advert

http://

Thursday 6 June 2013

Uvivu wamponza Mr Nice,atimuliwa Kenya.


Msanii kutoka Tanzania aliekuwa akifanya kazi chini ya Lebo ya Groundpa Records kutoka nchini Kenya Mr Nice ametoshwa na lebo hiyo kwa kuvunjiwa mkataba wa kazi,alikuwa amesaini chini ya Groundpa Records.
Kwa mujibu wa Groundpa Records wametoa sababu zilizowasukumua kumpiga chini Mr Nice kuwa ni msanii Mvivu,asie na ushirikiano wala kuaminika mbali na sababu hizo waliendelea kusema kuwa amekuwa akitumia vibaya pesa apatazo baada ya kufanya show,amekuwa bingwa wa kuwapa watu ofa za pombe
lakini sababu kubwa waliyoisema ni kwamba alikuwa amesaini mikataba miwili ni ule aliosaini kwa Lamar kutoka Tz na Sallam Sharaf CEO of Grandpa Records Refigah amesema kuwa Mr Nice amemkatisha sana tamaa na hamuitaji tena katika Lebo yao ya Groundpa tena maana habebeki.

Karibu nyumbani Morogoro Ngwear,leo tunakupokea kwa nyimbo za maombolezo,Hayo ni maneno ya Afande Sele aliyoyasema kwa huzuni kubwa mwili wa marehemu ilipowasili.

Msanii wa muziki wa Hip Hop bongo anaeishi Morogoro na kufanya shughuli ya Muziki akiwakilisha Mkoa wa Morogoro Afande Sele The King amewakaribisha watu wanaofuatana na Mwili wa Marehemu Albert Mangwear kwa ajiri ya kumpumzisha katika makazi yake ya kudumu kesho.
“Karibu nyumbani morogoro Ngwear leo tunakupokea kwa nyimbo za maombolezo, may your Soul Rest in Peace”
Mwili wa Msanii Ngwear umeagwa Leo jijini Dar es salaam katika viwanja vya Leaders na kupewa heshima ya mwisho na watu wengi waliojitokeza katika viwanja hivyo,baada ya kutoa heshima ya Mwisho mwili ulianza kusafirishwa kutoka Dar es salaam na kuelekea Mjini Morogoro kwa ajiri ya mazishi yatakayofanyika siku ya Kesho alhamisi ya Tarehe 6 June.