advert

http://

Sunday 29 September 2013

Serikali imeyafungia kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia 27 Septemba, 2013 kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano uliopo nchini.



Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne(14) kuanzia 27 Septemba,2013. Adhabu hii imetangazwa kwa Tangazo la Serikali (Government Notice ) Namba 333 la tarehe 27 septemba,2013.

Gazeti la MWANANCHI limepewa adhabu hiyo kutokana na hivi karibuni kuchapisha habari zenye mwelekeo wa uchochezi na uvunjifu wa amani, mfano tarehe 17 Julai, 2013 katika toleo Namba 4774 ilichapisha habari isemayo “MISHAHARA MIPYA SERIKALINI 2013” kwa kuchapisha waraka uliozuiliwa kwa matumizi ya vyombo vya habari waraka huo ulikuwa wa Siri haukupaswa kuchapishwa Magazetini. 


Aidha, katika toleo la Jumamosi, tarehe 17 Agosti,2013 lilichapisha habari yenye kichwa kisemacho “WAISLAM WASALI CHINI YA ULINZI MKALI” habari hiyo ilikolezwa na picha ya Mbwa mkali mwenye hasira. Habari na picha hiyo ilitoa tafsiri ya kuwa Jeshi la Polisi lilipeleka Mbwa katika maeneo ya ibada ya waumini wa dini ya kiislam. Jambo ambalo halikuwa la ukweli. Jeshi la Polisi katika doria siku hiyo halikupeleka mbwa katika maeneo ya Misikiti.

Serikali na jeshi la Polisi linaheshimu na kuzingatia maadili ya dini ya Kiislamu na kwa hiyo Jeshi lake hakiwezi kupitisaha au kuingiza Mbwa katika maeneo ya ibada. Hivyo basi, kwa gazeti hili kuchapisha habari iliyokolezwa na picha ya mbwa ni uchochezi wa kulichonganisha Jeshi la Polisi na waumini wa dini ya kiislam mbwa ni najisi hapaswi kuingia katika maeneo ya ibada.

Gazeti la MTANZANIA limefungiwa kutochapishwa kwa siku tisini(90) kuanzia tarehe 27 Septemba,2013 kwa kuchapisha habari zenye uchochezi. Gazeti hili limeonywa mara nyingi lirekebishe mtindo wake wa uandishi wa kichochezi na lizingatie maadili na Sheria na Kanuni za fani ya Habari.

Pamoja na kuonywa gazeti hili halikuonyesha kuzingatia maelekezo ya Msajili wa Magazeti, mfano; Katika toleo na 7262 la 20 Machi, 2013 liliandika habari yenye kichwa kisemacho “URAIS WA DAMU”, tarehe 12 Juni, 2013, toleo Namba 7344 lilichapisha makala isemayo “MAPINDUZI HAYAEPUKIKI”. Aidha, siku ya Jumatano,tarehe 18 Septemba,2013 katika toleo Namba 73414 ukurasa wa mbele lilichapisha Kichwa cha habari kisemacho “SERIKALI YANUKA DAMU” taarifa hiyo ilikolezwa na picha zilizo unganishwa kwa ustadi mkubwa kwa kutumia kompyuta kutapakaza rangi nyekundu mithili ya damu nyingi kumwagika. Katika habari hiyo gazeti hilo limedai bila uthibitisho kuwa Jeshi la Polisi linahusika na wahanga walioumizwa na watu wasiojulikana kwa kumwagiwa tindikali na waliyovamiwa na kujeruhiwa vibaya.

Vile vile gazeti hilo limeishutumu serikali kuwa goigoi katika kushughulikia matukio yenye sura ya kigaidi. Kwa ujumla wake habari hiyo ni ya kichochezi ina lengo la kuwafanya wananchi wavichukie vyombo vya ulinzi na usalama wavione kuwa haviwasaidii.

Kutokana na makosa yalitajwa hapo juu serikali imelifungia gazeti la Mtanzania kutochapishwa kwa muda wa siku tisini (90) kwa Tangazo la Serikali Namba 332 (Government Notice No.332) la tarehe 27 Septemba, 2013,. Serikali inawataka wamiliki, wahariri na wanahabari kwa ujumla kuwa makini, kuzingatia weledi,miiko na madili yataaluma uandishi wa habari.

Serikali inawataka wamiliki na hasa wahariri kuhakisha kuwa habari wanazoziandika na vipindi wanavyoviandaa vinazingatia taaluma, kuweka mbele maslahi ya taifa letu kwa kuwa na uzalendo wa hali ya juu. Serikali inavionya vyombo vya habari vinavyoutumia uhuru wa habari bila wajibu kuwa haitasita kuvichukulia hatua kali ikiwemo ya kuvifungia. Serikali haitakubali kuona vyombo vya habari kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani nchini.

Imetolewa na;

MKURUGENZI IDARA YA HABARI WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO 28 SEPTEMBA, 2013

YOUNG KILLER AONYESHA UMWAMBA KWA YOUNG DEE.TAZAMA MATOKEO.AIBU!!





Huwezi amini ila ndo ukweli.Young Killer 
Moto wa kuotea mbali.Ameonyesha umwamba
 kwa Young D.Tazama matokeo hapa Chini.AIBU.


NANI MKALI KATI YA HAWA WASANII 
KUPITIA BABAMZAZI.COM HAYA 
NDO MATOKEO HALISI.

YOUNG D
  24 (36%)
 
YOUNG KILLER
  41 (63%)
 

Votes so far: 65
Poll closed 
Hongera sana kwa Young Killer.


Photo: Dj manywele


Yule kahaba alofungwa kifungo cha miezi sita gerezani kwa kosa la kufanya ukahaba, mkazi wa jijini Dar, Blandina Barton amekamatwa tena kwa kosa  hilohilo ikiwa ni mwezi mmoja kabla ya kumaliza kifungo chake, Risasi Jumamosi linakupa mkasa mzima.

Habari za uhakika zilizopatikana katika Mahakama ya Jiji, Dar es Salaam zinasema kwamba mfungwa huyo alitumikia kifungo chake katika Gereza la Segerea jijini Dar na alipobakiza miezi michache kumaliza alionewa huruma na bibi jela na kutakiwa kumalizia kifungo hicho uraiani.
Inadaiwa kuwa kabla ya kuachiwa, bibi jela alimsihi Blandina kuhakikisha harudii kosa lililompeleka gerezani pindi atakapokuwa akimalizia kifungo chake nje ya gereza.
Blandina akamhakikishia bibi huyo kwamba atakuwa mtu safi kwani amejifunza vya kutosha.
Katika hali ya kushangaza, Jumatano iliyopita Blandina alipandishwa tena katika Mahakama ya Jiji iliyopo Barabara ya Sokoine jijini Dar akiwa amerudia kosa lililompeleka Segerea miezi michache iliyopita.
Imeelezwa mahakamani hapo kwamba, Septemba 24, mwaka huu Blandina na wenzake wanne walinaswa Buguruni usiku wakiwa katika mawindo ya ukahaba.
Bahati mbaya kwa Blandina alipofikishwa mahakamani hapo alikutana na hakimu yuleyule aliyemhukumu kifungo cha miezi sita kwa kosa la ukahaba.
Hakimu huyo, Timothy Lyon alipigwa na butwaa baada ya kumuona Blandina akiwa amesimama mbele yake.
Mtuhumiwa huyo aliyekuwa na wenzake, Husna Amos, Monica Denis, Esther Chizai na Angela Emmanuel wote kwa pamoja walisomewa mashtaka yao na kukana.
Hakimu Lyon aliwaambia watuhumiwa hao kwamba dhamana iko wazi na kuwataka kila mmoja kuwa na wadhamini wawili na shilingi laki mbili.
Sharti hilo lilionekana kuwa gumu kwa watuhumiwa wote, hivyo walipandishwa karandinga na kupelekwa Gereza la Segerea mpaka Oktoba 15, mwaka huu kesi yao itakapotajwa tena mahakamani hapo.
Mei mwaka huu gazeti dada na hili la Ijumaa liliandika habari za kifungo cha Blandina mara baada ya kuhukumiwa kwenda jela huku ikidaiwa kwamba msichana huyo ni mchumba wa mtu.


Source:GPL

Serikali imependekeza marekebisho ya sheria ya kudhibiti dawa za kulevya itakayotoa hukumu ya kifungo cha maisha na kufuta kipengele kwenye sheria ya sasa kinachompa mshtakiwa nafasi ya kulipa faini.


Sheria iliyopo sasa ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya ya mwaka 1995 (Sura ya 95, Ibara ya 16) inasema, endapo mtu atakamatwa kwa kosa la kumiliki, kusafirisha, kuzalisha au kutengeneza mashine ya dawa za kulevya, atahukumiwa kifungo cha maisha jela au kulipa faini ya Sh10 milioni.

Hatua hiyo inakuja wakati idadi ya Watanzania wanaosafirisha, kuzalisha na kutumia dawa hizo ikiongezeka hapa nchini.

Pamoja na mapendekezo hayo, wadau mbalimbali wamesema kufanyika kwa maboresho hayo hakutasaidia kupambana na tatizo lililopo hivi sasa, ikiwa maadili ya wananchi na viongozi yaliyoporomoka hayatarekebishwa.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk Kitila Mkumbo alisema sheria yoyote itakayowekwa haiwezi kuwa ‘mwarobaini’ wa kutibu tatizo la dawa za kulevya hapa nchini kama wanaohusika hawatawajibishwa.

“Hivi sasa zipo sheria, lakini hazitekelezwi. Kuna baadhi ya viongozi wakubwa kabisa wametajwa kujihusisha na dawa za kulevya, lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa,” alisema Mkumbo.

Mbunge wa Kawe na Mjumbe wa Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala ya Bunge, Halima Mdee, alisema Tanzania ina sheria nzuri na bora, lakini changamoto ipo katika utekelezaji wake kwa kuwa rushwa ina mchango mkubwa katika kudhoofisha maendeleo ya taifa.

Mdee alisema ingawa sheria ya rushwa iliyopo hivi sasa ni nzuri, ina kasoro kadhaa zinazohitaji kufanyiwa marekebisho ili kuipa nguvu zaidi.

Alisema baadhi ya viongozi waliopewa dhamana na wananchi wanatuhumiwa kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya.

“Kama mtandao wa dawa za kulevya tunaousikia upo kuanzia viongozi wakubwa hadi wa chini, unadhani hata ukiwa na sheria nzuri itatekelezwa na nani? alihoji Mdee.

Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya nchini, Godfrey Nzowa alisema mapendekezo ya sheria ya dawa za kulevya ni mazuri, lakini yana changamoto nyingi katika utekelezaji wake.

Alisema ingawa sheria mpya inayopendekezwa inataja adhabu ya juu kuwa ni kifungo cha maisha kwa mtu anayejihusisha na biashara ya dawa za kulevya, haijaweka wazi kiwango cha chini kwa mtuhumiwa atakayepatikana na kosa hilo.


“Kwa namna ilivyo sasa, sheria hii inaweza kuleta shida kwa sababu haitaji ‘minimum sentence’ (kiwango cha chini cha hukumu), hivyo mtu anaweza kusema mtuhumiwa afungwe mwaka mmoja,” alisema Nzowa.

Nzowa alisema sheria ya dawa za kulevya iliyopo inaweka kiwango cha chini cha adhabu kuwa kisiwe kifungo cha chini ya miaka ishirini.

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dk Hellen Kijo-Bisimba alisema kinachotakiwa si sheria kali, bali viongozi wawajibike kwa kuwa kuna baadhi ya watu walikamatwa na vidhibiti lakini wameachiwa huru.

“Sheria kali zitakuwa kwa ajili ya wafanyabishara wadogo tu kwa sababu wale wakubwa wana fedha nyingi, ndiyo maana tunahitaji viongozi kama Dk Harrison Mwakyembe (Waziri wa Uchukuzi)wanaopambana, ingawa anaonekana kama anapigana na maji yanayomrudisha nyuma,” alisema Dk Kijo-Bisimba.

Mmoja wa vijana walioathiriwa na dawa za kulevya, ambaye hakupenda kutaja jina lake kwa sababu za usalama, alisema sheria kali hazitasaidia chochote, kwa sababu wafanyabiashara wakubwa ndiyo wanaotoa rushwa ili waendelee kufanya biashara hiyo.

“Kama kweli wanataka biashara ya dawa za kulevya iishe kabisa hapa nchini, waanze kwanza kutokomeza rushwa,” alisema.

Mwanamke mmoja ambaye ametumia dawa za kulevya kwa muda mrefu, ambaye pia aliomba jina lake lisitajwe gazetini, alisema sheria hiyo ni kali na kwamba kama itatekelezwa kikamilifu ‘mateja’ wengi ndiyo watakaopelekwa gerezani, kwa sababu wengi wao ni maskini.

“Ninachoona sheria hii itaongeza viwango vya kutoa rushwa kwa viongozi wasio waaminifu na kuwaacha watumiaji wengi maskini wakiozea jela,” alisema.

Jitihada zaidi

Mbali na mapendekezo ya kuboreshwa kwa sheria ya dawa za kulevya, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi alisema Serikali pia imetoa mapendekezo ya kuundwa kwa chombo maalumu kitakachokuwa na mamlaka kamili ya kumshtaki mtuhumiwa.

“Tume ya Kuratibu Dawa za Kulevya haina mamlaka kisheria ya kukamata, kukagua na kumfikisha mtu mahakamani na badala yake majukumu hayo yako kwa Kikosi Maalumu cha Jeshi la Polisi(Task force),” alisema.

Aidha, Lukuvi alisema mbali na kuwapo kwa kikosi hicho kinachoshirikiana na tume kutekeleza majukumu hayo, changamoto bado ni kubwa.

Mwananchi

Amini usiamini Nigeria ina upungufu wa wanaume wa kuoa!! Kiasi kwamba wanawake wanaotamani kupata wenza na kutengeneza familia wameamua kuchukua hatua.Zaidi ya wanawake elfu 8 walio single jana wameandamana kutokana na upungufu wa wanaume wa kuwaoa.


Lengo la maandamano yao ni kuishinikiza serikali kuwasaidia waolewe, kivipi? (Ndio swali hata mimi nimejiuliza!)

Wanawake waliojikusanya na kuandamana ni mkusanyiko wa 5380 waliopewa talaka, 2200 ni wajane 1200 yatima, na 80 wengine. Wanawake hao wamedai kuwa hawana uwezo hata wa kununua chakula cha siku kwa sababu hawana wanaume wa kuwasaidia ndio maana wanahitaji wanaume wa kuwaoa na kuwasaidia mahitaji yao.


SOURCE: NAIJA GISTS


MWANAFUNZI wa darasa la kwanza Shule ya Msingi Kipwa mwambao mwa Ziwa Tanganyika wilayani Kalambo katika mkoa wa Rukwa mwenye miaka minane ameweza kujiokoa yeye na mtoto wa dada yake mwenye umri wa miezi mitano kwa kuogelea hadi ufukweni baada ya mtumbwi waliokuwa wakisafiria kuzama kwenye ziwa Tanganyika.


Manusura huyo aliyefahamika kwa jina moja la Prisca akiwa miongoni mwa wengine 15 walinusurika kufa maji ama kwa kuogelea au kuokolewa alipoona mtumbwi huo ukizama, inadaiwa alipiga mbizi majini akiwa na mtoto huyo mchanga mgongoni mwake na kuweza kuogelea kwa saa kadhaa hadi ufukweni wote wakiwa hai.

Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji hicho cha Kipwa katika mwambao wa Ziwa Tanganyika , Benson Silinjile alithibitisha mkasa huo wa aina yake akisema msichana huyo Prisca alikuwa amempeleka mtoto huyo kupata chanjo katika kituo cha afya kijijini Kapele kwa kuwa mama wa mtoto huyo alikuwa mgonjwa hivyo alimwomba msaada huo.

Licha ya msichana huyo kuweza kujiokoa yeye na mtoto huyo mchanga kwa kuogelea hadi ufukweni pia nahodha wa mtumbwi huo uliopata ajali hiyo iliyosababisa vifo vya watu 13 wakiwemo wanawake na watoto wenye umri chini ya miaka mitano , Lazaro Sikapote (26) aliweza kuokoa familia yake akiwemo mama yake mzazi Rose Sikapote , mkewe Rakadia Sikazwe na mwanae aliyefahamika kama Nazaro Sikapote.

_DSC1063 copy
Wema Sepetu alizaliwa tarehe 28 September hivyo leo ni birthday yake. Taja wasichana wote wa Bongo Movies wanaotamba Tanzania, usipoliweka jina la Wema Sepetu orodha haijakamilika. Wema Sepetu ni supastaa asiyefutika kwenye vichwa vya habari vya magazeti ya udaku na websites/blogs. Mfahamu zaidi kwa undani leo anaposherehekea siku yake ya kuzaliwa katika mahojiano haya aliyoyafanya na Bongo5 kwaajili ya jarida la Mzuka.

Kwenu mko wangapi na wewe ndio mtoto wa mwisho?
Kwetu sisi tuko wanne na mimi ndio mtoto wa mwisho, nina dada watatu. Wa kwanza na wa tatu wako Marekani, wa pili yupo hapa hapa, ameolewa ana familia yake. Wa kwanza yuko kule anafanya kazi ana mtoto mmoja. Wa tatu yuko kule anasoma na anafanya kazi 
Miaka mitano kabla ya mwaka 2006, Wema alikuwa ni msichana wa aina gani?
Wema alikuwa ni msichana wa kawaida. Wakati ule ulikuwa ukiniuliza unataka kuwa nani ukikua ningekujibu nataka kuwa air hostess sababu dreams zangu zilikuwa ni kuwa air hostess, sijawahi kufikiria kabisa kuingia kwenye fame. Though nilikuwa nawaangalia watu kama Ray C, K-Lynn, Kwasababu mimi nilikuwa nasoma academic na shuleni kwetu nakumbuka tulikuwa tukitoka ile home time kulikuwa na duka fulani hivi la mpemba tunaenda tunakula sambusa nini, so magari yatapita nini and we would see Ray C and everybody will go like ‘you see Ray C’ you know, kwahiyo we go crazy over superstars na watu famous. 
Kiukweli I never so myself kuwa katika this position ambayo niko. Kwahiyo nilikuwa tu msichana ambaye sina ndoto za kuwa star lakini nilikuwa tu nawashangaa masupastaa. My dad amekuwa anapenda sana mashindano ya Miss Tanzania and kila mwaka alikuwa anamake sure kwamba amenunua tiketi ya kwenda kuangalia Miss Tanzania. 
So nakumbuka ilikuwa ni mwaka wa akina Sylvia Bahame tumekaa nyumbani amekosa tiketi. Akakaa akasema ‘kumbe ukiwa umekaa nyumbani ndio unaenjoy vizuri kuliko hata kwenda pale’ akasema ‘one day nawish one of my beauties hata kama hatoshinda, nikilipia tiketi naenda nikijua kabisa nimeenda kumlipia binti yangu.
So sikukiweka kichwani hicho kitu lakini after kuingia katika whatever na nini, so siku nimekaa na dad nikamwambia ‘dad unakumbuka kuna siku ulisema hivi’ akasema ‘yes I remember’ . Hata Mange Kimambi alivyokuja kuniapproach, alivyoniona Sleep Way akaniambia kwamba anataka niingie katika mashindano, nikamwambia kwamba mimi nina wazazi wangu, siwezi nikaamua tu mimi mwenyewe na mimi nakaa na wazazi, so nilivyoongea na mama akasema ‘ongea na baba yako’ nikampigia simu baba alikuwa kipindi hicho Dodoma, akaniambia ‘fanya my beauty nitakusupport’, hakuthink twice alinipa go ahead kabisa.
Kabla ya Miss Tanzania, ni watu wachache sana waliokuwa wakimfahamu Wema Sepetu, ni vipi Miss Tanzania ilibadilisha maisha yako hasa kutokana na watu kuanza kufuatilia maisha yako na chochote unachofanya?
Ni kitu ambacho nilikipata bado nina umri mdogo and nilikuwa sijajiandaa, nilikuwa naichukulia tu poa this whole issue ya kuwa kwenye spotlight. Nilikuwa sidhani kama itakuwa vile kwasababu kama wanavyosema experience ni bora uexperience mwenyewe usione kwa wenzako so nilivyokuwa naichukulia ni tofauti na ilivyokuja kuwa kwasababu mimi nilikuwa naichukulia tu ‘kuwa star raha’ umeenda watu wamekushangaa nini lakini nilivyokuwa nimeingia sana katika ile spotlight nikasema kumbe ooh my God it’s this hard.
Kwahiyo ikawa ni kitu kilichonipa wakati mgumu sana kukizoea like mpaka sasa hivi naweza kusema kwamba ile umetoka kila mtu kakuangalia nini, it’s not an easy task, yaani haizoeleki hiyo hali yaani kila siku unazidi kuiona mpya kwasababu there is no place unaweza ukaenda ukawa na privacy yako, yaani upende usipende lazima utakuwa ni attention kwa watu, lazima watu watakuangalia. Sometimes natamani tu na mimi niwe Wema lakini huwezi sababu all eyes on you. And a lot of times as a normal human being kuna time unahisi you just be yourself lakini inakuwa ni time chache chache sana. The only place where I can be myself is in my room and in my house, out of my gate you cannot be yourself.
Kuna wakati wowote uliwahi kujuta maisha ya ustaa baada ya kuwa Miss Tanzania?
Yes, nimewahi kujuta lakini mwisho wa siku huwaga nasema kwamba mwenyezi Mungu ndio anapanga kwasababu kama mwenyezi Mungu ndio amenipangia hivi nisingefika hapa kwanza, kwahiyo regrets zinatokea kwa kila mtu, lakini siwezi kusema kwamba zimetoka kwa mara nyingi, labda mara moja mara mbili na zinatokea pale tatizo linapotokea, hauwezi ukapata regrets kama hakuna tatizo.
Ukiwa staa kila mtu atataka awe rafiki yako, na kabla ya kuwa Miss Tanzania ni wazi ulikuwa na marafiki uliokuwa ukihang out nao hapa na pale, uliendelea kuwa na urafiki nao, ama baada ya kuingia maisha hayo ikakuwia vigumu kuwa nao tena pamoja?
Nina marafiki mpaka sasa ninahangout nao wanakuja mpaka nyumbani lakini hatushei sana zile common interests kama zamani because once upon a time tulikuwa tuko wote on the same rank. So nilivyokuwa nipo kwenye spotlight obvious nimekutana na watu wengine wapya watu ambao naonana nao katika kazi zangu za kila siku, because apart from being Miss Tanzania, I am also an actress, kwahiyo nakutana na wasanii wengine ambao labda nakaa nao kwa muda mrefu sana kwahiyo utajikuta tu unashare nao common interests sababu unafanya nao kazi pamoja. 
Ulikuwa na boyfriend tayari? 
Yes nilikuwa naye
Kuna wakati wowote aliwahi kujihisi inferior kutokana wewe kuwa maarufu? Ulifanyaje kumweka sawa?
Well, si unajua zile za kishuleshule, zile za kitoto naweza kusema. Sana sana ukishafika ile o-level nini utakuwa na yule boyfriend ambaye unaamka tu asubuhi umeshavaa unasema sasa hivi naenda kuonana na boyfriend wangu, ukisharudi kutoka shuleni from there nyumbani, no boyfriend. Yeah nilikuwa naye, in the beginning alivyojua kwamba nashiriki Miss Dar Indian Ocean akaniambia kwamba ‘ukishiriki mimi nisahau, sitaweza kuwa na wewe tena’, nikamwambia, why? Akaniambia ‘utakuwa upo kwenye public’ nikamwambia ‘okay fine’, nikamdanganya kwamba sishiriki. 
So siku moja gazeti la Mwananchi pale katikati kulikuwa na picha yangu kubwa ‘Miss Dar Indian Ocean kushindana kesho’ and lile gazeti kuanzia naingia shuleni naingia kila mtu ananiambia ameniona kwenye gazeti. So kitu cha kwanza nikafikiria ‘Mungu wangu yule mtu akiliona’ so sikuonana naye the whole day.
Nikiwa nyumbani ndio nikamuona anakuja kalishikilia, nikawa namsikiliza. Akaniambia, ‘nimeona gazeti lako and ndio hivyo kwahiyo umeshanidhihirishia kwamba umechagua hiyo issue, so fine we endelea’. Basi nikajaribisha kuongea naye lakini hakuweza kunisikiliza lakini luckily the next day wakati ndio nashiriki nimekaa pale time ya kujibu swali namuona pale anapiga picha kwahiyo he was there na alinisupport mpaka nilipofika Miss Tanzania lakini after that sababu nilikuwa ambassador wa Vodacom nikawa nafanya kazi Vodacom nikawa sionani naye vile kama kawaida, kila akinipigia simu nipo busy, yeye mwenyewe akasema tu ‘bwana mimi siwezi’. Basi tulielewana vizuri na mpaka kesho tunaongea, tunasalimiana’ 
_DSC1055 copy
Uwewahi kusema bila Kanumba usingeingia kwenye movies, marehemu alikuwa ana mchango gani kwako?
Nakumbuka nilipokutana na marehemu nilikuwa niko na dada yangu mimi nilikuwa nakaa na dada yangu, kwasababu once nilishawahi kuishi na mama yangu and then from there unajua baada ya kuingia kwenye nini nini nikawa busy. Dada yangu mimi kaolewa lakini kwa dada yangu nilikawa nahisi kama pako free zaidi, kwamba mama ukirudi ‘umetoka wapi sijui nini na nini hivyo, alikuwa haelewi. So ikabidi tu nianze kuishi na dada yangu.
Kwahiyo dada yangu akawa ananielewa, kwasababu hayupo sana protective kama mama. Siku hiyo tunabadilisha seating arrangement ya pale nyumbani kwa dada yangu tukawa tunatafuta carpet like different furnitures, so tukawa tumeenda hapa kulikuwa na hili duka kubwa hivi la Mwanamboka kulikuwa kuna furniture center, Pentagon, so tukawa tumeenda pale wakati tunaenda tulimkuta Kanumba wapo nje wameweka makamera yao nini ,wanashoot Lost Twins. So sisi tumeingia tunaona tu makamera, tumepark gari tumeingia ndani tunaangalia furniture. Akatokea Maya tukasalimiana akaniambia, ‘ jamani nakupenda’ na mimi nikamwambia na mimi napenda unavyoigiza’ nini na nini.
Tukatoka nje tukakutana tena na Maya akaniambia ‘jamani jamani kama unaweza pita kidogo tu hata uonekane, hata usalimie’.
Nikamwambia siwezi kwasababu nipo kwenye mkataba, akina Uncle Hashimu wataniua wakiniona nimefanya kazi au nimetokea kwenye nini bila kuwaconsult so akaniambia ‘basi sawa tuachie namba yako’. Wakati ananiambia tuachie nambo yako, Kanumba huyo anapita, ‘Kaka kaka ngoja umemuona Wema?’ Aliniringia sana.
‘Mambo’ nikamwambia ‘fresh vipi’ ‘safi’ nikamwambia poa,’Kaka basi chukua namba yake ya simu tunaweza baadaye like tunaweza tukamtumia kwenye movies’, ,Kanumba akamwambia achukue simu yake ndani. Basi nikamwangalia mimi mwenyewe basi ndio ninamwona mara ya kwanza, ‘Hee Kanumba’, kwasababu nimeangalia sana michezo yao. 
Basi, so baada ya hapo akaleta akachukua namba yangu akanibeep nikamsave, basi mimi nikaondoka zangu. Sijafika mbali naona namba inanipigia ambayo nimeisave vilevile Steven Kanumba, nikapokea ‘Hello’ akaniambia ‘vipi, safi Kanumba hapa’ nikamwambia ‘namba yako nimeisave’ ‘haya basi sawa basi baadae’ nikamwambia ‘poa’.
Mara like jioni jioni hivi akaanza kunitext ‘mambo’ ‘Safi’ ‘vipi uko wapi?. Basi kila siku tukawa tumejengeana tabia ya kutextiana kila siku tunandelea for one weak tunatext mara yeye ataniuliza umekula nini, mara sijui nini, obvious kwa mwanamke unakua tu unajua kwamba mwanaume akiwa ana interest na wewe. Kidogo tukaanza kuulizana una boyfriend una girlfriend sijui nini, hivyo. Akaniambia mimi ‘nipo kambini Lamada’ akanielekeza nikafika.
Basi nimefika siku hiyo tumekaa pale garden akaniambia ananipenda na nini, hivyo. Kipindi hicho nilikuwa sina boyfriend nilikuwa very very single, so nikamdanganya nikamwambia ‘mimi na boyfriend wangu sijui nini’ akaniambia ‘naomba tu just like nifikirie basi’ Nakumbuka tulivyokuwa tunaondoka ndo tukakiss, it was our first kiss. Basi nikaondoka, akaniambia ‘unaweza kurudi tena nikamwambia siwezi akaniambia please, please naomba urudi tena unikiss’ nikamwambia ‘sawa’ basi nikarudi then akaniambia ‘l love you, love you too, mapenzi yakaanza.
Basi kwenye mapenzi yetu ndo akaniambia like ‘nataka kuact movies na wewe’ nikamwambia ‘mimi siwezi kuact’ akaniambia ‘mimi nahisi unaweza kuact hujajua tu’ nikamwabia sijawai kufikiria kuact, akaniambia ‘unaweza kulia’, nikamwambia ‘nilie nina sababu gani ya kulia’ akaniambia ‘basi kama huwezi kulia tutakumenyea vitunguu, ‘vitunguu ukimenya si unalia, basi tutakuwa tuna kumenyea vitunguu’ .
Akaniambia niende kuonana na bosi wake. Nilivyofika tu ofisini nikaonana na Mtitu Game. Akanipa script akaniambia nikasome kama story akaniambia ‘wakati unasoma uwe unasoma sana concentrate kwenye Dina. Basi vile tukiwa tukikutana tunafanya mazoezi nini, akaniambia ‘sawa basi wewe you are ready to shoot. Nilivyo shoot movie yangu kwanza, hauwezi amini, I just felt yaani kwanza niliona iko very easy. Kwa wengine wanaona it’s hard unajua.
Baada ya hapo ndo nilikuwa tayari nimetoa taji, I had to go back to school. Nikasafiri nikaelekea Malaysia kufanya kozi yangu ya mwaka ya International Business, wakati niko Malaysia nikatumiwa movie yangu ya Point of No Return. Tumekaa tunaangalia na marafiki zangu nikaona kwamba kumbe it’s nice, it’s fun. Nikampigia simu, ‘narudi for likizo soon naomba uniandalie script nataka ni shoot movie nyingine’
Nimerudi kweli ndo tukashoot Red Valentine, Family Tears, White Maria yaani tukashoot movie movie nyingi hivi so from there nikawa nimeshajikuta katika movie, so that why I keep saying kwamba without him nisingejua.
_DSC1040 copy 
Hebu tuzungumzie uhusiano wako na Diamond ambao katika mahusiano yako yote ndio ulioandikwa zaidi kwenye magazeti, unakumbuka mlikutana wapi?

Mi na Diamond tuliwahi kukutana mara moja tu Billcanaz na hatukuwahi kusalimiana kabla ya kuanza uhusiano lakini tulikuwa tunaangalia sana, so nakumbuka alikuwa yupo smoking room kwahiyo tukawa tumepeana migongo, nilikuwa na rafiki zangu wawili. Nikamuona akaniona yeye alikuwa na rafiki yake, hatujasaliamija hatujafanya chochote mimi nimechukua vinywaji tukatoka nje na marafiki zangu tumesimama hapo nje nikawa naambiwa ‘yule ndio ameimba Kamwambie’ kipindi hicho nilikuwa namuona wa ajabu sana ila tu alijiseksisha kiasi fulani (kicheko kirefu).
Kipindi hicho mimi nilikuwa natoka na Chaz Baba so nakumbuka hiyo ndio ilikuwa the first and last day tumeonana. Mimi nikasafiri nikaenda Marekani, nilipofika kipindi hicho Kamwambie ndio ilikuwa hot na Mbagala ndio karelease. Dada zangu walikuwa wanampenda sana Diamond yaani just from the songs. Dada yangu wa kwanza ana miaka 14 yupo Marekani na hajawahi kurudi Bongo toka aondoke kwahiyo alikuwa anaona Bongo inafanya vizuri sasa hivi akaniuliza kama tuna urafiki na Diamond nikasema sio sana tunajuana tu. 
Akaniambia nimwambia aende Marekani kufanya show sababu kila party tuliyokuwa tunaenda lazima watapiga Kamwambie halafu kila mtu anaipenda. So watu wakaanza kuniambia like ‘hebu find contact naye huku kuna mapromoter aje kufanya show’na kipindi hicho Profesa ndio alikuwa amekuja nikamwambia basi sawa mi nitamtafuta.
Nikamwabia Da Rehema, Ray C anitafutie contact zake. So siku moja nikaona anaplan kwenda kufanya show London, nika mclick Diamond Platnumz nikamtext, nikamwambia ‘hey mambo vp mzima upo London’ akaniambia ‘No mamie sipo London sijui ni nini’ nikamwabia ‘anyways Wema hapa nipo Marekani halafu it happens una fans wengi, akaniambia basi sawa acha nimalize issue ya London halafu nitakuambia. 
Basi tukajenga tu mazoea tukawa tunachat nini yaani ikawa yeye anaingia Facebook kuchat na mimi naingia kuchat naye, washkaji tu yaani. Akawa ananiambia ‘bado uko na Chaz na nini’ nikamwambia yeah nipo na Chaz. Sasa ilikuwa ni kama mwezi wa nane wa tisa kama sikosei. Mimi wakati nipo Marekani nilikuwa naambiwa sana news kuhusu Chaz, mara Chaz sijui yupo na mwanamke gani, hiyo hiyo Facebook watu wananitumia mpaka picha nikumuuliza anakataa.
Sasa mimi nakumbuka dada yangu alikuwa anampenda sana Chaz so siku ya siku amekutana naye yupo sijui na mwanamke gani alipoaniambia nikasema, basi. So nikajikuta namuelezea matatizo Diamond. Siku niliyoamua kabisa mimi and Chaz are done nikamwambia mimi siwezi. So tukawa tunawasiliana na Naseeb hivyo. Siku moja tukanuniana, alikuwa amealikwa Ikulu halafu nikawa namtext hajibu, nikimpigia simu hapokei akaja akatoka akanipigia simu nikawa sijibu. Akanitumia meseji ‘baby I am sorry, we ndio faraja yangu sijui ni nini…. I LOVE YOU. Sikuona kitu kingine chochote nikaona tu hiyo. Basi nami nikamjibu sawa nimekusamehe lakini sijakusamehe sana, nimekusame kidogo. Akaniambia ‘niambie kitu kizuri’ na mimi nikamwambia I LOVE YOU. Basi akaniambia ‘mwenzio nakupenda, nachanganyikiwa’ basi no mapenzi yakaanza hapo.So niliporudi kutoka Marekani mimi na Naseeb tukaanza kuishi pamoja. 
_DSC1061 copy
Mwaka jana alipooenda kutumbuiza kwenye Big Brother Africa, alidai kuwa ameweza kuongea Kiingereza kwasababu yako, ulikuwa ukimfundisha ama ulikuwa ukipenda kumuongelesha Kiingereza zaidi?
Yes. Naseeb alikuwa hajui Kiingereza, alikuwa anajua cha juu juu. Ila mimi na Naseeb tumekaa pamoja mwaka mzima kama mke na mume. So mimi nilivyo kidogo nimetupia Kiingereza kwahiyo hiyo ilikuwa inampa tabu kwenye the first two months kwahiyo most of the times nikawa naongea naye Kiingereza. Lakini he is smart, Naseeb is very smart yaani akiwa haelewi kitu ‘hivi baby hapa kwenye has na have unafanya nini, hapa natumia tense gani? Niweke ing niweke nini?’ mwisho wa siku nikajikuta like tunatumia most of the time kufundishana. Akisema kitu ambacho sicho namwambia ‘usije ukarudia tena kusema hivyo mbele za watu watakucheka’. So akajikuta tu anaweza.
Kwanini mliachana?
Mimi na Naseeb tuliachana baada ya yeye kunicheat na Jokate .Nilikuwa sijui and maisha yangu yote tangia nimeanza mapenzi na Naseeb naweza kusema kuwa sikuwahi kuwa unfaithful. I used to be very faithful to him na tulikuwa tunapendana sana. With Naseeb nilikuwa nimesharidhika na maisha ambayo niko nayo na hata kama yalikuwa not good, whatever lakini tayari nilikuwa nipo satisfied with me and him nilikuwa tayari nimesharidhika naye. 
Nadhani pia inacost mwanaume akishajua kwamba anakutawala in one way or another so labda ni shetani au ni ibilisi alimuingilia baada ya kutaka kuanza kushoot video ya Mawazo ndo rumors zilianza, nikawa siamini kwanza. Siku moja ndio nikapigiwa simu na rafiki yangu anafanya kazi Piccolo akaniambia ‘Diamond yuko hapa na Jokate na wanakiss’. Nilitoka, nikachukua taxi nikaenda mpaka Piccolo, kitu cha kwanza niliona gari yake. Nilivyofika nikawakuta sijui wamewekeana miguu. Nilivyofika pale nikawasalimia wakawa wako kimya na nimeona ile kitu nikawaaga nikaondoka zangu. Nikaliaaaa, amerudi wakati huo bado tunaishi pamoja akanikutana napanga nguo, hakutaka kuongea sikutaka kuongea, tukachuniana, sikulala mimi na Naseeb kitandani for one week. Anaiona ile hali lakini hataki kuanza. Nikachoka, nikaja tu siku nimepanga nguo zangu nikaenda kwa dada yangu ndio ikawa kimoja. Basi mimi nikamwacha akaendelea na maisha yake na mimi nikaendelea na maisha yangu. 

Neo-soul singer, Anthony Mwangi better known as Anto Neosoul is going to join Uganda’s Julianna Kanyomozi and Kenya’s Ian Mbugua on the judging panel during Tusker Project Fame season six.


The Kenyan star debuted his maiden album called StarBorn in mid-May,and has since been a force to reckon wit in Kenya’s music industry.

Despite criticism that he is not eligible to take up the spot as the 3rd judge for TPF6,it seems “haters” will just have to swallow the bitter pill and take it all as it comes!

He will be replacing Tanzania’s Hermes Bariki who has been sharing the judging table with Julianna and Ian since the show’s inception.

Neosul is not the only change that Tusker Project Fame 6 has brought, the show’s co-host, Sheila Mwanyigha has been replaced by Channel O presenter and radio personality, Joey Muthengi.

At the moment, each country produced around 15 contestants who are supposed to take on a stage of screening at which they will be reduced further to the number who will get into the final competition.

Friday 27 September 2013

HAWA NI WASANII 10 WA BONGO FLAVA WALIOINGIZA PESA NYINGI ZAIDI 2013.



1016243_622850427736775_2127148511_n
1. Diamond Platnumz
Hakuna ubishi kuwa, mwaka 2013 Diamond Platnumz ndiye msanii aliyeingiza fedha nyingi zaidi. Pesa nyingi ya Diamond imetokana na malipo ya show zake za ndani na nje ya nchi. Kwa uhakika, mwaka huu pekee, Diamond amefanikiwa kuingiza takriban shilingi bilioni 1.
Kwa show za ndani peke yake, Diamond hutoza si chini ya shilingi milioni 10 ama 15 na kila wiki hufanya show zaidi ya 2. Hivyo tangu mwaka uanze, Diamond amekuwa akiingiza shilingi milioni 40 kila wiki. Tour za nje alizofanya mwaka huu ni pamoja na zile za Uingereza ambako alifanya show kwenye miji mitatu, show ya Burundi na Congo, show mbili za Kenya (Nairobi na Mombasa), show ya nchini Comoro ambako alilipwa si chini ya dola 30,000 na show ya Malaysia wiki iliyopita.
Kwa upande wa show za hapa nyumbani ambazo ni nyingi mno zisizo na idadi, ukiachana na zile za kawaida, Diamond aliingiza shilingi milioni 40 kwenye show 4 za Kili Music Tour ambapo kila show alilipwa shilingi milioni 10. Ndiye msanii aliyelipwa fedha nyingi zaidi kwenye ziara hiyo.
Pia amefanya show kadhaa za Fiesta 2013, show za promotion za Tigo na makampuni mengine, Tamasha la Matumaini, show ya Tulizana Tuko Wangapi ya Leaders Club, show yake na Nay wa Mitego (Dar Live na Maisha Club). Mwezi February 16 mwaka huu, Diamond alifanya show jijini Arusha ambayo kiingilio chake kilikuwa ni shilingi 150,000 ndani ya Club Safari na ukumbi kufurika.
Miezi kadhaa iliyopita pia hitmaker huyo wa ‘Number 1’ ameshaalikiwa kwenye show corporate kuburudisha wafanyakazi wa benki na taasisi zingine pamoja na watu binafsi na zote hizo zimemuingizia fedha nyingi. Pamoja na show, Diamond amekuwa akiingiza fedha nyingi zaidi kwenye malipo ya ringtones ambapo kila baada ya miezi mitatu amekuwa akiingiza si chini ya shilingi milioni 20. Kwa mujibu wa Push Mobile, akaunti ya Diamond kwenye kampuni hiyo ndio inayoingiza fedha nyingi kuliko msanii mwingine yeyote wa Bongo Flava.
Mkataba exclusive alioingia na kampuni ya simu ya Vodacom kuuza wimbo wake mpya My Number One kama muito wa simu, umezidi kumpandisha juu na ikidaiwa kuwa mkataba huo ni wa mamilioni ya shilingi.
1239507_650218681669184_1372786191_n
Ikumbukwe pia, Diamond ni balozi wa Cocacola. Mkataba huo ambao haijajulikana umemuingizia shilingi ngapi, lakini ni fedha inayoweza kuwa si chini ya shilingi milioni 100.
584fe16a273711e3b8f522000a1fbce9_7
Diamond ni miongoni mwa wasanii wengine 23 wa Afrika akiwemo Lady Jaydee kwenye mradi mkubwa wa Cocacola wa Coke Studio Africa.
2. Lady Jaydee
1238789_10151593260760025_1742196233_n
Huwezi amini, vuguvugu la Anaconda limemsaidia Jaydee si tu kukusanya mashabiki wengi zaidi, bali pia limempa fedha nyingi mno. Zaidi ya tiketi 3,500 zilinunuliwa kwenye show yake ya mwezi June ya Miaka 13 ya Muziki na kuingiza takribani shilingi milioni 100. Haikuishia hapo, albam yake Nothing But The Truth ilinunuliwa kwa kiasi kikubwa na kumfanya kuwa msanii pekee wa Bongo Flava anayeendelea kufurahia mauzo ya albam zake.
Hits zake mbili, Joto Hasira na Yahaya kutoka kwenye albam yake hiyo, zimebadilisha maisha yake na kumfanya kuwa mwanamuziki mwenye show nyingi zaidi pia. Lady Jaydee ametumbuiza kwenye karibu show zote za Kili Music Tour ambako ameingiza shilingi milioni 25.
Mwaka huu pia Lady Jaydee amefanya show nyingi kubwa ikiwemo ile ya uzinduzi wa filamu ya Lulu, Foolish Age, show yake kwenye Miss Tanzania 2013, Family Day Show ya Arusha iliyofanyika Eid Pili, Anaconda Show iliyofanyika Triple A na nyingine iliyofanyika Snow View Hotel. Akiwa Arusha pia, Lady Jaydee aliuza kopi za albam yake kama njugu pamoja na tiketi za Anaconda zilizouzwa kwa shilingi 15,000 kila moja.
June mwaka huu pia, Lady Jaydee alitumbuiza kwenye semina ya kuwezesha wanawake kuondokana na njaa na umaskini, iliyofanyika chini ya mfuko wa fursa sawa kwa wote chini ya mama Anna Mkapa. Biashara yake ya Nyumbani Lounge, imeendelea kufanya vizuri pia kwa kupata wateja wengi wanaoenda kupata chakula, vinywaji na burudani kutoka kwa bendi yake ya Machozi.
Bado anaingiza fedha kupitia udhamini wa Airtel kwenye show yake ya TV ya Diary of Lady Jaydee. Msanii huyo ambaye jina lake ni Judith Wambura pia miongoni mwa wasanii 24 wa bara la Afrika waliochukuliwa kwenye mradi wa Coke Studio Africa wa kampuni ya Cocacola unaoendelea jijini Nairobi Kenya.
Coke Studio Africa – the new, exciting music show featuring incredible live performances by the very best in Africa
3. AY
421451_10150581514944221_264981067_n
Humsikii sana rapper huyu kwenye show za Tanzania. Tofauti na wasanii wengine, fedha anazoingiza AY zinatokana zaidi na endorsements na biashara zake anazofanya. Pesa nyingi alizoingiza zimetokana na mkataba wa mwaka mmoja na Airtel wa ubalozi uliokamilika mwezi May mwaka huu.
Katika ubalozi huo wa Airtel Africa, AY aliungana na wasanii wengine watatu wa Afrika ambao ni pamoja na Papa Wemba, Tuface na Daddy Owen wa Kenya. Katika mkataba huo AY alilipwa dola za Kimarekani 80,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 129.
Rapper huyo wa ‘Machoni Kama Watu’ ni balozi pia wa bia ya Peroni ya Italia na kupitia mkataba huo, AY ameingiza mkwanja mwingi. AY pia ni mwanzilishi mwenza wa kipindi cha Mkasi kinachoendeshwa na Salama Jabir. Kipindi hicho kina wadhamini wawili, Cocacola na Airtel na hivyo kupitia mgawanyo wa mapato, AY amekuwa akiingiza pia fedha ya kutosha.
AY ni CEO wa kampuni ya Unity Entertainment inayojihusisha na kuandaa show, matangazo, kuleta wasanii wa nje na mambo mengine. Mwaka huu pekee, ikishirikiana na kampuni ya SK Entertainment, kampuni yake imeandaa show kibao zikiwemo zile zilizofanyika Elements Lounge ambapo Avril, Prezzo, Huddah Monroe na J-Martins wamewahi kuhudhuria.
Maisha ya kawaida ya rapper huyu ndio yanayowafanya watu wengi wasijue ukubwa wa kile anachokiingiza. Macho yake ameyaelekeza zaidi kwenye uwekezaji na anawekeza haswaa. Kuna tetesi kuwa, AY anajenga ghorofa lake maeneo ya Kigamboni jijini Dar es Salaam. Anasemekana kuwekeza pia mkoani Mtwara alikonunua ardhi ya kutosha. Mungu ndio anajua ni wapi alikowekeza tena.
4. Ommy Dimpoz
e23fe27c081911e3a88722000a1f90d0_7
Ommy Dimpoz ambaye kwa sasa yupo kwenye ziara ya muziki nchini Marekani ameingiza fedha zake nyingi kupitia show alizofanya. Ziara zake za Ulaya na Marekani pekee zimemuingizia dola 50,000 ambazo ni sawa shilingi milioni 81.
Tangu aachie wimbo wake mpya Tupogo, tayari Ommy ameshaingiza shilingi milioni 50. Kwenye show yake ya hivi karibuni ya Tupogo Night iliyofanyika Club Billicanas, Ommy alipeleka nyumbani shilingi milioni 10 baada ya kukata gharama zote. Watu 1,770 walihudhuria show hiyo.
Show yake ya Burundi ya mwanzoni mwa mwezi uliopita ilimuingizia staa huyo shilingi milioni 30. Ommy hutoza si chini ya shilingi milioni 7 kwa show na kwa mwezi, amekuwa na uhakika wa kufanya show tatu ama nne za ndani bila kusahau show za Kili Music Tour.
Hivi karibuni kwenye segment ya Tell it All ya Bongo5, Ommy alifunguka kuwa makampuni mengi yamekuwa yakimfuata kumpa endorsements lakini msimamo wake wa kutaka kulipwa fedha ya uhakika imemfanya azikatae nyingi lakini yupo mbioni kupata deal kubwa. Mpaka sasa Ommy anajenga nyumba mbili kwa mpigo zenye thamani ya shilingi milioni 250 hadi zilipofikia. Tayari ana viwanja vingine viwili anavyotaka kuangusha mijengo mingine. Hivi karibuni pia atakuja na clothing line yake ya PKP.
5. Madee
7203_294710874001268_1825630445_n
Hii inaweza kuwa surprise kwa wengi lakini Madee ni mfano tosha wa jinsi single moja inavyoweza kubadilisha maisha ya msanii. Tangu atoe single yake, Sio Mimi, Madee ameshaingiza si chini ya shilingi milioni 200.
Mwaka huu ameshafanya show 10 za kampeni ya Tigo ambapo kila moja alilipwa shilingi milioni 3, show 15 za Airtel kwa kiwango hicho hicho. Alifanya show mbili za kampeni za Coca Cola, ile ya uzinduzi wa Coke Zero na Cocacola Bonanza Mlimani City. Bado ameendelea kufanya show za Fiesta 2013. Madee pia alikuwa miongoni mwa wasanii waliotumbuiza kwenye show ya Fuse ODG iliyofanyika September 7 kwenye viwanya vya ustawi wa jamii jijini Dar es Salaam.
6. Mwana FA
IMG_1010 (800x534)
Mwanzoni mwa mwaka huu, Hamis Mwinjuma aka Mwana FA alikuwa msanii wa tatu miongoni mwa wasanii waliongiza fedha nyingi kupitia malipo ya miito ya simu, RBT ambapo aliingiza shilingi milioni 18. Alifanya show mbili kwenye Kili Music Tour ambapo aliingiza si chini ya shilingi milioni 7 pamoja na show kadhaa za Fiesta 2013.
Show yake ya The Finest ilimuingizia shilingi milioni 19. Hivi karibuni alichukuliwa na kampuni ya Vodacom kuzunguka baadhi ya mikoa kwenye kampeni yao na CCBRT kuhusiana na kukuza uelewa wa tatizo la Fistula na kulipwa mkwanja kama balozi wa kampeni hiyo.
Mwaka huu FA amefanya matangazo kadhaa ya Vodacom. Hivi karibuni pia aliingia kile kilichoonekana mkataba kama balozi wa simu za Samsung Galaxy Tanzania japo haijulikani kama ulikuwa mkataba wa ubalozi kama ilivyo mingine.
Mwana FA pia amefanya show za nje zikiwemo za Kenya na Afrika Kusini aliyofanya siku ya Eid mwezi uliopita. Kama wasanii wengine pia, FA ameingiza fedha nyingi kwa show za kawaida za hapa nyumbani na zile za promotion.
7. Chege
3ec62770206d11e382b622000ae912ed_7
Mwaka huu Chege peke yake alifanya show sita nje ya nchi ambazo kila show alilipwa shilingi milioni 4. Akiwa na Temba ambao kwa pamoja hutoza shilingi milioni 6, Chege amefanya show zaidi ya 30 zikiwemo zile za Fiesta, za promotion mbalimbali na zile za kawaida.
Mwezi ujao yeye na Temba wataanza tour ya miezi mitatu barani Ulaya ambapo show ya kwanza itakuwa nchini Sweden, October 5. Pamoja na hivyo, Chege ana biashara ya salon.
8. Profesa Jay
1010701_10151711560347558_1761716231_n
Profesa Jay aliingiza shilingi milioni 20 za Kili Music Tour, alifanya show kubwa ya Jose Chameleone April mwaka huu, show kibao za promotion za makampuni, show ya kampuni ya IPP kwaajili ya Walemavu, Diamond Jubilee mwezi January, na show zingine za kawaida za Dar na mikoani. Pia nguli huyo wa rap ya Tanzania ameingiza fedha nyingi kupitia show nyingi za Lady Jaydee.
Prof J amewekeza kwenye biashara ya salon ambayo tayari inafanya vizuri na ameshafungua studio ya kurekodi muziki iliyopo kwenye hatua za mwisho kuanza kazi. Jize aliingiza pia fedha kupitia kampeni ya magazeti ya Mwananchi kwa kufanya matangazo na show za mikoani.
9. Nay wa Mitego
53c24b9c156c11e3959e22000aeb1b4e_7
Tangu mwaka uanze, Nay wa Mitego ameshafanya show zaidi 20 zilizomuingizia si chini ya shilingi milioni 60. Show hizo ni pamoja na zile za promotion za makampuni ya simu, show mbili za Muziki Gani, show ya Kili Music Tour, show za Fiesta na zile za kawaida. Pia ana biashara zake ambazo kwa pamoja humuingizia si chini ya shilingi milioni 4 kwa mwezi.
10. Temba
2648cdb8274f11e3a2f822000a1f985f_7
Fedha nyingi alizoingiza Temba mwaka huu zimetokana na show walizofanya pamoja na Chege. Ukitoa muziki, Temba pia ni mfanyabiashara na anamiliki duka la vifaa vya ujenzi.

Source:Bongo5.com

Picha za nje ya jengo la Westgate hazioneshi uhalisia wa hali iliyoko ndani ya jengo baada ya shambulio la kigaidi Jumamosi iliyopita jijini Nairobi, Kenya na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 70.

a7
Picha hizi zinatoa picha halisi ya jinsi jengo hilo lilivyoharibika vibaya kwa ndani baada ya ghorofa tatu za jengo hilo kudondoka baada ya kupigwa mabomu katika mchakato wa kukabiliana na magaidi. 
a6
Picha hizi pia zinaonesha jinsi magari yaliokuwepo eneo la maegesho ya magari katika jengo hilo yakiwa yameharibiwa kiasi kwamba kuna mengine ambayo huenda hata wamiliki wanaweza kushindwa kuyatambua.
a1
a2
a3
a4
a5
a8






Abdul Haji ni miongoni mwa mashujaa ambao hawatasahaulika nchini Kenya kutokana na kuamua kuhatarisha maisha yao ili kuokoa watu waliokuwa wamekwama ndani ya jengo la Westagate baada ya kushambuliwa na Al-Shabaab Jumamosi iliyopita.


Tangu asimulie namna alivyopambana na magaidi hao, Haji ametokea kuwa kipenzi cha watu wengi hasa wasichana na mmoja wa watu aliowagusa ni Rehema Chalamila ambaye amesema anatamani mwanaume mjasiri kama yeye ambaye watazaa naye watoto.

“In love with ths Soldier!i want a soldier like him to marry me,” ameandika Ray C kwenye picha ya gazeti aliyoipost kwenye Instagram ikimuonesha Abdul Haji.

“I love You Abdul Haji,You are my Heroooooooo,” aliandika Ray C kwenye picha nyingine.

Kwenye picha nyingine Ray C aliongeza, “My soldier,My Prince,My Love….Love You Abdul Haji.”

Kijana huyo ni mtoto wa waziri wa zamani wa ulinzi nchini Kenya ambaye alienda kwenye mall hiyo baada ya kupata ujumbe kutoka kwa rafiki yake kuwa kaka yake alikuwa ndani ya Westgate wakati watu hao wenye silaha walipovamia.

Akiongea na NTV, Haji ambaye sio mwanajeshi, alisema alifundishwa kutumia bunduki na baba yake ili kulinda mifugo yao isiibiwe na wezi.


Ujuzi huo ulimsaidia Jumamosi hiyo kuwasaidia wafanyakazi wa Red Cross wafanye kazi yao kwa usalama kwa saa tatu na kusaidia kuokolewa kwa watu wafikao 1,000 nje ya mall hiyo.

Binti wa umri wa miaka 15 tunayemtambulisha kwa jina moja tu la Zaina, mkazi wa Kimara jijini Dar ameamua kufunguka na kusimulia jinsi alivyokuwa akibakwa na baba yake mzazi aliyemtaja kwa jina moja la Mohamed.

  
ANAANZA KWA KUANIKA HISTORIA YAKE FUPI!
Akisimulia kwa uchungu, Zaina alianza kwa kuanika historia yake kwa ufupi kwamba tangu atoke tumboni, hakuwahi kumuona mama yake zaidi ya kuoneshwa kwenye picha tu!

Akasema hiyo yote ilitokana na hadithi aliyowahi kusimuliwa kwamba, akiwa kichanga, baba huyo alimuiba kwa mama yake anayeishi Kigamboni, Dar na kwenda kumlea Kimara kwa ushirikiano na mama yake wa kufikia.
  
Lakini akasema: Hata huyo mama wa kambo mwaka jana aliachana na baba baada ya kutufumania chumbani mimi na baba, akakasirika na kuondoka zake.

SIKIA FILAMU KAMILI SASA
“Nakumbuka ilikuwa mwanzoni mwa mwaka jana, nikiwa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kimara ndipo baba alipoanza tabia ya kunilazimisha tufanye mapenzi. Alisema anataka tufanye kwa njia ya kawaida na ya kinyume na maumbile.

“Nilikataa lakini akawa ananilazimisha na vitisho juu. Tulianza kwa kufanya mchezo huo na baba lakini si kwa kupenda kwangu, nililazimika kwa sababu niliamini ni baba ambaye anaweza kunifanya lolote kama nitakataa, mbaya zaidi hakuwa akitumia kinga,” alisema na kuongeza:

“Kuanzia hapo, zoezi hilo liliendelea kila siku hadi mwishoni mwa mwaka jana nilipoamua kutoroka na kwenda kuwaeleza ndugu wa baba, kule Tanga.” 

Binti huyo alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa,  kilichomsukuma kutoroka ni mateso, ukatili na udhalilishwaji uliopitiliza kwani baba yake wakati akimwingilia alikuwa akimkaba kooni ili asipige kelele.

“Yeye alijua anafanya kosa, akawa akiniingilia huku ananikaba koo nisipige kelele. Nilikuwa nasikia maumivu makali balaa,” alisema binti huyo.

ALIWAAMBIA MAJIRANI LAKINI WALIOGOPA KUMVAA BABAKE
“Kingine kilichonifanya nitorokee Tanga kuwaambia ndugu zake ni kwamba, niliwahi kuwaambia majirani kuhusu mchezo wa baba lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza kwa vile wanamuogopa,” alisema.

MAMA MZAA BABA AAMBIWA KILA KITU
Zaina alizidi kusema kuwa, baada ya kufika Tanga  alimweleza kila kitu bibi yake (mama mzaa baba’ke). 

Bibi huyo kwa sababu ni mzazi alimwita mwanaye na kumkanya kisha akafanyiwa mambo ya kimila ili kuondoa balaa hilo la baba mtu kutembea na mwanaye wa kumzaa la sivyo kwa mila za kwao ukoo mzima ungesambaratika.

BABA MTU AONDOKA TANGA USO UMEMSHUKA, YEYE AGOMA
“Baada kufanyiwa mambo ya mila, baba aliniambia turudi Dar lakini nilikataa kwa sababu niliamini tutakapofika bado atataka kuniingilia tena. Nasema hivyo kwa sababu pia baba amewahi kufanya mapenzi na dada’angu anaitwa Hamida mpaka akampa mimba.

“Huo ukatili wote alikuwa akitufanyia kwa nyakati tofauti tofauti, dada alipopata mimba siku moja alimwibia fedha ili akaitoe, alifanikiwa na akakimbia nyumbani, sijui alipo,” alisema.

Akaendelea: Basi, niliamua kubaki kwa bibi, lakini kuna siku alikuja mtu aliyekuwa anatafuta msichana wa kazi ‘hausigeli’, mimi nikakubali, nikaenda Moshi ambako nilikaa kwa muda.
Inatoka Uk. 2

“Hivi karibuni nilirudi Dar na kufikia kwa jirani, sikutaka kwenda nyumbani kwa baba, namuogopa atataka tena. Huyu jirani niliyefikia kwake, mtoto wake ni rafiki yangu tulikuwa tunasoma naye. Hapa nilipo natafuta msaada wa kumpata mama yangu mzazi. Kama atabahatika kulisoma gazeti hili namuomba anifuate jirani na kwa baba atanipata,” alisema Zainab.

Zainab hakuishia kwenye kufikia kwa jirani tu, anasema akiwa hapo jirani huyo kesho yake alimpeleka serikali za mitaa ili kutoa taarifa kuwa amerudi kwa vile alitafutwa kwa muda mrefu kwenye shule aliyokuwa akisoma.

MWENYEKITI WA MTAA AKIRI ZAINAB KUBAKWA NA BABA’KE
Naye mwenyekiti wa mtaa wa eneo hilo, Demetrius alikiri kumpokea mtoto huyo na kumsimulia yote kuhusu baba yake ambapo aliambatana naye hadi Kituo cha Polisi Mbezi kwa Yusuf kwa lengo la kutoa taarifa ili mzee huyo achukuliwe hatua za kisheria. Alisema binti huyo alifunguliwa jalada la kesi KMR/RB/114/2013  UCHUNGUZI.

BABA ANASEMAJE?
Baada ya kumalizana na binti huyo aliyeungwa mkono na mwenyekiti huyo, mapaparazi wetu walizungumza na baba mtuhumiwa ambapo alikuwa na haya ya kusema:

“Si kweli, huyo mtoto ananisingizia tu, mimi siwezi kufanya kitu kama hicho na binti yangu wa kumzaa hata siku moja.


-Gazeti  la Ijumaa  via  GPL


Huu wimbo hatari tupu.Inaelezea maisha ya Diamond kabla hajatoka kimuziki.Dogo aloimba anadai Diamond ni ndugu yake wa damu na hakumbuki alipotoka.Duuh kaongea mambo mengi sana.Sina mbavu kwa kweli.Isikilize hapa Chini.Ni balaa tupu.Ni bonge moja la Ngoma.

Polisi wa kimataifa Interpol, wamemuweka mwanamke aliyeshukiwa kuongoza mashabulizi ya kigaidi nchini Kenya raia Muingereza Samantha Lewthwaite, kwenye orodha ya watu wanaosakwa sana duniani.


Hatua hii ni kutokana na ombi la serikali ya Kenya kwa Interpol.

Anajulikana kama "white widow", na amehusishwa na kundi la kigaidi la Al Shabaab nchini Somalia.Bi Lewthwaite, mwenye umri wa miaka 29, ni mjane wa mlipuaji aliyefanya shambulizi la kujitoa mhanga mjini London Uingereza mwezi Julai mwaka 2005
Polisi wa Interpol hata hivyo hawakuhusisha hatua ya kumsaka Samantha na shambulizi la kigaidi dhidi ya jumba la maduka la Westgate mjini Nairobi lililowaua watu 67.
Hata hivyo, hatua hii ya kumsaka Bi Lewthwaite inakuja punde baada ya shambulizi hili la kigaidi nchini Kenya.
Al-Shabab ilikiri kufanya mashambulizi hayo yaliyotokana na kutekwa kwa jengo la Westgate na kisha kutekwa kwa raia wa kawaida waliokuwa ndani ya jengo hilo kwa siku nne.
Kwa mujibu wa polisi wa Interpol, mwanamke huyo anasakwa na serikali ya Kenya kwa kumiliki mabomu na kupanga njama ya kufanya mashambulizi kuanzia Disemba mwaka 2011.
Ikiwa mwanamke huyo atakamatwa katika nchi mwanachama wa Interpol, atazuiliwa na kusibiri kupelekwa katika nchi anayotakikana kwa kesi kufunguliwa dhidi yake.
Bi Lewthwaite anajulikana kwa jina bandia la, "Natalie Webb" –na alikuwa anasakwa kwa madai ya kumiliki hati bandia ya usafiri nchini Afrika Kusini.
Ni mjane wa Germaine Lindsay, mmoja wa washambuliaji wanne waliohusika na shambulizi la kigaidi mjini London ambapo watu 52 waliuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa.
Msanii wa kizazi kipya nchini Tunisia, Ahmed Ben Ahmed, anayejulikana kwa jina la kiusanii, Klay BBJ, amehukumiwa 
jela kwa miezi sita kwa kuwatusi maafisa wakuu kupitia
 kwa muziki wake.
Mahakama ilitupilia mbali kesi yake ya rufaa baada ya yeye na mwanamuziki mwenzake kupatikana na hatia mwezi jana ya kuwatusi maafisa wakuu katika tamasha la muziki eneo la Hammamet.
Wawili hao awali walihukumiwa bila ya wao kuwepo mahakamani kutumikia kifungo cha miezi 21 lakini hukumu hiyo iliondolewa.
Weld El 15, aliyepatikana na kosa kwa kuimba wimbo wake huo, kuwa 'Polisi ni Mbwa', hakukata rufaa na sasa yuko mbioni.
Hata hivyo Kaly BBJ lisema kuwa wimbo wao ulikuwa unaelezea hali ilivyo nchini Tunisia na kuhusu serikali.
Muungano wa vyama unaoongozwa na chama cha wanasiasa waisilamu wenye msimamo wa kadri, Ennahda, uliingia mamlakani baada ya mapinduzi ya kiraia yaliyomwondoa mamlakani aliyekuwa rais Zine el-Abidine Ben Ali mwezi Januari mwaka 2011 na uchaguzi kufanyika baadaye mwaka huo.
Klay anasemekana kuambia mahakama kuwa wimbo wao unakosoa hali ya sasa serikalini na kote nchini Tunisia tu.
Alisema yeye ni mmoja wa wanamuziki wanaokosoa sana serikali na ndio maana wamekuwa wakimsaka sana.
Lakini majaji walikataa rufaa aliyowasilisa na kusema hukumu yake ya miezi sita gerezani inastahili kuanza mara moja.

Wakili wake alisema kuwa watawasilisha rufaa nyingine kupinga hukumu dhidi yake.