advert

http://

Tuesday 29 October 2013

RAY C AWA BONDIA,AMTWANGA HUYU DADA WA BONGO MOVIE.


Na Musa Mateja
KATIKA hali ya kushangaza, siku chache baada ya kuripotiwa kupona na kuacha matumizi ya madawa ya kulevya, mwanamuziki Rehema Chalamila ‘Ray C’ anadaiwa kugeuka mwanamasumbwi na kumpa kipigo mwigizaji Nuru Nassoro ‘Nora’, Ijumaa Wikienda limenyetishiwa.



Kwa mujibu wa shuhuda wetu, tukio hilo lilijiri wiki iliyopita ndani ya studio moja ya kurekodia muziki iliyopo Kinondoni, Dar ambapo wawili hao walikutana walipokwenda kurekodi ngoma zao.
Ilidaiwa kuwa akiwa studio hapo, Nora alikutana na Ray C ambaye pia alizama mahali hapo bila mawasiliano na prodyuza anayemtengenezea ngoma mpya.


Chanzo hicho kilipasha kuwa baada ya Ray C kuingia studio hapo alimkuta prodyuza huyo akiandaa ngoma ya Nora ambapo alihoji kilichompeleka mwigizaji huyo mahali hapo.

Ilidaiwa kuwa prodyuza huyo ambaye jina halikupatikana alimwambia Ray C kuwa Nora alifika kurekodi wimbo wake.

Ilisemekana kuwa Ray C hakuridhishwa na majibu hayo, akaomba asikilizishwe ngoma hiyo ya Nora lakini baada ya kusikiliza ilidaiwa kwamba Ray C aliiponda mbele ya Nora, jambo ambalo mwigizaji huyo hakufurahishwa nalo.
Ilidaiwa kuwa Nora alipandwa hasira na kujikuta akimjibu mbovu Ray C.

Habari ziliendelea kutiririka kuwa siku hiyo walimalizana kwa kusonyana na siku iliyofuta walikutana tena studio hapo ambapo Ray C alidaiwa kutinga akiwa ‘masanga’.
Ilisemekana kuwa alipomuona Nora alianza kumpa vijembe, jambo lililosababisha Nora kushikwa hasira ndipo wakavaana na kuzichapa.

Hata hivyo, ilidaiwa kuwa Ray C ndiye aliyeibuka bingwa wa ndondi hizo kwa kumtwanga Nora hadi kumvimbisha jicho kabla ya maprodyuza na watu wengine kufanya kazi ya ziada kuwaamulia.
Ilisemekana kuwa baadaye Ray C alitolewa nje ndipo akahamishia hasira kwenye gari la Nora aina ya Toyota Vitz kisha akalivunja kioo na kutambaa zake.

Baada ya kupenyezewa ‘niuz’ hizo gazeti hili lilimtafuta Nora ambaye alikiri kutokea kwa sekeseke hilo huku akibainisha namna alivyoumizwa jicho lake na kuvunjiwa kioo cha pembeni cha gari lake.
Aliongeza kuwa siku hiyo alipoteza pochi wakati wa ugovi huo.

“Ray C alinikuta studio nikifanya wimbo, kilichonishangaza baada ya kuniona tu alibadilika ghafla.
“Nilijua angenishauri kwa kuwa ndiyo ninaanza gemu kumbe mwenzangu alifikiria vingine,” alisema Nora na kuongeza:
“Mbali na kuniumiza jicho lakini alinifanyia mambo ya ajabu sana, kama kusingekuwa na watu wa kutuamulia basi chochote kingetokea.

“Sikwenda kuripoti polisi. Niliamua kusamehe kwa sababu kuna watu walinisihi niachane naye kwa sababu bado kuna mambo yanamwendesha. 

Kwa upande wake Ray C alitafutwa kwa kila njia kupitia simu ya mkononi na kumvizia studio lakini hakupatikana hivyo juhudi za kumpata zinaendelea.


Source:GPL



Msanii wa Hip pop Ney wa mitego 'TRUE BOY' Amewaonyesha uso wa mbuzi Basata ambao awali walimwonya kutokana na tabia yake ya kuvaa mlegezo "KATA K" akiwa jukwaani kwa madai ya kuidhalilisha sanaa hiyo..


Katika hali ya kushangaza kabisa Msanii huyo ameonekana kupuuzia agizo hilo la basata na kendelea kuvaa mlegezo wakati akilishambulia Jukwaa huku akishangiliwa na mashabiki lukuki wa Bongo Fleva .


Tukio hilo lilitokea jana wakati wa Show ya FIESTA DAY 2 iliyofanyika kwenye viwanja vya Leaderz Club alipokuwa akiwapagawisha wapenzi wake na kibao chake cha "MUZIKI GANI" Akiwa sambamba na Msanii mwenzake Diamond Platinumz.

Sasa wapenzi wa Bongo fleva wanasubiri Rungu la Basata liweze kufanya kazi yake huku wengi wakionekana kumtetea kwa kudai kuwa kila mtu ana aina ya maisha yake 'Life Style'

Leo hii rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete amehudhuria msiba wa Balozi Abrahamu Sepetu (Baba mzazi wa Wema Sepetu) uliotokea hapo juzi jijini Dar es Salaam.


Mheshimiwa kiwete amefika msibani akiongozana na mkewe hapo kutoa pole kwa familia hiyo kwa  kuondokewa na Balozi Sepetu ambaye hapo alishawahi kushika nyadhifa mbalimbali kwenye serikali nchini ikiwemo ya kuwa waziri wa mambo ya nje kwenye miaka ya sabini (70) kabla  ya kuwa balozi wa urusi kwenye kipindi cha miaka ya 80. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Mchumba huyo wa mtu aliyejitambulisha kwa jina moja la Diva alitoa kali ya mwaka baada ya kuzimia ghafla huku akitokwa na mapovu kinywani baada ya kunaswa na OFM akijiuza. 


Tukio hilo lilitokea wiki iliyopita maeneo ya Kimboka, Buguruni, Dar ambapo msichana huyo pamoja na ‘madadapoa’ wenzake walikuwa wakifanya biashara hiyo haramu bila kificho.

Mara baada ya kuona wenzake wakiwa mikononi mwa nguvu za dola katika kamatakamata ya polisi, mrembo huyo ambaye baadaye alijitambulisha kama mchumba wa mtu, alianguka ghafla na kuzimia kiasi cha kuzua hofu miongoni mwa machangu wenzake walioangua kilio wakidhani mwenzao amekata ringi (kufa).

Baada ya muda msichana huyo alirejewa na fahamu akiwa mikononi mwa polisi na kuanza kuangua kilio akiomba asikamatwe kwa kuwa yeye ni mchumba wa mtu na atakuwa kwenye wakati mgumu kama mchumba’ke atajua anajiuza.

“Naomba msinikamate. Mimi ni mchumba wa mtu afande. Mtaniweka kwenye wakati mgumu kama akijua nilikuwa nikijiuza. Jamani nitamkosa mchumba wangu Luka,” alisema mrembo huyo huku akiomba maji ya kunywa.

Hata hivyo, kilio chake hakikuwazuia ‘OFM’ kufanya kazi yake ndani ya Kituo cha Polis.


GPL

Katika mahojiano yake na gazeti moja hapa jijini nimesikia aunt lulu akisema wanaume wamemla sana uroda bure kwa miaka mingi sana bila faida, 


ila kwa sasa harudii kosa hilo ni mwendo wa faranga kwa kwenda mbele, sincerely kwa hizo pics hapo juu nani anaweza akawa na mwanamke kama huyu and shower her dollazzzz?? men also haaaaa as they say one man's meat is another man's poison.

 kwahio tusiliongelee sana ila wakati mwingine maneno tunayaongea ktk media yanafanya wasanii waonekane kituko katika jamii kabisa na akili zako na unajitambua wewe ni msanii  unaweza ukaongea pumbaless kama hii na watu wakasoma na kukuelewa ??

WANAUME WAMENILA URODA BURE MIAKA MINGI SANA BILA FAIDA SASA HIVI SIRUDII KOSA NG'OO: ANT LULU!

hiki ni nini wajameni? nikisema mtasema Sintah anaongea?? niko hapa kwaajili ya kurekebisha watu na jamii inachukulia wasanii kama kioo chao, sasa kwa matendo haya ya lulu na alivyoongea wengine tunaonekana vipi,

ni wakati umefika sasa tujue kuna wasanii na wanaotafuta umaarufu ili ya kwao yawaendee eg kupata mabwana na wanawake 

yaani nimekereka sana na hii kauli ya Aunt Lulu so sasa hivi anauza rasmi na ameamua kujitangaza kama tunavyojua biashara ni matangazo ?? God  forbid.


i do the seeking n u do the judging...

Gari la Madam Rita, Mercedes Benz lateketea kwa moto likiwa barabaraniGari aina ya Mercedes Benz la Rita Paulsen aka Madam Rita limeteketea kwa moto likiwa barabarani Jumamosi iliyopita, Oct 26.
Hata hivyo kwenye gari hilo lililozimika barabarani na kuanza kuwaka moto, hakuwemo Madam Rita bali dereva wake, Julius Kanwakaita.
Chanzo kilichopelekea gari hilo kuwaka moto hakijafahamika mara moja.
August 21 mwaka jana, ofisi za kampuni yake ya Benchmark Productions zilizopo Mbezi Beach ziliteketea pia kwa moto

Daktari wa Michael Jackson Aliyekuwa daktari wa mfalme wa Pop duniani marehemu Michael Jackson, Conrad Murray ameachiwa huru baada ya kukaa jela miaka miwili kwa kosa la kusababisha kifo cha Michael bila kukusudia.
Dr. Murray ambae mwaka 2011 alihukumiwa kifungo cha miaka minne jela, kifungo  ambacho mama yake Michael Jackson alisikika akisema kwa uchungu mahakamani hapo “haitoshi”, ameachiwa huru mapema kutokana na mwenendo wake katika kutumikia kifungo hicho.
Kuachiwa kwa Murray mwenye miaka 60, huenda kukaikasirisha zaidi familia ya Michael Jackson na mashabiki wake ambao wanaamini kifo chake kilisababishwa na daktari huyo.
Kwa mujibu wa Sky News, bado mahakama imezuia kutumika kwa leseni yake ya udaktari katika majimbo matatu ambayo alikuwa akifanyia kazi hapo awali.
Lakini ripoti kutoka kwa watu wa karibu wa Murray zinadai kuwa huenda akafuatilia kwa undani uamuzi huo na kufanya jitihada za kuzirejesha utumikaji wa leseni yake katika majimbo hayo.
Conrad Murray alifungwa jela baada ya kukutwa na hatia ya kusababisha kifo cha Michael Jackson mwaka 2009, kwa kumpa dawa zilizomzidi nguvu (Overdose) na kupelekea kifo chake.

source:Times fm.


Linex azipa likizo ya miezi minne kumbi za Dar, asema hatofanya show kwenye kumbi za Dar hadi February mwakaniMkali wa mashairi yenye ujumbe mzito Linex Sunday, ameamua kuzipa likizo kumbi za bongo kwa muda wa miezi minne kuanzia leo (October 28,2013) hadi February 14,2014. Ambayo itakuwa siku yake ya kuzaliwa.
Mwanahisa huyo wa kampuni ya Kigoma All Stars ameweka katika maandishi uamuzi wake kupitia Instagram jana, muda mfupi kabla hajapiga show ya mwisho kwa mwaka huu aliyoifanya jana usiku Club Billicanas.
“[ @ ] linexsundaymjeda Najiandaa kwenda bills kwenye show ya Bob jr show ambayo itakua ya mwisho kufanya kwenye club za dar mpaka next year 14/2/2014 siku ambayo itakua ni b day yangu na siku hiyo ntaitumia kuintroduce Muziki wangu mpya ambao kila mtu atanishangaaa so kama uko dar lets meet there#Voa”. Ameandika Linex.
Uamuzi wake unaweza kukupa maswali mengi, kwa nini hivi, lakiini katika post yake ya pili, Sunday Mjeda alisisitiza na kutoa sababu kwa ufupi, “Yah sure Najipanga#Voa”


Chris Brown anaweza kufungwa jela miaka minne baada ya kumpiga mtu ngumi na kumchana puaMwimbaji wa ‘Fine China’ Chris Brown, ametupwa selo za polisi huko Washington, D.C, baada ya kumpiga mtu mmoja asiyemfahamu na kumjeruhi usoni.
Kwa mujibu wa TMZ Chris  na mlinzi wake walikamatwa jumapili asubuhi, na kwamba Chris alimpiga ngumi usoni mtu huyo majira ya saa kumi na nusu alfajiri nje ya hotel baada ya kutokea hali ya kutoelewana kati yao.
Mtu huyo aliyepigwa na Chris aliiambia TMZ kuwa ngumi ya Chris imepasua pua yake na inambidi leo (jumatatu) aende hospitali kufanyiwa upasuaji.
 Amesema yeye sio shabiki wa Chris na alikuwa anawapiga picha wasichana wawili ambao walikuwa wanapiga picha mwimbaji huyo nje ya hotel, na haelewi ni kwa nini Chris alikuwa kichaa vile na kumshambulia.
Hata hivyo mtu huyo amesema angeweza kumsamehe Breezy kama angeomba msamaha pale pale, lakini sasa hivi atamfunguliaa kesi dhidi yake na tayari ameshampata mwanasheria.
Lakini chanzo ambacho kiko karibu na Chris Brown kimesema kuwa mtu huyo hakuwa anataka kupiga picha nje ya hotel, bali alikuwa anataka kuingia kwenye ‘tour bus’ ya Chris ili apige picha akiwa ndani, na mwimbaji huyo alikuwa anajaribu kumzuia.
Kwa mujibu wa sheria za Washington, D.C, endapo Chris atapatikana na hatia anaweza kufungwa jela miaka minne.
Tukio hili linamuweka matatani zaidi mwimbaji huyo ambae bado yuko katika probation ya adhabu aliyopewa baada ya kumpiga mpenzi wa zamani ‘Rihanna’mwaka 2009.
Hii inaweza kutumiwa na mahakama kuwa Breezy amekiuka masharti ya probation hiyo.

Muhudumu wa kiume wa baa moja maarufu iliyopo Posta Jijini Dar hivi karibuni alinaswa akifanya ufuska kwa kumnyonya maziwa hadharani mteja wake wa kike.
 
Tukio hilo ambalo lilishuhudiwa pia na wahudumu wa baa hiyo  lilitendwa  na  jamaa  huyu  kwa  mrembo  ambaye  alionekana  kunywa  pombe  kupita kiasi , hali  iliyomfanya  asijitambue
 
 1
Kijana huyo aliyefahamika kwa jina la Emmanuel Chambuso alijikuta kwenye wakati mgumu baada ya menejaa wake kufika na kushuhudia tukio hilo, hali  iliyomlazimu  meneja  huyo  kuchukua   uamuzi  mgumu  wa  kumtimua  kazini.

Rapper Young Killer anampango wa kuingiza hizi T Shirt sokoni hivi karibuni ila anachosubiri ni Mtazamo wa mashabiki zake kuhusu T Shirt Hizi.

Diamond kuja na video ya Diamond Platinumz anaendelea kuuongezea maisha marefu wimbo wa ‘Number One’, baada ya kuifanya Remix ya wimbo huo na msanii toka Nigeria ‘Davido’ ikiwa na muunganiko wa style ya ‘Ngololo’ na ‘Skelewu’, sasa ameamua kuwa serious zaidi na kufanya video ya ngoma hiyo (remix).
Diamond amefunguka kuhusu kuwepo kwa video hiyo kupitia Instagram, ambapo ameonesha pia nia ya kuwaalika watu ambao wanapenda kuwa sehemu ya video hiyo, ‘Do you wanna be a part ov it..? Aliuliza Diamond.
Kwa maelezo ya Diamond aliyoyaweka jumamosi kwenye Instagram, video hiyo ilitakiwa kufanyika jana jumapili, lakini hakuna taarifa za kufanyika video hiyo hapo jana, huenda video hiyo ikafanyika leo.
C.E.O wa Wasafi, aliweka picha inayoonesha yuko studio na 'Skelewu hit maker' Davido wakiipika remix ya Number One.
"[ @ ] diamondplatnumz I said NGOLOLO Dance, and he said Nah man! SKELEWU Dance... then we decided to put it in a song....and show each other what we gat, we are on tommorow for the new Video #NumberOneRemix @Diamondplatnumz ft @lifeofdavido .. Do you wanna be a part ov it...?" Aliandika Diamond.

Baada ya uchaguzi uliofanyika kwenye ukumbi wa NSSF Water front kumpata Rais mpya wa TFF kati ya Athumani Nyamlani na Jamal Malinzi, hatimaye TFF imepata Rais mpya ambaye ni Jamal Malinzi.
Mashuhuda waliokuwepo hapo ukumbini wanasema kwamba mpinzani wa Jamal Malinzi alitoka kabla ya utaratibu mzima wa uchaguzi kuisha. Baada ya matokeo kutangwaza Jamal Malinzi alimzidi kura Athumani Nyamlani na hatimaye kupata nafasi ya kumrithi Leodigar  Tenda.

Kama ulikuwa hujui ni kwamba  Rais huyu wa TFF Jamal Malinzi ndiyo baba wa Diva Loveness wa Ala za Roho ya Clouds FM

Timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania kwa vijana chini ya miaka 20 imeanza vizuri kampeni zake za kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia 2014 kwa vijana chini ya miaka 20 baada ya kuichapa Msumbiji 10-0 katika mechi iliyochezwa jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Vijana hao wa Tanzania waliianza mechi hiyo kwa kasi, ambapo katika dakika ya 6 walipata bao la kwanza lililofungwa na Neema Paul baada ya kupata pasi ya Therese Yona.

Mfungaji wa bora wa mashindano ya Airtel Rising Stars yaliyofanyika

Nigeria mwaka huu, Shelder Boniface aliiandikia Tanzania bao la pili katika dakika ya 24.

Kama hiyo haitoshi, vijana wa Tanzania walizidi kulisakama lango la Msumbiji, ambapo katika dakika ya 32 Tanzania ilipata bao la tatu ambalo lilifungwa na Deonisia Daniel kwa mpira wa faulo uliokwenda moja kwa moja nyavuni.

Katika dakika ya 41 vijana wa Tanzania ambao waliibuka mabingwa kwa upande wa wanawake katika mashindano ya Airtel Rising Stars yaliyofanyika Nigeria walipata bao la nne ambalo lilifungwa na Amina Ali kwa shuti kali akiwa nje ya 18.

Vijana hao wa Tanzania walifunga bao katika dakika ya 45, lakini likakataliwa na hivyo kwenda mapumziko ikiongoza 4-0.

Kipindi cha pili Tanzania ilianza kwa kasi tena na kupata bao la tano katika dakika ya 47 ambalo lilifungwa na Neema Paul baada ya kuunganisha kwa kichwa krosi ya Therese Yona.

Tanzania ilipata bao la sita ambalo lilifungwa na Shelder Boniface baada ya kumalizia mpira uliotemwa na kipa wa Msumbiji kutokana na shuti la Stumai Abdallah.

Dakika ya 82, Tanzania iliandika bao la saba lililofungwa na Amina Ali kwa shuti kali, pia dakika 86 Tanzania iliandika bao la nane kwa mkwaju wa penalti iliyofungwa na Deonisia Daniel baada ya Shelder kuangushwa katika eneo la hatari.


Vijana hao wa Tanzania hawakutosheka na ushindi kwani katika dakika ya 89 walipata bao la tisa lililofungwa na Amina Ali, pia katika dakika ya 90 walifunga bao la 10 lililofungwa na Stumai Abdallah.


Kwa taarifa tulizozipata hivi sasa ni kwamba Jamal Malinzi ameshinda kitu cha urais wa shirikishi la soka nchini TFF baada ta kumshinda mpinzani wake Athumani Nyamlani.


Pia Wallace Karia amewabwaga Iman Madega na Ramadhan Nassib katika kiti cha umakamu, kwa taarifa zaidi endelea kutembelea mtandao huu