advert

http://

Monday 13 April 2015

Nigeria:APC yatwaa majimbo19 kati ya 29


 mwenzako
Nigeria:APC yatwaa majimbo19 kati ya 29
Chama cha rais mteule wa Nigeria APC, kimesajili ushindi mkubwa wa majimbo 19 kati ya 29 katika matokeo ya hivi punde yaliyotangazwa na tume huru ya uchaguzi INEC.
Awali INEC ilikuwa imethibitisha kuwa chama cha rais mteule The All Progressives Congress (APC) kilikuwa kimetwaa miji mikuu ya Lagos Kaduna na na Katsina.
Matokeo haya ya hivi punde ni dhihirisho kuwa raia wa Nigeria walipigia Kura kiongozi wa upinzani Jenerali mtaafu Muhammadu Buhari.
Ushindi huo ni dhidirisho ya kuwa chama kinachoondoka madarakani cha Rais Goodluck Jonathan PDP kimepata kichapo chake kikubwa zaidi tangu kukamilika kwa utawala wa kijeshi mwaka wa 1999.
APC, kimeshinda majimbo makuu ya Lagos kaduna na Katsina katika uchaguzi mkuu wa Nigeria
Jenerali mstaafu Muhammadu Buhari anatarajiwa kuapishwa rasmi kama rais wa taifa hilo lenye uchumi mkubwa zaidi barani Afrika mwishoni mwa mwezi Mei.
Mwandishi wa BBC aliyeko Abuja Bashir Saad Abdullahi anasema kuwa chama cha jenerali mstaafu Muhammadu Buhari The All Progressives Congress (APC)
Kilihifadhi jimbo la Lagos mbali na kutwaa majimbo zaidi ya Kaduna naKatsina.
Ushindi huu wa majimbo zaidi unaiongezea pondo serikali mpya haswa baada ya kutwaa ushindi mkubwa dhidi ya Rais Goodluck Jonathan.
Matokeo kamili ya kura za majimbo 39 na magavana 29 unatarajiwa kutolewa baadaye.
Jenerali mstaafu Muhammadu Buhari anatarajiwa kuapishwa rasmi mwishoni mwa mwezi Mei.
Magavana 29 wa Nigeria wanaushawishi mkubwa kutokana na uwezo wao mkubwa wa kiuchumi
Lagos
Uchaguzi huu wa majimbo umeendeleza dhana ya kuwa APC itazoa maeneo wakilishi mengi kufuatia ushindi wa wa kihistoria wa jenerali mstaafu Muhammadu Buhari.
Siku ya jumapili, tume huru ya uchaguzi nchini humo (Inec) ilitangaza rasmi kuwa chama cha Jenerali mtaafu Buhari APC ilikuwa imetwaa jimbo la Lagos mbali na kushinda ugavana wa majimbo ya Kaduna na Katsina majimbo
ambayo yaliongozwa na kudhaniwa kuwa ni ngome ya PDP
Chama cha PDP hata hivyo kilihifadhi jimbo la Rivers
Kwa wadadisi wengi utawala wa Jenerali mstaafu Buhari utakuwa utawala wa kwanza kutawala nchi na vilevile mji mkuu wa kiuchumi nchini humo wa Lagos tangu kumalizika kwa utawala wa kiimla mwaka wa 1999.
Vilevile hii ndio itakayokuwa mara ya kwanza kwa chama ambacho sio PDP kuwahi kuiongoza majimbo ya Kaskazini mwa taifa hilo.
Uongozi wa majimbo 36 unaumuhimu mkubwa haswa kiuchumi kwani magavana wengi katika maeneo yenye utajiri mkubwa wa mafuta huwa wana makadirio ya bajeti makubwa hata zaidi ya mataifa mengine ya Magharibi mwa Afrika.
Chama cha PDP hata hivyo kilihifadhi jimbo la River

Hatimaye waliombaka Liz wahukumiwa Kenya

Mshirikishe mwenzako
Hatimaye haki imetendeka baada ya watu watatu waliombaka msichana mdogo Liz kuhukumiwa kifungo cha mika 15 jela nchini Kenya
Mahakama moja mjini Busia, imewahukumu washukiwa watatu vifungo vya kati ya miaka saba na kumi na tano gerezani,baada ya kuwapata na hatia ya kumbaka na kumjeruhi msichana mmoja, aliyefahamika kama Liz.
Liz inasemekana alishambuliwa na vijana hao na kubakwa wakati alipokuwa akirejea nyumbani kutoka kwa mazishi ya babu yake katika eneo la Busia Magharibi mwa Kenya.
Tukio hilo lilizua mjadala mkali nchini Kenya huku wanaharakati wa kijamii wakishinikiza serikai kuwachukulia washukiwa hao hatua kali.
Watatu hao walikuwa wamehukumiwa ''kufyeka nyasi katika kituo cha polisi'' na kuachiliwa huru.
Hata hivyo msichana huyo alikuwa amepooza kiwiliwili chake kuanzia kiunoni kufuatia kutupwa katika shimo ilikuficha ushahidi alipata
msaada baada ya wanaharakati wa kupigania haki za kibiniadamu kuishinikiza polisi kuchukua hatua dhidi ya polisi waliotoa hukumu hiyo nyepesi dhidi ya watu hao watatu.
Mamake Liz ameiambia BBC kuwa hatimaye haki imetendeka.
Mamake Liz ameiambia BBC kuwa hatimaye haki imetendeka.
Watatu hao sasa wamepatikana na hatia ya kumjeruhi Liz na kuhukumiwa kifungo cha miaka 7 Jela.
They were also found guilty of causing bodily harm and sentenced to 7 years in prison.
Harakati za kumtafutia haki msichana huyo ziligonga vichwa vya habari mwaka uliopita watu zaidi ya miklioni 2
kote duniani walipotia sahihi kampeini ya kumlazimisha Inspekta mkuu wa Polisi
kuwachukulia hatua watatu hao ambao walikuwa wamedaiwa kuwahonga maafisa polisi huko Busia Magharibi mwa Kenya.
CHANZO: BBCSWAHILI.COM

Sunday 12 April 2015

Ubalozi wa K Kusini washambuliwa Libya


Libya
Watu wasiojulikana wameushambulia ubalozi wa Korea Kusini kwenye mji mkuu wa Libya Tripoli ambapo walinzi wawili wa ubalozi huo waliuawa.
Wizara ya mashauri ya kigeni nchini Korea Kusini imesema kua watu hao walifyatua risasi wakilenga ubalozi huo wakiwa ndani ya gari.
Hakuna raia yeyote wa Korea Kusini aliyeripotiwa kujeruhiwa wakati wa shambulizi hilo.
CHANZO.BBCSWAHILI.