advert

http://

Tuesday 3 December 2013

TAZAMA HII GARI YA AJABU!!



5921_643916678955211_694058705_n-4570-600-600-80Mara nyingi tumezoea kuziona Limousine ndefu kwenye harusi tofautitofauti lakini Range hii ambayo ipo Kenya inaweza kuwa ndio ndefu zaidi kuliko Range zote ambazo zipo Afrika Mashariki ambapo unaweza kutazama picha zake za ndani na nje hapa.
58873_618020604878152_762034716_n-4569-600-600-80
64755_590187184328161_235651424_n-4568-600-600-80
226879_590182380995308_543629288_n-4565-600-600-80 (1)
226879_590182380995308_543629288_n-4565-600-600-80
383670_557935277553352_1184415968_n-4571-600-600-80
529115_615751478438398_1881184687_n-4566-600-600-80
545705_590182444328635_1651343247_n-4564-600-600-80



Admin
Mimi ni Msichana wa Miaka 21 , Nasoma chuo kimoja hapa dar ..nimetokea mkoa niko mwaka wa Pili sasa , huko nilipotokea nina Boyfriend ambae nimekuwa nae kwa muda mrefu toka secondary ila swala mapenzi hatujawahi fanya kwa vile kabla ya kuja chuo nilikuwa Bikira ..


Baada ya kuja chuo naweza sema nimekutana na vijana wajanja na nadiriki kusema sina tena Bikira washaitoa ...Sasa nashindwa ni namna gani nimwambie boy wangu huyo wa mkoa ..Likizo nilienda nikamtega tufanye ili nijidai yeye ndio kaitoa lakini aliniambia tutafanya mapenzi siku ya ndoa ...Naombeni ushauri mie nataka nimwambie kwamba sina tena na tuwe tunafanya mapenzi ..Nitaanzia wapi ? 

CHOAMVA 2013: Uvivu wa Wabongo kupiga kura umemkosesha tuzo AY

Jumamosi ya November 30, tuzo za 10 za video za Channel O aka CHOAMVA zilitolewa huko Kliptown, Soweto (Johannesburg) nchini Afrika Kusini.

Mwaka huu ni AY pekee ndiye alikuwa msanii wa Tanzania aliyekuwa akiwania tuzo hizo. AY alikuwa akishindania kipengele cha video bora ya Afrika mashariki na video bora ya msanii wa kiume Afrika.
Bahati mbaya, AY hakufanikiwa kututoa kimasomaso na P-Unit kuchukua tuzo ya video bora ya Afrika Mashariki. Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa Twitter, utagundua kuwa AY alikuwa akipiga kampeni ya nguvu kuwaomba watanzania wampigie kura. Marafiki zake, wasanii wenzake na vyombo vya habari vilimsaidia pia kuufisha ujumbe huo bila kuchoka.
Kampeni ilikuwa kali kiasi cha kumtia yeye mwenyewe moyo kuwa huenda mwaka huu angeibuka na tuzo pia na kutupa sifa Tanzania. Hata hivyo mambo yalienda tofauti na AY hakufanikiwa kupata tuzo.
Lakini ukweli unaouma ni kwamba, wabongo tumekuwa ni watu wa kuongea bila vitendo. Hakuna ubishi kabisa kuwa Watanzania wengi waliokuwa na uwezo wa kumpigia kura hususan kwenye internet ambako ni bure, hawakufanya hivyo sembuse kwa sms ambako fedha hukatwa?
Tumekosa uzalendo na kupenda vya kwetu. Badala yake tumekuwa ni watu wa kupuuzana na kuchukuliana poa tukiwathamini watu wa nje kuliko wazawa.
P-Unit hawakuwa na nguvu kama aliyonayo AY lakini wamefanikiwa kuitwaa tuzo hiyo kwakuwa Kenya ilikuwa nyuma yao. Tujifunze kuwa nyuma ya wasanii wetu pale wanapokuwa wanahitaji kura zetu kwenye mashindano ya kimataifa kwakuwa bila support ya nyumbani hawawezi kufika popote.
Mpaka sasa AY bado hajasema chochote lakini swahiba wake walienda naye Afrika Kusini, Mwana FA alitoa shukrani kwa niaba yake.
“Tunamshukuru kila mmoja aliyemuunga mkono @AyTanzania kwa namna yeyote ile kwy huu mchakato...haikuwa yetu safari hii!all good,hakuna malalamiko KABISA. Mapambano yanaendelea. Mwaka ujao pia kuna nyingine...na kuna muziki wa kuendelea kufanya..keep listening."
Naye Salama Jabir aliandika: S/O kwa mwanangu @aytanzania na kila mmoja alom support...kwenye macho yangu na yako naamini ni mshindi toka siku ya kwanza. tugange yajayo.”
Ni kweli tugange yajayo kwakuwa ni wasanii wengi tu wakubwa pia waliokosa tuzo mwaka huu.
Stori:  Hamida Hassan na Gladness Mallya
MASKINI! Malkia wa Mipasho Afrika Mashariki na Kati, Khadija Omary Kopa amevamiwa na vijana wahuni wakitaka kumfanyia fujo kwa madai ya kukatiza mitaani akiwa ameongozana na ‘mwaume tata’.
Baadhi ya vijana wakiwa wamelizingira gari alilokuwemo Malkia wa Mipasho, Khadija Kopa na mwanaume aliyedaiwa kuwa tata.
Tukio hilo lilijiri maeneo ya Kariakoo, Dar wiki iliyopita ambapo vijana hao walianza kwa kuzomea wakitaka kumshika mwanaume huyo waliyedai alikuwa amevaa nguo za jinsia ya kike.
Alichokifanya Khadija ni kuingia kwenye gari na kumwambia dereva aondoke haraka kukwepa kufanyiwa vurugu huku mwanaume huyo naye akiungana na malkia huyo kuondoka eneo hilo.
Vijana wakimzingira Khadija Kopa aliyekuwa ameambatana na 'mwanaume tata'.
Wakizungumza na gazeti hili, vijana hao walidai kuwa Khadija alijiabisha kwa kuongozana na mwanaume huyo.
Khadija aliliambia gazeti hili kuwa alishangazwa na tukio hilo lililomkuta na kusema kuwa mwanaume aliyeongozana naye ni mwimbaji mwenzake ambaye pia ni shemeji yake.
Alifunguka: “Hivi kuwa mwimba taarabu wa kiume ndiyo ushoga jamani? Au kuvaa kaptura ya kitenge ni tatizo? Mbona alikuwa amevaa mavazi mazuri tu ya kiume?”
...Vijana wakizidi kulizingira gari alilokuwemo Khadija Kopa.
Khadija alisema kuwa amewazoea mashabiki wake wa Kariakoo kwani huwa wakiwaona mastaa huwa na tabia hiyo na ndiyo maana walianza uzushi huku wakisema kuwa waimba taarabu wote ni wanawake, kitu ambacho si kweli.
“Sikuona sababu ya kuchukua hatua, nilikuwa najaribu kuwaelewesha lakini hawakunielewa, wakazidi kuzomea na kutuzingira ndiyo maana tuliamua