advert

http://

Saturday 21 September 2013

Afisaa mmoja mkuu wa kundi la kigaidi la Alshabaab, amefahamisha BBC kuwa kundi hilo ndilo limehusika na shambulizi dhidi ya duka la kifahari la Westage mjini Nairobi Kenya.


Kwa mujibu wa Afisaa huyo mashambulizi hayo yalikuwa ya kulipiza kisasi kwa Kenya kwa kujihusisha na vita vya Somalia ambako wanajeshi wake wanakabiliana na kundi hilo.
Wanajeshi wa Kenya wamekuwa nchini humo tangu mwaka 2011 kama sehemu ya juhudi za muungano wa Afrika kutaka kurejesha uthabiti nchini Somalia.
Afisaa mkuu wa mambo ya ndani Kenya amesema idadi ya waliofariki ni kumi na moja lakini shirika la msalaba mwekundu linasema idadi hiyo imefika watu 30 huku zaidi ya hamsini wakijeruhiwa.
Taarifa kutoka Ikulu ya Rais Kenya zinasema kuwa mshukiwa mmoja aliyekamatwa alifariki kutokana na majeraha yake.
Wanamgambo wa Al Shabaab kupitia kwa mtandao wao wa Twitter , wanasema kuwa Kenya haikuchukulia kwa uzito onyo walilotoa kwa taifa hilo kwa hatua ya kuwapeleka wanajeshi wake nchini humo kupambana dhidi yao.
Kundi hilo limesema limekuwa likitoa onyo mara kwa mara kwa Kenya kuwa ikiwa haitaondoa vikosi vyake nchini Somalia, athari zitakuwa mbaya mno.
Kupitia mtandao wao wa Twitter, Al Shabaab limesema kuwa Kenya ilijidai kutosikia onyo hizo, na kuendelea kuwaua waisilamu wasio na hatia nchini Somalia.
Taarifa hiyo ya Twitter ilisema kuwa Shambulio la Westgate ni tone katika bahari tu ya mfano wa yanayowakumba wasomali waisilamu nchini Somalia.
Taharuki ilianza hii leo saa saba mchana wakati watu wanaokisiwa kuwa kumi walipovamia jengo la kifahari la Westgate la kuwapiga risasi kiholela wakenya waliokuwa wanaendelea na shughuli zao za kawaida.
Kwa mujibu wa shirika la msalaba mwekundu , takriban watu 30 walifariki kwa kupigwa risasi au kutokana na majeraha yao na wengine wengi wenye majeraha ya risasi kukimbizwa hospitalini kwa matibabu.

DIAMOND AMFANYIA KWELI OMMY DIMPOZ!!



Haya ndo matokeo ya my no 1 ya Diamond na Tupogo ya Ommy Dimpoz kupitia babamzazi.com


MY NO 1 YA DIAMOND
  79 (68%)
 
TUPOGO YA DIMPOZ
  37 (31%)
 

Votes so far: 116
Poll closed 

MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi Mukubu, Wilaya ya Ngara mkoani Kagera, Silidion Kaiza (43), anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kukutwa na bangi gunia sita.

  
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Philip Kalangi alisema kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 17, mwaka huu, shuleni hapo katika kata na kijiji cha Muganza majira ya saa tano asubuhi.
 
Alisema kuwa raia wema walitoa taarifa kituo cha polisi Rulenge kwamba kuna mwalimu anajihusisha na biashara ya kuuza dawa za kulevya, jambo walilohofia kuwa huenda akawaathiri wanafunzi wa shule hiyo kwani anazihifadhi shuleni.
 
Kalangi alifafanua kuwa baada ya polisi kupata taarifa hiyo walifika shuleni hapo na kumhoji mwalimu Kaiza, na alikiri kufanya biashara hiyo kisha akawapeleka katika moja ya darasa ambalo alikuwa akitunza bangi hiyo.
 
Kamanda alisema kuwa baada ya polisi kukamata bangi hiyo, waliifikisha kituoni na kwamba mwalimu huyo anaendelea kuhojiwa kisha atafikishwa mahakamani wakati wowote ili kujibu tuhuma hizo.
 
Aliwataka wananchi kuendelea kuwafichua wahalifu wanaojihusisha na vitendo vya uuzaji wa dawa za kulevya ambavyo vimekuwa tishio kwa taifa.


Source:Boss Ngasa.

BINAFSI nafahamu kwamba Irene Uwoya aliwahi kuwa staa mkubwa nchini lakini akafanya makosa na sasa ameshuka chati. Ameporomoka kwa kiasi kikubwa sana.


Elizabeth Michael ‘Lulu’, baada ya ‘ajali’ yake na marehemu Steven Kanumba, alikaa mahabusu kwa zaidi ya mwaka mmoja lakini baada ya kutoka ameonekana kuwa na mafanikio makubwa kuliko Uwoya ambaye siku zote yupo mtaani.

Pengine kuna aina fulani ya maisha ambayo Uwoya amejichagulia maana akina Rose Ndauka, Aunt Ezekiel, Wema Sepetu na wengineo wamekuwa wakifanya vizuri, wanamfunika sana. Ameshindwa kujisahihisha, ataendelea kusugua.

Najua kwamba Uwoya ana hali mbaya kisanii, amechoka, muonekano wake hausisimui tena, amepoteza mashabiki, kwa maana hiyo hauzi. Dili za kucheza filamu zinaota mbawa kila kukicha, maprodyuza wanataka wakali ambao wanafanya biashara sokoni.

Naelewa kuwa hivi sasa katika ulimwengu wa masupastaa, Uwoya amebaki msindikizaji lakini sikuwahi kufikiri kwamba anaweza kufikia hatua mbaya kiasi hicho. Kafikishwa mbaroni kwa wizi wa simu? Yaani wizi wa simu ya mkononi! Anatia huruma.

Yamemfika yapi? Sitaki kuamini kama Uwoya anashindwa kununua simu halali. Akili nyingine inaniambia kuwa hawa dada zetu wanaharibiwa na uchu wa kupenda vitu vya juu lakini uwezo ni mdogo. Je, huo wizi wenyewe alifanyaje?
Atakapofikishwa mahakamani pengine itajulikana kama kweli amehusika na wizi huo, basi itafahamika ameufanyaje. Ni yeye moja kwa moja au kupitia kwa mtu mwingine? Dunia ina mengi, ni vizuri hili jambo likafika kortini, huko tutajua ukweli halisi.
Swali langu ni hili, kama kweli ile simu alinunua kwa nini pale kituoni hakutoa risiti? Hata kama ingekuwa nyumbani, alishindwa nini kuagiza aletewe kuthibitisha kama ni mali yake? Maswali hayo mawili yanaongeza uzani kwenye madai kwamba ile simu ni ya wizi.
Ni ya wizi sawa, je, ni kweli Uwoya anaweza kuiba simu? Inawezekana kabisa akatega Kariakoo halafu amvizie mtu na kumchomolea? Maana mashtaka dhidi yake ni Wizi wa Maungoni, yaani wizi wa kumchomolea mtu kitu kutoka mwilini.
Kesi ipo Msimbazi Polisi na imeandikwa kwenye kitabu cha ripoti za kumbukumbu (report book ‘RB’) kwa nambari MS/RB/8522/2013. Hata hivyo, simu yenyewe iliyoibwa ina thamani kubwa, nahisi Uwoya aliinunua kwa mtu ambaye ndiye mwizi.
Mikono ya Uwoya na vidole vyake vilivyo, haoneshi kama anaweza kuwa mkali wa kuchomolea watu. Hata kama kaishiwa na kupigika, siyo rahisi akafanya hivyo. Sura yake haioneshi ushujaa wa ‘kupiga ndole’ lakini ya Mungu mengi.
Labda kauziwa lakini yeye ndiye kakutwa na mali ya wizi (aliyekutwa na ngozi ndiye aliyeiba ng’ombe). Kama ipo hivyo, hilo nalo ni tatizo kubwa. Maana yake yeye naye ni mmoja wa watu wanaowafanya wezi waendelee kufanya uporaji. Anawafadhili kwa mlango wa nyuma.
Tusimamie hapa kwamba kama alinunua, basi Uwoya ni mfadhili wa wezi kwa sababu mtu anayenunua mali ya wizi, anawasaidia wezi kuendelea kuishi kwa uporaji. Kwa maana hiyo siyo mtu mzuri, hafai kwenye jamii.
Kwa mwenendo huo, naamini ndiyo maana ameporomoka, anakosa sifa ya kuitwa kioo cha jamii. Inawezekanaje awe mfano wa kuigwa ikiwa yeye ni kirusi katika hiyohiyo jamii? Mtu unajua kabisa hii mali ya wizi unainunua kwa bei chee halafu unaona raha.
Kununua mali ya wizi ni hujuma nzito, ni ukosefu wa huruma kwa sababu wakati wewe unauziwa mali hizo kwa bei nafuu sawa na bure, halafu unaitumia kwa nafasi huku ukijionesha, mwenzako anateseka mno.
Fikiria kama wewe umejibana, ukajitutumua kununua simu aina ya iPhone 5 kwa shilingi milioni 1.6. Umeitumia wiki mbili tu unaibiwa, halafu mtu mwingine anakuja kuuziwa kwa shilingi 400,000  au 300,000. Itakuuma kiasi gani?
Bila shaka utamchukia mwizi na yule aliyeuziwa, kwani angekuwa muungwana asingekubali kununua. Laiti angekuwa raia mwema, angesaidia huyo muuzaji akamatwe ili aliyeibiwa arudishiwe mali yake. Kutumia mali ya wizi ni dhuluma, ni wizi.
Uwoya alikamatwa na simu ya wizi aina ya iPhone 5, kwa hiyo kama aliuziwa, na kwa mujibu wa tafsiri ambayo nimeielezea hapo juu ni wazi kwamba yeye siyo raia mwema. Ukweli uzidi kusimama kwamba hafai kuitwa kioo cha jamii.
Je, ni tamaa ya kutaka vitu vizuri wakati pesa hana? Ajioneshe mjini kwamba anamiliki iPhone 5 kumbe ni ya wizi, ameipata kimagumashi. Namshauri Uwoya aache mtindo wa kuishi kimagumashi, kama hana akubali hali halisi. Si kulazimisha maisha ya gharama, matokeo yake ndiyo haya.

ANGEMTII MUMEWE YASINGEMFIKA HAYA
Nikiongoza jopo la waandishi kutoka Global Publishers Ltd, mwaka jana, tulifanikisha kumsuluhisha Uwoya na mumewe, Hamad Ndikumana ‘Kataut’ kutokana na mgogoro wa nguvu ambao ulikuwa unaitikisa ndoa yao.
Malalamiko ya Kataut yalijikita katika uaminifu, kwamba Uwoya alikuwa anaonesha alama nyingi kuwa si mwaminifu kwenye ndoa yao. Mume huyo, alisema kwamba amenunua vifaa na kuanzisha kampuni ili mkewe ajisimamie katika kazi zake za filamu lakini mke hataki.
“Analipwa pesa kidogo ambayo akifanya shopping tu zinakwisha, maprodyuza wanapata fedha nyingi, yeye anafanya kazi, anauza sura tu lakini pesa hakuna. Nataka atengeneze filamu zake ili apate pesa za kuonekana lakini haelewi wakati kila kitu nimeshanunua,” Kataut alilalamika.
Kataut alikuwa na nia ya dhati kabisa ya kumwokoa Uwoya na pengine kama angefuata mwongozo wa mumewe leo hii asingeporomoka kama alivyo. Pengine yanayomkuta leo ni malipo ya kile ambacho alimtendea mwanamme huyo.
Mke wa mtu kunaswa hotelini na kijana wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, ni aibu sana! Kabla ya hapo zilishaibuka stori kwamba amegombana na supastaa Jacqueline Wolper kisa mwanaume. Alimtesa sana Kataut wa watu.
Akiwa yupo ndani ya ndoa, akaingia kwenye mgogoro na boyfriend wake wa zamani, Hamis Ramadhan Baba ‘H-Baba’, akadai eti katika wanaume wake wote waliopita, ambaye hawezi kurudiana naye ni H-Baba. Huyu ni mke wa mtu.
Tafsiri; kumbe pamoja na kuwa kwenye ndoa, anaweza kurudiana na wanaume wake wote waliotangulia isipokuwa tu H-Baba. Je, unamuonaje huyo? Ni mke wa mtu kweli?
Mke wa H-Baba, Flora Mvungi naye akamvaa Uwoya, akamchamba, wakachambana. Mke wa mtu anagombana na mwanamke mwingine kisa mwanaume tofauti na mumewe. Ninaposema hafai kwenye jamii namaanisha kweli.
Matukio ambayo anakumbana nayo hususan hili la wizi wa simu, achukue kama changamoto na ajisahihishe pale alipojikwaa. Amwangukie mumewe pengine mambo yakamnyookea. Iwe kama ameiba yeye moja kwa moja au aliuziwa, ajisahihishe.

Source:Global Publishers
Ni umbali wa kilomita saba kutoka katikati ya Mji wa Dodoma upande wa Mashariki barabara iendayo Morogoro, kipo kijiji maarufu cha Nzuguni.


Katika Mtaa wa maarufu wa Mapinduzi iko familia ambayo wakati mwingine kwa mtu wa kawaida unaweza usiamini simulizi yake lakini ni ukweli mtupu kwamba kuna tatizo katika familia hiyo jambo ambalo linahitaji juhudi za makusudi kuwasaidia.

Waswahili wanasema ‘kama hujui kifo basi kachungulie kaburi’ hivyo basi, hali ya maisha ya familia hii kwa ujumla inahitaji kusaidiwa, wanaishi kwenye katika kibanda kidogo cha tope.

 Ni katika familia ya Lameck Mwitewe Senyagwa na mkewe Anastazia Alfred yupo Stephen Lameck (21), kijana ambaye hajui mwanga wa jua la kijiji hicho ukoje, wala haijulikani ni lini kijana huyo ataishi walau kama binadamu wengine.

Stephen (Leba) ni mtoto wa kwanza katika familia ya  watoto wanne wote wakiwa wa kiume, lakini yeye pekee ndiye ambaye hajawahi kuyafaidi maisha katika kipindi chote cha uhai wake.

Ni mlemavu wa miguu, mgongo na hazungumzi chochote ingawa kwa ishara anaweza kueleza nini anachotaka kutendewa wakati huo.

Kwa namna ilivyo, angeweza hata kuendesha baiskeli ya miguu mitatu, lakini nani wa kumpa baiskeli hiyo ili imsaidie kijana huyo kuona mwanga wa jua, ni tabu na mateso makubwa juu yake.

Nilifika katika kibanda kidogo ambacho familia hiyo ya watu sita (watoto wanne na wazazi wawili wanaishi), inatia huruma lakini ndiyo hali halisi waliyo nayo, na haikuwa mara ya kwanza kuona maisha duni kama hayo isipokuwa mateso yapo kwa Stephen.

Simulizi ya mama mzazi

Katika kibanda hiki, nakutana na mama mzazi wa kijana huyu, mara baada ya kujitambulisha anaonyesha ushirikiano,  isipokuwa anapinga mimi kuingia ndani huku akitaka historia ya kijana wake niipate nikiwa nje. Baada ya dakika kadhaa tunakubaliana kuingia ndani aliko Leba.

Nilitaka kujua historia kamili na yeye alianza kwa kusimulia “Leba ni mwanangu wa kumzaa, ndiye mtoto wangu mkubwa kati ya watoto wanne,” anaanza kusimulia Anastazia Alfred.

Mama huyo anasema kuwa tatizo la kutokutembea kwa Leba halikumuanza hivi karibuni, bali ni tangu alipokuwa tumboni na lilitokana na tatizo alilokuwa nalo mama yake mzazi kabla ya kuzaliwa kwa mtoto.

Chanzo cha ulemavu

Anasema tatizo la mwanaye lilianza katika ugonjwa ambao yeye mzazi aliupata wakati akiwa na mimba ya miezi sita.

“Niliambiwa kuwa ninaumwa kifafa cha uzazi, wakati huo nilikuwa siwezi kufanya jambo lolote na hata macho yangu yalikuwa hayaoni,” anasimulia Anastazia.

Mama huyo anasema  mara baada ya ugonjwa huo kumzidi, alipelekwa katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma ambako alijifungua mtoto wakati huo akiwa na mimba ya miezi saba.

Anasema baada ya kujifungua, mtoto alikuwa ni dhaifu kiasi kwamba wengi walikata tamaa kuwa asingeliweza kupona. Hata hivyo kwa mapenzi ya Mungu akapona.

Atoroka na kumwacha mtoto

Kwa maneno yake anasema kuwa alitoroka hospitalini na kwenda kwa ndugu zake katika Mtaa wa Makole ambako aliwaeleza kuwa asingekuwa tayari kuendelea kuishi na mtoto ambaye watu walishamwambia kuwa ni mkosi kuishi naye.

Hata hivyo, alikumbana na changamoto nyingine kutoka kwa watu ambao walimtaka arudi tena kwa ajili ya kumchukua mtoto  na kwamba wasingekuwa tayari kumpokea mahali popote kama angerudi bila ya Leba.


“Nilikuwa nimechanganyikiwa na wakati mwingine utoto ulikuwa bado unanisumbua na kwa kuwa sikuwa na mama wakati huo ambaye angeweza kunifunda zaidi hivyo nikaona njia njema ya kunisaidia ni kumtelekeza mtoto,” anasimulia.

Hata hivyo, anampongeza marehemu baba yake kuwa alikuwa ni msaada mkubwa kufanya mtoto huyo aendelee kuishi kwani aliposikia mambo hayo, alimwita kijijini kwao Kwamtoro Wilaya ya Chemba (zamani Kondoa) ambapo alimketisha chini na kumwonya juu ya tendo hilo.

Anasema baba yake huyo alimtaka kuishi na mtoto bila ya kumtenga, na akampa mifano hai ya watu wenye ulemavu ambao wanaishi hadi wakati huo.

Mateso ya mtoto

Mbali na kukubaliana na kuishi na mtoto huyo, hali ya Leba kwa sasa inatisha, hana msaada wowote. Hawezi kutoka nje, amekuwa akifichwa ndani kwa zaidi ya miaka 12 sasa.

Chakula ni tabu, mazingira anayoishi hayaendani na hali yake na haijulikani ni lini atapata nafasi ya kuona mwanga.

Ni zaidi ya miaka 12 sasa kijana huyo anaishi ndani ya nyumba na watu wengi hawamjui licha ya kuwa mama yake anajulikana kwa jina la Mama Leba, mwenye jina majirani hawamjui.

Hiyo itatokana na kushindwa kupata msaada wowote walau wa baiskeli au hata njia nyingine, zaidi ya kutegemea mama yake mzazi ambaye anasema kuwa kijana huyo amekuwa mzito hawezi kumbeba.

Hali ya familia

Maisha ya familia ya Lameck ni magumu, hawana nyumba, wanaishi katika kibanda kidogo ambacho wamepewa na mlo wao ni shida, humlazimu baba wa familia kutafuta kwa bidii huku watoto wote watatu wakimtegema kwa masomo mmoja akiwa kidato cha nne, mwingine amemaliza darasa la saba na wa mwisho  darasa la pili.

Hata hivyo, upendo wa kuwa pamoja bado umeendelea kuwafanya wasitupane wala kuwa na migogoro.

Nini wanahitaji


Anastazia anasema kama watapata nafasi ya kusaidiwa baiskeli kwa ajili ya Leba akaweza kutoka nje, naye angepata nafasi ya kupumua na kutafuta biashara yoyote ya kumsaidia mumewe kwani kwa sasa hawezi kutoka umbali wa mita 100 na kumwacha mtoto.

Anasema katika umri wa miaka mitatu wa kijana huyo, walikutana na mtaalamu kutoka Asia ambaye alisaidiana na wataalamu wa hospitali ya mkoa kumfanyia mazoezi kijana huyo, kiasi cha kumwezesha kwa sasa akipewa baiskeli anaweza kuendesha japo kwa shida.

Kwa sasa ni kama wamepoteza matumaini lakini wanaamini kwa misaada kutoka kwa wasamaria wema labda hali ya maisha yao inaweza kubadilika na kuwa nzuri zaidi ya ilivyo sasa.


-Mwananchi

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimemtaka Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa kujiuzulu kwa kushindwa kulipa madeni ya walimu nchini.


Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana pia ametoa muda wa miezi sita kwa Waziri huyo na Naibu wake Philip Mulogo kutekeleza hilo agizo hilo vinginevyo chama kitawatumia wabunge wake kuwatimua kwa nguvu.

Kwa mujibu wa taarifa za madeni zilizokusanywa na Chama cha Walimu Tanzania (CWT), hadi sasa walimu wanadai malimbikizo yao ya Sh bilioni 49 ambayo hajalipwa na Serikali.

Kinana alikuwa akihutubia mikutano ya hadhara jana katika wilaya za Bariadi na Busega.

Alisema CCM haiko tayari kuona walimu wakinyanyaswa wakati wana madai ya msingi.

Hivi sasa imejengeka tabia kwa baadhi ya mawaziri na watendaji wa wizara ya kuwadharau walimu na hata kuwanyanyasa huku wengine wakishusha utu na heshima ya walimu kwa kuwatukana, alisema.

Kinana ambaye yupo katika ziara ya mikoa ya Kanda ya Ziwa alisema kwa mawaziri kushindwa kutatua kero za walimu, imefika wakati wahusika waondoke wenyewe na wasipofanya hivyo chama kitawaagiza wabunge wake wawafukuze kwa nguvu.

“Ninatoa muda wa miezi sita kwa Waziri wa Elimu na wasaidizi wake wakiwamo watendaji kuhakikisha wanalipa madeni ya walimu haraka. Haiwezeni hii ni nchi ya watu wote wakiwamo walimu wadharauliwe na hata kunyanyaswa kwa maneno ya matusi

Hili hapana CCM haiko tayari kuona walimu kila siku wakipigwa danadana kutokana na uzembe wa watu waliokabidhiwa dhamana za kuongoza sekta ya elimu katika nchi yetu,” alisema.

MTANZANIA ilimtafuta Katibu Mkuu wa CWT, Ezekiah Oluoch ambaye alisema hadi sasa madeni ya walimu yamefikia Sh bilioni 49 ambayo ni malimbikizo ya mishahara na mapunjo.

Kila mara tunawaambia kuwa ni vema Serikali itafute Sh bilioni 100 katika fungu la dharura ili iweze kulipa madeni ya walimu na iachane nao lakini hawasikii,” alisema Oluoch.


SOURCE MTANZANIA

Wadau nipo njia panda naombeni ushauri wenu, nimefanya kosa kubwa na nalijutia Tafadhali naomba ushauri badala ya kunituhumu.



nilikuta na demu mmoja tulisoma naye chuo kitambo alikuwa demu wangu for time being, so baada ya miaka kadhaa tukaja kukuta sehemu, shetani akanipitia nikavunja amri ya sita naye.

Baada ya kurudi home nikagundua sina pete, nikajaribu kukumbuka nilipoiweka sikupata majibu.


Baada ya siku kadhaa yule demu akzidi kunisumbua na kutaka niwe karibu naye sana lakini nikaona si vyema maana anaweza kusababisha mtafaruku kwa ndoa yangu

Baada ya kuona nampotezea akaniambia sasa unajifanya mjanja pete yako ni nayo na nahitaji sh 500,000 cash ama sivyo naharibu kwa mkeo kwamba pete ninayo na ulinikopa.

Kibaya zaidi wife aliniuliza pete umepeleka wapi nikadanganya nimeisahau ofisini nilikuwa nafungua printer sasa pete ikawa inani disturb nikaivua , nilipoenda jumatatu nikamwambia nahisi wahudumu wa usafi wameiiba maana siiona pale nimeiweka naendelea na uchunguzi.

Mwanzo nilimpuuzia lakini mshenzi yule kapeleleza hadi wife anapofanya kazi na kapata simu yake, juzi kampigia kamwambia "naomba mkumbushie mumeo deni langu mimi xxxxx nampigia simpati" halafu akakata simu.


Niliporudi wife kanibana nikamwambia ni mambo ya kazi tu akataka kujua no yake kaipataje, nikazuga zuga na ubabe wa kiume yakaisha

Nikipiga akili nimuendee Polisi naona kama kitanuka na wife atajua
Nikifikiria kumlipa akili hainipi kabisa....kilo tano?
Sijui nimueleze wife ukweli?

Nimejaribu kumpigia simu na kumbembeleza kagoma anachohitaji ni kilo tano au aniharibie kwa wife.


Tafadhali ushauri wakuu lawama na madongo hayatanisaidia.

Sayansi maana yake ni maarifa . Tunapo zungumzia dhana ya sayansi ya kiafrika , tunakuwa tunamaanisha matumizi ya maarifa ya kiafrika katika kukabiliana na mazingira ya mwanadamu pamoja na changamoto mbalimbali zinazo mkabili .

Tafiti mbalimbali za ki akiolojia na ki-anthropolojia zinaonyesha kuwa sayansi ya kiafrika imekuwapo kwa takribani miaka bilioni mbili sasa, hii ikiwa na maana kuwa sayansi ama ustaarabu wa kiafrika ndio ustaarabu mkongwe kupita ustaarabu mwingine wowote ule katika sayari ya dunia.

Hata ustaarabu wa jamii mbalimbali duniani kama vile waajemi, wayunani (Ugiriki ya kale ), wamisri, wasumeri ( Mesopotamia/babiloni ) ya kale nakadhalika, unatokana na ustaarabu ambao msingi wake ni sayansi ya kiafrika.

• Sayansi ya kiafrika imethibitika kumsaidia mwanadamu katika kukabiliana na mazingira yake kwa zaidi ya asilimia tisini na tisa (99%).

• Kwa bahati mbaya sana, sayansi ya kiafrika imepewa jina baya kwa kuitwa uchawi na kupigwa vita mbaya tangu mamia ya miaka iliyopita, lengo kuu likiwa ni kumuondolea mwanadamu uwezo wa kiungu ulio wekwa ndani yake wa kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazo mkabili katika maisha yake ya kila siku.

• Hata hivyo watu hawa walio mstari wa mbele katika kuipiga vita sayansi ya kiafrika, bado wanaendelea kuitumia sayansi ya kiafrika katika maisha yao ya kila siku japo kwa usiri mkubwa sana, ilihali wakati huo huo wakiendelea kuipiga vita sayansi hii. Watu hawa wanataka maarifa haya yawe ni kwa watu wachache.

• “ The Choosen Few “ huku mamilioni ya walio baki wakiendelea kuishi katika giza bila kujua kitu chochote kile kinacho endelea kwenye maisha yao. Hali hii imewafanya waendelee kuitawala dunia kwa muda mrefu sana kwa kutumia nyenzo mbalimbali za ku-control fikra za wanadamu.

Hofu kuu ya watu hawa ni kwamba, endapo kila mwanadamu ataifahamu vyema misingi ya sayansi ya kiafrika, itakuwa vigumu sana kwa wao kumtawala kwa sababu kila mtu atakuwa na uwezo wa kuyatawala mazingira yake na kukabiliana na changamoto za aina yoyote ile zinazo yakabili maisha ya kila siku ya mwanadamu…

• Sayansi ya kiafrika humjengea mwanadamu uwezo wa kuwa na mamlaka juu ya vitu vyote vilivyopo hapa duniani, vinavyo onekana na visivyo onekana. Humpa uwezo wa kuvitiisha vitu vyote vilivyo na uhai na visivyo na uhai.. Kwa ufupi inamfanya kuwa na umoja na Mungu.

• Miongoni mwa mambo ya kawaida kabisa anayo fundishwa mwanadamu katika sayansi ya kiafrika ni pamoja na :

• Somo la AKILI-UMEME-SAUTI ama MIND-ELECTRICITY-SOUND . Elimu hii humpa mwanadamu uwezo wa kuwa- control wanadamu wenzake kifikra, uwezo wa kuwatawala majini na viumbe wasio onekana na macho ya nyama, uwezo wa kuumba vitu, mambo na hali za aina mbalimbali kwa kutumia maneno, uwezo wa kupeleka heri au shari kwa wanadamu, wanyama, mimea na roho, uwezo wa kuvitiisha viumbe vyote vya nchi kavu,uwezo wa kutumia nguvu ya akili katika kufanya mambo mbalimbali nakadhalika.

• Somo la UMEME & HEWA au ELECTRICITY & AIR. Elimu hii humpa mwanadamu uwezo wa kupaa angani, uwezo wa kuitiisha anga na viumbe vyote vya angani, uwezo wa kuwasiliana na kuvi control viumbe vinavyo ishi kwenye upepo, uwezo wa kupeleka ujumbe kutoka sehemu moja ya dunia kwenda sehemu nyingine yoyote ile, uwezo wa kusafiri angani nakadhalika.

• Somo la NECROMANCIA ama NEGROMANCIA ambalo humpa mwanadamu uwezo wa kuwasiliana na kuzungumza na roho za watu walio kwisha kufa.

• Uwezo wa kuwasiliana na viumbe vya mtoni, ziwani na baharini
• Mamlaka ya kuvitiisha viumbe vyote vya duniani, vya nchi
kavu, baharini, na angani, vinavyo onekana na visivyo onekana.
• Uwezo wa kuona vitu visivyo onekana na wanadamu
• Uwezo wa kusikia sauti zisizo sikiwa na wanadamu.
• Uwezo wa kufanya mambo katika namna ya kiungu.
o Hayo ni moja kati ya maaarifa machache yanayo patikana katika sayansi ya kiafrika.

• Kwa ufupi, sayansi ya kiafrika inampa mwanadamu mamlaka kamili ya kuwa kitu kimoja na Mungu. Mfalme Suleiman ni miongoni mwa wanadamu walio pata bahati ya kupewa maarifa haya, habari zake nadhani wengi wetu tuna zifahamu.

• Endapo wanadamu watazingatia misingi ya sayansi ya kiafrika, basi wataweza kuyatawala mazingira yao pamoja na changamoto mbalimbali zinazo wakabili kwa kiwango kikubwa sana.

• MUNGU NI NANI KWA MTAZAMO WETU?
• Kwetu sisi MWENYEZI MUNGU ni NGUVU KUU YA UHAI ( THE MOST GREATEST FORCE OF LIFE ). Nguvu Ya Uhai ni nini ? Nguvu ya uhai ni roho ama nishati inayo vifanya viumbe viishi na/ama viwepo au ni roho ama nishati inayo weka uhai kwenye viumbe vyote vinavyo onekana na visivyo onekana. Hivyo basi kwetu sisi MWENYEZI MUNGU ndio NGUVU KUU YA UHAI, kwa maana yeye ndio chanzo cha uhai wa kila kiumbe cha hapa duniani, kinacho onekana na kisicho onekana.

• Wakati mwingine huwa tunamtaja Mungu kama MOVENS IMMOBILE yaani UNMOVED MOVER.

• UHUSIANO KATI YA MUNGU NA MWANADAMU.
• Sisi tuna amini kuwa MUNGU NA MWANADAMU ni kitu kimoja.

Mwanadamu anatoka kwa MWENYEZI MUNGU. Kama nilivyo eleza hapo awali, Mwenyezi Mungu ndio NGUVU KUU YA UHAI, ndio CHANZO KIKUU CHA UHAI, hivyo basi kila kiumbe chenye uhai kinatoka kwenye chanzo cha uhai, nguvu inayo mfanya mwanadamu aishi, inatoka kwa Mungu, nguvu hiyo ni Mungu mwenyewe, kwa maana nyingine mwanadamu ni muungu mdogo, Mungu anajidhihirisha kupitia huyu mwanadamu. Kwa lugha nyingine ni kwamba, wanadamu ni vidhihirisho vya pembeni vya CHANZO KIKUU CHA UHAI.

Vidhihirisho hivi, vinapotambua nguvu iliyopo ndani yake na kuanza kuitumia vyema, NGUVU KUU YA UHAI ambayo ndio chanzo kikuu cha uhai, hujidhihirisha pamoja navyo, inapofikia hatua hii, vidhihirisho hivyo huwa kitu kimoja na kidhihirisho kikuu na hufanya mambo yake katika mfano wa CHANZO KIKUU CHA UHAI.

YESU alilitambua hili ndio maana ali fanikiwa ku atain eternity akiwa duniani, mara nyingi alikuwa akisema “ MIMI NA BABA TU KITU KIMOJA “. Hapa alimaanisha kuwa yeye na Mungu ni kitu kimoja, sio katika form ( muundo) bali katika consciousness. Wayahudi hawakulitambua hili ndio maana walidhani anakufuru.

• Kwa wale mnao taka kujifunza zaidi kuhusu sayansi ya kiafrika, tafadhali tuandikieni : ungoafrika@gmail.com au Tembeleenihttp://www.ungoafrika.blogspot.com