advert

http://

Sunday 27 October 2013

Ney wa Mitego apewa Salaam zake na Baraza la Sanaa Tanzania,apigwa marufuku kuvaa mlegezo.


Ney wa Mitego 1Ney wa Mitego ambae ni staa wa single za ‘muziki gani’ na ‘salamu zao’ amethibitisha kupewa barua na baraza la sanaa Tanzania ikiwa ni onyo la kutoendelea kuvaa suruali mlegezo kwenye majukwaa mbalimbali anayoonekana.

Kwenye interview yake na millardayo.com Ney amesema alipigiwa simu sana na namba moja lakini alikua amelala, alipoamka akakuta missedcalls nyingi so ikabidi apige ndio akaambiwa BASATA kuna barua yake ambapo baada ya kushindwa kwenda alipelekewa Manzese.
Ney anasema ‘sielewe kama BASATA ndio wameamua kudili na milegezo, sijaelewa wao wanaangalia nini zaidi, nimejaribu kuuliza wakasema nikiendelea watanifungia kazi zangu, ni kweli navaa mlegezo lakini kuna vitu vingi sana vya kufanyia kazi wao kama BASATA manake tunaibiwa kazi zetu kila siku mbona hawashughulikii hizo?’ mi tangu niko shule mlegezo ni tatizo langu kubwa ila nitajitahidi kupunguza japo nashangaa nimeandikiwa barua mimi mwenyewe wakati kuna wasanii wanavaa mlegezo hata kuliko mimi’
Ney wa Mitego
Source:Millardayo.



Ukraine ProtestLeo October 26 2013 ndio Wanawake nchini Saudi Arabia wamepanga kuandamana kupinga wao kunyimwa kuendesha magari sehemu yoyote nchini humo ikiwa ni nchi pekee duniani ambayo inakataza Wanawake kuendesha magari hata kama wanaweza.

Unaambiwa kwa sasa Mamlaka za Saudi Arabia zimewaonya Wanawake hao kutoandamana  katika maandamano hayo yatakayokua ya aina yake na ya tatu kutokea nchini humo toka mwaka 1990 ambapo Wanawake kadhaa walikamatwa na wengine kuachishwa kazi, onyo hilo linakwenda pia kwa Mwanamke yeyote ambae amepanga kuendesha gari.
Msemaji wa Serikali amesema Mwanamke yoyote atakae endesha gari leo atachukuliwa hatua za kisheria ambapo wakati siku hii ya kuandamana ikisubiriwa Wanawake kadhaa wa Saud Arabia tayari walishaweka video zao wakiendesha magari sehemu mbalimbali za Saudia lakini mpaka sasa hawajakamatwa.
Mpaka sasa zaidi ya watu elfu 17 wamesain kura ya ndio itakayo waruhusu Wanawake wa Saudi kuendesha magari ambapo pia idadi ya Wanaume wanaosupport imeendelea kuongezeka kwa kasi.
saud arabia 7
saud arabia 8
saudia 4



 Picha Zaidi Ziko Hapa



Kwenye toleo jipya la 25 la jarida la GQ Rihanna anaonekana kwenye cover la jarida hilo kwa style hii. Jarida hili linatoka October 31 2013. Picha zingine ziko hapa.



Dunia ilishtuka miaka 3 iliyopita baada ya rapper Bow Wow kutangaza kuwa amepata mtoto wa Kike. Bow Wow amekuwa akiweka picha za mtoto wake na za Mama yake Miss Joie kwenye account yake ya Instagram kitu kinacho onyesha mahusiano mazuri kati yao.


 Noorah alia na muziki wa bongo, awapinga wanaosema wana pesa nyingi bank, "muziki umekuwa na siasa nyingi"Noorah aka Baba Styles, ambae ni moja kati ya wasanii waliofanya vizuri sana miaka mingi katika kiwanda cha muziki Tanzania, ameutupia lawama mfumo wa game la muziki wa bongo kibiashara.
Mwana Chember ameyatoa ya moyoni wakati akipiga story na Moko Biashara aka One B, katika kipindi cha Bongo Dot Home cha 100.5 Times fm.
Noorah amepiga mahesabu ya gharama na kipato kinachopatikana katika biashara hii ya muziki na kuonesha kwamba uwezekano wa kupata hasara ni mkubwa kuliko uwezekano wa kupata faida.
“Kwanza Industry ya muziki sasa hivi imekuwa kubwa sana, kwa kiasi ambacho kama mtu unataka kufanya muziki sasa hivi…kwa watu tunaofahamika kama sisi, doing music sasa hivi is doing business sio show tu. Lazima uwe unafanya biashara na ili kufanya biashara ni lazima uwe na mtaji mzuri,  kwa sababu kama mtu anapotoa single anakuwa na budget ya kufanya promotion.
“So  vitu kama hivyo vinahitaji budget kubwa sana kwa sababu right now in order to have a good video lazima uwe na sio chini ya 2 to 3 million, na hiyo ni ya director bado hujaingia kwenye maswala ya vifaa, location na kuwahudumia watu wanaoshoot..in short we need money.” Amesema Noorah.
Noorah alihit the point kwa mfano wake mwenyewe, “In short muziki sasa hivi una hitaji pesa, na nikijitazama sasa hivi mimi nimeshatumia zadi ya miaka 11 kwenye entertainment industry, the very same industry, na nikijiangalia kwenye upande wa kipato, yaani hairidhishi.”
Kuhusu watu wanaosema na kuonesha kuwa wana pesa na game linalipa, Noorah akatoa mtazamo wake.  
“Muziki wa sasa hivi umekuwa ni muziki ambao una siasa nyingi, siasa ni kile kitu ambacho unasema hata kama hakiko halisi, lakini unakisema kwa benefit flani ya baadae, kwa hiyo kuna watu ambao right now, we know wanasema kwamba they have a lot of money, lakini lengo la kusema mtu ana pesa ni kwamba kama kwa mfano wewe ni promoter uko kule Geita unamtaka yule msanii kuja kufanya show, na yeye ameshasema kwenye akaunti yake ana sio chini ya million 500 lazima ujiulize kwamba huyu mtu wewe utampa shilling ngapi? Hiyo ni mikakati tu ya kibishara tu. “
Noorah anaamini kama watu wangekuwa na access ya kucheck bank akaunti za wasanii wanaodai kuwa wana pesa nyingi bank, huenda wasikutwa hata na Million 150.
Source:Times fm.
Forbes wamtaja Michael Jackson kuwa namba moja kati ya Celebs waliofariki waliongiza pesa nyingi mwaka 2013, awafunika walio haiMfalme wa Pop, Marehemu Michael Jackson ametajwa na Forbes kuwa ni mmoja kati ya watu maarufu waliokwisha fariki ambao kazi zao zimeingiza pesa nyingi zaidi katika kipindi cha mwaka mmoja kuanzia October 2012 hadi October 2013.
kwa mujibu wa Forbes,Michael Jackson aliyefariki mwaka 2009 akiwa na umri wa miaka 50, ameingiza $160 million, kiasi ambacho ni kikubwa na kimezidi hata kiasi walichoingiza wasanii ambao bado wako hai, ambapo Madonna ndiye mtu maarufu aliyetajwa kuingiza pesa nyingi zaidi kwenye ‘100 Celebrities list’ akiwa ameingiza kiasi cha $125 million.
Hii ndiyo orodha ya ‘Top Earnign Dead Celebrity’ iliyotolewa na Forbes:
  1. Michael Jackson – $160 million
  2. Elvis Presley - $55 million
  3. Charles Schulz -$ 37 million
  4. Elizabeth Taylor - $25 million
  5. Bob Marley - $18 million
  6. Marilyn Monroe -$15 million
  7. John Lennon - $12 million
  8. Bettie Page& mwanasayansi Albert Einstein - $10million (wamefungana)
  9. Steve McQueen& mwandishi wa vitabu Theodor Geisel – 9 million (wamefungana)
  10. 10. Bluce Lee, na Jenni Revera (wamefungana)- $7 milllion

Jose Chameleone ameibuka mshindi kwenye tuzo za BEFFTA, tuzo kubwa za Ulaya kwaajili ya watu weusi ambazo huwatuza watu kwenye burudani, fashion, televisheni na sanaa.

Chameleone alikuwa ametajwa kuwania kipengele cha Best International Act na alikuwa akishindana na wasanii wengine wakiwemo Rihanna na D'Banj.
Tuzo hizo zimetolewa jana Ijumaa na leo Jumamosi pia huko jijini London.
Kupitia Facebook, Chameleone ameandika kuelezea furaha yake baada ya kutwaa tuzo hiyo:
"It's hard to fully express my gratitude towards all of you who appreciate My MUSIC, and love AFRICAN music at large. You are the reason I have managed to add another onto my list and rankings. Am fresh and still jubilating with you This joyous feeling in me i congratulate my fans worldwide, we did this together i have just won BEFFTA AWARDS BEST INTERNATIONAL ACT- DR JOSE CHAMELEONE."

 Makala: Wasanii kuimba juu ya nyimbo zao wakiwa jukwaani Kujifunza au kufanya kazi bora hakuhitaji kutafuta uafadhali, bali kutafuta uhalali wa cheo na dhamana uliyopewa, hicho ndicho nachoamini mimi.
Imani hii ambayo haina dini iliyosajiliwa inanifanya nikubaliane na mtazamo wangu wa kupinga wasanii wa muziki wanaoimba kwa kufuatisha nyimbo zao jukwaani kuanzia mwanzo hadi mwisho, yaani Play back’, wakati mimi shabiki nimelipia kuona anachofanya jukwaani kiuhalisia, sio video shooting.
Cha ajabu kabla ya show utasikia ‘leo ntafanya kweli pale msikose’, ila nikifika nakuta naimbishwa na wimbo ule ule kama msanii anafanya video shooting, kufuatisha tu kile kilichoimbwa huku anafanya mbwembwe.
Huenda tunatofautiana nia na madhumuni ya kuhudhuria show ya msanii flani, mimi kwangu nia hua sio kumuona msanii, bali kumuona anatumbuiza kweli ule wimbo wake ninaokubali hadi nimeuweka kama mlio wa kuniamsha kwenda kazini, na mlio wa kupokelea simu.
 Njia sahihi ya yeye kuperfom mimi simchagulii, lakini ni mwepesi wa kuona makosa ya wazi anayofanya ambayo kwa upande wangu naona hajanitendea haki. Pamoja na kukubaliana na yote na mbwembwe zinazofanyika jukwaani, sauti ya msanii husika kuimba kweli my favourite song pale jukwaani huwa ni kitu nachokipa priority.
Kama shabiki wa show, nimekuwa nikichukizwa na kitendo cha wasanii kuimba juu ya wimbo ‘play back’,mimi binafsi kwa kuwa naamini na naona kuna wengine tena wa level hiyo hiyo wanaimba Live, sio lazima iwe na band lakini angalau wameweka CD yenye beat kavu, ama beat chorus, au beat chorus na back vocal za studio. Hapo nafurahi, kuona energy ya msanii na kupata ladha mpya pale jukwaani.
Mi ni mmoja kati ya watu walioshuhudia performance ya rapper wa Tanzania ‘Webiro Wasira aka Wakazi kwenye Jukwaa la BBA 2013 kwenye Eviction, mwezi July na kuikubali sana show yake, aliimba kweli kama nilivyomuona pia Young Killer, Stamina, Weusi, Nikki Mbishi na wengine wakifanya hivyo.
Bahati nzuri nikakutana na Wakazi na hii ilikuwa ni mara ya kwanza kukutana nae, sasa baada ya salaam ilibidi nimuombe muda tupige story kidogo kwa kuwa nilikuwa na kiu ya kutaka kujua na yeye kama msanii anachukuliaje swala la kupiga ‘Play Back’.
“Kusema ukweli navyoona unapokuwa unafanya kazi kama msanii lazima uoneshe reality na maturity kwamba umekuwa kisanii.” Wakazi alinambia.
 Nilipigia mstari neno ‘reality’ kwa Kiswahili ‘Uhalisia’, na ndicho hicho nachokitaka kwenye show nazolipia mimi. Back vocal zinakuwepo kusapoti, lakini main ni kwake kweli.
 Sasa hivi mimi naona baadhi ya wasanii wa Bongo wamejikita zaidi kutafuta dancers na kulipamba jukwaa na hao dancers, ni kweli wanafanya vizuri, lakini bado sioni kama ni sababu ya wao kuacha kuimba live kwa kuwa wana dancers na wanacheza pia, eti wanachoka sana! Kwangu mimi hainishawishi, mbona wapo wanaocheza na wanaimba pia, au wale wa bendi za dansi wao wanawezaje.
Ama kwa jinsi Young Killer anaweza kuweka pia break dancers na wao wakacheza wakati anaendelea kuimba hivyo hivyo, kama wakazi aliponda na wasichana waliopamba show wakati akikamua kweli.
Nilimuuliza pia Wakazi kuhusu hili, ili nipate wazo la msanii pia kwa sababu mimi ni kama mlalamikaji tu mwenye mantiki lakini.
“Maturity ni pale ambapo unakuwa unafanya mazoezi vizuri na umejidhatiti ili uwe na uwezo wa kucheza na kuimba, na uwe unajua wapi unapumzika na sehemu gani, kwa hiyo unaweza kucheza na ukaimba vilevile.” Wakazi alinipa hii.
Hapo nikapata wazo jingine, baadhi ya wasaniii wengi wa Tanzania tena wakubwa hunishangaza sometimes, pamoja na kutaja kiasi kikubwa cha pesa wanacholipwa kwenye shows, bado utaona wakialikwa sehemu kwenye show watakuja na crew ya watu sita au saba hivi, na kati ya hao utakuta wacheza show 4, na mpiga picha na mpambe wa ziada, hakuna Dj, mtu wa back vocal, mabaunsa wenye miwani mwieusi..! wala hawana muda wa kuajiri mweledi wa mambo ya kuhakikisha sauti zinatoka vizuri ( sound engineer). Hapo ni kama wanaandaa mazingira ya kushindwa kukwepa hiyo ‘Play Back’.
Hapo utasikia wanatoa vijisababu, utasikia amecheza sana hawezi kuimba Live, au vyombo havisikiki vizuri, mic sometimes zinakata sauti.
Hapo naona umuhimu wa kumtaja Profesa Jay na kumpa big up kwa kumtambulisha Dj Choka aliyekuwa Dj wa Choka Mbaya Crew, na pia mtu wake wa back vocal aliyekariri nyimbo nyingi za Profesa, na Dj Choka ameendelea kufanya kazi na wasanii wengine kama AY,Roma, Lady Jay Dee na wengine ambao kwa pamoja wamehakuwa wakihakikisha show zinaenda vizuri kama ‘Live show kweli’.
Nilipata pia mawazo ya Banana Zorro ambae ana uwezo mkubwa wa kuimba Live tena na Band, huku akipiga gitaa. Yeye aliongea kupitia The Chart ya 100.5 Times fm. Lakini yeye alinipa point nyingine tofauti kidogo na mtazamo wangu.
““Unajua kwa kawaida sio kwamba play back ni kitu kibaya, ama play back sio kwamba sio sanaa ama msanii akifanya play back hapaform, bali aina ya jinsi anavyofanya play back. Kwa sababu hata wasanii wakubwa wanafanya play back.”
Napata kigugumizi kidogo kuiga kila wanachofanya wasanii wakubwa wa nje kuwa kitakuwa sahihi, ndo nakumbuka mwalimu wangu wa chuo Mr. Sijjo alikuwa anasisitiza kuwa ‘dhambi ni dhambi’ tu hata kama akiifanya malaika itabaki kuwa dhambi.
Lakini point yake ya mfano wa baadhi ya wasanii wa bongo wanavyofanya inanishawishi kwa kuwa imekuwa funny lakini ina maana sana ya kile nilichokuwa nikikisema mimi.
“Sasa hivi unaangalia kuna show za Akon anafanya mchanganyiko play back, lakini aina gani, make sasa hivi kinachotokewa ni kwamba mtu leo akishasikia play back ndo dah..anaondoka na CD yake tena ile yenye cover ambayo inauzwa sokoni, anaenda kuiplay back sasa kwelikweli.”
Lakini kauli hii ya Banana Zorro kuwa hata wasanii wan je pia wanafanya play back, niliirudisha tena kwa wakazi kama swali, kutaka kufahamu yeye anadhani kwa nini hata hao wanaoitwa wakubwa wanaimba sometimes juu ya wimbo, na sometimes wanasimama kweli.
“Unajuwa kwa upande wa wasanii wakubwa unakuta anaamua kufanya hivyo kwa kuwa anakuwa na show 30 katika siku 20, kwa hiyo show nyingine anaweza asiipe umuhimu sana, kuona kama kuna umuhimu wa yeye kujionesha kuwa yuko katika kiwango flani, kwa hiyo akaamua tu kuwapa show ya kawaida, kwa kuwa anajuwa tu atashangiliwa, ni kitu kibaya kusema ukweli.”
Kumbe tatizo hapa inaweza kuwa ni uchaguzi wa umuhimu wa show, kwa ufupi inamaanisha kudharau baadhi ya show. Mi naona kama msanii amedharau pesa, ni vyema angedharau kile kiasi cha pes alicholipwa ili asije kwenye show mapema. Sio, kwenda kwenye show kutimiza tu ratiba.
Kama ulipata nafasi ya kuangalia ‘Coke Studio’, utaona jinsi ambavyo wasanii wa Afrika wana uwezo mkubwa sana wa kufanya kazi kwa kuimba Live kama wale wa nchi za nje, ulimuona Diamond akiiua vilivyo ‘Temptetion ya P-Square’ , na Lady Jay Dee ambae ni kawaida yake kufanya na Live.
Hii inanisababisha nikubali kabisa kuwa wasanii wa kibongo wanaweza kufanya poa sana na kuachana na ‘Play back’.
Utajiuliza inakuwaje msanii anashindwa kuimba wimbo wake Live jukwani bila hiyo CD iliyoko radioni, wakati hata katika mashindano ya kuimba kama TPF6 na EBSS, washiriki wanaimba vizuri nyimbo za wasanii hawahawa wa bongo na wa nje, wanaziimba vizuri bila Play Back. Sasa inakuwaje mwenye wimbo mwenyewe ashindwe kuutendea haki jukwaani?
Hali hii inanifanya niungane na kauli ya Master J, jaji wa EBSS wakati akitoa maoni yake kwa baadhi ya washiriki wa EBSS.
“Narudia na ntaendelea kurudia sana hili, kuna watu wanaperform chini ya hapo huko nje, na wanamiliki magari na majumba.”
Sasa kwa mtindo huu nadhani huu ndio nauita ‘unyonyaji’ kwa kuwa msanii hufanya kazi chini ya kiwango japo anafanya vizuri kwa kiasi flani, na kwa kuwa mashabiki wengi hawajashitukia kudai haki yao, basi unakuwa ‘Unyonyaji uliohalalishwa’ kwa kupoozwa na neno ‘alishangiliwa sana, alifunika sana.
Wasanii wanaofanya hivyo kwa kisingizio chochote, na mnalipwa vizuri na mnatangaza, kumbukeni kauli ya Bob Marley, “You can fool all the people for sometimes, but you can’t fool all the people all the time.”
Badilika, fight for excellence, sio kwa mazoea na kuiga mfano wa aliyekosea hata kama ni msanii kutoka mwezini.
source:Josefly Muhozi
Mwimbaji wa nyimbo za injili toka nchini Nigeria  ajulikanaye  kwa  jina  la  Maheeda  amejikuta  akitengwa  na  kanisa  baada  ya  picha  zake  za  uchi  kuvuja….

Taarifa  zinadai  kwamba kabla  ya  kuanza  kuimba  nyimbo  za  dini, mrembo  huyo  alikuwa  akijihusisha  na  mziki  wa  kidunia ambao  kwa  tanzania  unajulikana  kwa  jina  la  Bongo Fleva


MKALI wa songi linalotamba runingani na redioni ndani na nje ya Bongo la Number One, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond Platnumz’ amefunguka na kuanika siri tano za kurudiana na Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.



Wiki mbili zilizopita, wakiwa Hong Kong, China, vyombo vya habari na mitandao ya kijamii viliripoti kurudiana kwa Diamond na Wema waliomwagana takriban mwaka mmoja uliopita ambapo staa huyo wa Bongo Fleva aliibuka na kukanusha vikali akidai kuwa picha zinazomwonesha yuko na Wema ni za Filamu ya Temptations.

Akizungumza na Risasi Jumamosi kwa dakika ishirini katika mahojiano maalum jijini Dar mara tu baada ya kutua kutoka China Jumatano iliyopita, Diamond alikiri kufaidi penzi la Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006.

Diamond alisema kuwa, Wema ndiye aliyetangulia kwenda China ambapo yeye aliungana naye siku kadhaa baadaye akitokea kwenye shoo nchini Malaysia.

SIRI YA KWANZA
Akianika siri za kujikuta mikononi mwa mwigizaji huyo mwenye mashabiki wengi zaidi katika tasnia ya filamu za Kibongo, Diamond alisema kwanza ni ukarimu aliopewa na mrembo huyo.

Alisema kuwa alipotua Hong Kong alishangaa kukutana na mapokezi ya Wema kwenye uwanja wa ndege jambo ambalo hakulitegemea.

“Alinionesha ukarimu wa hali ya juu mno. Wakati tulipokuwa hapa Bongo tulikuwa hatusalimiani.
“Kuna vitu vingi vya ajabu vilitokea huko nyuma kati yangu na Wema. Sikufikiria wala kuwaza kama anaweza akawa mkarimu kwangu kiasi kile.

Akaongeza: “Kwa mazingira yalivyokuwa, kwa namna yoyote lazima mwanaume aliyekamilika arudishe moyo nyuma na kuacha mambo mengine yaendelee.


“Kiukweli nisema tu kuwa hata tungekutana Morogoro au Dodoma kwa ukarimu ule mwisho wa siku tungerudisha uhusiano wetu.”

SIRI YA PILI
Diamond alisema baada ya mapokezi ya nguvu, Wema alimpeleka kwenye hoteli ya nyota tano (five stars) ambapo huko alipatiwa huduma ‘klasiki’ na kujiona kama yupo kwa mama Nasibu vile.

SIRI YA TATU
Alifunguka kuwa kitendo cha Wema kuwa mwenyeji wake China ambako alikuwa mgeni hadi akapazoea nacho ni siri nyingine iliyochangia wao ‘kukumbushiana’.

SIRI YA NNE
Alisema kuwa mwanadada huyo alimuonesha mapenzi mazito (yaani kutekwa kimapenzi) hivyo haikuwa rahisi kumchomolea kwani waliishi kama ndiyo penzi jipya linachipuka, akajikuta akiogelea naye. 

SIRI YA TANO
Diamond alisema kuwa bado ana ndoto ya kupata mtoto kupitia kwa Wema ambaye anajua kuwa alishamwambia lengo lake juu ya kupata naye uzao hivyo katika nyakati za kukutana kwao anaamini ndoto itatimia.

HAKUNA CHA FILAMU
Alipoulizwa juu ya madai kuwa walikuwa wakirekodi filamu, Diamond alifunguka kuwa hakuna cha filamu wala sinema na kama kuna mtu anasubiri filamu atakaa sana.

“Naomba nikiri kuwa kweli zile picha hazikuwa za filamu wala nini bali ndivyo hali halisi ilivyokuwa kati yangu na Wema kule China.


“Pia naomba niseme kuwa uhusiano wetu wa kimapenzi uliishia China na sasa hivi tumebaki kama kaka na dada na ni ruksa kila mtu kumtumia mwenzie katika kazi mbalimbali kama ataona kuna ulazima wa kufanyika hivyo,” alisema Diamond.


Hii ni mara ya kwanza kwa Diamond au Sukari ya Warembo kukiri kuwa kweli alirudisha penzi lake kwa Wema walipokuwa nchini humo wakijiachia.

PENNY HANA CHAKE?
Kwa mujibu wa watu wa karibu wa Diamond, ukifuatisha simulizi hiyo ya mapenzi kati ya msanii huyo na Wema, ni dhahiri kuwa mpenzi wa sasa wa jamaa huyo, Penniel Mungilwa ‘VJ Penny’ hana chake kufuatia usaliti huo.


Hata hivyo, jitihada za kumtafuta Penny ziligonga mwamba kufuatia simu yake kuita bila kupokelewa lakini juzi wanahabari wetu walipofika nyumbani kwa Diamond, Sinza-Mori, Dar waliambiwa mrembo huyo alilala hapo na kuondoka asubuhi.

GPL
JESHI la Polisi nchini limewafukuza kazi askari wake 56 katika kipindi cha mwaka mmoja, kutokana na makosa ya kuomba na kupokea rushwa pamoja na utovu wa nidhamu.
  


Kamishna msaidizi wa jeshi hilo, Patrick Byatao, alisema hayo jana alipokuwa akitoa ufafanuzi juu ya mambo mbalimbali hususan masuala ya nidhamu kwa askari wake katika warsha ya siku maalumu ya polisi iliyofanyika mjini Bukoba.
  
Alisema kuwa askari waliofukuzwa ni kutoka katika mikoa mbalimbali nchini ambao wamekutwa na tuhuma za utovu wa nidhamu ikiwemo kuomba rushwa kwa wananchi. Kwa kipindi cha mwaka 2012, waliwafukuza askari 35 na mwaka huu 21.
  
Kwa mujibu wa Byatao, wapo baadhi ya askari ambao wamekuwa wakitoa visingizio vya kuomba rushwa kwa sababu mishahara yao ni midogo na haitoshelezi mahitaji yao.
  
Alisema ni heri askari wa aina hiyo wakaacha jeshi, vinginevyo wataendelea kuchukuliwa hatua kama hawatafuata masharti ya kazi yao.

Akitoa mada juu ya kuimarisha maadili ndani ya jeshi hilo, Mrakibu Msaidizi wa Polisi kutoka makao makuu, Andrew Makungu, alisema wameanzisha mkakakati wa kudhibiti vitendo vya ukiukwaji maadili kwa askari wake ikiwemo rushwa.
  
Alitaja maeneo lengwa kuwa ni chumba cha kupokea taarifa za mashitaka, usalama barabarani na upelelezi wa makosa ya jinai. Bado juhudi zinaendelea ili kuboresha maeneo mengine.
  
Makungu alisema ubia wa kiutendaji wa jeshi hilo umekuwa ukiimarika kila siku baada ya sehemu kubwa ya jamii kutambua nafasi yao katika jukumu hilo. 
  
Alisema mambo hayo yanaonekana kutokana na wananchi kufanya ulinzi wa maeneo yao, kuchangia rasilimali kwa jeshi, kutoa taarifa sahihi za uhalifu, kujenga vituo vya polisi na kuanzisha vikundi vya ulinzi shirikishi. Hadi sasa viko vikundi 5,344 nchi nzima huku Mkoa wa Kagera ukiwa na 431.
  

Naye mgeni rasmi katika warsha hiyo, Meya wa Manispaa ya Bukoba, Anatory Amani, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu Fabian Massawe, alisema kuwa Jeshi la Polisi limekuja na mkakati wa polisi jamii/ulinzi shirikishi unaoelekeza kuwapo kwa mashauriano, majadiliano ya kiutendaji yanayosisitiza uwepo wa maadili katika kazi, ikiwemo mapambano dhidi ya rushwa ndani ya jamii.

Chuo cha st.John's pale Dodoma kuna tatizo kubwa la walimu kuwakamata wananfunzi na kuwalazimisha ngono.



Nimeshuhudia mwanafunzi last week amekamatwa na mwalimu kamwambia