advert

http://

Friday 6 December 2013

Viongozi wa kiafrika wamlilia Madiba


Viongozi mbali mbali barani Afrika nao wametoa rambi rambi zao na kumwelezea Nelson Mandela kama mfano mwema kwao, wakisema pengo lake haliwezi kuzibwa kirahisi.
Marehemu Nelson Mandela
Marehemu Nelson Mandela
Rais wa Halmashauri ya Umoja wa Afrika Dr Dramini Nkosazana Zuma amesema kifo cha Nelson Mandela ni pigo si kwa Afrika Kusini na Afrika tu, bali kwa jamii nzima ya binadamu.
Bi Zuma amesema kuwa Mandela alikuwa alama ya mshikamano katika mapambano ya umma dhidi ya utawala dhalimu wa ubaguzi wa rangi, unyanyasaji na ukoloni, na kuitolea wito Afrika wa kukumbatia yale aliyoyathamini.
Rais wa Halmashauri kuu ya AU, Nkosazana Dlamini Zuma
Rais wa Halmashauri kuu ya AU, Nkosazana Dlamini Zuma
Nchini Tanzania siku tatu za maombolezo zimetangazwa kuomboleza kifo cha Nelson Mandela. Rais wa Tanzania Nelson Mandela amemtaja marehemu Mandela kuwa sauti ya ushujaa na chanzo cha hamasa, na kuongeza kuwa ni kipenzi cha watu aliyetoa mfano mwema.
Katika nchi jirani ya Kenya, rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyata amesema Mandela alikuwa kiongozi alitoa matumaini na mwenye kutoa msukumo wa maridhiano. Kenyatta amesema maisha ya Mandela yanatoa somo muhimu kuwa nguvu ya dhamira inaweza kuugeuza uhasama kuwa ushindi.
Rais wa Rwanda Paul Kagame amesema ingawa Mandela ameaga dunia ataendelea kuishi mioyoni mwa wapenzi wake kwa muda mrefu. Nchini Nigeria, rais wa nchi hiyo Goodluck Jonathan amesema Mandela alitoa matumaini kwa wanyonge wanaonyanyasika kote ulimwenguni, na kuongeza kuwa itakuwa vigumu kuliziba pengo lililoachwa na shujaa huyo.
Goodluck Jonathan, rais wa Nigeria
Goodluck Jonathan, rais wa Nigeria
Askofu mkuu wa zamani wa kanisa la Kianglikana nchini Afrika Kusini Desmond Tutu ambaye amehutubia umati wa waumini waliohudhuria ibada maalumu ya kumkumbuka Mandela, amesema Afrika Kusini imefiwa na baba, na kusema zawadi nzuri ambayo nchi hiyo yaweza kumpa Mandela, ni kujenga jamii iliyoungana.
Mtangulizi wa Nelson Mandela kwenye wadhfa wa urais wa Afrika Kusini Fredrick W de Klerk, amesema nchi hiyo imempoteza mmoja wa waasisi wake na raia mwenye heshima ya hali ya juu.
Huko huko Afrika Kusini, aliyekuwa mkuu wa gereza alilofungiwa Mandela kwa muda mrefu kwenye kisiwa cha Robben, Christo Brand, amesema Mandela alikuwa mfungwa wake, rafiki yake, baba yake na rais wake.
Kifo cha Mandela kimeughubika mkutano wa marais wapatao 40 wanaokutana mjini Paris kuzungumzia usalama barani humo na kupelekwa kwa wanajeshi wa Ufaransa kutuliza hali katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Akizungumza katika mkutano huo, rais wa Jamhuri ya Kongo Sassou Ngueso amesema mkutano wenyewe unakwenda sambamba na yale aliyopigania Mandela wakati wa uhai wake, ambayo ni uhuru na amani kwa watu wa Afrika.
Mwandishi: Daniel Gakuba/afpe/dpae
Mhariri: Sekione Kitojo


DW.DE

SAKATA LA RAY NA WAREMBO LAFIKA PABAYA-MAINDA AMCHANA JOHARI LIVE BILA CHENGA-HATARII.


Hapo majuzi kupitia mtandao mmoja wa kijamii mwanadada Mainda aliamua kuvunja ukimya baada
ya kuamua kuwachana live ‘wabaya’ waka Chuchu hans, na Johari kuhusu sakata linaloendelea la wao kumgombania mwigizaji Vicent kigosi ambaye anadaiwa alikuwa mpenzi wa mrembo huyo. Bila kupoteza muda soma hapo chini alivyofunguka mwanadada huyu…

"...Hizi salamu zako Johari, ni hivi naomba usinitaje kwenye huo upumbavu wenu, Huyo mwanaume mnae mzungumzia mimi kwangu namuona mtu wa kawaida tu ndio maana nikatupa kule. Nadhani umenipata alafu sitaki kumpandisha mtu jina sawa?. Ni hivi mimi si mpinzani wako, nadhani mpinzani wako unamjua mliopiganana (Sakata la Johari na Chuchu hans kupigana)  mkataka kutoana roho kisa shingo ya kuku mlivyokuwa wajinga na malimbukeni wa mapenzi wanaume hapawiganiwi. Nimewakalia kimya naona wewe mwenye kilanga umejitoa kimasomaso ukaenda kiu ukasema Mainda amebip wewe unataka kumpigia, ni hivi usiniweke kwenye upumbavu wenu, mimi huyo mwanaume wenu kwangu ni kuku kama kumtafuna nimemtafuna mpaka mifupa alafu nikatupa kwenye shimo la taka, sasa nyiyni mbwa koko mlio kosa wafugaji ndio mnaruka ovyo hamjui mle nini, pumbavu kabisa wewe na mke mwenzio sindio amkauki kunisema me mgonjwa, sasa kama me mgonjwa huyo bwana wenu ni hivi wewe mwenye shape kama ubao usiejielewa nakushauri achaha na mimi nenda sinza.


Bofya hapa kulike page yetu https://www.facebook.com/pages/Djaro-Arungu/311726042292359


Mwanamke Polisi aliejiua baada ya kukosea msg ya mpenzi wake na kutuma kwa mume wake Dec 5 2013Mwanamke huyu aitwae Gail Crocker ambae alikua Polisi nchini Uingereza imefahamika kwamba alijiua baada ya kumtumia mume wake meseji badala ya kumtumia mpenzi wake ambae alikua polisi mwenzake.

Kwenye msg yenyewe, Gail aliandika kumshukuru mpenzi wake kwamba aliinjoy walipotoka pamoja usiku mmoja, na kumwambia ‘natamani tungekua tunafanya hivi mara kwa mara’
Taarifa imesema Askari huyu ambae ni mama wa watoto wawili alikua akishiriki kwenye penzi la nje na askari mwenzake wakati mumewe akiwa kwenye safari za kibiashara ambapo baada ya kukosea msg aliamua kujiua kwa kunywa vidonge vingi na kujilaza kwenye buti ya gari.

Hata hivyo pamoja na Mwanamke huyo kutoka nje ya ndoa, mume wake ambae wamekua kwenye ndoa kwa miaka 30, Peter Crocker mwenye miaka 49, amesema Gail alikua Mwanamke wake wa maisha.

Bofya hapa kulike page yetu kwa habari zaidi.https://www.facebook.com/pages/Djaro-Arungu/311726042292359?ref=hl

Jamaa mmoja mwenye umri wa miaka 28 amehukumiwa kwenda jela miaka kumi mara baada ya kukutwa na hatia ya kufanya tendo la ngono na mbuzi.


Katana Kitsao Gona toka Malindi nchini Kenya wiki iliyopita alikiri kufanya ngono na mnyama.

Shuka chini kuangalia Video hiyo..... Mbuzi huyo wa kike kwa utulivu alikuwa pembeni ya chumba cha mahakama wakati hukumu hiyo ilipokuwa inatolewa.
 Jamaa huyo alikamwatwa mnamo tarehe 25 Novemba mara baada ya mkazi mmoja wa eneo hilo kumbamba akiwa uchi wa mnyama akimla uroda mbuzi huyo ambaye alikuwa amefungwa kamba, hii ni kwa mujibu wa The Star.

Mmiliki wa mbuzi huyo alifahamishwa na kufika eneo la tukio akiwa na majirani wengine ambao pia walimshuhudia Gona akiwa anafanya ngono na mnyama.

Jamaa alikamatwa na polisi na vipimo vya hospitali vinakaonyesha kweli kwamba tukio la ngono lilifanyika.
Gona aliomba msamaha kwa mahakama kwa kujitetea kuwa mke wake ni mlemavu na anamtegemea yeye ila mahakama ikajibu kuwa kosa hilo ni kubwa na akapewa siku 14 za kukata rufaa.

Tazama Video Hapa Chini!!


Bofya hapa kulike page yetu ili upate habari zaidi.https://www.facebook.com/pages/Djaro-Arungu/311726042292359

Mnamo siku ya Jumatano watunga sheria nchini Ufaransa walipitisha muswada ambao utawafanya wateja wa makahaba kutozwa faini kuanzia kiasi cha €1 500.

Sheria ya kupinga ukahaba ilipitishwa na mkutano mkuu ambapo Manaibu 268 wakipiga kura ya kukubali, 138 walipinga na 79 hawakupiga.

Sheria hiyo ambayo kwa sasa inahitaji kukubaliwa na Bunge la nchi hiyo, imekuja mara baada ya kupitishwa nchini Sweden ambapo kwa sasa inatumika ambapo wateja wa makahaba hutozwa faini kwenye nchi hiyo katika kile kinachoonekana kutaka kuitokomeza taaluma hiyo kongwe.


Kama umevutiwa na Habari zetu plz bofya hapa kulike page yetu.https://www.facebook.com/pages/Djaro-Arungu/311726042292359

Rais wa Marekani Barack Obama mnamo siku ya Jumatano alikiri kuwa alikatazwa kutotumia simu
aina ya iPhone kwa sababu za kiusalama, hii ilikuja kipindi ambacho alikuwa akifafanua ni kwa nini wakati mwengine huonekana akitumia simu kubwa aina ya Blackberry.

“Siruhusiwi kwa sababu za kiusalama kuwa na iPhone,” Obama alilieleza kundi la vijana ndani ya White House kwenye tukio la kuhamasisha sheria ya kujali afya.



Photo: Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amedai bungeni (leo) kwamba mshahara wake hauzidi Shilingi za kitanzania Milioni SITA na akadai wanaodai analipwa zaidi ya hapo ni wazushi wakubwa  Taarifa zaidi, soma hapa => http://bit.ly/1biHqVH
Waziri Mkuu amedai bungeni muda huu kwamba mshahara wake hauzidi Tsh. 6mil na akadai 
wanaodai analipwa zaidi ya hapo ni uzushi mkubwa kiasi kwamba yeye ni mkopaji tu katika mabenki na kuwa mshahara huo ni pamoja na mapato ya mkewe. 

Source: leo bungeni -tbc

Elizabeth Michael "Lulu " Amedai hajakutana na mtu yoyote kimapenzi toka atoke Jela ...



Kwa mujibu wa chanzo chetu Muigizaji huyo nyota amesema licha ya Vishawishi vingi  vya wanaume na wasagaji lakini hakuna alie bahatika kumnasa mpaka sasa 
Inasemekana toka apatwe na Masahibu ya Kanumba Lulu ni Kama mtu Aliyeng'atwa na Nyoka kwa kuogopa hata kuguswa na Nyasi..
Lulu Ameshabadilisha number mara 13 na tatu kuepukana na Usumbufu . 

ACHANA na mabifu yaliyotangulia, hili ni jipya kabisaa! Msanii wa sinema na Bongo Fleva, Baby 
Joseph Madaha ameingia kwenye bifu zito na Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ na kudai staa huyo wa Wimbo wa Number One ni mzinzi ‘fuska’


Bila kumung’unya maneno, mapema wiki hii, Baby Madaha alimvaa Diamond ambaye ni Rais wa Wasafi Classic Baby (WCB) akimtuhumu kuwa na tabia za kifuska.
Baby Madaha alidai hata muziki anaoufanya Diamond kamwe hauwezi kulingana na mafanikio makubwa ya jina lake zaidi ya kubebwa na skendo tu.

CHOKOCHOKO ZILIVYOANZA
Kupitia mitandao ya kijamii, ilivuja posti ambayo ilidaiwa kutoka kwa Baby Madaha ikimpaka Diamond kuwa siyo mwanamuziki kama ilivyo kwa wasanii wengine wenye uwezo mkubwa, akitolea mfano Elias Barnaba wa THT.
Sehemu ya posti hiyo ilionesha kuwa, Diamond si msanii wa muziki bali ni mzinzi f’lani hivi anayefanya biashara ya muziki kupitia mapenzi.

“Siku wanawake maarufu nchini Tanzania watakapojitambua na kuacha kulewa penzi la Diamond, huo ndiyo utakuwa mwisho wa maisha yake kimuziki kwa sababu hatakuwa na jipya na hivyo soko lake litaporomoka,” ilisomeka posti hiyo.
UKWELI NI UPI?
Baada ya ishu hiyo kugeuka habari ya mjini na kuibuka kwa makundi mawili yanayokinzana, Amani lilimtafuta Baby Madaha ili kujua ukweli wa posti hiyo ndipo akatiririka aya za kuthibitisha kuwa picha haziivi, hamkubali Diamond na kudai hata kimuziki hamkubali kwani anaamini wapo wanamuziki wanaofanya vema katika gemu kuliko yeye.

“…tuseme ukweli, Diamond ni mfanyabiashara siyo mwanamuziki. Kuhusu hiyo posti iwe ni mimi nimeandika au si mimi lakini kimsingi hayo maneno yanamstahili kabisa. Mzinzi tu.
“Diamond anabebwa na media (vyombo vya habari). Kuna wanamuziki wengi wazuri sembuse yeye? Ana nini haswa?” alihoji Baby.

AMANI LAMGEUKIA DIAMOND
Baada ya kusikia maelezo ya Baby kwa kifupi, Amani lilimuweka ‘pending’ kwa muda na kumwendea hewani Diamond ili liweze kujua upande wake analizungumziaje bifu hilo ambalo lilikuwa likienea mitandaoni kama moto wa kifuu.
Tofauti na matarajio ya mapaparazi wetu kwamba huenda angejibu mashambulizi makali kwa Madaha, Diamond au ‘Sukari ya Warembo’ aling’aka huku akimponda mwanadada huyo na kumshangaa:

DIAMOND SASA
“Daaah! Huko ni kunishusha…mimi na huyo (Baby) wapi kwa wapi kamwe huwezi kunilinganisha na mtu ambaye yupo chini yangu sana, nikijibizana naye nitajishusha tu. Ingekuwa ni mtu mkubwa mwenye levo yangu hapo ningesema natakiwa kusema neno.
“Hana lolote huyo anatafuta ‘kiki’ tu kupitia mimi, nipo na dili zangu za maana nipoteze muda kwake? Atafute wa levo yake na wala si mimi.”

UZINZI VIPI?
Alipoulizwa kuhusu suala la uzinzi ambalo Baby Madaha aliumaanisha katika posti yake, Diamond aliendelea kukazia kuwa hana muda wa kupoteza kwa mtu kama Baby Madaha ambaye kimsingi ni kama ardhi na mbingu.
“Huyo anatafuta kiki tu, aachane na mimi…mbona hatufanani kabisa mimi na yeye wapi kwa wapi?” alikazia Diamond a.k.a Weka Mbali na Watoto Wazuri wa Kike.

BABY AREJEA HEWANI
Wakati mapaparazi wetu wakimalizana na Diamond, kilongalonga kimoja cha paparazi wetu kilikuwa kikionesha kinaita, ilivyokatika ya Diamond, Baby akapanda hewani kwa mara nyingine.

Safari hii alimchana laivu: “Nimeisoma upya posti yenyewe, kilichopo humu ni ukweli mtupu. Hakuna hata tone la uongo, wewe utamlinganisha Diamond na mtu kama Barnaba? Huyu ni mfanyabiashara tu, hajui kuimba kwa kutumia vyombo kama mimi.
“Diamond hawezi kupiga chombo hata kimoja cha muziki atajiitaje mwanamuziki? Anastahili kabisa ujumbe huu.”

UFUSKA
Mapaparazi wetu walilazimika kumtwanga swali Baby Madaha kuhusiana na ufuska ambao ulikuwa umetajwa katika maelezo ya awali, kama endapo Diamond ni mzinzi au yeye ndiyo mzinzi.
Katika maelezo yake, Baby Madaha aliwashangaza mapaparazi wetu kwa kutaja namna gani anaweza kumuita Diamond mzinzi. Sikia:

Amani: “Umesema Diamond si mwanamuziki, je, suala la uzinzi ni nani analo kati yako na yeye?”
Baby: “Mimi si mzinzi. Diamond ndiyo mzinzi tena sana tu.”
Amani: “Uzinzi wake upo wapi?”
Baby: “Kitendo cha kubadilisha wanawake, kufumaniwa na Wema Sepetu akiwa na Jokate Mwegelo ndiyo uzinzi wenyewe huo.”

Amani: “Kwani wewe hujawahi kuwa na wanaume tofauti? Hujawahi kufumaniwa?”
Baby: “Mimi sijawahi, yeye amewahi na hakuwahi kukanusha hivyo inadhihirisha kuwa ni kweli. Kwangu mimi kila aliyetajwa kutoka na mimi kama haikuwa kweli, nilikanusha mara moja yeye mbona hakanushi?”
Amani: “Kwani Diamond alifumaniwa na nani?”
Baby: “Acha hizo, kwani hukumbuki kipindi cha Wema? Mara alinaswa na Aunt mara na… yule ndiyo mzinzi sasa.”

KWANI WALITONGOZANA?
Kuhusu suala la kutongozwa, Baby alisema Diamond hajawahi. Cha kushangaza zaidi, alisema hata kama ikitokea siku staa huyo akamtongoza kamwe hawezi kumkubalia kwani hawaendani hata kidogo.
Alisema yeye ni mtu wa kutembea na vigogo na si vitoto kama Diamond.

“Hana hela, kamwe siwezi kumkubalia. Ni mtu ambaye ana vihela mbuzi sasa mtu kama yeye mimi wa nini? Ndiyo maana aliwahi kukimbiwa na mwanamke kwa kuwa hana hela.
“Tena yule mwanamke akaenda kwa kigogo mwenye hela, mimi na yeye ni mbalimbali kabisa. Hata muziki ninaofanya hauwezi, mimi ninaimba RnB yeye anafanya Pop, tuko tofauti kabisa,” alisema Baby pasipo kumtaja mwanamke aliyemkimbia Diamond.

TUJIKUMBUSHE PANDE ZOTE
Diamond aliwahi kuripotiwa kutoka kimapenzi na ‘totoz’ kibao wakiwemo yule wa mwanzo aliyemzingua aitwaye Sarah, Rehema Fabian, Jacqueline Wolper, Upendo Mushi ‘Pendo wa Maisha Plus’, Wema Sepetu, Natasha (Video Queen wa Wimbo wa Moyo Wangu), Najma (aliwahi kuwa mpenzi wa Mr. Blue), Jokate Mwegelo, yule demu wa Kenya na aliyekuwa mwigizaji aliyefulia ambaye ni mke wa mtu.

Kwa upande wake Baby Madaha anayekimbiza na ngoma yake ya Summer Holiday

Source:GPL

Mkuu wa Idara ya Uendeshaji kutoka Tigo Tanzania Bw. Deon Geyser akionyeshea  waandishi wa habari tuzo ya mtandao bora wa mwaka 2013 walioshinda 
kutoka kwa umoja wa makampuni ya simu GSMA katika kongamano la mawasiliano na mitandao ya simu Africa Com, iliyofanyika Capetown Afrika Kusini mwezi Novemba. Kushoto ni Mkuu wa Mipango na Uboreshaji wa mitandao kutoka Tigo Bi. Halima Idd..
Kampuni ya Tigo Tanzania imeshinda tuzo ya kuwa mtandao wa simu ulioboreshwa zaidi katika mwaka 2013 barani Afrika. Tuzo hiyo iliyotolewa katika kongamano la umoja wa makampuni za mawasiliano duniani, GSMA, liliyofanyika mwezi Novemba mjini Capetown, Afrika Kusini.

 Jay-Z na Beyonce kutotumia vyakula vya nyama kwa siku 22Jay Z ametangaza kuwa yeye na mke wake Beyonce wameamua kutumia siku 22 kutotumia kabisa vyakula vya nyama.
Jay alitangaza mabadiliko yake ya chakula kwenye maelezo aliyoyaandika kwenye website yake lifeandtimes.com.
"Wanasaikolojia wamesema kuwa huchukua siku 21 kutengeneza ama kuvunja tabia," Jay Z alisema kwenye maelezo yake.  “Siku ya 22, utakuwa umepata njia.”
"December 3, siku moja kabla ya siku yangu ya kuzaliwa ya kutimiza miaka 44, ntaanza challenge ya siku 22 kutotumia kabisa nyama.”
Jay Z amesema umri wake ni sababu kubwa ya uamuzi huo.

Exclusive: Mshindi wa EBSS 2013 Emmanuel Msuya aandaliwa mapokezi ya kiserikali Musoma, atasindikizwa na Top 6Mshindi wa shidandano la Epiq Bongo Star Search 2013 Emmanuel Msuya atafanyiwa mapokezi ya kiserikali mjini Musoma ambapo ndipo makazi yake yalipo.
Msuya amesema kuwa amefurahi sana kupokea simu ya mkuu wa wilaya ya Musoma, Joseph Msome na mbunge wa jimbo la Musoma Mjini, Vicent Nyerere ambao walimpongeza na kumuahidi kumfanyia mapokezi ya kiserikali kutokana na sifa nzuri aliyoiletea wilaya hiyo na mkoa wa Mara kwa ujumla.
“Mkuu wa Wilaya ya Musoma na Mbunge wamenifanya niwe na furaha ya ziada kwa kuwa wameniambia wako katika maandalizi na watafanya kikao ili kuhakikisha napokelewa vizuri nyumbani. Ntaenda na washiriki wenzangu waliofika Top 6 pamoja watu wengine.” Amesema Emmanuel Msuya.
Mshindi huyo wa EBSS atasindikizwa na washiriki sita wa shindano hilo ambao ni Maina Thadei, Elizabeth Mwakijambile, Amina Chibaba, Melisa John na Mandela Nicholous.
Timu hiyo inatarajia kuingia Musoma Mjini Jumamosi (November 14).  

 Nando apata shavu la kuigiza kwenye filamu nchini Cameron Aliyekuwa mwakilishi wa Tanzania kwenye shindano la Big Brother Africa The Chase, Ammy Nando, amepata mchongo wa kuigiza filamu nchini Cameron.
Utengezaji wa filamu hiyo iitwayo ‘Scam Republique’ utaanza mwakani.
“Yeeapp there goes the Name "Scam Republique" film from The Movie Makers in Cameroon Coming out 2015 !!!.....who wana see NANDO win AWARDS from his First Leading Role...?????? #AMEN,” ameandika Nando kwenye ukurasa wake wa Facebook.