advert

http://

Thursday 16 January 2014

B12, ADAM MCHOMVU NA DIVA WAMEPIGWA CHINI CLOUDS FM.



Stori:  MUSA MATEJA
WATANGAZAJI maarufu Bongo wa Redio Clouds Fm ya jijini Dar es Salaam, Hamis Mandi ‘B 12’, Adam Mchomvu na Loveness Malinzi ‘Diva’, wamepigwa chini na kituo hicho, Risasi Mchanganyiko linakupa zaidi.


Habari za chini kwa chini kutoka kwa chanzo chetu zinasema kuwa uongozi wa Clouds umefikia hatua hiyo baada ya kuchoshwa na tabia ya utovu wa nidhamu wa watangazaji hao.

Hata hivyo, madai ya mitaani yanasema kwamba watangazaji hao wamepigwa chini kwa kosa la kukacha sherehe za maadhimisho ya miaka 14 ya Clouds FM,yaliyofanyika hivi karibuni katika Viwanja vya Mwembeyanga, Temeke, Dar.

Risasi Mchanganyiko lilimvutia waya Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba na kumwuliza juu ya ishu hiyo ambapo alikiri.


“Ni kweli tumefikia uamuzi wa kuwasimamisha B 12, Diva na Mchomvu baada ya kukiuka baadhi ya makubaliano baina yao na ofisi hivyo kusababisha usumbufu mkubwa ambao ulitulazimu kuingia gharama ambazo hazikutarajiwa.

“Hatutakuwa nao kwa muda usiojulikana ingawa watu wengi wamekuwa wakinihoji juu ya hilo lakini watachotakiwa kuelewa ni kwamba hakuna ofisi isiyokuwa na sheria na taratibu za kuongoza watu wake, sasa hao wamevunja taratibu zetu,” alisema Ruge bila kufafanua zaidi.

Alipoulizwa ni taratibu zipi watangazaji hao walizovunja alisema: “Nashindwa kueleza kosa la kila mmoja ila naomba nieleweke kuwa hao watangazaji kwa sasa tumewasimamisha kwa muda usiojulikana wakati tukifikiria cha kufanya. Muhimu hapo ni kwamba wamekwenda kinyume na tulivyokubaliana.”


Credit:GPL


Utata umeibuka kuhusu alipo mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Masawe baada ya kuwepo kwa tetesi kuwa ameachiwa huru huko Dubai, Falme za Kiarabu (UAE) alikokuwa akishikiliwa.


Masawe ambaye alikamatwa katika uwanja wa ndege huko UAE akitokea Afrika Kusini, kati ya Juni 20 na 25, mwaka jana, anatuhumiwa kwa makosa mbalimbali yakiwamo ya mauaji.

Mkuu wa Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol) - Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile alikiri kuwapo kwa taarifa kwamba Masawe ameachiwa huru na hayupo Dubai ingawa bado tawi la Interpol katika nchi hiyo halijatoa taarifa yoyote.

“Tumejaribu kuwasiliana nao mara kwa mara kuhusu kumrudisha nchini lakini hawajajibu lolote. Hivi karibuni tuliwasiliana nao lakini hawajatujibu, kwa hiyo tumebaki na maswali. Kwa kifupi hatujui alipo hadi sasa,” alisema Kamishna Babile.

Alisema awali, baada ya kukamatwa huko Dubai, Tawi la Interpol Tanzania lilikuwa linafanya mchakato wa kumrudisha nchini ikiwamo kutuma ombi la kumrejesha mhalifu nchini, lakini ghafla mawasiliano yakakatika.

“Taarifa zilizopo ni kuwa Masawe ameachiwa huru, kwa vigezo gani hatuelewei,” alisema Babile.

Babile alisema iwapo atakuwa ameachiwa na polisi wa UAE, basi itakuwa ameachiwa kutokana na sheria za nchi hiyo ingawa bado Tanzania itaendelea kumsaka kwa udi na uvumba.

“Sisi tutaendelea kumsaka kama kawaida, iwapo atakamatwa nchi nyingine au ikitokea akaonekana hapa nchini, tutaendelea na mchakato wa kumfungulia kesi kwa sababu sisi tunajua kuwa ana makosa,” alisema Babile.

Massawe alitajwa mahakamani Aprili 4, mwaka jana katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara, Onesphory Kituly ambaye aliuawa katika mazingira ya kutatanisha Novemba 6, 2011 nyumbani kwake Magomeni, Dar es Salaam.

Katika kesi hiyo, mshtakiwa wa kwanza ni mfanyabiashara Abubakar Marijani, maarufu kama ‘Papaa Msofe’ na mshtakiwa mwingine ni Makongoro Joseph Nyerere.

Nyerere aliwahi kulalamika mbele ya Hakimu Mkazi, Agnes Mchome anayesikiliza kesi hiyo, akidai kwamba kumekuwa na ucheleweshaji wa shauri hilo kutokana na ndugu wa marehemu Kituly kutaka Massawe akamatwe ili ajumuishwe.

Mtuhumiwa huyo aliomba jalada la kesi yao lipelekwe mahakamani hapo kwa ajili ya kulifanyia kazi. Alitoa malalamiko hayo baada ya Wakili wa Serikali, Mwanaisha Kombo kudai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuomba tarehe mpya ya kutajwa kwake.


Rosemary Namubiru, 64, was produced before Buganda Road Court to answer to charges of 
attempted murder. She denied the charges


Chief Magistrate Olive Kazaarwe sent her to Luzira prison until January 31 following her failure to apply for bail. She also never had a legal representative in court.

Over the weekend, the country was thrown into dismay after Namubiru was arrested by Wandegeya police for maliciously infecting her patients mainly the children with her HIV positive blood.

Prosecution led by Martin Rukundo, alleges that on January 7, 2014 at Victoria Medical Centre, along Lumumba Avenue in Kampala, Namubiru with intent to unlawfully cause the death of two year-old Mathew Mushabe, pricked her finger and used the same syringe to inject the same child well knowing that she was HIV/Aids positive.

According to police records, on the fateful day the child was showing signs of tonsillitis, an inflammation of the tonsils.

The mother of the victim decided to take her sick son to Victoria Medical Centre, one of the health centers on the family’s health insurance scheme.

Unfortunately on her arrival, she found that the doctor who normally attends to her family was absent before the medical facility assigned nurse Namubiru.

But to the mother’s surprise, the nurse got hold of a syringe, first pierced one of her fingers, drew out some blood, and then injected the baby.

The terrified mother shouted at the nurse to stop injecting her child before reporting the matter to the in-charge of the facility leading to her arrest.

Later the victim’s family demanded to know Namubiru’s HIV status and upon testing, she was found to be positive.

Immediately, the child was transferred to another health centre and put on PEP treatment for the next 30 days with the aim of avoiding the contraction of the deadly virus.

Source: Redpepper


Waumini wa Mchungaji Daniel walijikuta wakianza kuumwa mara baada ya Mchungaji huyo kuwafanya wale wale majani.

Picha zinazofuata zinaonyesha watu tofauti wakiwa wagonjwa kwenye vyoo -  picha za vyooni zinawaonyesha wanawake wakishikilia matumbo yao, huku wanaume wakiwa wanatapika kwenye masinki.

Japokuwa Mchungaji huyo bado hajasema lolote juu ya tukio hilo ila kupitia ukurasa wake wa Facebook hapo jana aliandika: 'Mungu yupo kazini na watu wake wanatoa ushuhuda sasa'

Taarifa za kuibuka kwa kainsa hilo zilianza kusamba katika mitandao mbalimbali ya kijamii ambayo kwa nyakati tofauti iliripoti kuwepo kwa kanisa linaloimiza waumini wake kula nyasi kama ishara ya kutangaza miujiza ya Mungu.

Uchunguzi uliofanywa na Wadadisi wa Habari, ulibaini uwepo wa kanisa wa aina hiyo maeneo ya Upanga jijini Dar es salaam na huduma yao inafanywa kwa kutumia jina la Rabboni Centre Ministries yenye makao yake makuu jijini Pretoria, Afrika Kusini.

Waandishi wa Habari hizi, walifika Upanga, kwenye nyumba inayodaiwa kuwa ndilo kanisa hilo lakini hakuna mtu aliyekutwa hapo.

Hata hivyo, baadhi ya majirani walisema huwa wanawaona watu wakiingia katika nyumba hiyo lakini ajabu kunakuwa hakuna kelele zozote.

Chanzo chetu cha habari kimesema kuwa waumini wa kanisa hilo hula nyasi na baadaye kutapika, hali inayowafanya waamini kuwa kwa kufanya hivyo, wametakasika kiroho kwa kujazwa Roho Mtakatifu.

“Mchungaji wao huwakusanya waumini wake wanaopandisha mashetani wakiwa kanisani, hiyo hufanya shetani kumtoka mtu haraka,” kilisema chanzo.

Habari zinasema huduma hiyo ilianzishwa Afrika Kusini na Mtu anayejiita kuwa ni Mchungaji na Nabii Daniel Lesego mwaka 2002.

Imedaiwa kuwa kwa sasa waumini hao wapo kwenye mfungo ambao watu hufika kanisani na baadaye kula majani yaliyopo nje ya kanisa hilo wakisema kwamba Roho Mtakatifu huongoza mtu kula chochote huku ikidaiwa kuwa manyasi hayo ni chakula kutoka mbinguni