advert

http://

Wednesday 22 May 2013

Upinzani walaani uvamizi Uganda


Upinzani walaani uvamizi Uganda


Ofisi za Gaeti la Daily Monitor zilizovamiwa na polisi wa Uganda
Mkuu wa majeshi wa zamani nchini Uganda ambaye sasa ni kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for democratic Change FDC Meja Generali Mustaafu Mugisha Muntu amelaani hatua ya sasa ya serikali ya amiri jeshi mkuu wake wa zamani ya kuandama na kuzingira ofisi za magazeti ya The Daily Monitor pamoja na Redpepper.
Akiongea na waandishi wa habari nchini Uganda, Bwana Muntu alisema kuwa Rais Museveni anahofia kuwa udhibiti aliokuwa nao kwa vyombo vya usalama na ulinzi umeanza kusambaratika na hivyo kumtia hofu zaidi Museveni.
Polisi nchini Ugandan waJumatatu walivamia ofisi za magazeti kufuatia taarifa kwamba Rais Yeweri Museveni anamuandaa mwanawe wa kiume kumrithi urais.
Vituo viwili vya Redio pia vilivamiwa na kuzimwa , hii ni kwa mujibu wa gazeti la serikali la New Vision.
Wiki iliyopita magazeti ya Uganda yalidai kuwa kuna njama za kuwaua wale watakao pinga mpango wa Rais Museveni kumuandaa mwanawe kuchukua madaraka ya Uganda.
Magazeti hayo yalidai kuwa mipango hiyo ya mauaji yalitolewa na Mkuu fulani wa jeshi la Uganda.
Bwana Museveni, ambaye amekuwa madarakani tangu 1986, anatarajiwa kung'atuka uongozini mwaka 2016.
Kwa muda mrefu kumekuwa na madai kwamba Museveni anamuandaa mwanawe Muhoozi Kainerugaba,ambaye ni brigadier jeshini kushikilia uongozi wa Uganda.
Lakini serikali ya Museveni imekanusha kwamba kuna mipango kama hiyo.

Mwanawe Museveni Brig. Kainerugaba.

Wiki iliyopita gazeti la, the Daily Monitor,na jengine la , Red Pepper, lilichapisha barua ya siri ikidai ilikuwa imeandikwa na Jeneral David Sejusa, ikitaka uchunguzi ufanywe kuthibitisha madai kwamba kuna mipango ya kuwauwa wote watakao piga mipango ya Rais Museveni kumpachika mwanawe uongozini.
Uvamizi huo wa polisi umeidhinishwa na mahakama ya Uganda na ulikuwa unalengo la kutafuta barua hiyo inayodaiwa kuandikwa na mkuu huyo wa Jeshi akifichua njama za mauaji.
Vituo viwili vya Redio vinavyohusiana na Daily Monitor, Dembe FM na KFM, pia vilivamiwa na kuzimwa.

Rais Yoweri Museveni
Mkurugenzi Mkuu wa Daily Monitor Bwana Alex Assimwe aliambia BBC kwamba Chumba chao cha Habari kilivamiwa na polisi wapatao 50 waliojihami kwa silaha.
Lakini wachanganuzi wa maswala ya kisiasa wanadai kuwa ikiwa barua ya Jenerali Sejusa ni ya kweli basi ni dalili kuwa kuna hali mvutano ndani ya jeshi huku ikidhaniwa kuwa wanajeshi wakongwe huenda wanapoteza uwezo kwa wanajeshi chipukizi wanaoongozwa na mwanawe Museveni Brigadia Kainerugaba.
Jenerali Sejusa ni mwanajeshi mkongwe aliyekuwa katika vita vya ukombozi uliyomuweka Rais Museveni madarakani mwaka1986.
Kwa muujibu wa taarifa za AP kamanda mmoja wa jeshi Jenerali Aronda Nyakairima amenukiliwa akisema kuwa Jenerali Sejusa kwa wakati huu anachunguzwa kutokana na barua anayodaiwa kuiandika.

Wengi wafariki kufuatia Kimbunga, Oklahoma


Kimbunga kikubwa kimepiga Jimbo la Oklahoma, nchini Marekani na kuharibu kabisa mitaa.
Maafisa wanasema zaidi ya watu tisini wamefariki, wakiwemo takriban wanafunzi ishirini ambao shule yao ya msingi iliporomoka.
watoto wakipata tabu
ana
Wanafunzi wengine wanahofiwa kufunikwa na vifusi.
Kimbunga hicho kilipiga mji wa Moore kwa takriban dakika arobaine, na kurusha magari katika vifusi vya nyumba na maduka.
Rais Obama ametangaza hali ya mkasa mkubwa na kuahidi usaidizi wa serikali kwa utawala wa jimbo hilo.
Takriban watu 120 wanaendelea kupokea matibabu hospitalini
Masaa kadhaa baada ya Kimbunga hicho kupiga, shughuli za kuwatafuta manusura ingali inaendelea.
Wanatumia mashine kubwa kujaribu kuwatafuta waliokwama chini ya kifusi ili kuwaokoa.
Mji wa Moore ulipigwa na kimbunga kikubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa kwa muda wa miaka 14 wakati kimbunga kingine kikubwa kilipopiga eneo hilo.
Watu wengine zaidi wanajulikana kuuawa katika Kimbunga hicho.
Hospitali zimekuwa zikiwapokea majeruhi , wengine wakiwa katika hali mbaya zaidi na maafisa wa utawala wanaonya kuwa idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka.
Maafisa wakuu wa serikali ya jimbo walitakiwa kuungana katika juhudi za kuwasaka manusura usiku kucha.
Kwa mujibu wa afisaa mkuu wa afya, angalau watoto 20 walikuwa miongoni mwa wale waliofariki.
Shule ya msingi ya Plaza Towers ndiyo iliyoathirika zaidi kuliko sehemu zingine , kimbunga kiliharibu paa ya shule na kuangusha kuta zake zote.
Shule nyingine moja pia ilipigwa na kimbunga hicho lakini walimu walifanikiwa kuwaokoa wanafunzi.

Drogba atemwa na kocha wa Ivory Coast


Aliyekuwa nahodha wa timu ya taifa ya Ivory Coast na
didier drogba
nyota wa Chelsea, Didier Drogba, ameachwa nje ya kikosi kitakachoakilisha Ivory Coast kwenye mechi ya kufuzu kwa kombe la dunia dhidi ya Gambia na Tanzania.
Hii ni mara ya pili mtawalia kwa kocha wa timu hiyo Sabri Lamouchi kumuacha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka Thelathini na Tano.
Mchezaji huyo hakuonyesha mchezo mzuri wakati wa fainali za kombe la mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini hatua iliyomlazimisha kocha huyo kumuacha nje ya kikosi chake kilichocheza na Gambia mwezi Machi mwaka huu.
Mlinda lango wa Manchester City, Kolo Toure, vile vile ameachwa nje ya kikosi hicho cha wachezaji 26.
Lamouchi alisema uamuzi huo ni changamoto kwa Drogba kuimarisha mchezo wake ili aweze kujipa nafasi katika timu hiyo ya taifa.
''Drogba ni mchezaji wa kimataifa na mwenye hadhi kuliko mchezaji yeyote wa timu ya taifa, lakini amekuwa na matatizo katika kipindi cha miezi minane iliyopita'' Alisema Lamouchi.

Dalili za Drogba kustaafu?


Licha ya kocha huyo kusisitiza kuwa Drogba, angali na nafasi ya kucheza mechi za kimataifa, wengi wataanza kujiuliza ikiwa mshambuliaji huyo atapata fursa ya kuongeza idadi ya mechi alizocheza na timu hiyo ya taifa, kutoka tisini na sita hasa kutokana na hali yake kwa sasa baada ya kuisaidia klabu yake ya Galatasaray kunyakua kombe la ligi kuu ya soka nchini Uturuki.
Kocha huyo amewaita Romaric N'Dri Koffi

Madrid yathibitisha kuachana na Mourinho


Klabu ya Real Madrid imethibitisha kuwa kocha wa timu hiyo Jose Mourinho ataondoka kwenye kibarua cha kuifundisha timu hiyo mwishoni mwa msimu.

Rais wa klabu ya Real Madrid,Florentino Perez amewaambia waandishi wa habari jumatatu jioni kuwa Mourinho hatofukuzwa bali wamekubaliana kumaliza mkataba wao na kocha huyo raia wa Ureno.
Aidha Madrid, imeongeza kuwa haijaanza mazungumzo na kocha yeyote kwaajili ya kuchukua nafasi ya Mourinho lakini vyanzo mbalimbali vya habari za michezo zinamtaja kocha wa PSG ya Ufaransa, Carlo Ancelloti kuchukua jukumu la kuifundisha Madrid msimu ujao.
Duru za kimichezo zinasema, Jose Mourinho huenda akarejea nchini Uingereza kuifundisha klabu yake ya zamani ya Chelsea baada ya kuwepo makubaliano baina yake na uongozi wa klabu hiyo.