advert

http://

Wednesday 12 February 2014

Wanasayansi wa kampuni ya Google:Wabuni magari yasiyotumia dereva.


Inawezekana kuwa na magari yasiyokuwa na dereva? Kampuni ya mawasiliano ya kompyuta ya Google inasema ndiyo. Magari hayo yapo na yataongozwa kwa kutumia kompyuta pekee, huku yakiwa na uwezo mkubwa wa kuepuka au kutosababisha ajali barabarani.
Wanasayansi wa Google wanaosimamia teknolojia hiyo mpya, wanaamini kwamba madereva wanafanya makosa mengi wawapo barabarani, yakiwepo ya kizembe ama bahati mbaya na ndiyo yanakuwa chanzo cha ajali mbaya barabarani.
Wakati teknolojia ya kompyuta ilipogundulika, wanasayansi walisema wamegundua mbinu ya kufuta makosa ya kibinadamu katika shughuli za hesabu.
Waliamini kuwa kila hesabu 500 afanyazo mtu ambaye ni mtaalamu wa fani hiyo, lazima kuwepo na makosa yasiyopungua mawili. Lakini baada ya kugundua kompyuta, maelfu kwa maelfu ya hesabu yanaweza kufanyika bila makosa.
Makosa hayo ya kibinadamu yanayoweza kufanywa na mtu bila kukusudia, ndiyo yanayoaminika kuweza kufanywa na dereva yeyote akiwa barabarani.
Magari hayo yako je?
Mtaalamu wa kompyuta katika Chuo Kikuu cha Stanford, Profesa Sebastian Thrun, anayesimamia, teknolojia hiyo akisaidiana na mhandisi wa kampuni ya Google, Chris Urmson, wanasema teknolojia hiyo itasaidia kuepusha ajali, foleni na pia kupunguza kiwango cha mafuta yanayopotea kutokana na uendeshaji usiofaa.
Mhandisi Urmson anasema magari hayo hayatakuwa na tofauti kwa kiasi kikubwa na mwonekano au miundo ya magari yaliyopo sasa. Kama haitoshi yana chaguo la ama liendeshwe kwa kompyuta ama na dereva.
Mwonekano wake
Kimwonekano, magari hayo anayaelezea yatatofautiana na mengine, kwa kuwa na kifaa maalumu juu ambacho kinasaidia mawasiliano na kutambua maeneo.
Anasema kwenye mfumo wa kompyuta zitatumika programu mbalimbali kama vile ya 3D, ambayo itasaidia kuliongoza gari kulingana na ramani ya eneo.
“Hii ina maana kwamba magari yote yatakuwa yanatumia ramani ambayo lazima iingizwe kwenye mfumo wake ili itambue barabara itakazopita ili kufika aneo ambalo mhusika ama wahusika wanataka” anasema.

Mwigizaji wa filamu na mtangazaji wa kipindi cha redio cha Paradise, Irene Uwoya, amesema licha ya kwamba wasanii wanafanya bidii kuyafikia mafanikio, kikwazo kikubwa katika safari yao ni kutokuthamini muda.
Akizungumza katika mafunzo maalumu ya wasanii na wafanyakazi wa Kampuni ya uzalishaji na usambazaji wa filamu 5 Effect, Uwoya alisema kinachokwamisha tasnia ya filamu kufika katika nafasi za juu kimafanikio ni kutokujali muda.
“Tatizo kubwa ni kutokuthamini muda, unakuta mmekubaliana kwamba mkutane saa nane mchana katika eneo la kutengenezea filamu (Location), unafika pale mtu unayetakiwa kushirikiana naye katika (Scene) kile kipande hajafika, anafika saa kumi jioni, kazi inachelewa kuanza na muda unapotea,” alisema Uwoya.
Alisisitiza kwamba ikiwa tasnia hiyo itajali muda ipasavyo, inaweza kupiga hatua kubwa kwa mwaka huu, hasa ukizingatia sanaa imerasimishwa na Serikali hivyo ni kazi inayotambulika kwa sasa.
“Serikali yetu imerasimisha sanaa, kwa sasa ni kazi kama ya ofisini, inatakiwa sisi wasanii tulitambue hili na kila mmoja kwa nafasi yake kuhakikisha anatekeleza majukumu yake ipasavyo.Pia mtu wa kamera naye lazima ajue script (muswada) inasema nini.
Vivyo hivyo kwa upande wa masoko na wasambazaji tunahitaji watu wenye uelewa na elimu kuhusu kazi hizi ili tusonge mbele,” alisisitiza.
Aliongeza kuwa viongozi ni kama dira, hivyo wanapaswa kutoa mwongozo mzuri kwa wasanii na kusimamia kampuni vema ili kujikwamua na wizi wa kazi za sanaa nchini.
“Lazima tuondoe dhana kuwa bila watu wa jamii ya Asia hakuna usambazaji,” anasema.
 Mwanamuziki Vivian Wambui, amewaomba wapenzi wa muziki kumheshimu na kuacha kumuhusisha na tuhuma za uhusiano wa kimapenzi na Jaguar.
Amesema anaweza kuwa na uhusiano na mtu yeyote anayempenda lakini siyo kwa watu anaowaheshimu kama Jaguar.
“Naomba mniheshimu, Jaguar ni kama kaka yangu jinsi tunavyoheshimiana na anavyonishauri kwa nia njema, sioni sababu ya kila kukicha kusema ni mpenzi wangu mnanidhalilisha,” alisema Vivian, alipohojiwa kwa njia ya simu na mtandao wa Bigeye.
Vivian alifafanua kuwa jambo la maana kwao ni kutathmini muziki wanaokufanya badala ya kuanzisha maneno ya ajabu ambayo yanaishushia hadhi tasnia ya muziki, kwa kuonekana ni kama kituo au kazi ya kuendeshea uhuni.

Vigogo sita ambao wanatajwa kuwa wanajiwinda kwa ajili ya kuwania urais kupitia CCM katika uchaguzi mkuu ujao, wameitwa mbele ya Kamati ya Ndogo ya Maadili ya chama hicho, kwa ajili ya kuhojiwa kwa tuhuma za kukiuka maadili.
Habari ambazo zililifikia gazeti hili jana zinawataja vigogo hao kuwa ni Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Steven Wassira na Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye.
Wengine ni Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, aliyewahi kuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba.
“Wote wamepelekewa barua za wito wa kufika mbele ya Kamati ya Maadili inayoongozwa na Mzee Mangula (Philip, Makamu Mwenyekiti wa CCM, Bara), ambayo itakutana mjini Dodoma, Februari 14 (kesho kutwa) ,” kilisema chanzo chetu cha habari kutoka Ofisi Ndogo ya CCM, Lumumba, Dar es Salaam na kuongeza:
“Barua hizo zimesainiwa na Mzee Kinana (Abdulrahman, Katibu Mkuu wa CCM) mwenyewe na tayari zimeanza kusambazwa leo (jana) mchana.”
Kamati hiyo ndogo ya maadili, inaundwa na Mangula, Kinana, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, Shamsi Vuai Nahodha, Dk Maua Daftari na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk Pindi Chana.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye jana alithibitisha kuwapo kwa Kikao cha Kamati ya Maadili Februari 14 pamoja na kuitwa kwa baadhi ya wanachama kwa ajili ya kuhojiwa.
Hata hivyo, hakuwa tayari kutaja majina yao wala idadi ya walioitwa... “Wewe fahamu tu kwamba kikao hicho kitafanyika tarehe hiyo uliyoitaja, lakini masuala ya majina na idadi ya walioitwa yatajulikana kwenye kikao, mimi sina kwa sasa,” alisema Nnauye.
Katika siku za karibuni kumekuwa na vita ya maneno baina ya makada wa chama hicho, wakituhumiana kutangaza mapema kugombea urais kabla ya ruhusa rasmi ya chama.
Kauli za walioitwa
Jana, gazeti hili lilizungumza na baadhi ya walioitwa na wengi wao walisema hawakuwa wamepokea barua za wito huo.
Sumaye kwa upande wake alisema: “Kwa sasa niko Mwanza na sijapata barua yoyote ya kuitwa katika kikao chochote cha chama.”
Chanzo:Mwananchi.
Linex akanusha kuwa na uhusiano wa mapenzi na Agnes Masogange, Linex Sunday Mjeda, ambaye hivi karibuni ameonekana kwenye picha kadhaa akipoz na video Queen maarufu Tanzania, Agnes Gerald (Masogange), amekanusha kuwa na uhusiano wa mapenzi na mrembo huyo kama baadhi ya blogs ilivyoripoti.
Kupitia akaunti yake ya Facebook, mkali huyo wa ‘Kimugina’ ameonesha kusikitishwa na habari iliyoandikwa na tovuti moja kuwa yeye na Agnes wako kwenye mapenzi mazito.
“ni kweli watu wa blog mnapush sana kazi zetu but nimesikitishwa na habari hii iliyoandikwa na blog kadhaa mtasababisha tutashindwa ata kukaa na Dada zetu au marafiki zetu Uliza b4 Hujaandika ujinga am single na sina haraka ya kua na mpenzi.” Ameandika kwenye Facebook.
Wikendi hii, Linex alipost picha mbili Instagram akiwa na mrembo huyo, moja wakiwa wamepoz ufukweni, na nyingine akiwa naye katika mechi ya mpira wa kikapu kati ya timu za madirector wa video za muziki Tanzania, Adam Juma na Karaban.

Young Dee kumfungulia mashitaka mtu anayetumia jina lake Facebook kufanya utapeli, Kumekuwepo malalamiko mengi kutoka kwa watu maarufu kutokana na kuwepo kwa watu wanaofungua akaunti za facebook  kwa majina yao na kufanya utapeli.
Rapper anaewakilisha kundi la Mtu Chee, Young Dee, amedai kuwa ingawa hayuko kabisa facebook, kuna mtu ambaye amekuwa akitumia jina lake kufanya utapeli licha ya kuzungumzia mara kwa mara kuhusu mtu huyo kwenye vyombo vya habari.
Rapper huyo wa ‘Kijukuu’, ameiambia tovuti ya Times Fm kuwa japokuwa alitangaza zawadi kwa mtu atakayefanikisha zoezi la kumpata mtu huyo bado hajafanikisha na kwamba mtu huyo anaendelea hadi leo.
Amesema aliwahi kwenda polisi kufungua mashitata dhidi ya mtu huyo akiwa na utambulisho wa BASATA kuwa yeye ndiye ‘Young Dee’, lakini polisi walidai ampeleke mtu ambaye ametapeliwa ndipo aweze kufungua kesi hiyo.
Tayari Young Dee ameshajipanga kwa ajili ya kuupeleka ushahidi utakaofanikisha zoezi la kumpandisha kizimbani tapeli anayetumia jina lake kwenye Facebook.
“Bado naendelea na zoezi langu, lakini sasa hivi nachokitafuta…kuna mtu wa sheria amenishauri kuna jinsi ambavyo hiyo kesi tunaweza kuifungua ikamake sense. Kwa hiyo ndio niko nae naconfirm naye, lakini bado tunakusanya ushahidi, kuna mtu mmoja nimempata ambaye ameshatapeliwa, natafuta mwiningine. Kwa hiyo tukishapata ushahidi wa kutosha tunaweza kum-sue. Young Dee ameiambia tovuti ya Times Fm.
Kama uko facebook na unachat na Young Dee, sanuka, jamaa hayuko facebook kabisa!
Mwenyekiti wa kundi la Bongo Movie Unity, Steven Mangere ‘Steve Nyerere’ amesema wasanii wengi wa filamu hawajitambui, mbumbumbu na wabinafsi katika kila kitu, jambo linaloleta ugumu katika harakati zao za kujikwamua.

Steve Nyerere ambaye pia ni mwigizaji na mchekeshaji, amesema wasanii wengi wanakosa umoja wa kudai haki zao kutokana na uelewa mdogo walionao huku wengine wakitazama maendeleo yao binafsi.
“Wasanii tumekuwa mbumbumbu wa kila kitu, tumeyumba kwa kuuza na kuibiwa kazi zetu na maharamia. Dada zetu nao wanafanya Bongo Movie ni sehemu ya kufanyia ukahaba.
Pia amesema yeye kama kiongozi anapigania haki za wasanii zisisahaulike katika mchakato wa katiba mpya ili waweze kupata nafuu ya kazi zao.

Source, Mwanaspoti 
DDDDDDDDDDDDD
Siku kama ya leo miaka 32 iliyopita alizaliwa Kelly Rowland ambaye aliwahi kuja Tanzania na kufika hadi Uwanja wa fisi.

Kelly alikuja kwa ajili ya kampeni ya Staying Alive Foundation  ambapo alikuwa balozi wa MTV AIDS Awareness.
kelly-r5bc
imageLeo pia ni siku ambayo hayati Nelson Mandela aliachiwa huru kutoka kwenye gereza baada ya kuwa mfungwa hadi 11 February 1990.
Unaambiwa akiwa anatoka kwenye gerezani vyombo vya habari kutoka sehemu mbalimbali za dunia walizunguka kuihabarisha dunia kwa kilichokuwa kinaendelea.
outside homes trees street signKama haujawai kusikia sehemu inaitwa Silicon Valley huko Marekani basi jua kwamba hili ni eneo ambalo makampuni makubwa ya teknolojia yameweka makao makuu yao huko.
Ndani ya eneo hilo  utakutana na makao makuu ya Google,Facebook,eBay,Adobe,Apple,Yahoo,HP,Intel,Mozilla Foundation,Linkedln,Twitter na mengine mengi.
dimondiDiamond aliwahi kusikika akizungumzia kuhusu kuja kwa nguo zake ambazo zitakuwa na brand ya WCB na kuuzwa kwenye maduka mbalimbali.

Mwaka jana Diamond alikaa China zaidi ya wiki nzima kabla ya kufanya show ambapo moja ya mipango iliyomuweka ni kufanya maandalizi ya nguo hizo.
Muda wa kuzitoa unaonekana umekaribia kutokana na teaser aliyoitoa kupitia account zake za mitandao ya kijamii kuhusu hizo nguo.
millard
millard2


Mama wa star wa filamu na kipenzi cha wengi duniani muigizaji  Sylvester Stallone aka Rambo
ameonekaha hivi karibuni akiwa na muonekano tofauti na kwamba kafanya kila jambo kukimbia uzee.
Mama huyu mwenye miaka 92 amefanyiwa Upasuaji Wa Kubadili Sura sura na kuwa na muonekano wenye mvuto zaidi.
rambo 2rambo 3rambo 4rambo
Magazeti ya ufaransa yadai Obama ana uhusiano wa kimapenzi na Beyonce, waandishi wa Marekani wakanusha

Kuna mgongano wa habari kati ya baadhi ya vyombo vya habari vya Ufaransa na vile vya Marekani kuhusu uhusiano uliopo kati ya Beyonce Knowles na rais wa Marekani, Barack Obama.

Gazeti la Ufaransa la Le Figaro liliripoti kuwa kuna uhusiano wa siri wa kimapenzi kati ya rais wa Marekani, Barack Obama na mwimbaji ambaye ni rafiki wa karibu wa familia ya Obama, Beyonce Knowles.
Habari hizo zilishindiliwa msumari na mpiga picha Mfaransa Pascal Rostain, ambaye ni rafiki wa mke wa rais wa zamani wa Ufaransa, Carla Bruni, aliyelieleza gazeti hilo kuwa habari hizi hivi karibuni zitaandikwa na waandishi wa habari wa Marekani na inaweza kuwa kama ile scandal iliyomtesa Bill Clinton, kuhusu Monica Lewinsky (1995/1996).
“Kuna kitu kikubwa kinachoendelea kati ya wawili hawa, tusisahau Marilyn (Monroe) au Monica Lewinsky. Unaweza kuwa rais wa nchi ya kwanza yenye nguvu duniani…hiyo haikufanyi usiwe mwanaume kamili.” Rostain aliliambia gazeti hilo.
Hata hivyo, ingawa Rostain alidai kuwa Washington Post lingeandika habari hiyo leo (February 11), Washington Post imeandika habari tofauti kabisa huku baadhi ya waandishi wakikanusha habari hizo.
“Sio kweli hata kidogo”, msemaji wa Post Kris Coratti ameiambia Poynter.com kwa njia ya barua pepe. 
Naye mwandishi wa wa New York Times, Dave Itzkoff ametweet kuhusu tuhuma hizo na kuonesha kutokubaliana kabisa na kilichoandikwa na gazeti la Ufaransa.
“It doesn’t seem plausible to me that the most powerful person in the world would have time for an affair with Barack Obama.”
Ni kama vyombo vya habari vya ufaransa vimeiwashia taa familia ya Obama kuhusu mahusiano ya mapenzi. Wakati gazeti la Le Figaro likiandika hayo, jarida la Gala la nchini humo limeandika kuwa Obama na mkewe Michelle wanaelekea kupeana talaka.
Familia ya Jay Z ni rafiki wa familia ya Obama, ambapo kuna wakati Michelle na Beyonce waliandikiana barua za wazi, huku familia ya Jay Z ikialikwa mara kwa mara katika ikulu ya Marekani.
Mwaka 2012, Beyonce alimuandikia Obama barua kwa mkono wake na kuipost kwenye tovuti yake, kumsapoti katika uchaguzi wa Urais.
“President Obama,
Everyday we see your heart and character, inspiring all of us to give more of ourselves.
You are the leader to take us from where are to where we need to be.
You are the reason my daughter and nephew will grow up knowing that they can truly be ANYTHING they want to be.
All my respect and adoration,
Beyoncé.” Inasomeka barua ya Beyonce kwa Obama.
Wakati hayo yote yanaandikwa, leo rais wa Ufaransa Francois Hollande ambaye amekuwa na matatizo katika ndoa yake, ameitembelea ikulu ya Marekani na kuzungumza na rais Obama.









Muimbaji wa kike wa muziki wa kizazi kipya nchini Lady Jaydee afikiria kubadilisha jina la band yake kutokana na machozi yaliyokuwa yakimliza kipindi hicho yameshafutika.


Amefikiria kubadilisha jina hilo la bendi yake na isiitwe Machozi Band kama ilivyozoeleka kutokana na sasa hatowi tena machozi kama ilivyokuwa hapo awali.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook aliandika hivi " Nafikiria kubadilisha jina la band sababu Machozi Machozi niliolia zamani yashafutika. Mnashaurije???" alitupia swali hilo kwa mashabiki wake.