advert

http://

Thursday 17 October 2013

KARIBU KATIKA KONGAMANO KUBWA LA AFYA NA MAHUSIANO LITAKALOFANYIKA KATIKA CHUO CHA SAUT: JUMAMOSI HII




Jumamosi tar.19/10/2013 kutakuwa "KONGAMANO KUBWA LA AFYA NA MAHUSIANO" litakalofanyika katika Chuo Kikuu Cha St.Augustine, ukumbi wa M13 kuanzia saa tatu (03) asubuhi hadi saa saba (07) mchana. 
Mgeni Rasmi ni Waziri wa Afya Mh.Husein Mwinyi,mgeni Maalumu ni Mh.James Mbatia (Mbunge na Mwenyekiti wa asasi ya Utu-Mtanzania)

Kongamano hili lilikuwa liende sambamba na uzinduzi wa Kitabu kiitwacho “TUMAINI LANGU, ELIMU YANGU”kilichoandikwa na Godlisen Malisa aliyekuwa rais wa chuo mwaka 2012-2013. 

Kongamano hili nimeandaliwa mahususi kutoa nafasi kwa vijana wasomi kujadili kuhusu afya zao, mahusiano yao, na hatari ya maambukizi ya VVU kwa wasomi wetu.

Kongamano litajumuisha uwasilishaji wa mada zilizofanyiwa utafiti wa kina juu ya MAHUSIANO HATARISHI yanayoweza kupelekea maambukizi ya virusi vya UKIMWI kwa vijana wasomi.

Karibu uje ukutane na Waziri mwenye dhamana ya Afya uweze kuuliza mambo yote muhimu kuhusu wizara yake.

Karibu ukutane na mwanaharakati James Mbatia, akuelimishe na kukufundisha umuhimu wa Elimu yako na namna ya kuepuka maambukizi hatarishi. Karibu utoe maoni, uulize maswali, uchangie hoja etc.

Kongamano litajumuisha wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali vya kanda ya ziwa ikiwemo CBE, IJA, DIT, TIA, OPEN University, Chuo cha waalimu Butimba, Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya Bugando, Chuo cha Uuguzi Bukumbi, Chuo cha Uvuvi Nyegezi, Chuo Kikuu Kishiriki cha Mt.Meru Mwanza campus, nk.

Kwanini vijana wengi wasomi wanajiiingiza katika Mahusiano hatarishi? Ni kweli kuchelewa kwa “boom” kunachangia mabinti wasomi kujiuza? Je ni kweli WATOTO WA MAMA SALMA wapo vyuoni? Je haiwezekani kuwa na mpenzi mmoja kuanzia First year hadi third year? Etc.

Hayo na mengine mengi utayapata ukihudhuria Kongamano hili la kwanza na la aina yake kuwahi kufanyika nchini hasa kanda hii ya ziwa.

Mada zitawasilishwa na wahadhiri kutoka chuo kikuu cha SAayansi ya Tiba Bugando na Chuo Kikuu SAUT.

Pia kongamano hili litafungua rasmi mashindano ya uandishi wa Insha juu ya sababu za wasomi wa vyuo vya elimu ya juu kujiingiza katika mahusiano hatarishi na suluhisho lake. Mshindi katika uandishi wa Insha atazawadiwa Sh.200,000/= Taslimu.

Burudani zitakuwepo za kusisimua na tragicomedy za kuelimisha pia zitakuwepo.

Vyombo mbalimbali vya habari vitakuwepo, ikiwa ni pamoja na ITV, StarTv, na magazeti mbalimbali. Radio SAUT Fm watarusha kongamano hilo na baadae litarudiwa kwenye vipindi vya usiku, kwa wale watakaoshindwa kusikiliza mchana.

Shukrani za dhati ziende kwa Uongozi wa Chuo cha SAUT, Radio SAUT Fm, Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Asasi ya Utu Mtanzania, Shirika la Pensheni kwa watumishi wa Serikali za Mitaa (LAPF), Moil Petroleum, AprilMey Entertainment, Wizara ya Afya na Mazingira SAUTSO na wengine wote ambao kwa namna moja au nyingine wamefanikisha kuandaa kongamono hili.

Shukrani pia zikufikie wewe utakayesoma hapa na kuhamasisha wenzio kushiriki. Fikisha taarifa hizi kwa watu wengi kadri uwezavyo. Pia Jitahidi sana kuwahi ili usikose nafasi.! Ukipata ujumbe huu wajulishe wenzio

HUYU NDO MTOTO ASIYETAKIWA NA NDUGU ZAKE NA WANATAKA WAMUUWE!!


MTOTO aitwaye Mwajuma Haji (16) ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili anayesumbuliwa na  ugonjwa wa kusinyaa kwa viungo
yuko katika hali mbaya baada ya baadhi ya ndugu kudaiwa kutaka auawe ili kutoa uchuro katika familia.
Kwa mujibu wa mama mzazi wa mtoto huyo, Tatu Musa baadhi ya ndugu (siyo wote) wamekata tamaa ya kumuuguza mtoto huyo na kupendekeza heri mtoto huyo akatishwe maisha yake.
“Mwanangu haumwi wala hajawahi kuumwa ila ghafla alianza kusinyaa na kukosa nguvu, kinachoniuma baadhi ya ndugu zangu wamekata tamaa wanataka wamuue, waniachie mwanangu,” alisema mama huyo huku akilia mfululizo.
Mwandishi wetu amemshudia mtoto huyo akiwa amesinyaa viungo kiasi cha kutoweza kufanya kitu chochote zaidi ya kulala.
Mama mzazi wa mtoto huyo alisema kuwa alijifungua mtoto huyo akiwa na afya njema lakini alipofikisha umri wa miaka mitatu hali ikabadilika na viungo vyake kuanza kusinyaa.
Mama huyo amedai kwamba  kutokana na hali hiyo hakuweza tena kufanya shuguli za kumwingizia kipato zaidi ya kukaa na mwanaye kijijini kwao, Kiamange, Bagamayo mkoani Pwani bila ya kupata matibabu ya uhakika.
Alisema kwamba   maisha ya mtoto wake yameendelea kuwa mabaya bila ya kupata msaidizi kutokana kutengwa na baadhi ya ndugu zake waliokata tamaa ya kumuuguza.
Aidha, Mama Mwajuma amedai kwamba kuna wakati alikuwa akimfungia ndani mwanaye  kuanzia asubuhi ili aende kulima na kupata chochote, lakini aliporudi nyumbani alimkuta katika hali mbaya sana.
Kutokana na mazingira kuwa magumu, mama huyo alidai kwamba hakuwa na msaidizi wa kuweza kumwachia mwanaye  ili aweze kuhangaikia kipato.
Mbali na mtoto huyo, mama huyo alibahatika kupata mtoto mwingine ambaye sasa ana umri wa mwaka mmoja na nusu lakini baada ya kujifungua mwanaye mkubwa akatokwa na vidonda mgongoni

Mama mzazi wa Shaban Maulidi, Aziza Ramadhan.
WATU zaidi ya 10 wasiojulikana wakiwa na mapanga na nondo waliivamia familia ya mtoto aliyedaiwa kufufuka,
Shaban Maulidi kisha kuwajeruhi kwa silaha hizo watu saba, akiwemo mama mzazi wa mtoto huyo, Aziza Ramadhan, Uwazi lina kisa kamili.
Tukio hilo lilitokea usiku wa saa 9 Jumamosi iliyopita katika Kitongoji cha 14 Kambarage, Kata ya Kalangalala mjini Geita ambapo mama huyo na familia yake walikuwa wamelala ndani.
Inadaiwa watu hao kabla ya kufanya ukatili huo walizizingira nyumba za jirani pia na kuingia moja baada ya nyingine kwa kugonga milango kwa nguvu na kuwashambulia kwa mapanga na nondo wakazi wake huku wakiwalazimisha watoe pesa.
Maneno Sungura ambaye naye alijeruhiwa.

Habazi za ndani zinadai kuwa, watu hao walikuwa wakimtafuta Shaban ili wamuue ikiaminika kuwa, hatakiwi kuishi kwa sababu kifo chake kilikuwa cha kishirikina iweje afufuke, baada ya kumkosa ndipo walipoamua kumjeruhi mama yake kisha kuvamia nyumba za majirani wa familia hiyo wakijua mtoto huyo alifichwa humo.
Hata hivyo, kwa mujibu wa mama, baada ya mwanaye kuruhusiwa kutoka Hospitali ya Wilaya Geita alikolazwa aliondoka na baba yake na kwenda kufichwa sehemu ili kuepusha msongamano wa watu ambao wangefurika nyumbani hapo kumtazama.
Mtoto aliyedaiwa kufufuka, Shaban Maulidi.

Akisimulia jinsi watu hao walivyompora fedha, mwanamke huyo alisema:
“Wakiwa wameshanijeruhi sehemu mbalimbali kwa mapanga na nondo, wakataka hela. Nilikuwa na shilingi elfu kumi nimeifungia kwenye nguo, nikafungua nikawapa, chini ya kitanda nilikuwa na shilingi laki mbili nilizochangiwa na ndugu na jamaa waliokuwa wanakuja kumwona mwanangu hospitali, nazo wakachukua,” alisema Aziza.
Alipoulizwa kama tukio hilo linahusiana na kufufuka kwa mwanaye kama ilivyoenezwa na baadhi ya watu kwamba mtoto huyo hatakiwi kuishi, mama huyo alijibu:
Aziza Ramadhan akiwa na jeraha kichwani.

“Yawezekana maana waliniambia wametumwa kutuua mimi na mtoto wangu lakini wakasema endapo nina pesa niwapatie wasiniue. Kwa hiyo sijui kama lengo lao lilikuwa ni mtoto au la!”
Wengine waliojeruhiwa katika tukio hilo ni Maneno Sungura (36), Peter Kulwa (23) na  Doto Lucas ambaye umri wake haukujulikana mara moja.
Majirani Zachary Petro, Bahati Musa na Samuel Runguya licha ya kujeruhiwa, pia waliporwa zaidi ya Sh. 388,000 na simu moja ya mkononi yenye thamani ya Sh. 45,000. Majeruhi wote walikimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Geita kupatiwa matibabu na baadaye kuruhusiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, ACP Leonard Paulo alipotafutwa kwa njia ya simu na kuulizwa kuhusu tukio hilo hakukiri wala kukanusha kutokea na badala yake alisema: ”Niko sehemu mbaya sana,” akakata simu.


Source:GPL.

Kesi ya Kikatiba inayomkabili Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), inaanza kuunguruma leo katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam.
Kesi hiyo ilifunguliwa kwa ushirikiano wa Kituo cha Msaada wa Kisheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS).
Katika kesi hiyo namba 24 ya mwaka 2013, LHRC na TLS, wanadai kuwa Pinda alivunja katiba kwa kauli aliyoitoa Bungeni kuhusu polisi kuwapiga raia wanaokaidi amri.
Walalamikaji hao wanadai kuwa kauli hiyo ni amri kwa vyombo vya dola kutekeleza sheria ya kuwapiga wananchi, wakati wa vurugu.
Hata hivyo Pinda na AG katika majibu yao, wamewasilisha pingamizi la awali ambalo pamoja na mambo mengine wanadai kuwa walalamikaji na watu waliorodheshwa katika kesi hiyo, hawana mamlaka kisheria kufungua kesi hiyo.
Pingamizi hilo limepangwa kusikilizwa leo na jopo la majaji linaloongozwa na Jaji Kiongozi, Fakihi Jundu.

Mwananchi.
Tanzania yasaini mikataba mitano na ChinaSERIKALI ya Tanzania imesaini mikataba ya makubaliano  mitano na China ambayo itasadia kutoa fursa za biashara,mafunzo na masuala ya sayansi na teknolojia kwa Watanzania.
Mikataba hiyo imetiwa saini leo  mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri Mkuu wa China, Li Keqiang mara baada ya viongozi hao kufanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali jijini Beijing,China.
Mikataba hiyo ni ya Ushirikiano baina ya Tanzania na China kwenye masuala ya Sayansi na Teknolojia; Mkataba wa Kuruhusu bidhaa za baharini ziweze kuuzwa China na Mkataba wa Ushirikiano baina ya Tanzania na China kwenye masuala ya Utalii.
Mingine ni Mkataba wa Makubaliano baina ya Tanzania na China wa kuanzisha Ukanda wa Kisasa wa viwanda vya nguo pamoja na kukuza zao la pamba pamoja na mkataba wa kutoa vitalu namba 60 na 61 kwa ajili ya ujenzi wa ubalozi wa China jijini Dar es Salaam

Yep, all that used to be male. Her name is Amiyah Scott, but she was born ‘Arthur Scott’ in New York in 1988. She's a transgender model and make-up artist. Arthur started the process of turning into a woman when he was 17. He got breast augmentation, booty shots, light filler in the cheeks etc etc. See more photos of her/him after the cut... 
 
 Arthur Scott turns to Amiyah Scott 


Raia wawili wa Uingereza waliomwagiwa tindikali visiwani Zanzibar miezi mitatu iliyopita, wamepanga kurejea tena visiwani humo kuendelea na kazi za kujitolea ikiwemo kuwahudumia watu wasiojiweza. 

  
Raia hao wa Uingereza, Kirstie Trup na Katie Gee, hivi sasa wanaendelea kupata matibabu katika Hospitali za Chelsea na Westminster London na taarifa zinaeleza kuwa afya zao zimeimarika kwa kiwango cha kuridhisha.

Interview kuhusu africa tazama  alivyo wakilisha Tanzania na wasanii kadhaa wa bongo kwenye album hii iitwayo imagine africa,ni compilation ya jamaa wa mjini norway wakifahamika kama kirkelig 
kulturverksted na artwork kava imefanyika na mbongo mwenzetu,na ndani ya compilation hii ziliingia nyimbo mbili za Witness, moja ikiwa ni attention please iliyopata nomination chanel o music video awards 2010 na moja kwenye album yake iuzwayo mjini norway iitwayo khaya khaya na wimbo uliochaguliwa unaitwa umwe!

Posted: 17 Oct 2013 02:42 PM PDT
3TV star Kim Kardashian ambae ni baby mama wa rapper Kanye West ameingia tena kwenye headlines baada ya picha zake kusambaa akiwa ameziba tu sehemu ndogo ya mwili wake huku akiweka msisitizo kwenye instagram kwamba #Nofilter yani hajaongeza mbwembwe zozote za kiteknolojia kwenye muonekano wa picha.

Kanye West alipoiona hiyo post aliiRETWEET na kuandika ‘naelekea home now’ ambapo kwa fans walioziona picha hizi kila mmoja kaandika la kwake ila amepata lawama nyingi za kushindwa kujiheshimu na kutambua kwamba yeye ni Mama wa mtoto mmoja sasa hivi.


nayHabari mpya kutoka kwa msanii Ney wa Mitego ni kwamba hivi sasa amepata nomination mbili kwenye category mbili tofauti katika Nzumari awards.

Mwaka jana Diamond alishinda tuzo hizi na mwaka huu ni kwamba wimbo wa Ney utashindanishwa na nyimbo za wasanii wengine wa Africa Mashariki kwenye category ya wimbo bora wa Afrika Mashariki.
Ney amesema,”Nimepata nomination mbili, ya kwanza kwenye kipengele cha msanii bora wa kiume kutoka Tanzania ambapo tupo mimi,Diamond,Ommy Dimpoz na Rich Mavoko. Kipengele kingine ni wimbo bora wa Afrika mashariki ambapo nipo mimi na wimbo wa Muziki gani,Mobima wa P unit na Badilisha wa Jose Chameleone”
All the best kwenye category wimbo bora wa Afrika mashariki.
Exclusive: Dj Choka kuwapa Member wa B Hitz Music Group Dj Choka ambae anafanya project za Hip Hop kwa kuwaunganisha wasanii wenye uwezo mkubwa wa kurap na kuwaweka kwenye wimbo mmoja,amesema anampango wa kuwapa deal hiyo pia wasichana watatu wanaojua kurap vizuri lakini hawajatoka.
Dj Choka amesema kuwa ameona kwenye ngoma zake wanahitajika wasichana wengine wanaoweza kuchana, huku akipigia mstari uwezo wa wasichana hao(wawe wakali).
 “Nafikiria tena kufanya ngoma na wasichana wanaorap lakini wakali, yaani nataka nikipata wawili lakini wawe wanarap ile yenyewe yani, haijalishi Kiswahili au kiingereza. Unajua kwenye ngoma zangu mi naona namuweka tu Vanessa Mdee, unajua Vanessa anaimba lakini akija kwenye project yangu inabidi achane.” Amesema Dj Choka.
Kuhusu sifa na jinsi ya kuwapata wasichana hao, alifunguka, “nafikiria kufanya Ki-search kidogo hivi lakini ntawaambia kwa kuwa bado ni mapema, nataka kufanya search ndogo tu ili nipate wasichana kama watatu hivi ambao watakuwa wanarap,ntafanya search siku si nyingi tu halafu ntawapata hao, kwa hiyo wakae mkao wa kula .”
Dj Choka hivi sasa anapika project yake anayofanya na wasanii kadhaa wenye umri mdogo na tayari Young Dee, M-Rap, Janjaro na Country Boy wameshaweka vocal ndani ya studio za BHitz, lakini Dj amesema zipo project nyingine zitakazotangulia kutoka kabla ya project hiyo.
.
Mchungaji Mayanga (mwenye kipaza sauti) akitoa ushuhuda. 

Mwanaume aliyetambulishwa kwa jina la Mchungaji Mayanga amewashangaza waumini baada ya kudai kanisani kuwa yeye ndiye aliyewaua mastaa wawili Bongo, Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’ na
Steven Kanumba ‘The Great’.



Tukio hilo lilitokea Jumapili iliyopita ya Oktoba 13, mwaka huu, huko Mzambarauni, Mbagala-Charambe jijini Dar katika Kanisa la Powerful Gospel Ministry lilipo chini ya Mchungaji Meshak Punkanya ambapo Mayanga alipewa nafasi ya kutoa ushuhuda.
VIFO MILIONI 605
Mchungaji huyo alielezea kujuta kwake mbele ya kanisa kwa kudai kuwa kabla ya kuokoka alikuwa mchawi mkubwa aliyeishi kuzimu na kufanya kazi za mauaji sambamba na shetani mkuu (Lusifa) kwa kuwatumia vibaraka wake na majini.
Mchungaji Mayanga alikiri kutekeleza vifo vya watu wapatao milioni 605 wakiwemo waigizaji hao.

Steven Kanumba. 

WAMO FIVE STARS, MTOTO WA DANDU
Alisema kuwa kati ya watu aliowaua kwa njia za kishirikina wamo waimbaji wa Taarab wa Kundi la Five Stars wapatao 14, Kanumba, Sharo Milionea na mwanamuziki James Dandu ‘Mtoto wa Dandu’.
Pia alidai kuwa alihusika katika vita kati ya aliyekuwa Rais wa Iraq, Sadam Hussein na Marekani kwa kutumia pepo la uchonganishi alilolitaja kwa jina la ‘Magweju’.
Pia mchungaji huyo alidai kuhusika na shambulio la hivi karibuni la Al-Shabaab katika maduka ya Westgate la Nairobi nchini Kenya na matukio mengine mengi hadi kufikia idadi hiyo ya vifo vya watu milioni 605.

Hussein Ramadhan Mkiety ‘Sharo Milionea’. 

AWAONEA HURUMA WASANII, AWAONYA
Mchungaji huyo aliendelea kusimulia kuwa alipokuwa katika ulimwengu wa giza aliwahi kuwaonea huruma wasanii kama Kanumba, Sharo Milionea na Mtoto wa Dandu na kuwatokea kimiujiza akiwaonya waokoke kabla ya kuchukua roho zao huku mashabiki wao wakibaki na simanzi wakiamini kuwa vifo vyao ni vya kawaida.
Alidai kuwa baada ya kuwafuata mastaa hao na kuwaonya walikataa na badala yake akawaua.
Akiendelea kulishuhudia kanisa, Mchungaji Mayanga alisema kuwa kwa sasa ameokoka na kuachana na mambo ya giza, hivyo haogopi kuzungumza ukweli kwa kuwa roho wa Bwana anamuongoza kushuhudia kila kitu alichokifanya ili waumini watambue uwezo wa Mungu.

Gari la Sharo baada ya ajali.
ANA SIRI NZITO ZA VIGOGO
Huku akiomba hifadhi ya majina ya wahusika, mchungaji huyo alihitimisha ushuhuda wake kwa kudai kuwa ana siri nzito za vigogo au watu wakubwa ambao aliwahi kwa namna moja au nyingine kuwapa utajiri wa nguvu za giza.
UTABIRI
Hata hivyo, baadaye jamaa huyo alijitabiria kuwa atakamatwa na kufungwa siku moja kutokana na siri alizonazo.
“Yaani nina siri za watu wengi sana, nikiwaambia mtaogopa na nchi itatikisika. Najua siku moja watu watanikamata na kunifunga pingu kwa siri nilizonazo, lakini kamwe siogopi kwa kuwa Bwana ananiongoza,” alisema Mchungaji Mayanga.

Jeneza la Kanumba.


KANUMBA, SHARO MILIONEA
Kanumba alifariki dunia mwaka jana akiwa nyumbani kwake Sinza-Vatican, Dar huku Sharo Milionea akipoteza uhai kwenye ajali ya gari iliyotokea wilayani Muheza, Tanga wakati msanii huyo akienda kwao mkoani humo akitokea Dar.
Show ya TV ‘In my shoes’ ya mwigizaji Wema Sepetu kutoka bongo movie imeanza kuonyeshwa Eatv 
October 16 2013 ambapo Episode hii ya kwanza imeanza kwa kumuonyesha Wema kwanza akieleza yeye ni nani, anafanya nini, ni mtu wa aina gani na mengine kama hayo ambapo yafuatayo hapa chini ni maswali aliyoulizwa na kuyatolea majibu.

Swali: Wema ni nani?

Jibu: Wema Sepetu is a girl, i can say a Lady mwenye umri wa miaka 24 kutoka familia ya Isack Abraham Sepetu, a darling, a libra.. a girl who is very ambicious, i love my self…

Swali: Siku yako ya kwanza shuleni ilikuaje?

Wema: Siku ya kwanza tumeenda nikakutana na msichana flani hivi anaitwa Shubira nakumbuka mpaka leo, alikua rafiki yangu wa kwanza tulikutana shuleni nilikua na miaka minne… tumekaa nikaanza kulia kwa sababu ilikua sehemu mpya, mazingira mapya baada ya hapo tukazoea.

Shule ilikua vipi kipindi unasoma?

Wema: Naweza kusema kipindi ambacho niko shule, Mwalimu wangu sijawahi kukaa hata siku moja kumfikiria mara mbili na haijawahi kutokea kwamba hata mwalimu akaweza kufanya labda matamanio au kutaka kitu chochote, hamna kitu kama hicho

 Swali: Utafanya nini ikitokea umerudi shule?

Wema: Ningepata nafasi ya kurudi shule, academic nini uniform na nini… ningejaribu kuifanya more fun, a place where everybody can be just himself or herself and just be Wema Sepetu kwa sababu right now this is my time!!

Swali: Ni nani ambae uko karibu nae kwenye familia yenu?

Wema: Dada yangu wa kwanza kuzaliwa anaitwa Tunu, tunakwenda sawa kwenye many many ways, kipindi mama yangu alivyonizaa aliumwa akalazwa hivyo dada yangu ndio akawa ananihudumia kama mtoto wake, ananinywesha uji… anahakikisha nimekunywa maziwa on time na mpaka leo ananiita my baby and I call her my mami… mtu wa pili ni dada yangu wa tatu, she is my bestfriend… baba yangu atabaki kuwa baba yangu tu, mama yangu ni my gurdian Angel, my heart my darling.
Swali: Ulishawahi kugombana na ndugu zako?

Wema: Yeah nimegombana na dada yangu mpaka sasa hivi hatuongei, sio kitu chepesi….

Swali: Unaamini Mama yako ni mkorofi?

Wema: Linapokuja swala la mama yangu huwezi ukasema kwamba ni mkorofi lakini hapendi nikikosea wala kufanya kitu ambacho sicho…. kutokupenda kwake inafikia point anakua na hasira sana alafu njia ya kuonyesha hasira yake ndio level ya juu, yeye anafikiria kwamba anatengeneza ila badala ya kutengeneza ndio anaharibu.

Swali: Wema ni mkorofi?

Wema: Mimi sio mkorofi, mtu ambae hanijui ndio ataniita mkorofi ukishanijua yani tutafika mbali lakini usiponijua na hujui ninachonitaka ndio tatizo.

Swali: Unajisikiaje kuwa Wema Sepetu?

Wema: Kuwa Wema Sepetu sio kitu rahisi, haiwezi kuwa kama watu wanavyofikiria na haitakua hivyo kwa sababu ni maisha ambayo naishi, ni mpaka uone maisha ninayoishi ndio unielewe… yani hata kujaribu kuieleza ili uielewe napata tabu… mashabiki wangu wananielewa sana na uhusiano wangu na wao ni mzuri na ni tofauti na uhusiano kati yangu na familia yangu’

Swali: Unachukulia vipi unaposemwa ama kuandikwa vibaya?

Wema: Katika vitu vyangu ambavyo mtu wa nje anaweza kuviona kama vile… Mungu wangu Wema ana nini, mi navichukulia kama changamoto… mi naona kuna kitu special kuhusu mimi, kwa nini wasiseme watu wengine?

Swali: Unaamini wewe ni mrembo?

Wema: I am beautiful, naamini kwamba mimi ni beautiful kwa sababu nina pure heart… ni kitu Mwenyezi Mungu alichonibariki nacho.
STAA wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amekataa kabisa suala la kuolewa kwa sasa akidai moyo wake haupo tayari kwa tendo hilo.


Lulu alifunguka hayo Jumatatu iliyopita katika kipindi cha Mkasi kinachorushwa kupitia Runinga ya East Africa ambacho humpa nafasi staa kuzungumzia mambo mbalimbali yanayohusu maisha yake na sanaa kwa jumla.

Wakati mahojiano hayo yakiendelea, mmoja wa watangazaji wa kipindi hicho anayefahamika kwa jina la Muba, alimtupia Lulu swali ambalo lilimtaka aeleze utayari wake endapo mtu akijitokeza na kutaka kumuoa.

“Sitaki kuolewa kwa sasa, muda wa kuolewa haujafikia. Ukifika nitafanya hivyo lakini kwa sasa sipo tayari kuolewa,” alisema Lulu.
Aidha, Lulu alikiri kuwa licha ya kutokuwa tayari kuolewa lakini amekuwa akipata usumbufu mkubwa wa kutongozwa na wanaume. Aliainisha kuwa alikuwa akitongozwa kabla na baada ya kutoka Segerea alipokuwa akishikiliwa kwa kesi ya kifo cha aliyekuwa mpenzi wake, marehemu Steven Kanumba.
 “Watu wananitongoza sana, walikuwa wakifanya hivyo kabla hata sijaingia China (gerezani Segerea) na wameendelea kufanya hivyo hata baada ya kutoka,” alisema Lulu na kuongeza:
“Siwezi kuwakubalia sababu sipo tayari kuolewa kwa sasa…muda wa kufanya hivyo haujafika.”
Kuhusu suala la kudaiwa kutembea na bosi wa Kampuni ya Proin Promotion ambayo inamsimamia kisanii kwa sasa, Lulu aliruka viunzi na kudai taasisi hiyo inamlea kama mtoto wa familia na siyo vinginevyo.
Alisema hata madai yanayoelekezwa kwake kuwa Proin wamempa gari na nyumba kama sehemu ya kuhongwa na bosi wa kampuni hiyo, hayana ukweli wowote kwani yeye anafanya kazi kama msanii chini ya kampuni hiyo na hakuna kitu cha ziada.
“Hahahaha! Salama (mtangazaji) acha mambo yako bwana… mimi nipo chini ya Proin kwa sasa kwa kipindi flani ambacho nimesaini nao mkataba. Wananilea kama msanii wao, hakuna cha ziada,” alisema Lulu.

Akiendelea kubwabwaja maneno ndani ya kipindi hicho, Lulu aliweka wazi kuwa alikuwa akishindwa kuanika penzi lake na marehemu Kanumba kwa kuwa muda muafaka ulikuwa haujafika na kudai waliishi kama mtu na baba yake kabla hawajawa wapenzi, wakawa wapenzi na mauti yakamkuta Kanumba kabla hawajalianika penzi lao.

Solo Thang kuachia wimbo mpya Msafiri Kondo a.k.a Solo Thang yuko tayari kuhit radio waves hivi karibuni na ngoma mpya aliyomshirikisha Mr. Blue iliyopewa jina la ‘Mdudu’.
Mkali huyo wa michano ametumia akaunti yake ya twitter kuwapa fans wake taarifa za kutoka kwa ngoma yake hiyo.

Mwanzilishi wa Facebook Zuckerberg anunua nyumba zote za jirani zake,ni baada ya kusikia kuna mtu anataka kukaa karibu nae ili ajitangaze  Inawezekana mwanzilishi na C.E.O wa facebook Mark Zuckerberg anahitaji faragha ya aina yake au hatakiusumbufu wa jirani yeyote karibu nae, kwa kuwa ana pesa ya kutosha kufanya yake ameitumia kuwafukuza majirani zake katika eneo hilo, hasa aliposikia kuna mtu anataka kukaa karibu nae ili ajitangaze!
Ripoti zilizotelewa na gazeti la The San Jose Mercury News zimedai kuwa chanzo kimoja ambacho hakikutaka kutajwa kililiambia gazeti hilo kuwa Zuckerberg alisikia kuna mtu aliyetaka kununua sehemu ya eneo hilo kwa lengo la kukaa karibu nae ili baadae atangaze kuwa anaishi karibu na mmiliki wa mtandao wa kijamii wa facebook.
Hali iliyomfanya Zuckerberg kutoa $30 million na kununua eneo lenye nyumba nne zilizo karibu na nyumba yake iliyoko Palo aloto, Calfornia.

Steven asema kama Yanga itafungwa jumapili ijayo, atajinyongaSHABIKI wa Yanga, Steven Mwamwala amedai kuwa,kama wakifungwa na Simba mechi ya Jumapili ijayo itakayochezwa Uwanja wa Taifa, atajinyonga.
Mwamwala ana historia na Yanga ilipopigwa mabao 5-0 aliangua kilio cha nguvu na video zake kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.
Kauli ya shabiki huyo inakuwa mzigo kwa wachezaji wa Yanga kama, Athuman Idd ‘Chuji’, Kelvin Yondani, Mrundi Didier Kavumbagu na  Wanyarwanda Mbuyu Twite, Haruna Niyonzima ‘Fabregas’ kuhakikisha wanafanya vizuri na kuokoa maisha ya kijana huyo mwenye miaka 31.
Alisema “Nimeandaa kamba ya katani kabisa, nimeificha na siwezi kusema nilipoiweka kama Yanga itafungwa mchezo huo, nitajinyonga ili kupoteza uhai wangu. Unajua inauma sana mnapofungwa, nataka timu yangu ishinde Jumapili ili niwe na amani kwa ushindi wowote ule ilimradi tutoke na pointi tatu’Alisema Steven Mwambala.

 Mke wa mtayarishaji muziki Timberland, Monique ameripotiwa kuanzisha mchakato wa kuachana na producer huyu na hii ikiwa ni baada ya miaka 5 ya kuishi pamoja kama mke na mume.

Katika nyaraka za talaka ambazo amezifile mwanamama huyu, madai ya Monique baada ya kutengana na Timberland ambaye utajiri wake ni zaidi ya dola milioni 80, ni malipo ya gharama zote za malezi ya watoto pamoja na gharama za kesi hii ambayo amedai kuwa amemkopa rafiki yake pesa za kumlipa mwanasheria anayesimamia madai haya.
Kimbembe kikubwa katika madai ya Monique ni juu ya malezi ya moja ya watoto wake ambaye Timberland siye baba yake halisi, ambapo mama wa mtoto amedai kuwa ni jukumu la Timberland kumlea vile alishamkubali kama mtoto wake 
.