advert

http://

Tuesday 19 November 2013

Hotel hii ya kipekee iliyo visiwani Zanzibar yawa gumzo Duniani.



Hotel hii ya kipekee iliyo visiwani Zanzibar yawa gumzo kwenye Vyombo vya Habari vya Kimataifa.


- Ina vyumba chini ya maji
- Bei ya kulala kwa siku ni $900 single na a$1,500 double

Katika vitu naona kuna makosa makubwa yanafanyika ni hili kawaida naona Baadhi ya wanaume hupata shida sana ya kuishi na wapenzi 
wao kwa mda mrefu na pengine kuona anamchoka mpenzi wake mapema mpaka anakuwa na mahusiano ya kukusudiwa na wala siya bahati mbaya!Lakini Wanaume wenzangu nawakumbusha hili huwa tunapotea kwakushindwa kuzingatia haya!
Mpenzi wako unatakiwa umthamini umuone kuwa niyule yule wawakati unamtongoza!!Siyo umeisha mkula unamtema hapana!
Pili ukiona mwanamke anaumbozuri mwone wakawaida!
Ukimuona wamwenziyo anapendeza na wewe wakwako mpendezeshe kwa value ile ile!
Hakikisha safari zako zakutoka unakuwa naye hata kama anasafari zingine mwambie mama hairisha twende huku nahitaji kampani yako!
Umwambie kitu gani unahitaji na usichokihitaji nasikuzote akikukosea jaribu kuongea naye taratibu na kama yamekuzidi jitahidi ukifika nyumbani kula,oga ukiingia kitandani mwulize "Mpenzi leo umenikosea sijapenda je wewe hili ukuliona??"
Usipende kumtegemea katika Budget zako atakuchoka!


Sasa kwa akina Dada..

Dada inatakiwa kujua Mpenzi wako ni waina gani!
Unatakiwa kujua yeye kipato chake kikoje!
Unatakiwa umjue mpenzi wako kampani yake ni yawatu wa aina gani!
Unatakiwa kumuona mpenzi wako ni Someone very special na hafanani na mpenzi wa Clara!
Napale anapokugombeza pale ulipo mkosea jaribu kujishusha na kumsikiliza kwa makini na kumuomba je na mimi naweza kuongea??Umsikie ansemaje!
Kamwe usije ukamwambia hivi wewe ukoje uoni Mpenzi wa fulani yuko msikivu!hivyo basi utakuwa umemkwaza kwani inaonyesha unakuwa unampenda yule wamwenziyo kuliko uliyenaye!
Mpenzi wako upende kujivunia naye mbele ya marafiki zako wawe wamtaani wawe wamaofisin hata vyuoni!
Usije ukamwambia kwanini uvai kama fulani!kama uridhishwi na kuvaa kwake na unajua anapesa basi tafuta mda mwende shopingi mchagulie wewe uone akivaa chaguo lako anaonekana vipi!

Katika haya niliyoyasea haya ni baadhi ya mambo unayoweza kuyafanya na kumfanya mpenzi wako akawa kama unavyotaka!Wewe ndiye mwenye kumbadili mpenzi wako!


Credit:Udakuspecially.

Show ya rapper wa Kenya, Cannibal mjini Dubai yabuma,atumbuiza mbele ya vitiShow iliyokuwa ikiongelewa sana ya rapper wa Mombasa, Kenya, Cannibal Shattah mjini Dubai imebuma vibaya.
Mahudhurio yalikuwa hafifu kiasi cha waandaji kula hasara na kushindwa kurudisha gharama walizotumia.
Cannibal alidaiwa kushikiliwa kwenye hoteli aliyokuwa amefikia kwa kushindwa kulipa gharama na meneja wake aitwaye Waziri aliambulia kichapo kutoka kwa Wakenya waiishio Dubai na kujeruhiwa usoni.
Cannibal alitumbuiza kwenye ukumbi wa at RockCity Club uliopo kwenye hoteli ya  Howard Johnson, mjini Dubai, November 8.



Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa risasi na mzazi mwenzake, Anthery Mushi, amefanya ibada na kusema: “Namshukuru Mungu kwa kuniponya.”


Ni mara ya kwanza Saro kuzungumza tukio hilo tangu aliporuhusiwa kutoka Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu, MOI ya Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa.

Katika ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la Kilutheli Tanzania (KKKT) Usharika wa Kibamba, Jimbo la Magharibi, Ufoo huku akitokwa na machozi na wakati mwingine kushindwa kuzungumza alisema: “Ni miujiza tu ya Mungu yeye kunifanya mimi kuwa hai leo.”

Mtangazaji huyo ambaye alilazwa kwa zaidi ya wiki mbili, aliwashukuru watu wote waliomtia moyo, kumsaidia kipindi chote alichokuwa mgonjwa.

“Sina cha kuwalipa, ninawashukuru sana kwa wema wenu, pia kwa kuniombea. Mungu ni mkubwa na amenipigania, naendelea vizuri kwa sasa,” alisema na kuongeza:

“Mungu alinisimamia na nyinyi pia mliniombea, hakika sina budi kushukuru kwa kila jambo. Nitasoma zaburi ya 146 katika Biblia Takatifu ili kumshukuru Mungu kwa kunisaidia.”

Ufoo alisema kuwa ameamua kumshukuru Mungu kwa sababu siyo watu wote wanaopata matatizo kama yake wanapona.

Mchungaji aliyeongoza misa hiyo iliyoanza saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana, Joseph Maseghe alisema Mungu hakupanga Ufoo afariki dunia kwa kupigwa risasi.

“Mungu bado anakuhitaji, hakupanga ndiyo maana upo nasi leo. Hautakiwi kulia huu ni mwanzo wa maisha yako mengine, usilie unachotakiwa ni kumshukuru Mungu kwa kila jambo,” alisema.

Misa hiyo ilihudhuliwa na watu mbalimbali wakiwamo wafanyakazi wa ITV pamoja na Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Grace Kihwelu, Mwenyekiti wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), John Heche.

Baada ya kumalizika kwa misa hiyo, ndugu na marafiki wa karibu wa Ufoo walialikwa na mtangazaji huyo katika hafla fupi ya chakula cha mchana.

Akizungumza wakati akiwakaribisha wageni katika chakula cha mchana, alisema: “Nimepata pigo kubwa katika maisha yangu, familia yetu sasa haina baba wala mama, kweli namshukuru Mungu na nawaombea kwa Mungu wote walioniombea na kunitakia mema, sijui nimpe nini Mungu, sijui kwa kweli.”


Credit-Mwananchi.

Bilionea reginald mengi ameandika twitter jana kuwa kama tunalitakia amani hili taifa basi ni lazima watu flani wapelekwe milembe kwa nguvu na sio kwa hiari yao.

Je,unadhani mengi anataka watu gani wapelekwe milembe na kwa sababu gani?? 


Credit:Udakuspecially.

Akifunguka kikamilifu kuhusiana na ‘saga’ hilo, kwa sauti imara bila wasiwasi, Kapuya alisema kuwa anamjua mwanafunzi husika, kisha akasema:
“Kuna watu wanamtumia. Hili suala limetengenezwa ili kuniharibia malengo yangu.”


ACHAMBUA UTAPELI WA MWANAFUNZI
KESI A; Mwanafunzi aliyedai kubakwa, alinukuliwa mitandaoni akisema kuwa yeye ni mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Turiani, Magomeni, Dar es Salaam.
Kapuya anapangua: “Huyo muongo, alinifuata kuniomba ada ya chuo. Aliniambia anasoma Chuo Kikuu cha Tumaini.”
KESI B; Mwanafunzi huyo alisema anasoma kidato cha tatu na alibakwa mara mbili na mheshimiwa huyo.
Kapuya anajibu: “Achilia mbali yeye, mimi sijawahi kubaka katika maisha yangu yote. Kuhusu kidato cha tatu, yeye mwenyewe aliniambia anasoma Tumaini University na aliomba nimlipie ada ya miaka miwili ambayo ni shilingi 3,000,000.
“Kwa mara ya kwanza nilimpa shilingi 2,300,000 na baadaye nilimpa shilingi 700,000. Kipindi hicho nilikuwa sijagundua kama ni tapeli, ila baadaye nilipogundua utapeli wake, nilihakikisha hanisogelei. Hapa nawajua watu wengi aliowatapeli.”
Kuthibitisha anachokisema, Kapuya alitaja jina la mkurugenzi wa benki moja nchini (jina tunalihifadhi) kuwa alishalizwa na mwanafunzi huyo.
KESI C; Denti huyo alidai ana umri wa miaka 16.
Hilo nalo Kapuya analipangua hivi: “Hata mimi mwanzoni aliponifuata nilijua ni binti mdogo, yatima anayehitaji msaada lakini ukweli ni kwamba yule ni mama mzima na ana mtoto. Ameshazaa yule.
“Hasomi popote, Mungu amemsaidia kuwa na umbile dogo ambalo analitumia kuwatapeli watu kwamba ana umri wa miaka 16, ni tapeli mkubwa, tena wa kuogopwa kabisa.”
KESI D; Mwanafunzi mwenyewe alidai kuambukizwa Ukimwi na kiongozi huyo aliyewahi kuongoza wizara mbalimbali nchini.
Kuhusu hilo, Kapuya alicheka kidogo halafu akajibu: “Sina Ukimwi, afya yangu ipo imara sana. Kama yeye ana Ukimwi, basi aseme mahali alipoutoa, siyo kusema uongo na kutaka kunichafua mbele ya jamii ambayo inaniheshimu.”
KESI E; Denti amedai kutumiwa SMS za vitisho kwamba mheshimiwa huyo amedai atamuua.
Hivi ndivyo Kapuya anavyojibu: “Sijawahi kutuma SMS za vitisho. Unajua haya mambo nashangaa sana, nipo huku kijijini Kaliua, kwa hiyo mambo mengi nafanya kuambiwa kwa sababu sipati magazeti kwa wakati.
“Nina laini tatu, Tigo, Airtel na Vodacom, hata siku moja sijawahi kutuma SMS ya kumtishia mtu kumuua. Hao wanaomuamini, waendelee kumuamini huyo tapeli lakini lazima nimfikishe kwenye vyombo vya sheria.”
KESI F; Yapo madai kuwa Kapuya alitishia kujiua baada ya kugundua ameshikwa pabaya na denti huyo.
Hilo nalo Kapuya alilijibu hivi: “Nimesema sijatuma SMS yoyote, wala siwezi kutishia kujiua. Nitishie kujiua kwa lipi?”
KESI H; Miongoni mwa madai yaliyotajwa ni kwamba Kapuya anajindaa kuwa waziri mkuu baada ya Uchaguzi Mkuu 2015.
Kuhusu hili, Kapuya alicheka akasema: “Nilimwalika Lowassa (Edward) jimboni kwangu. Akiwa huku na maeneo mengine ya Mkoa wa Tabora, wananchi walisema mimi ndiye nitakuwa waziri mkuu wake.
“Yalikuwa ni maneno tu na mimi nilianza kuyasikia kipindi hicho. Kwa hiyo sijawahi kutamka popote kuwa mimi najiandaa kuwa waziri mkuu.”
MTAZAMO WAKE
Pamoja na kupangua madai yote hayo, Kapuya aliongeza kuwa yapo makundi mawili ambayo anayahisi kuwa ndiyo yapo nyuma ya denti huyo ambaye yeye amemwita ni mama mtu mzima.
Alisema: “Kuna majambazi fulani alikuwa anawatumia kunishawishi niwape pesa, baadaye waligombana. Wale majambazi walimwambia watamuua ikiwa yeye ataniendekeza.
“Nahisi hao ndiyo yupo nao kundi moja kuhakikisha wananichafua baada ya mimi kugundua uhuni wao ambao walikuwa wananifanyia. Nitakapoanza kuwashughulikia kisheria, itajulikana tu nani na nani anahusika nyuma yake.”
Aidha, Kapuya alimtaja mwanasiasa mmoja mwandamizi nchini (jina tunalo), mwenye asili ya Mkoa wa Tabora, mwanachama wa CCM kuwa anamhisi yupo ndani ya mkakati huo wa kumchafua.
“Ni hivi, … (anataja jina la mwanasiasa huyo), ameshapandikiza vijana wawili ili waniangushe kwenye Uchaguzi Mkuu 2015. Hao vijana wametengeneza tovuti ambayo imekuwa ikinichafua sana.”
MADAI YA MSINGI
Mwanafunzi huyo ambaye Kapuya amemwita ni mama mwenye mtoto, aliripotiwa na mitandao mbalimbali ya kijamii akidai kubakwa kisha kuambukizwa Ukimwi na kiongozi huyo.
Katika madai yake, mwanafunzi huyo alisema kwamba zahama hiyo ilimpata baada ya kwenda kwa Kapuya kuomba msaada wa ada ya shule ndipo kiongozi huyo alimgeuzia kibao.

chanzo:globalpublishers

No comments: