advert

http://

Monday 24 June 2013

ALIYOYASEMA MBUNGE ZITTO KABWE KUHUSU UKWEPAJI WA KODI



G8 Tanzania na Ukwepaji Kodi

Wakati dunia nzima ipo kwenye kampeni kubwa dhidi ya ukwepaji kodi unaofanywa na kampuni kubwa duniani zinazowekeza kwenye nchi zinazoendelea, Tanzania ipo kimya kabisa kana kwamba hakuna linalotokea. Licha ya kwamba Bunge la Tanzania ni Bunge la Kwanza katika nchi za SADC kupitisha Azimio kuchunguza utoroshwaji wa Fedha (Azimio la Bunge namba 9/2012), Serikali ya Tanzania imekaa kimya kabisa kupaza sauti yake kuhusu ukwepaji kodi mkubwa. 
Tanzania inapoteza mapato ya ndani sawa na asilimia tano (5) ya Pato la Taifa kupitia kodi za kimataifa ambayo ni sawa na shilingi trilioni mbili kila mwaka. Uchunguzi unaonyesha kwamba katika orodha ya walipa kodi wakubwa 10, kampuni saba zinatumia ‘tax havens’ kukwepa kodi. Katika kampuni kubwa tatu za simu hapa nchini kampuni mbili zimesajiliwa ‘tax havens’ za Uholanzi na Luxembourg na hivyo kukwepa kodi mbalimbali hapa nchini. Kampuni moja kubwa ya madini hapa nchini ina kampuni dada tisa (9) katika offshore hali kadhalika kampuni moja kubwa ya kutafuta mafuta na gesi hapa nchini. Katika mahojiano na gazeti la Financial Times la Uingereza la mwezi June, 2013 kampuni ya African Barrick Gold imetangaza kufunga baadhi ya kampuni zaidi ya 24 iliyoyasajili maeneo kama Cayman Islands.

Mheshimiwa Spika, bila Serikali ya Tanzania kuamua kwa dhati kusafisha nyumba yake, hata juhudi kubwa zinazofanywa na asasi za kiraia kama Oxfam, ActionAid, Tax Justice Network nk katika kupambana na ukwepaji kodi na utoroshaji wa fedha hazitafua dafu. Wakati nchi za G8 zinaweka mipango ya kutusaidia na sisi kama nchi tuweke mipango yetu wenyewe. Kambi ya Upinzani Bungeni inapendekeza hatua za awali zifuatazo zichukuliwe ili kukabiliana na utoroshaji mkubwa wa fedha unaotokana na ukwepaji wa kodi;
(i) Tanzania ijiondoe kabisa katika mfumo wa kodi unaopendekezwa na OECD (OECD model treaty) kwani mkataba huu wa kikodi unalinda kampuni kubwa za nje dhidi ya nchi changa kama Tanzania.
(ii) Tanzania ijondoe katika mikataba yote ya kikodi na nchi ambazo ni ‘tax havens’ kama Mauritius, Uingereza (City of London and British overseas territories), Luxembourg, Netherlands n.k.
(iii) Kampuni yoyote ya ndani na nje yenye kampuni dada zilizosajiliwa kwenye ‘tax havens’ zitangaze bayana na kuweka wazi hesabu zao kwa miaka mitano iliyopita kwa ukaguzi wa TRA na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.
(iv) Bunge litunge sheria kudhibiti matumizi ya ‘tax havens’ yanayofanywa na kampuni za uwekezaji na haswa kwenye sekta za Mawasiliano, Madini, Mafuta na Gesi na nyinginezo.

PEP GUARDIOLA ATAMBULISHWA RASMI KUWA KOCHA WA BAYERN MUNICH





AMRI KIEMBA NA SURE BOY NDIO WANASOKA BORA WA TANZANIA

 Katibu Mkuu wa Chama cha Wachezaji Mpira Tanzania (SPUTANZA), Said George, akiongea huku akiwa na baadhi ya viongozi wenzake wa chama hicho wakati wa utoaji wa tuzo za wachezaji Bora wa Chama hicho kwa mwaka 2013, ukumbi wa Diamond Jubilee usiku wa kuamkia leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk-bayana.blogspot.com)
Makamu wa Pili wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Athuman Nyamlani, akizungumza wakati alipokuwa akifungua utoaji wa tuzo ya Mwanasoka bora wa SPUTANZA, ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo. Kulia ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Said George.
Baadhi ya vingozi wa Kishen Enterprises, moja ya wadhamini wa tuzo hizo, wakiwa katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo, ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.
 Wasanii wa Sky Light Band wakitumbuiza katika utoaji wa tuzo hizo, ukumbini humo.
Mkurugenzi wa Kishen Eterprises, wauzaji wa pikipiki za Lifan, ambao ni moja ya wadhamini wa tuzo hizo, Rajen Solank (kushoto), akimkabidhi Meck Mexime tuzo ya kocha bora wa msimu.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah, akiongea kabla ya kumtaja mchezaji boara anayechipukia, ambaye alikuwa Salum Abubakar tuzo ya Sputanza, baada ya kuwashinda wenzake kadhaa katika katagoria hiyo.
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Angetile Osiah, akimkabidhi mchezaji boara anayechipukia, Salum Abubakar tuzo ya Sputanza, baada ya kuwashinda wenzake kadhaa katika katagoria hiyo.
Mwenyekiti wa SPUTANZA, Mussa Kissoky, akimkabidhi tuzo ya golika bora Kocha wa Mtwibwa, Mecky Mexime.
Mkurugenzi wa Kishen Eterprises, wauzaji wa pikipiki za Lifan, ambao ni moja ya wadhamini wa tuzo hizo, Rajen Solank (kulia), akizungumza kwa ajili ya kumtambulisha kwa mashabiki wa Mwakilishi wa Kampuni ya Lifan, Nasikiwa Benya (kushoto), wakati wa hafla hiyo. Katikati ni Katibu Mkuu wa SPUTANZA, Said George.
Makamu wa Pili wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Athuman Nyamlani, akipanda kuijaribu pikipiki ya kike, aliyozawadiwa mke wa Rais, Mama Salma Kikwete na kukabidhiwa yeye na Mkurugenzi Kishen Enterprises, katika hafla hiyo usikuwa wa kuamkia leo, ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo. 
Makamu wa Pili wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Athuman Nyamlani, akikabidhiwa zawadi na Mmoja wa wanafamilia ya Pepsi, ambao ni moja ya wafadhili wa tuzo hizo, Fadi El-Khalil.
Wanafamilia ya Pepsi, Fadi El-Khalil (kulia) na Meneja Mkuu wa Uhasibu Taifa wa Kampuni ya Pepsi, ambao ni moja ya wafadhili wa tuzo hizo, Bhank Patwa, wakifungua bahasha yenye jina la mchezaji bora wa jumla SPUTANA, ambapo Amri Kiemba wa Simba aliibuka kinara.
Meneja Mkuu wa Uhasibu Taifa wa Kampuni ya Pepsi, ambao ni moja ya wafadhili wa tuzo hizo, Bhank Patwa (kushoto), akiwa na mwanafamilia ya Pepsi, Fadi El-Khalil (katikati), akimkabidhi Mohamed Bhinda kwa niaba ya mchezaji bora wa jumla wa SPUTANA, Amri Kiemba wa Simba ambaye hakuwepo katika hafla hiyo. 
(PICHA ZOTE KWA HISANI YA http://wwwbayanablogspotcom.blogspot.com)

MAGAZETI YA LEO!

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
_SC06886
.
_SC06885
.
.
..
_SC06882
.
_SC06883
.
_SC06884
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.