advert

http://

Friday 27 September 2013

HAWA NI WASANII 10 WA BONGO FLAVA WALIOINGIZA PESA NYINGI ZAIDI 2013.



1016243_622850427736775_2127148511_n
1. Diamond Platnumz
Hakuna ubishi kuwa, mwaka 2013 Diamond Platnumz ndiye msanii aliyeingiza fedha nyingi zaidi. Pesa nyingi ya Diamond imetokana na malipo ya show zake za ndani na nje ya nchi. Kwa uhakika, mwaka huu pekee, Diamond amefanikiwa kuingiza takriban shilingi bilioni 1.
Kwa show za ndani peke yake, Diamond hutoza si chini ya shilingi milioni 10 ama 15 na kila wiki hufanya show zaidi ya 2. Hivyo tangu mwaka uanze, Diamond amekuwa akiingiza shilingi milioni 40 kila wiki. Tour za nje alizofanya mwaka huu ni pamoja na zile za Uingereza ambako alifanya show kwenye miji mitatu, show ya Burundi na Congo, show mbili za Kenya (Nairobi na Mombasa), show ya nchini Comoro ambako alilipwa si chini ya dola 30,000 na show ya Malaysia wiki iliyopita.
Kwa upande wa show za hapa nyumbani ambazo ni nyingi mno zisizo na idadi, ukiachana na zile za kawaida, Diamond aliingiza shilingi milioni 40 kwenye show 4 za Kili Music Tour ambapo kila show alilipwa shilingi milioni 10. Ndiye msanii aliyelipwa fedha nyingi zaidi kwenye ziara hiyo.
Pia amefanya show kadhaa za Fiesta 2013, show za promotion za Tigo na makampuni mengine, Tamasha la Matumaini, show ya Tulizana Tuko Wangapi ya Leaders Club, show yake na Nay wa Mitego (Dar Live na Maisha Club). Mwezi February 16 mwaka huu, Diamond alifanya show jijini Arusha ambayo kiingilio chake kilikuwa ni shilingi 150,000 ndani ya Club Safari na ukumbi kufurika.
Miezi kadhaa iliyopita pia hitmaker huyo wa ‘Number 1’ ameshaalikiwa kwenye show corporate kuburudisha wafanyakazi wa benki na taasisi zingine pamoja na watu binafsi na zote hizo zimemuingizia fedha nyingi. Pamoja na show, Diamond amekuwa akiingiza fedha nyingi zaidi kwenye malipo ya ringtones ambapo kila baada ya miezi mitatu amekuwa akiingiza si chini ya shilingi milioni 20. Kwa mujibu wa Push Mobile, akaunti ya Diamond kwenye kampuni hiyo ndio inayoingiza fedha nyingi kuliko msanii mwingine yeyote wa Bongo Flava.
Mkataba exclusive alioingia na kampuni ya simu ya Vodacom kuuza wimbo wake mpya My Number One kama muito wa simu, umezidi kumpandisha juu na ikidaiwa kuwa mkataba huo ni wa mamilioni ya shilingi.
1239507_650218681669184_1372786191_n
Ikumbukwe pia, Diamond ni balozi wa Cocacola. Mkataba huo ambao haijajulikana umemuingizia shilingi ngapi, lakini ni fedha inayoweza kuwa si chini ya shilingi milioni 100.
584fe16a273711e3b8f522000a1fbce9_7
Diamond ni miongoni mwa wasanii wengine 23 wa Afrika akiwemo Lady Jaydee kwenye mradi mkubwa wa Cocacola wa Coke Studio Africa.
2. Lady Jaydee
1238789_10151593260760025_1742196233_n
Huwezi amini, vuguvugu la Anaconda limemsaidia Jaydee si tu kukusanya mashabiki wengi zaidi, bali pia limempa fedha nyingi mno. Zaidi ya tiketi 3,500 zilinunuliwa kwenye show yake ya mwezi June ya Miaka 13 ya Muziki na kuingiza takribani shilingi milioni 100. Haikuishia hapo, albam yake Nothing But The Truth ilinunuliwa kwa kiasi kikubwa na kumfanya kuwa msanii pekee wa Bongo Flava anayeendelea kufurahia mauzo ya albam zake.
Hits zake mbili, Joto Hasira na Yahaya kutoka kwenye albam yake hiyo, zimebadilisha maisha yake na kumfanya kuwa mwanamuziki mwenye show nyingi zaidi pia. Lady Jaydee ametumbuiza kwenye karibu show zote za Kili Music Tour ambako ameingiza shilingi milioni 25.
Mwaka huu pia Lady Jaydee amefanya show nyingi kubwa ikiwemo ile ya uzinduzi wa filamu ya Lulu, Foolish Age, show yake kwenye Miss Tanzania 2013, Family Day Show ya Arusha iliyofanyika Eid Pili, Anaconda Show iliyofanyika Triple A na nyingine iliyofanyika Snow View Hotel. Akiwa Arusha pia, Lady Jaydee aliuza kopi za albam yake kama njugu pamoja na tiketi za Anaconda zilizouzwa kwa shilingi 15,000 kila moja.
June mwaka huu pia, Lady Jaydee alitumbuiza kwenye semina ya kuwezesha wanawake kuondokana na njaa na umaskini, iliyofanyika chini ya mfuko wa fursa sawa kwa wote chini ya mama Anna Mkapa. Biashara yake ya Nyumbani Lounge, imeendelea kufanya vizuri pia kwa kupata wateja wengi wanaoenda kupata chakula, vinywaji na burudani kutoka kwa bendi yake ya Machozi.
Bado anaingiza fedha kupitia udhamini wa Airtel kwenye show yake ya TV ya Diary of Lady Jaydee. Msanii huyo ambaye jina lake ni Judith Wambura pia miongoni mwa wasanii 24 wa bara la Afrika waliochukuliwa kwenye mradi wa Coke Studio Africa wa kampuni ya Cocacola unaoendelea jijini Nairobi Kenya.
Coke Studio Africa – the new, exciting music show featuring incredible live performances by the very best in Africa
3. AY
421451_10150581514944221_264981067_n
Humsikii sana rapper huyu kwenye show za Tanzania. Tofauti na wasanii wengine, fedha anazoingiza AY zinatokana zaidi na endorsements na biashara zake anazofanya. Pesa nyingi alizoingiza zimetokana na mkataba wa mwaka mmoja na Airtel wa ubalozi uliokamilika mwezi May mwaka huu.
Katika ubalozi huo wa Airtel Africa, AY aliungana na wasanii wengine watatu wa Afrika ambao ni pamoja na Papa Wemba, Tuface na Daddy Owen wa Kenya. Katika mkataba huo AY alilipwa dola za Kimarekani 80,000 ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 129.
Rapper huyo wa ‘Machoni Kama Watu’ ni balozi pia wa bia ya Peroni ya Italia na kupitia mkataba huo, AY ameingiza mkwanja mwingi. AY pia ni mwanzilishi mwenza wa kipindi cha Mkasi kinachoendeshwa na Salama Jabir. Kipindi hicho kina wadhamini wawili, Cocacola na Airtel na hivyo kupitia mgawanyo wa mapato, AY amekuwa akiingiza pia fedha ya kutosha.
AY ni CEO wa kampuni ya Unity Entertainment inayojihusisha na kuandaa show, matangazo, kuleta wasanii wa nje na mambo mengine. Mwaka huu pekee, ikishirikiana na kampuni ya SK Entertainment, kampuni yake imeandaa show kibao zikiwemo zile zilizofanyika Elements Lounge ambapo Avril, Prezzo, Huddah Monroe na J-Martins wamewahi kuhudhuria.
Maisha ya kawaida ya rapper huyu ndio yanayowafanya watu wengi wasijue ukubwa wa kile anachokiingiza. Macho yake ameyaelekeza zaidi kwenye uwekezaji na anawekeza haswaa. Kuna tetesi kuwa, AY anajenga ghorofa lake maeneo ya Kigamboni jijini Dar es Salaam. Anasemekana kuwekeza pia mkoani Mtwara alikonunua ardhi ya kutosha. Mungu ndio anajua ni wapi alikowekeza tena.
4. Ommy Dimpoz
e23fe27c081911e3a88722000a1f90d0_7
Ommy Dimpoz ambaye kwa sasa yupo kwenye ziara ya muziki nchini Marekani ameingiza fedha zake nyingi kupitia show alizofanya. Ziara zake za Ulaya na Marekani pekee zimemuingizia dola 50,000 ambazo ni sawa shilingi milioni 81.
Tangu aachie wimbo wake mpya Tupogo, tayari Ommy ameshaingiza shilingi milioni 50. Kwenye show yake ya hivi karibuni ya Tupogo Night iliyofanyika Club Billicanas, Ommy alipeleka nyumbani shilingi milioni 10 baada ya kukata gharama zote. Watu 1,770 walihudhuria show hiyo.
Show yake ya Burundi ya mwanzoni mwa mwezi uliopita ilimuingizia staa huyo shilingi milioni 30. Ommy hutoza si chini ya shilingi milioni 7 kwa show na kwa mwezi, amekuwa na uhakika wa kufanya show tatu ama nne za ndani bila kusahau show za Kili Music Tour.
Hivi karibuni kwenye segment ya Tell it All ya Bongo5, Ommy alifunguka kuwa makampuni mengi yamekuwa yakimfuata kumpa endorsements lakini msimamo wake wa kutaka kulipwa fedha ya uhakika imemfanya azikatae nyingi lakini yupo mbioni kupata deal kubwa. Mpaka sasa Ommy anajenga nyumba mbili kwa mpigo zenye thamani ya shilingi milioni 250 hadi zilipofikia. Tayari ana viwanja vingine viwili anavyotaka kuangusha mijengo mingine. Hivi karibuni pia atakuja na clothing line yake ya PKP.
5. Madee
7203_294710874001268_1825630445_n
Hii inaweza kuwa surprise kwa wengi lakini Madee ni mfano tosha wa jinsi single moja inavyoweza kubadilisha maisha ya msanii. Tangu atoe single yake, Sio Mimi, Madee ameshaingiza si chini ya shilingi milioni 200.
Mwaka huu ameshafanya show 10 za kampeni ya Tigo ambapo kila moja alilipwa shilingi milioni 3, show 15 za Airtel kwa kiwango hicho hicho. Alifanya show mbili za kampeni za Coca Cola, ile ya uzinduzi wa Coke Zero na Cocacola Bonanza Mlimani City. Bado ameendelea kufanya show za Fiesta 2013. Madee pia alikuwa miongoni mwa wasanii waliotumbuiza kwenye show ya Fuse ODG iliyofanyika September 7 kwenye viwanya vya ustawi wa jamii jijini Dar es Salaam.
6. Mwana FA
IMG_1010 (800x534)
Mwanzoni mwa mwaka huu, Hamis Mwinjuma aka Mwana FA alikuwa msanii wa tatu miongoni mwa wasanii waliongiza fedha nyingi kupitia malipo ya miito ya simu, RBT ambapo aliingiza shilingi milioni 18. Alifanya show mbili kwenye Kili Music Tour ambapo aliingiza si chini ya shilingi milioni 7 pamoja na show kadhaa za Fiesta 2013.
Show yake ya The Finest ilimuingizia shilingi milioni 19. Hivi karibuni alichukuliwa na kampuni ya Vodacom kuzunguka baadhi ya mikoa kwenye kampeni yao na CCBRT kuhusiana na kukuza uelewa wa tatizo la Fistula na kulipwa mkwanja kama balozi wa kampeni hiyo.
Mwaka huu FA amefanya matangazo kadhaa ya Vodacom. Hivi karibuni pia aliingia kile kilichoonekana mkataba kama balozi wa simu za Samsung Galaxy Tanzania japo haijulikani kama ulikuwa mkataba wa ubalozi kama ilivyo mingine.
Mwana FA pia amefanya show za nje zikiwemo za Kenya na Afrika Kusini aliyofanya siku ya Eid mwezi uliopita. Kama wasanii wengine pia, FA ameingiza fedha nyingi kwa show za kawaida za hapa nyumbani na zile za promotion.
7. Chege
3ec62770206d11e382b622000ae912ed_7
Mwaka huu Chege peke yake alifanya show sita nje ya nchi ambazo kila show alilipwa shilingi milioni 4. Akiwa na Temba ambao kwa pamoja hutoza shilingi milioni 6, Chege amefanya show zaidi ya 30 zikiwemo zile za Fiesta, za promotion mbalimbali na zile za kawaida.
Mwezi ujao yeye na Temba wataanza tour ya miezi mitatu barani Ulaya ambapo show ya kwanza itakuwa nchini Sweden, October 5. Pamoja na hivyo, Chege ana biashara ya salon.
8. Profesa Jay
1010701_10151711560347558_1761716231_n
Profesa Jay aliingiza shilingi milioni 20 za Kili Music Tour, alifanya show kubwa ya Jose Chameleone April mwaka huu, show kibao za promotion za makampuni, show ya kampuni ya IPP kwaajili ya Walemavu, Diamond Jubilee mwezi January, na show zingine za kawaida za Dar na mikoani. Pia nguli huyo wa rap ya Tanzania ameingiza fedha nyingi kupitia show nyingi za Lady Jaydee.
Prof J amewekeza kwenye biashara ya salon ambayo tayari inafanya vizuri na ameshafungua studio ya kurekodi muziki iliyopo kwenye hatua za mwisho kuanza kazi. Jize aliingiza pia fedha kupitia kampeni ya magazeti ya Mwananchi kwa kufanya matangazo na show za mikoani.
9. Nay wa Mitego
53c24b9c156c11e3959e22000aeb1b4e_7
Tangu mwaka uanze, Nay wa Mitego ameshafanya show zaidi 20 zilizomuingizia si chini ya shilingi milioni 60. Show hizo ni pamoja na zile za promotion za makampuni ya simu, show mbili za Muziki Gani, show ya Kili Music Tour, show za Fiesta na zile za kawaida. Pia ana biashara zake ambazo kwa pamoja humuingizia si chini ya shilingi milioni 4 kwa mwezi.
10. Temba
2648cdb8274f11e3a2f822000a1f985f_7
Fedha nyingi alizoingiza Temba mwaka huu zimetokana na show walizofanya pamoja na Chege. Ukitoa muziki, Temba pia ni mfanyabiashara na anamiliki duka la vifaa vya ujenzi.

Source:Bongo5.com

Picha za nje ya jengo la Westgate hazioneshi uhalisia wa hali iliyoko ndani ya jengo baada ya shambulio la kigaidi Jumamosi iliyopita jijini Nairobi, Kenya na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 70.

a7
Picha hizi zinatoa picha halisi ya jinsi jengo hilo lilivyoharibika vibaya kwa ndani baada ya ghorofa tatu za jengo hilo kudondoka baada ya kupigwa mabomu katika mchakato wa kukabiliana na magaidi. 
a6
Picha hizi pia zinaonesha jinsi magari yaliokuwepo eneo la maegesho ya magari katika jengo hilo yakiwa yameharibiwa kiasi kwamba kuna mengine ambayo huenda hata wamiliki wanaweza kushindwa kuyatambua.
a1
a2
a3
a4
a5
a8






Abdul Haji ni miongoni mwa mashujaa ambao hawatasahaulika nchini Kenya kutokana na kuamua kuhatarisha maisha yao ili kuokoa watu waliokuwa wamekwama ndani ya jengo la Westagate baada ya kushambuliwa na Al-Shabaab Jumamosi iliyopita.


Tangu asimulie namna alivyopambana na magaidi hao, Haji ametokea kuwa kipenzi cha watu wengi hasa wasichana na mmoja wa watu aliowagusa ni Rehema Chalamila ambaye amesema anatamani mwanaume mjasiri kama yeye ambaye watazaa naye watoto.

“In love with ths Soldier!i want a soldier like him to marry me,” ameandika Ray C kwenye picha ya gazeti aliyoipost kwenye Instagram ikimuonesha Abdul Haji.

“I love You Abdul Haji,You are my Heroooooooo,” aliandika Ray C kwenye picha nyingine.

Kwenye picha nyingine Ray C aliongeza, “My soldier,My Prince,My Love….Love You Abdul Haji.”

Kijana huyo ni mtoto wa waziri wa zamani wa ulinzi nchini Kenya ambaye alienda kwenye mall hiyo baada ya kupata ujumbe kutoka kwa rafiki yake kuwa kaka yake alikuwa ndani ya Westgate wakati watu hao wenye silaha walipovamia.

Akiongea na NTV, Haji ambaye sio mwanajeshi, alisema alifundishwa kutumia bunduki na baba yake ili kulinda mifugo yao isiibiwe na wezi.


Ujuzi huo ulimsaidia Jumamosi hiyo kuwasaidia wafanyakazi wa Red Cross wafanye kazi yao kwa usalama kwa saa tatu na kusaidia kuokolewa kwa watu wafikao 1,000 nje ya mall hiyo.

Binti wa umri wa miaka 15 tunayemtambulisha kwa jina moja tu la Zaina, mkazi wa Kimara jijini Dar ameamua kufunguka na kusimulia jinsi alivyokuwa akibakwa na baba yake mzazi aliyemtaja kwa jina moja la Mohamed.

  
ANAANZA KWA KUANIKA HISTORIA YAKE FUPI!
Akisimulia kwa uchungu, Zaina alianza kwa kuanika historia yake kwa ufupi kwamba tangu atoke tumboni, hakuwahi kumuona mama yake zaidi ya kuoneshwa kwenye picha tu!

Akasema hiyo yote ilitokana na hadithi aliyowahi kusimuliwa kwamba, akiwa kichanga, baba huyo alimuiba kwa mama yake anayeishi Kigamboni, Dar na kwenda kumlea Kimara kwa ushirikiano na mama yake wa kufikia.
  
Lakini akasema: Hata huyo mama wa kambo mwaka jana aliachana na baba baada ya kutufumania chumbani mimi na baba, akakasirika na kuondoka zake.

SIKIA FILAMU KAMILI SASA
“Nakumbuka ilikuwa mwanzoni mwa mwaka jana, nikiwa darasa la tano katika Shule ya Msingi Kimara ndipo baba alipoanza tabia ya kunilazimisha tufanye mapenzi. Alisema anataka tufanye kwa njia ya kawaida na ya kinyume na maumbile.

“Nilikataa lakini akawa ananilazimisha na vitisho juu. Tulianza kwa kufanya mchezo huo na baba lakini si kwa kupenda kwangu, nililazimika kwa sababu niliamini ni baba ambaye anaweza kunifanya lolote kama nitakataa, mbaya zaidi hakuwa akitumia kinga,” alisema na kuongeza:

“Kuanzia hapo, zoezi hilo liliendelea kila siku hadi mwishoni mwa mwaka jana nilipoamua kutoroka na kwenda kuwaeleza ndugu wa baba, kule Tanga.” 

Binti huyo alikwenda mbele zaidi kwa kusema kuwa,  kilichomsukuma kutoroka ni mateso, ukatili na udhalilishwaji uliopitiliza kwani baba yake wakati akimwingilia alikuwa akimkaba kooni ili asipige kelele.

“Yeye alijua anafanya kosa, akawa akiniingilia huku ananikaba koo nisipige kelele. Nilikuwa nasikia maumivu makali balaa,” alisema binti huyo.

ALIWAAMBIA MAJIRANI LAKINI WALIOGOPA KUMVAA BABAKE
“Kingine kilichonifanya nitorokee Tanga kuwaambia ndugu zake ni kwamba, niliwahi kuwaambia majirani kuhusu mchezo wa baba lakini hakuna aliyethubutu kumuuliza kwa vile wanamuogopa,” alisema.

MAMA MZAA BABA AAMBIWA KILA KITU
Zaina alizidi kusema kuwa, baada ya kufika Tanga  alimweleza kila kitu bibi yake (mama mzaa baba’ke). 

Bibi huyo kwa sababu ni mzazi alimwita mwanaye na kumkanya kisha akafanyiwa mambo ya kimila ili kuondoa balaa hilo la baba mtu kutembea na mwanaye wa kumzaa la sivyo kwa mila za kwao ukoo mzima ungesambaratika.

BABA MTU AONDOKA TANGA USO UMEMSHUKA, YEYE AGOMA
“Baada kufanyiwa mambo ya mila, baba aliniambia turudi Dar lakini nilikataa kwa sababu niliamini tutakapofika bado atataka kuniingilia tena. Nasema hivyo kwa sababu pia baba amewahi kufanya mapenzi na dada’angu anaitwa Hamida mpaka akampa mimba.

“Huo ukatili wote alikuwa akitufanyia kwa nyakati tofauti tofauti, dada alipopata mimba siku moja alimwibia fedha ili akaitoe, alifanikiwa na akakimbia nyumbani, sijui alipo,” alisema.

Akaendelea: Basi, niliamua kubaki kwa bibi, lakini kuna siku alikuja mtu aliyekuwa anatafuta msichana wa kazi ‘hausigeli’, mimi nikakubali, nikaenda Moshi ambako nilikaa kwa muda.
Inatoka Uk. 2

“Hivi karibuni nilirudi Dar na kufikia kwa jirani, sikutaka kwenda nyumbani kwa baba, namuogopa atataka tena. Huyu jirani niliyefikia kwake, mtoto wake ni rafiki yangu tulikuwa tunasoma naye. Hapa nilipo natafuta msaada wa kumpata mama yangu mzazi. Kama atabahatika kulisoma gazeti hili namuomba anifuate jirani na kwa baba atanipata,” alisema Zainab.

Zainab hakuishia kwenye kufikia kwa jirani tu, anasema akiwa hapo jirani huyo kesho yake alimpeleka serikali za mitaa ili kutoa taarifa kuwa amerudi kwa vile alitafutwa kwa muda mrefu kwenye shule aliyokuwa akisoma.

MWENYEKITI WA MTAA AKIRI ZAINAB KUBAKWA NA BABA’KE
Naye mwenyekiti wa mtaa wa eneo hilo, Demetrius alikiri kumpokea mtoto huyo na kumsimulia yote kuhusu baba yake ambapo aliambatana naye hadi Kituo cha Polisi Mbezi kwa Yusuf kwa lengo la kutoa taarifa ili mzee huyo achukuliwe hatua za kisheria. Alisema binti huyo alifunguliwa jalada la kesi KMR/RB/114/2013  UCHUNGUZI.

BABA ANASEMAJE?
Baada ya kumalizana na binti huyo aliyeungwa mkono na mwenyekiti huyo, mapaparazi wetu walizungumza na baba mtuhumiwa ambapo alikuwa na haya ya kusema:

“Si kweli, huyo mtoto ananisingizia tu, mimi siwezi kufanya kitu kama hicho na binti yangu wa kumzaa hata siku moja.


-Gazeti  la Ijumaa  via  GPL


Huu wimbo hatari tupu.Inaelezea maisha ya Diamond kabla hajatoka kimuziki.Dogo aloimba anadai Diamond ni ndugu yake wa damu na hakumbuki alipotoka.Duuh kaongea mambo mengi sana.Sina mbavu kwa kweli.Isikilize hapa Chini.Ni balaa tupu.Ni bonge moja la Ngoma.

Polisi wa kimataifa Interpol, wamemuweka mwanamke aliyeshukiwa kuongoza mashabulizi ya kigaidi nchini Kenya raia Muingereza Samantha Lewthwaite, kwenye orodha ya watu wanaosakwa sana duniani.


Hatua hii ni kutokana na ombi la serikali ya Kenya kwa Interpol.

Anajulikana kama "white widow", na amehusishwa na kundi la kigaidi la Al Shabaab nchini Somalia.Bi Lewthwaite, mwenye umri wa miaka 29, ni mjane wa mlipuaji aliyefanya shambulizi la kujitoa mhanga mjini London Uingereza mwezi Julai mwaka 2005
Polisi wa Interpol hata hivyo hawakuhusisha hatua ya kumsaka Samantha na shambulizi la kigaidi dhidi ya jumba la maduka la Westgate mjini Nairobi lililowaua watu 67.
Hata hivyo, hatua hii ya kumsaka Bi Lewthwaite inakuja punde baada ya shambulizi hili la kigaidi nchini Kenya.
Al-Shabab ilikiri kufanya mashambulizi hayo yaliyotokana na kutekwa kwa jengo la Westgate na kisha kutekwa kwa raia wa kawaida waliokuwa ndani ya jengo hilo kwa siku nne.
Kwa mujibu wa polisi wa Interpol, mwanamke huyo anasakwa na serikali ya Kenya kwa kumiliki mabomu na kupanga njama ya kufanya mashambulizi kuanzia Disemba mwaka 2011.
Ikiwa mwanamke huyo atakamatwa katika nchi mwanachama wa Interpol, atazuiliwa na kusibiri kupelekwa katika nchi anayotakikana kwa kesi kufunguliwa dhidi yake.
Bi Lewthwaite anajulikana kwa jina bandia la, "Natalie Webb" –na alikuwa anasakwa kwa madai ya kumiliki hati bandia ya usafiri nchini Afrika Kusini.
Ni mjane wa Germaine Lindsay, mmoja wa washambuliaji wanne waliohusika na shambulizi la kigaidi mjini London ambapo watu 52 waliuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa.
Msanii wa kizazi kipya nchini Tunisia, Ahmed Ben Ahmed, anayejulikana kwa jina la kiusanii, Klay BBJ, amehukumiwa 
jela kwa miezi sita kwa kuwatusi maafisa wakuu kupitia
 kwa muziki wake.
Mahakama ilitupilia mbali kesi yake ya rufaa baada ya yeye na mwanamuziki mwenzake kupatikana na hatia mwezi jana ya kuwatusi maafisa wakuu katika tamasha la muziki eneo la Hammamet.
Wawili hao awali walihukumiwa bila ya wao kuwepo mahakamani kutumikia kifungo cha miezi 21 lakini hukumu hiyo iliondolewa.
Weld El 15, aliyepatikana na kosa kwa kuimba wimbo wake huo, kuwa 'Polisi ni Mbwa', hakukata rufaa na sasa yuko mbioni.
Hata hivyo Kaly BBJ lisema kuwa wimbo wao ulikuwa unaelezea hali ilivyo nchini Tunisia na kuhusu serikali.
Muungano wa vyama unaoongozwa na chama cha wanasiasa waisilamu wenye msimamo wa kadri, Ennahda, uliingia mamlakani baada ya mapinduzi ya kiraia yaliyomwondoa mamlakani aliyekuwa rais Zine el-Abidine Ben Ali mwezi Januari mwaka 2011 na uchaguzi kufanyika baadaye mwaka huo.
Klay anasemekana kuambia mahakama kuwa wimbo wao unakosoa hali ya sasa serikalini na kote nchini Tunisia tu.
Alisema yeye ni mmoja wa wanamuziki wanaokosoa sana serikali na ndio maana wamekuwa wakimsaka sana.
Lakini majaji walikataa rufaa aliyowasilisa na kusema hukumu yake ya miezi sita gerezani inastahili kuanza mara moja.

Wakili wake alisema kuwa watawasilisha rufaa nyingine kupinga hukumu dhidi yake.