi yenye soni kwenye akaunti zao mbalimbali za mtandaoni ikiwemo Twitter.

Letu ni jicho tu maana hatujui picha hii mbaya kati ya wawili hawa itaishia wapi, au labda ndio suala nzima la kusaka umaarufu.

nicki-minaj-birthdayFirst lady wa label ya YMCMB Nicki Minaj amesherekea birthday yake akitimiza miaka 31 na mafanikio ya kujivunia kwenye kazi yake ya muziki.

Party hiyo ikifanyika huko L.A na restaurant nzima ilibadilika rangi yake na kuwa ya pink maalum kwa ajili ya party ya Minaj ambayo ilihudhuliwa na Lil Twist,Safaree boyfriend wa Nicki Minaj na watu wengine.
Nicki aliletewa keki mbalimbali pamoja na stripper pole maalum kwa ajili ya party hiyo.
nicki-minaj-birthday2
nicki-minaj-birthday-3
nicki-minaj-birthday-4
nicki-minaj-birthday-5
nicki-minaj-birthday-6
nicki-minaj-birthday-7
nicki-minaj-birthday-8
nicki-minaj-birthday-9




Msanii maarufu wa Marekani Kelly Rowland, ametinga uwanja wa fisi Manzese Dar es salaam jana jioni baada ya kusikia sifa za maeneo hayo ya Uswahilini tangu akiwa USA. Msanii huyo ametua nchini kwa tiketi ya MTV kupitia taasisi yake inayojishughulisha na kampeni za kupambana na Ukwimwi (Staying AliveFoundation) ya nchini Marekani, Kelly akiwa balozi wake. Akiwa Uwanja wa Fisi, ambako kunasifika kwa ufuska wa kupindukia na rate kubwa ya maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa wasichana wadogo, Kelly alitembelea NGO ya EYG (Elizabeth Youth Group) inayojishughulisha na kutoa misaada ya elimu ya HIV/AIDS, uchangudoa, ulevi pamoja na uvutaji bangi kwa vijana nchini. 

jkuhuruRais Jakaya Mrisho Kikwete leo ameongoza maadhimisho ya miaka 52 ya uhuru wa Tanganyika uliopatikana Desemba 9, 1961.

Miaka 52 imetimia tangu Tanganyika (sasa Tanzania), kupata uhuru wake kutoka kwa wakoloni wa Kiingereza, Desemba 9, mwaka 1961.
Maadhimisho haya yamefanyika uwanja wa uhuru hapa Dar es salaam,Rais Jakaya Kikwete amekagua gwaride la vikosi mbalimbali vya ulinzi na usalama ambavyo pia vimetoa heshima kwa kiongozi huyo kwa mwendo wa pole na haraka.kikosi cha anga pia kimetoa heshima zake na burudani mbalimbali ikiwamo ngoma na michezo ya halaiki. Sherehe hizi zimehudhuriwa na wageni mbalimbali waalikwa wa ndani na nje ya nchi, wakiwamo mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini.
Katika maadhimisho haya kwa mwaka jana, yaliyohudhuriwa na viongozi 14 wa kutoka Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC), Rais Kikwete aliwataka Watanzania kujivunia na kuyaenzi mafanikio ya kisiasa, kiuchumi na kijamii yaliyopatika tangu nchi ilipopata uhuru. 

Tundaman asema alimlazimisha Madee kuacha kurap ili apate shows nyingi kama yeye

Tundaman wa Tip Top connection amesema kuwa alichangia kwa kiasi kikubwa kumbadili mwana familia mwenzake wa Tip Top Connection Madee kuacha kurap na kuimba ili aongeze kipato zaidi.

Tundaman amefunguka katika kipindi cha Bongo Dot Home cha 100.5 Times Fm, alipokuwa akifanya mahojiano na Jabir Saleh aka Kuvichaka na Dj K_U.
Tunda amedai kuwa hakupenda kumuona Madee akiendelea kukaa wakati yeye anapiga shows nyingi mikoani, hivyo akamlazimisha kubadilika ili naye apate mashavu zaidi.
“Madee mimi nimemlazimisha asilimia mia, hebu acha kule njoo huku. Ndio maana umesikia Pombe yangu, umesikia Tema Mate Tuwachape. Nimembadilisha mimi kutokana na kuona mwanangu mimi naenda mkoani kila siku nabeba begi yeye mwanangu yuko nyumbani tu. Nikaona kwa nini abaki nyumbani wakati mimi Tip Top chama moja?” Amesema Tundaman.
Ameelezea kuwa baada ya kukubali ushauri wake na kubadilika siku hizi ana mfululizo wa shows.
“Sasa hivi kila wikendi ukimpigia simu Madee ujue haumkuti, yuko mkoa. Zamani ilikuwa kila siku yuko maskani pale.” Amefunguka Tundaman.
Kipindi cha Bongo Dot Home kinakuwa hewani kupitia 100.5 Times Fm kila Jumamosi, kuanzia saa kumi kamili jioni hadi saa moja kamili.
Unaweza kusikiliza Online kupitia tovuti hii, bofya sehemu iliyoandikwa ‘Listen’.
Credit:Times fm.

 Rais Kikwete awashauri wanaopanga kulipa kisasi wakipata madaraka, kuiga mfano wa Mandela

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amewashauri watu wanaopanga kulipa kisasi pindi watakapopata madaraka kuachana na mawazo hayo.

Rais Kikwete ametoa ushauri huo wakati akitoa hotuba yake kwenye sherehe za maadhimisho ya siku ya uhuru wa Tanzania Bara, ambapo ameelezea mengi mazuri aliyoyafanya rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela na kuwataka viongozi wa Tanzania kuiga mfano wa maisha yake ikiwa ni pamoja na kusamehe na kusahau bila kulipa kisasi.
“Najua kuna wengine hapa wamepanga kulipa kisasi, wanasema nikipata watanikoma.” Amesema rais Kikwete na kuwataka waache yaliyopita yapite na kuendelea kuganga yajayo, “acheni kulipa kisasi.” Rais Kikwete amesisitiza.
Hotuba ya Rais Kikwete ilijikita zaidi katika maisha ya mzee Nelson Madiba Mandela, katika kuungana na Afrika Kusini kuomboleza kifo cha kiongozi huyo shupavu na kutoa mfano wa jinsi viongozi wa Afrika wanapaswa kuiga mfano wa uongozi.

Mimi ni Msichana wa Miaka 26 ..uwezi amini mpaka sasa sijawahi guswa na Mwanaume hata mmoja kwa maana hiyo nipo Bikira Kabisa...


Mimi ni Mwalimu wa Shule ya Msingi moja hapa Dar ..Wenzangu nikiwaambia hawaamini kabisa kuwa mpaka umri huu nipo Kigoli wengine wanasema eti nina matatizo..

NAPENDA KUSEMA HAYA

"With the influence of sex almost everywhere in the world of today I will still remain a virgin until my wedding night. It is the only respect I can reward my body. And this way I cannot worry about sexual transmitted diseases and unwanted pregnancies.

I believe that I am not abnormal as others may think. I am physically and mentally fit. I am just keeping myself clean."
Jesca. 


Amini Usiamini Wachina sasa Wameamua kuwekeza mpaka kwenye Ukahaba , Kama unataka kushuhudia hilo basi tembelea hotel za hapa dar zilizopo katika fukwe za bahari ya hindi ukajionee wadada wa kichana wana vyouza mapenzi kama karanga...Bei zao ni kuanzia 20,000 mpaka 60,000 .....Dahhhh 

Mkutano wa Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willbroad Slaa uliofanyika Uwanja wa Kiganamo, Kasulu Mjini leo umevunjika baada ya polisi kupiga mabomu ya machozi wakikabiliana na vijana waliorusha mawe kupinga mkutano usiendelee. Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo, vijana hao wanadaiwa kuwa kati ya 10-15 ambao walirusha mawe baada ya wananchi kuwafukuza wakitaka kuwapiga wakipinga kitendo chao cha kupiga kelele ili mkutano usiendelee ndipo polisi walianza kulipua mabomu ya machozi na mkutano kuvunjika.

Credit:http://www.udakuspecially.com/2013/12/chae.html


Stori:  Issa Mnally na Richard Bukos
MREMBO wa haja ambaye jina halikupatikana amenusurika kubakwa na wanaume baada ya kuvaa kivazi kilichoacha wazi sehemu kubwa ya maungo yake nyeti.



Tukio hilo lilijiri sehemu yenye mkusanyiko mkubwa, Kariakoo jijini Dar ambapo mrembo huyo alikuwa kwenye ‘shopping’ kwa ajili ya sikukuu ijayo ya Krismasi.

Likiwa linarandaranda maeneo hayo, Ijumaa Wikienda lilinasa laivu tukio hilo ambapo mrembo huyo alivuliwa nguo hadharani na kuacha ‘vitu’ njenje vikishuhudiwa hata na watoto waliokuwa wakimzomea.

Wanaume hao waliokuwa wakiongezeka na kuanza kumshika sehemu nyeti, walisababisha dada huyo kuanza kutoka nduki ambapo alizama kwenye duka moja kisha akasitiriwa kwa khanga na mama mmoja msamaria mwema.

Alipotoka bado wanaume waliendelea kumzingira ambapo ilimlazimu kutoa shilingi elfu hamsini kisha kurukia kwenye ‘kenta’ iliyomuondoa eneo hilo na haikujulikana alikoelekea kwa sababu gari hilo lilichomoka mbio huku akiwa amekoma ubishi wa kutembea nusu utupu.

Mapenzi ni kitu kingine kabisa chali yangu usisikia mtu kajiua na Bastola ukadhani ni uchizi tu ..hiyo tunaita ni dhuluma ya penzi...Inauma sana jamani..

Unakuta upo mapenzini na Binti unampenda kupindukia na yeye unaona anakupenda unamfanyia kila kitu unamtoa katika hali fulani na kumpeleka katika daraja fulani kwa mfano unamsomesha mpaka anapata degree ukitegemea labda akimaliza mtaoana na kusaidiana maisha lakini pindi anapomaliza tu na kupata kazi nzuri anaanza kukuonyesha madharau na kuanza kutoka na watu wengine ,,wewe unakuwa Fala tu tena Boyaaa la kutupwa ....Ebu niambie hapo utachukua hatua gani? 




Huyo Ndio Shemeji yetu kwa Mbwana Samatta ..She is Cute No Doubt 



ANAVYOKUTAZAMA
Mwanasaikolojia Zick Rubin kutoka Chuo cha Havard nchini Marekani aliwahi kusema kwamba watu wanaopendana hutumia asilimia 75 kutazamana kuliko wasiopendana, ambao kiwango chao ni asilimia 30-50. 



Hii ina maana kwamba mwanaume anapotumia muda wake mwingi kumtazama msichana na kugeuka taratibu kuangalia vitu vingine kama mtu asiyependa kuacha kumwangalia, ujue anampenda.

MIPANGO 
Mwanaume anayekupenda atakushirikisha kwenye mipango yake hasa ya muda mrefu. Mfano akitaka kununua kiwanja, kujenga nyumba atakuambia na pengine kutaka mchango wako wa hali na mali katika kulifanikisha hilo. Ukiona mwanaume anakuficha mambo yake, tambua kuwa huyo ana walakini kwenye penzi la dhati na la muda mrefu.

ATAONESHA HUZUNI
Katika maisha ya mapenzi kuna wakati wa kuhuzunika. Mwanaume mwenye upendo wa dhati atashirikiana nawe wakati wa huzuni na kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa unapata furaha. 





ATAKUAMINI
Dalili nyingine ya kupendwa na mwanaume ni kuaminiwa kwenye maisha kwa ujumla. Yaani mwanaume anayekupenda hatakuficha kitu, mfano pesa zake, atakupa uhuru kwenye simu yake na kukuamini katika usimamizi wa miradi yake.

ATAKUPA NAFASI
Ninapozungumzia nafasi nina maana atakukaribisha kwake bila hofu na kukupa nafasi ya kuingia na kutoka bila mipaka, atakupa nafasi ya kuweka vitu vyako kwenye kabati na kuruhusu nguo, picha na vitu vyako kuonekana wakati wote chumbani kwake.

UTAKUWA MWANAFAMILIA
Mwanaume aliyefikia chaguo la mwisho kwa mwanamke humshirikisha mpenzi wake kwenye masuala yake ya kifamilia, mfano atamwalika kwenye vikao vya harusi, kipaimara, atatoa nafasi ya kuambatana naye kuona wagonjwa, kusalimia ndugu na atakuwa huru kukutambulisha kwao.

ATAZUNGUMZA NAWE KUHUSU WATOTO
Kwa kuwa wanaume wengi hufikiria kuwa na familia, mwanaume anayekupenda atazungumza nawe mipango ya kupata watoto kwa kuwa atakuwa amekuchagua wewe kuwa mama wa wanaye na atapenda mazungumzo hayo.

ATAKUSAIDIA
Kwa kuwa kukwama ni sehemu ya maisha yetu, mwanaume anayekupenda atakuwa tayari kukusaidia unapokwama. Kila mara atahakikisha kuwa unakuwa na mafanikio na yeye atakuwa tayari kukupunguzia usumbufu wa maisha, kwa kukufuata kazini, kukusaidia baadhi ya mambo na hata ya nyumbani.

ATAJITOLEA
Ninaposema kujitolea ninamaanisha atakuwa tayari kufanya mambo yako na kuyaweka yake nyuma. Kwa mfano akiwa anapenda mpira na siku hiyo kuna mechi, lakini muda huo ukamwambia akufuate kwa mjomba wako atakuwa tayari kuacha furaha yake na kukujali wewe. Huyu ni mwanaume anayekupenda kwa dhati.

ATAAMBATANA NAWE
Wapenzi wengi wasiokuwa na mapenzi ya dhati huona aibu kuambatana na wapenzi wao kwenye mikusanyiko ya watu, lakini mwanaume anayekupenda atafurahia kutoka moyoni kuongozana nawe kwenye halaiki ya watu na kufurahia uwepo wako bila kuona aibu.


Kijana mmoja anayeaminika kuwa shabiki wa Manchester United Football Club amejiua jana usiku jijini Nairobi baada ya timu yake kufungwa 1-0 to Newcastle.


Polisi imesema kwamba John Jimmy Macharia, 23, alijirusha kutoka ghorofa ya 7 baada ya kujua timu yake imepoteza mchezo wa jana jioni. Kwa mujibu wa mkuu wa polisi jiji la Nairobi Benson Kibue, Macharia aliwaambia rafiki zake hawezi kuendelea kuangalia timu yake ikifungwa kila siku kabla ya kuruka ghorofani. “Mashahidi wote waliokuwepo wakati wa tukio bado wapo mikononi mwa polisi wanahojiwa,” alisema. Kibue aliwashauri vijana wa jiji la Nairobi kufahamu English Premier League ni mchezo tu kama ilivyo michezo mingine na hivyo waache kuchukua hatua za namna hii kisa michezo. Hii si mara ya kwanza kwa kwa kijana kupoteza maisha kwa ajili ya michezo inayochezwa  England,” alisema Ki