advert

http://

Thursday, 3 October 2013

MTOTO WA MIAKA 13 AJIFUNGUA MTOTO WA MIEZI 6 SEBULENI BILA KUJIJUA.

MSICHANA aliyejitambulisha kwa jina la Salma Hemedi (13) mwanafunzi wa Shule ya Msingi Ubungo Plaza, Dar amejifungua  maiti ya kichanga cha miezi 6 bila mwenyewe kujijua.
Tukio hilo lilitokea Septemba 25, mwaka huu maeneo ya Ubungo National Housing jijini Dar ambapo asubuhi ya siku hiyo, Salma alilalamikia maumivu ya tumbo lake kiasi cha mama yake aliyejitambulisha kwa jina la Rahma Shabani kwenda kuomba msaada wa kitabibu.

Mwanamke huyo alieleza kwamba baada ya kurudi ndani alikomuacha mwanaye, alimkuta akiwa amejifungua kichanga sebuleni, kitu ambacho hakukitarajia kwa kuwa alizoea kumnunulia vifaa vya kujisitiri wakati wa hedhi kila alipomlalamikia maumivu ya tumbo akijua yupo kwenye siku zake.

Akiwa na manesi walioongozana naye, walimsaidia Salma huku kila mtu akiwa amepigwa na butwaa kwa kilichotokea kwani hakuna aliyekuwa anajua kama Salma alikuwa na ujauzito.

Akiongea na waandishi wetu, Salma alisema alipewa ujauzito na mwanaume aliyemtaja kwa jina la John Vicent ambaye alikuwa mtoto wa mwenye nyumba wao wa zamani.

Salma alisema kuwa John alikuwa akimshawishi kila mara kufanya mapenzi japo alimkatalia kwa kuwa alijua akifanya kitendo hicho atapata mimba.

Salma alizidi kutiririka kuwa John alikuwa akimpa dawa alizodai ni za kuzuia ujauzito.

Baada ya kupata taarifa hizo mama wa Salma pamoja na ndugu zake walitoa taarifa Kituo cha Polisi Urafiki ambapo walifungua jalada la mashtaka lenye namba RB, URP/RB/7316/2013 KUBAKA na kupewa PF3 kwa ajili ya matibabu na uthibitisho wa daktari.

Walimu wa shule anayosoma Salma, walipigwa na butwaa baada ya kupata taarifa hizo na kueleza kwamba hawakuwa na taarifa kwamba denti huyo alikuwa mjamzito.

ZAIDI ya wanafunzi 50 waliochaguliwa kujiunga  katika vyuo vikuu mbalimbali nchini kwa mwaka huu, jana waliandamana kwenda Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kwa lengo la kukutana na Waziri Shukuru Kawambwa, baada ya kukosa mikopo.

Wakizungumza na mwandishi wetu, wanafunzi hao walisema zaidi ya wanafunzi 200  wenye sifa za kupewa mikopo ya elimu na Bodi ya Mikopo (HELBS), wamenyimwa bila maelezo.

Walisema kuwa tangu mwisho wa wiki wamekuwa wakihangaika kujua sababu za kutopewa mikopo kutoka katika bodi hiyo bila mafanikio.

Mwanafunzi Ayoub Suleiman aliyechaguliwa katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), alisema kuwa wameamua kumfuata Waziri Kawambwa ili wajue ni kwa nini hawajapewa mikopo hiyo.

Alisema majibu ya wanafunzi walioomba mikopo hiyo yalitoka Septemba 27 mwaka huu, miongoni mwao hawakuwepo kwa maelezo kuwa bajeti imekwisha.

“Waliotupa majibu haya ni wafanyakazi wa mapokezi na walinzi pale bodi ya mikopo, sio wahusika wenyewe kwa kuwa kila tulipoomba kukutana na mkurugenzi, hatukupata nafasi hiyo,” alisema Suleiman.

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe, Godwin Uledi, alisema kuwa juzi waliwashuhudia baadhi ya wazazi wakiwa na suti  na magari ya kifahari wakifika kwenye ofisi za bodi hiyo na watoto wao, na kuingia moja kwa moja kuonana na watendaji, walipotoka walikuwa wakitabasamu, hali iliyoonyesha kuwa wamefanikiwa.

Alisema, wanataka wapewe sababu kwa nini hawajapewa mikopo ilhali wenzao wenye vigezo kama vyao wamepata?

“Taasisi ya vyuo vikuu nchini ‘TCU’ ilitoa mwongozo kuwa wanafunzi wanaotarajia kujiunga na vyuo vikuu wakiomba vitivo vya elimu, uhandisi, udaktari, kilimo na sayansi watapata kipaumbele katika mikopo, hivyo nasi tulifuata mwongozo huo ili tupewe mikopo lakini hatujafanikiwa.

“Isingekuwa tunahitaji mikopo hii tungeomba katika maeneo mengine ambayo tulikuwa tukikidhi vigezo. Tumeomba katika vitivo hivi ili tupate mikopo,” alisema.

Kwa upande wake mwanafunzi aliyechaguliwa katika Chuo Kikuu cha Mt. Augustine, Revocatus Baltazary, alisema kuwa wamefungua chuo tokea Septemba 18, lakini ameshindwa kuripoti kutokana na wazazi wake kuwa na kipato cha chini.

“Sasa sina hata kianzio cha kwendea huko, kwa kuwa wazazi wangu hawana uwezo nitakwendaje?,” alihoji.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Ntambi Bunyazu, alisema kuwa wizara imewasiliana na bodi ya mikopo, kwamba wanafunzi hao warudi kule wakapewe maelezo zaidi kwa kuwa kila mmoja ana tatizo lake.

Hadi mwandishi wetu  anaondoka katika maeneo hayo, wanafunzi hao waliambiwa waorodheshe tena majina ili wizara iyapeleke HELBS, baada ya wiki moja watakuwa wamepata majibu.

Jitihada za kumtafuta Mkurugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa HELBS, Cosmas Mwaisobya, kwa ajili ya ufafanuzi wa suala hilo, ziligonga mwamba baada ya simu yake ya kiganjani kuita kwa muda mrefu bila majibu

Leo nimekabidhi madawati 120 Kata ya Manzese kwa shule tatu za msingi fedha kutoka katika mfuko wa jimbo. Bado kuna upungufu wa madawati 570 ambapo dawati moja linagharimu Tsh. 80,000 hadi 100,000.


Binafsi nachangia asilimia 20 ya kila mshahara wangu kuboresha Elimu ndani ya Jimbo la Ubungo!

Ungana nami tuboreshe elimu na kuimarisha pia maabara kwa kuchangia kupitia MPesa 350350.

Pamoja Tunaweza.

Waswahili husema, ‘nyumba ni choo’, wakiwa na maana kuwa nyumba haiwezi kuwa kamili bila kuwa na huduma hiyo ya choo.


Hata hivyo, pamoja na umuhimu wa choo, lakini si kila nyumba iliyo na choo au hata zile ambazo zina huduma hiyo, basi vyoo ni vibovu, havina hadhi. Zipo aina mbalimbali za vyoo kwa matumizi ya binadamu katika maisha yake ya kawaida.


Vyoo vina matumizi mengi ingawa bado watu wengi hasa katika nchi maskini na zinazoendelea ikiwamo Tanzania wanatumia choo cha kuchuchumaa wakati wa kujisaidia, lakini mijini na katika nchi zilizoendelea, wao hutumia vyoo vya kukaa.

Nyumba nyingi mijini na ofisi mbalimbali zinazojengwa hivi sasa, huwekewa vyoo vya kukaa. Hata zile za zamani zinakarabatiwa na kubadilishwa kwa kuwekewa hivi ambavyo vinaonekana vya ‘kisasa’.
Mgunduzi wa vyoo vya aina hii, Thomas Crapper anasema kwa mtazamo wake aliona kukaa wakati wa kujisaidia ni utambulisho wa ustaarabu na maendeleo.


Hata hivyo, madaktari wanapingana naye wakisema kujisaidia katika vyoo vya kukaa kuna madhara kiafya kwa kuwa mkao huo unaweza kuleta matokeo mbalimbali ndani ya mwili.


Utafiti uliofanywa na mtandao wa ‘naturesplatform’ umegundua kuwa matumizi ya choo cha kukaa huweza kusababisha matatizo mbalimbali ikiwemo kansa ya utumbo mkubwa.


Mtaalamu wetu wa afya wa gazeti la MWANANCHI, Samwel Shita anasema, madhara ya vyoo vya kukaa ni makubwa kwani wakati mwingine yanaweza kuwa chanzo cha saratani ya utumbo mkubwa kutokana na haja kubwa kubaki kwa muda mrefu katika utumbo huo.


Shita anasema mtu anapojisaidia haja kubwa katika choo cha kuchuchumaa, kinasaidia haja yote kutoka kwa sababu ya msukumo unaosababishwa na mkao huo.


“Unapokaa unakuwa umekaa katika choo mwili unakuwa umelegea, hivyo inabidi utumie nguvu kubwa kujikamua kutoa haja, tofauti na unapochuchumaa,” anasema Shita na kuongeza:
“Matatizo huanza hapo, unapojisaidia ukiwa umekaa na kulazimisha kujikamua unaweza kusababisha vimishipa vidogo katika utumbo mpana sehemu ya haja kubwa ya ndani na ya nje kuvimba na maumivu makali husababishwa na ugonjwa unaojulikana kama ‘hemorrhoid,” anasema.


Anasema ‘hemorrhoid’ ni ugonjwa ambao pia huitwa bawasiri. Mgonjwa hupata uvimbe katika njia ya haja kubwa na hivyo kupata maumivu wakati wa kujisaidia na haja yake mara nyingine huambatana na damu.


Aidha, anasema vyoo hivi pia vinaweza kuwa chanzo cha magonjwa yanayotokana na shambukizi katika utumbo mpana, kitaalamu ‘Inflammatory Bowel Disease’.


“Kila binadamu anapaswa kujisaidia na kuhakikisha haja yote imetoka na kwisha kabisa, inapobakia inaweza kusababisha maambukizi katika utumbo mpana kwa kuwa ule ni uchafu wenye mchanganyiko wa vitu vingi,” anasema Shita.


“Haja kubwa inapokuwa tayari imeshajitengeneza inapaswa kutoka yote, kama itabaki kipindi kirefu inaweza pia kuleta uambukizi katika utumbo mkubwa na hata katika kidole tumbo,” anasema Shita.


“Uchafu huu si tu unaweza kusababisha maambukizi, lakini pia unaweza kuwa chanzo cha saratani ya utumbo mkubwa. Wote tunajua kuwa mkusanyiko wa sumu mbalimbali mwilini unakuweka katika hatari ya kupata saratani, hivyo tatizo hili lisipotafutiwa ufumbuzi mapema linaweza kufikia huku,” anasema Shita.


Daktari Berko Sikirov kutoka Misri ambaye alifanyia utafiti matumizi ya vyoo vya kukaa anasema kuwa iwapo mtu ana tatizo la vivimbe vya ‘hemorrhoid’ linaweza kumalizika iwapo ataacha kutumia vyoo vya kukaa.


Hata hivyo, anasisitiza kuwa tatizo hili linaweza kwisha kama litakuwa katika hatua za awali. Kwa wenye tatizo lililokomaa watalazimika kufuata matibabu kulingana na ukubwa wake.


Dk Sikirov anaongeza kuwa mbali na kupata vivimbe, pia mgonjwa anaweza kupata tatizo la kutokupata choo kwa muda mrefu.


Anabainisha kuwa kitendo cha haja kutoka kidogo na nyingine kubakia husababisha kuganda katika ukuta wa utumbo na zoezi hilo huendelea mpaka kuwa tatizo sugu.


“Haja kubwa huganda katika kuta za utumbo, hali hii huifanya haja izunguke kwa muda mrefu na ndiyo tatizo hili huanzia hapa,” anasema na kuongeza:
“Unapojisaidia ukiwa umekaa, ile njia ya haja kubwa huwa kama imejifunga, inabidi utumie nguvu nyingi sasa ukiwa na tatizo hili la kukosa haja kubwa huifanya itoke kwa uchache zaidi,” anasema Dk Sikirov.


Aidha, anasema kupata haja kubwa mara kwa mara ni muhimu kwa kuwa usipoitoa maana yake inazungusha sumu katika damu jambo ambalo ni hatari kwa afya.


Anaongeza kuwa kutopata haja kubwa ni kichocheo chenye uwezo mkubwa wa kusababisha saratani ya utumbo mkubwa na uambukizi katika kidole tumbo.


Tafsiri ya kitabibu inasema hali ya kukosa haja kubwa ni pale mtu anaposhindwa kuipata angalau mara tatu kwa wiki. Hata hivyo, ili ujue afya yako ni njema unapaswa kuwa unapata haja kubwa angalau mara moja kila siku.
Daktari Denis Burkitt aliwahi kuandika kitabu cha maelekezo ya chakula ili kuepuka ugonjwa wa saratani. Katika kitabu hicho alieleza namna ambavyo watu wanaweza kujikinga na saratani za aina mbalimbali.


Akizungumzia saratani ya utumbo mpana pamoja na kuelezea vyakula na aina ya maisha, pia aliwaasa watu kutumia choo cha kukaa ili kujiepusha na tatizo hilo.


Anaeleza kuwa kwa Marekani pekee, watu zaidi ya 150,000 hufa kila mwaka kutokana na ugonjwa wa saratani ya utumbo mkubwa.


Mtaalamu wa Ngozi katika Chuo Kikuu cha Sayansi ya Afya na Tiba Muhimbili (MUHAS), Profesa Kisali Pallangyo anasema matumizi ya vyoo hivyo yanaweza kuwa chanzo cha maambukizi ya magonjwa ya ngozi. Profesa Pallangyo anasema ni rahisi kuambukizwa magonjwa ya ngono na ngozi kwa urahisi pale unapotumia vyoo vya kukaa tofauti na vile vya kuchuchumaa.


Aidha, anayataja magonjwa yanayoweza kuwambukizwa kwa kutumia vyoo vya kukaa kuwa ni kaswende, harara, mba, kisonono, upele na mengine.


“Mtu mwenye magonjwa ya ngozi au ya ngono, anaweza kuyaacha katika ‘sink’ anapolikalia, hivyo ni rahisi kwa mtu mwingine ‘kuyachukua’ mara atakapokaa wakati wa kujisaidia,” anasema Prof Pallangyo.


Anasema vyoo hivi ni hatari kwa afya hasa pale vinapotumika katika jumuiya na kuongeza kuwa ni bora kutumia vile vya kukaa ili kujikinga na magonjwa.
Source: MWANANCHI


Kwa jina unaweza muita Leilani Franco  ana urahia wa nchi mbili (Uingereza / Philippines) alisafiri katika nafasi backbend umbali wa 20m  katika muda wa 10.05 dk katika  tamasha la Royal Hall mjini London Uingereza, tarehe 11 Machi 2013. Backbend binadamu ambaye ana uwezo wa kutembealea mikono na miguu kwa umbali mrefu.


Pia kama inavyothaniwa kwa kawaida Mtu anaweza tumia mikono kwa kulia chakula na kufanya shughuli nyingine, lakini kwa mwanamke huyu imekuwa ni tofauti kabisa, Mwamake huyu ana uwezo wa kutumia miguu yake  katika shughuli zake binafsi kama Kula na kadhalika.....
Hatimaye, Leilani pia anashikilia rekodi ya Dunia kutokana na uwezo wake katika kuuzungusha  Mwili wake. 




TAZAMA MAAJABU YA HUYU MREMBO KATIKA VIDEO!!
Anasema yeye mwenyewe binafsi katika kazi zake za ujasiriamali mtaji wake ameupata kwa kuhongwa na mpenzi wake akachanganya na fedha yake na maisha yanakwenda.


Anafafanua kuwa siku zote mpenzi wako hawezi kuacha kukuhonga kwakuwa kwenye mapenzi kusaidiana ni lazima,kwahiyo haoni ajabu yoyote mtu kuhongwa.

"Kusema ukweli mimi mwenyewe boy friend wangu kanisaidia sana na bado anaendelea kunisaidia,mimi sijali mtu aseme lolote analotaka lakini kama nahongwa for benefit sina tatizo na hilo"alisema Linah.

Ameongeza kuwa tatizo watu wamekuwa wana maneno maneno sana na kufuatilia ya watu badala ya kufanya mambo yao lakini ili mradi mambo yake yanakwenda safi hajali lolote anatazama maisha yake zaidi.

 Mwanalizombe Studios Ni Recording Lebel Inayomilikiwa na Rapper Profesa Jay, Studio ipo msasani na Ameamua kuipa Jina la Mwanalizomba kwasababu Jay Ni mtu wa Ruvuma na Mwanalizombe maana yake ni Mwana Ruvuma na kufanya hivyo ameonyesha mapenzi ya mkoa wake wa Ruvuma. Producer kwenye studio hii ni Duke Touchez.


 Profesa ameshindwa kusema amewekeza kiasi gani cha fedha kwenye studio hio ila fahamu kuwa vifaa vilinunuliwa kwa wakati tofauti na ni vifaa vya hali ya juu sana.



Rapper Prezzo wa Kenya aliyehusishwa hivi karibuni na msako wa polici baada ya kusemekana alirushiana risasi na askari, Prezzo amejitokeza na kuweka mambo wazi kuhusu issue hizo na nini hasa kilitokea siku hio na kuhakikisha jina lake linasafishwa. Prezzo ni moja ya rappers wenye aka ya Bad Boy so sio issue mpya kusikia story kama hizi.



Sasa Bwana Jackson Makini aka Prezzo ana habari mpya kwa shabiki wake kuhusu muziki wake. Kaa tayari kwa ngoma mpya kutoka kwa Prezzo Itaitwa " 7 Am" na itatoka siku yoyote mwezi huu. Star huyu kwa sasa bado anatamba na wimbo wake wa ‘Celebration Of Life’aliyomshirikisha Chess .

Rita Paulsen aka Madam Rita wa Bongo Star Search na Walter Chilambo tayari wameshazijibu Salamu za Nay wa Mitego na jana ilikuwa zamu ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe .

Kwake mbunge huyo, Nay ni msanii wa pili wa Hip Hop anayemkubali zaidi Tanzania baada ya Roma na kwamba anakiheshimu kile alichokisema kwenye wimbo huo kwakuwa ni kazi ya sanaa.

Tazama tweets hizi.



CarolNdosi @CarolNdosi
I wonder if @zittokabwe  ever listens to hip hop..local or international..



@CarolNdosi: I wonder if @zittokabwe ever listens to hip hop..local or international..” I do. Roma is my favourite followed by Ney
@zittokabwe @CarolNdosi surprising, after everything Nay Wamitego said in his new truck Salam zao ft Neiba Hon: Zitto still ranks him his n2


@SadiqAbdallah @CarolNdosi Ney amefanya sanaa. Nachukua maneno yake kama changamoto. Ni kazi ya Sanaa ninayoithamini sana.


 Leo tar 2|10 STARBOY was born... el presidente Diamond Platinumz beibb... ikisemekana Penny na Diamond wameachana lakini Penny alivunja ukimya baada ya kupost huo ujumbe on Instagram.

Pichani juu ni taswira mbalimbali za muonekano mpya wa Video Queen wa Bongo, Agnes Gerald Waya ‘Masogange’ ambaye kwa sasa yupo uraiani baada ya kufutiwa mashitaka yaliyokuwa yakimkabili ya kukamatwa na madawa ya kulevya aina ya crystal methamphetamine yenye thamani ya shilingi bilioni 6.8, Julai 5, mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg, Afrika Kusini.


MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), jana alitikisa Jiji la Arusha baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha kumfutia kesi ya uchochezi iliyokuwa ikimkabili.


Lema alidaiwa kutoa kauli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo alienda kwenye Chuo cha Uhasibu Arusha kama anaenda kwenye sherehe za kuaga mtoto wa kike “send off”.
  
Uamuzi huo ulitolewa jana na Hakimu Mkazi, Devota Msofe baada ya wakili wa serikali, Eliananyi Njiro, kutumia kifungu cha 20 kifungu kidogo cha 1 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai kuliondoa shauri hilo ambalo lilikuwa lianze kusikilizwa kwa siku mbili mfululizo. Upande wa serikali ulipanga kuleta mashahidi tisa.
  
Wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliofurika mahakamani hapo kusikiliza mwenendo wa kesi hiyo waliupokea uamuzi huo kwa shangwe kubwa.
  
Akizungumza nje ya mahakama mara baada ya uamuzi huo, Lema alisema kuwa alikuwa anajua shauri hilo ni la kutengenezwa ndiyo maana mashahidi wengi walikuwa ni polisi.
  
“Ni kama nimeshinda kesi, na Mungu ameendelea kutupigania, na tutaendelea kupambana kutafuta haki bila hofu maana miili yetu na nafsi zetu zimeishapoteza maumivu kwa sababu ya mateso yaliyojaa uongo na hila.
“Tutaendelea na kelele zetu za kupigania haki bila kurudi nyuma huku uvumilivu ukiwa nguzo yetu kubwa,” alisema Lema.
  
Hata hivyo, alikiri kutamka kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mulongo alienda Chuo cha Uhasibu kama anaeenda kwenye “send-off” kwani yeye ndiye alimpigia simu akimtaka afike kusikiliza kero za wanachuo, lakini hakulipa uzito unaostahili suala hilo hasa ikizingatiwa kuwa pale kuna mwanachuo alikuwa amepoteza maisha.
  
Lema alisema kuwa wanaweza kuwa wamemfutia kesi hiyo ili kesho wamfungulie nyingine jambo alilodai kuwa yuko tayari kwani anaelewa kuwa lengo ni kutaka kumuogopesha ili aache kuwatetea wananchi kitu alichodai kuwa hawatafanikiwa kwani tayari ana ganzi mwilini mwake, hivyo haogopi kufa, kesi wala kufungwa.
  
Kwa upande wake wakili wa Lema, Method Kimomogoro alisema kuwa ni vema kama serikali ingeamua kutumia busara ya kuona hakuna kesi toka awali, hivyo wasingefungua kabisa shauri hilo lililopoteza muda wa mahakama na mteja wake, kwani hata maelezo ya kesi yalionyesha dhahiri hakukuwa na kosa la uchochezi.
  
Alisema kuwa sheria inaruhusu kumfurahia, kumkejeli au kumzomea mtu, ndiyo maana hata bungeni wanaonekana waheshimiwa wakizomeana na kurushiana vijembe, na akadai hata kauli iliyodaiwa kutolewa na Lema dhidi ya mkuu wa mkoa ilikuwa kijembe tu.
  
Kimomogoro alilitaka Jeshi la Polisi kutenda kazi zao kwa mujibu wa sheria, huku akiwataka warudi kwenye hoja ya msingi na wawaeleze wananchi endapo wameshawakamata waliohusika na mauaji ya mwanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha.
  
Awali, ilidaiwa mahakamani hapo kuwa mnamo Aprili 24, mwaka huu, mshtakiwa Lema akiwa eneo la Freedom Square ndani ya Chuo cha Uhasibu, alitoa maneno ya uchochezi yaliyosababisha uvunjifu wa amani.
  
Maneno hayo yanayodaiwa kutamkwa ni kinyume na kifungu cha 390 sura ya 35 cha sheria ya kanuni ya adhabu, marejeo ya mwaka 2002 .
  
“RC anakuja (Chuo cha Uhasibu) kama anaenda kwenye send-off, hajui chuo kilipo wala mauaji ya mwanafunzi wa chuo hicho... (RC) Ameshindwa hata kuwapa (wanafunzi) pole kwa kufiwa na amesema hawezi kuongea na wanafunzi wasio na nidhamu.” Yalinukuliwa baadhi ya maneno yaliyodaiwa kuwa yalitamkwa na Lema.
  
Kauli hizo zinadaiwa zilipandisha hasira za wanafunzi ambao walianza kumrushia mawe na chupa Mkuu wa Mkoa, Mulongo alipokuwa akiwahutubia kuhusiana na tukio la kifo cha mwanafunzi, Henry Koga kilichotokea Aprili 23, mwaka huu.

Kwa miaka mingi Coca cola imekuwa ni bidhaa namba moja yenye ubora wa kimataifa lakini mwaka huu Bidhaa Apple ikiwemo simu za Iphone imechukua namba moja kwa kuwa ni bidhaa boraDuniani.


Namba mbili imechukuliwa na Google kwa bidhaa zake mbali mbali...Namba tatu ndio imechukua Coca Cola


From New York Times 
Apple is the new most valuable brand in the world, according to a closely followed annual report. The report, to be released next Monday, is from Interbrand, a corporate identity and brand consulting company owned by the Omnicom Group that has been compiling what it calls the Best Global Brands report since 2000. The previous No. 1 brand, Coca-Cola, fell to No. 3.
Not only has Apple replaced Coca-Cola as first among the 100 most valuable brands based on criteria that include financial performance, this is the first time that the soft drink known for slogans like “It’s the real thing” has not been No. 1.

Wednesday, 2 October 2013

DAWA YA FUNGUS YA MIGUU YAONEKANA KUWA NA UWEZO WA KUTIBU UKIMWI.


A drug commonly prescribed to treat nail fungus appears to come with a not-so-tiny side effect: killing HIV in cell cultures.

In a study performed at Rutgers New Jersey Medical School, not only does the drug Ciclopirox rid infectious HIV from cell cultures, but the virus also doesn't bounce back when the drug is withheld.
The same group of researchers had previously shown that Ciclopirox -- approved by the FDA and Europe's EMA as safe for human use to treat foot fungus -- inhibits the expression of HIV genes in culture. Now they have found that it also blocks the essential function of the mitochondria, which results in the reactivation of the cell's suicide pathway, all while sparing the healthy cells.
The researchers said that one aspect of HIV that makes it particularly persistent, even in the face of strong antiviral treatments, is its ability to disable a cell's altruistic suicide pathway -- which is typically activated when a cell is damaged or infected. In other words, infected cells that would normally commit suicide to spare healthy cells no longer pull any altruistic kamikaze missions. Ciclopirox tricks these cells back into their old ways with a double negative, disabling the disabling of the suicide pathway.
"The key thing these drugs do is, unlike anti-retrovirals in the current clinical arsenal, and there are lots of them and they have controlled this disease pretty successfully, these drugs kill the HIV-infected cell," says Michael Matthews, lead researcher and chair of the school's department of biochemistry and molecular biology. "That's what's so new and so promising about it."
It's obviously still going to take clinical trials on humans to study the safety and efficacy of Ciclopirox as a potential topical HIV treatment, but the fact that it's already deemed safe for one type of human use could make the regulatory process faster than usual.
Unfortunately, says Dr. Robert Gallo, a professor of medicine at the University of Maryland best known for co-discovering HIV in 1984, even if the topical antifungal treatment successfully kills HIV-infected cells in clinical trials, it would need to be a systemic treatment, not a topical one, to actually treat (instead of simply prevent) HIV.
"On the positive side, I know Mike Matthews, and he's a superb scientist, probably the lead guy on this," says Gallo, who did not participate in this research. "And that is exciting that it kills cells. That would be very exciting if you could give it systemically and it kills only HIV-infected cells. But topical treatment would be for prevention, not as a therapy. The only way you could use it as a therapy is systemically, and it would be unlikely this could be used systemically."
Posted: 01 Oct 2013 03:41 PM PDT
Matukio yote mawili yametokea jijini Dar es Salaam na kuacha vilio kwa ndugu na jamaa wakiwa hawaamini kilichowakumba wapendwa wao. 

WALIOTENDWA
Wanawake waliojulikana kwa majina ya Mwanahamisi na mwenzake Waisiko Robert Mtundi ndiyo waliodaiwa kuuawa na waume zao, kisa kikubwa kikidaiwa ni hofu ya wanaume hao kusalitiwa katika mapenzi.
WANAODAIWA KUTENDA
Juma Shaban, mkazi wa Manzese Kwamfuga Mbwa na Samuel Gesire Mlimi, mwenye makazi yake Msongola, maeneo yote hayo yapo Dar ndiyo wanaodaiwa kutekeleza ukatili huo wenye kutoa machozi mpaka basi.
MWANAHAMISI ALIVYOUAWA
Ilikuwa saa tatu usiku, Septemba 21, mwaka huu, kila familia ya eneo la Kwamfuga Mbwa ilikuwa ndani kwa chakula cha usiku au maandalizi ya kulala, ndipo waliposikia zogo kutoka ndani ya chumba cha kwa wanandoa hao.
ZOGO NA MANENO
Kwa mujibu wa majirani hao waliozungumza na gazeti hili baada ya tukio, zogo hilo liliambatana na maneno ya shutuma kutoka kwa Juma kwamba mkewe huyo si mwaminifu ndani ya uhusiano wao.
Majirani walisema shutuma za Juma ziliambatana na kelele za Mwanahamisi kuomba msaada akisema ‘nauawa jamani! Nauawa mwenzenu!’
Wakasema baada ya kama saa moja ya mzozo ulipita ukimya, ndipo kila jirani alitoka nje na kuulizana nini kinaendelea ndani ya chumba cha Mwanahamisi na mumewe!
“Baada ya dakika kumi, tulimwona Juma akitoka chumbani kwake huku akiwa anabofyabofya simu yake ya mkononi na kutokomea kusikojulikana,” alisema jirani mmoja huku macho yakiwa yamevimba kwa sababu ya kumlilia Mwanahamisi ambaye wakati huo alikuwa chini ameshakata roho.
Akaendelea: “Baada ya Juma kuondoka tulipatwa na wasiwasi, tukaenda kumwangalia Mwanahamisi chumbani na kumkuta hajitambui, amelala kifudifudi, ana majeraha sehemu mbalimbali za mwili huku akiwa ametapakaa damu. Alikuwa akipumua kwa mbali.
“Alikuwa hawezi kuongea vizuri, mimi nilimsikia akisema hana uhai tena, tumwombee mtoto wake. Ndani ya chumba tuliona viroba vya pombe kali na kisu kikiwa kimelowa damu, nahisi ndicho alichotumia Juma kufanyia ukatili wake.
“Tuliamua kumwahisha hospitali Mwanahamisi lakini kutokana na hali yake tuliona ni vizuri kuwasiliana na polisi ambao walifika baada ya muda.
“Lakini siku yake Mwanahamisi ilitimia kwani wakati polisi wakijiandaa kumchukua kumkimbiza hospitali aliaga dunia.”
KUMBE NI MWEZI MMOJA BAADA YA KUHAMIA
Wengine waliozungumza na gazeti hili siku ya tukio huku wakitoa machozi, walisema Juma ambaye alitoroka baada ya ukatili huo, alihamia kwenye nyumba hiyo mwezi mmoja nyuma lakini walipata umaarufu mtaani hapo kutokana na tabia yao ya kupigana mara kwa mara.
MJUMBE WA MTAA NAYE ANENA
Akizungumza na gazeti hili katika eneo la tukio, Mjumbe wa Nyumba Kumi, Techla Tesha aliwalaumu majirani na wapangaji wa nyumba hiyo kwa kushindwa kumpelekea taarifa mapema huku wakijua mtuhumiwa alikuwa na tabia ya kumpiga mkewe mara kwa mara.
WAISIKO ALIVYOUAWA
Awali ya yote, inadaiwa Waisiko ni mke mkubwa, mke mdogo jina lake halikupatikana mara moja.
Siku ya tukio, saa tatu usiku inadaiwa Samuel alikwenda nyumbani kwa Waisiko ambapo si mbali sana na nyumbani kwa mke mdogo na kuangusha timbwili zito.
“Samuel aliingia ndani na kuanza kumpiga mkewe mkubwa huku akionya majirani kuwa asiwepo mtu wa kwenda kuamua ugomvi wao.
“Sisi kama majirani tuliogopa kwa sababu Samuel alikuwa akitishia kuwa atakayeingia atamchoma kisu.
“Licha ya vitisho hivyo, tulisimama nje ya chumba chao huku vitisho vikiongezeka lakini namna ya kutoa msaada tulishindwa. Hatukujua chanzo cha ugomvi wao.
“Kauli za mwanamke kila wakati ziliashiria alichokuwa akitendwa kwa wakati huo, mfano kuna wakati tulimsikia akisema anavunjwa mgongo, akasema anang’olewa kucha. Pia kuna muda alilalamikia kuvunjwa mkono. Jamani, marehemu aliteswa sana kabla ya kufariki dunia,” alisema shuhuda mmoja.

NI MATESO YA USIKU KUCHA!!
Shuhuda huyo aliongeza: “Mateso ya mwanamke huyo huenda yalikuwa ya usiku kucha kwani nakumbuka mpaka alfajiri ndipo tukasikia sauti ya mwisho ya Waisiko akisema Samuel umeshaniua,  nimalizie kabisa basi. Baada ya hapo hatukusikia tena sauti wala vurugu.

SERIKALI YA MTAA YAZUNGUMZA
Makamu Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Msongola, Juma Chacha alipohojiwa kuhusiana na mauaji hayo, alisema ana taarifa lakini mtuhumiwa alikimbia baada ya kutenda unyama huo na anatafutwa na polisi.

UWAZI LABAINI KISA
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kuwa chanzo cha ugomvi huo ni wivu wa mapenzi kwani ilidaiwa kuwa Samuel alikuwa akimhisi mkewe huyo kutoka nje ya ndoa. 
Chanzo chetu kilisema siku ya tukio, Samuel aliwachukua baadhi ya marafiki zake na kwenda nao baa ambako aliwaambia kuwa anahisi mkewe huyo ana jambo kwani akimuuliza kitu anamjibu jeuri.
Mtoa habari wetu alisema Samuel akiwaambia marafiki hao kwamba siku hiyo akirudi nyumbani, mwanamke huyo atamtambua.

POLISI WALIVYOIKUTA MAITI
Polisi walipofika na kuichunguza maiti waliikuta imevunjwa mkono wa kushoto na kung’olewa kucha za miguu huku uti wa mgongo nao ukiwa umevunjika.
Habari zinasema mara baada ya mtuhumiwa kufanya mauaji hayo, alikwenda kwa mkewe mdogo na kumtaka akamuone mke mwenzie, alipokwenda yeye nyuma akatoroka.
Polisi Mkoa wa Ilala tayari wamemfungulia jalada mtuhumiwa huyo lenye namba STK/RB/10058/2013 MAUAJI.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, ACP Marietha Minangi amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo.


SOURCE:UWAZI.


HATIMAYE siri ya kutekwa, kupigwa na kuumizwa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania (MAT), Dk. Steven Ulimboka,  imefichuka baada ya raia wa Kenya, Joshua Muhindi, kuiambia mahakama kuwa polisi walimlazimisha kusema uongo juu ya kuhusika na tukio hilo.


Alidai polisi walimpa vitisho vingi ambavyo vilimfanya aseme ili kunusuru maisha yake. Muhindi, alitoa siri hiyo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mjini Dar es Salaam mbele ya Hakimu Mkazi, Aloyce Katemana baada ya Wakili wa Serikali Mwandamizi, Tumaini Kweka kumsomea maelezo ya awali.

Mshtakiwa anadaiwa alifika katika Kanisa la Ufufuo na Uzima lililopo Kawe mbele ya Mchungaji Joseph Kiliba kuungama kwa kushirikiana na watu wengine, waliomtesa Dk. Ulimboka katika msitu wa Pande.

Kweka alidai alichukuliwa na kwenda kuhojiwa Oysterbay Polisi, alikubali kufanya kitendo hicho, akapelekwa kwa mlinzi wa amani Mahakama ya Mwanzo, akakataa ndipo alipofunguliwa shtaka la kutoa taarifa ya uongo.

Muhindi alikiri maelezo yote ni sahihi na Kweka aliomba apewe adhabu inayostahili kisheria kwa kuangalia mazingira ya kesi hiyo ilivyojengeka katika jamii na dhima iliyojificha katika jambo hilo. Hakimu Katemana, alimtaka Muhindi kujitetea ili mahakama iweze kumpunguzia adhabu, mshtakiwa alitumia nafasi hiyo kutoa siri ya sakata zima hadi alipofikishwa mahakamani kwa mashtaka hayo.

“Nilitokea Kenya kuingia Tanzania kwa ajili ya kufanya biashara ya nguo, nikiwa Arusha Juni 27, 2012 nilitekwa, nilihamaki na niliweza kufanya chochote alichokuwa akitaka nifanye aliyeniteka.

“Aliyeniteka alikuwa na silaha, aliniambia kila atakachoniambia nikaseme kwa atakayeniambia nikamwambie, kwa vitisho vyake nilipelekwa hadi Tanga mahali nisipopajua wala sijawahi kufika.

“Kaniambia mimi ni Mkristo, ananituma kwa Mkristo mwenzangu, alinipa taarifa ambazo zimesomwa hapa mahakamani na Wakili wa Serikali, nilienda kanisani kutokana na vitisho, yule alikuwa mtu wao ningesema vinginevyo angewaambia ikabidi nimpe taarifa mchungaji kama nilivyoambiwa niseme.

“Nilipokubali kosa kwa kuogopa vile vitisho walinitoa pale kanisani na kunipeleka Polisi Oystebay, Polisi waliniambia ukiendelea kusema vile tulivyokwambia tutakurudisha kwenu na kukubadilishia maisha yako.

“Mimi ni Mkristo, ile kubadilishiwa maisha isingenifanya niseme uongo bali nilisema uongo kwa kuhofia vitisho, Polisi wakubwa walikuja kuniambia tuambie vile vile watu walivyokwambia kusema, walinirekodi nikaona haina haja ya kubishana na Serikali,” alidai.

Alidai baada ya kurekodiwa alipelekwa kwa mlinzi wa amani akaeleza vile vile, lakini alishangaa kuona anafikishwa mahakamani kwa mashtaka ya kujaribu kumteka Dk. Ulimboka.

“Siilaumu Serikali, Polisi, Mungu wala Wakili wa Serikali kwa kukaa gerezani zaidi ya mwaka, najilaumu mwenyewe kwa sababu hata ningekufa kwa kutokubaliana nao mimi si bora kuliko watu wengi katika nchi hii.

“Suala hili lilileta shida katika Serikali ya Tanzania, naiomba mahakama iniamini kwamba taarifa hizi nilizitoa kwa hiari yangu kwa sababu nilikubaliana nao kwa kuhofia kutendewa vitendo vya kuhatarisha maisha yangu.

“Nimekosa mbele ya Mungu na mahakama, naomba kwa ubinadamu na upendo nifikiriwe adhabu kwa sababu nina miaka 23, sijajipanga kimaisha na mkiwa kama wazazi mfikirie kwani hamjui kitakachokuja watokea watoto wenu, katika adhabu mzingatie hayo,” alimaliza kuomba.

Akisoma hukumu hiyo, hakimu Katemana alisema kazingatia maelezo ya pande zote mbili, mshtakiwa alikaa gerezani zaidi ya mwaka, adhabu ya makosa yanayomkabili kisheria ni miezi sita jela au faini ya Sh 1,000.

“Mahakama imezingatia hoja za pande zote mbili, mshtakiwa amekiri kosa hivyo mahakama inamuhukumu kwenda jela miezi sita au kulipa faini ya Sh 1,000,” alisema Hakimu Katemana.

Muhindi aliyefikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Julai 2012, alikuwa hana fedha ya kulipa faini hiyo hivyo mwandishi wa Redio Times FM, Chipangule Nandule, alitoa Sh 1,000 kwa ajili ya kumnusuru kwenda jela miezi sita

Wema kunyongwa China’ ndio kichwa cha habari iliyomtoa machozi Miss Tanzania (2006) Wema Abraham Sepetu leo iliyoandikwa na gazeti liitwalo ‘Filamu’ katika ukurasa wake wa mbele.


Wema ambaye ni CEO wa kampuni ya Endless Fame leo alianza kwa kupost picha ya gazeti hilo na kuandika “Hahahahha.. haya niombeeni watanzania…. aisee… magazeti ni noumerrr… mambo ya kunyongwa tena na wakati sufuria zina shake zenyewe… dah… this made my day”

Na masaa mawili baadaye hiki ndicho Wema alikiandika kupitia Intagram kuhusiana na kilichoandikwa na gazeti hilo.

Dah, Siwezi sema niko happy, im not at all, na sikuwahi kufikiria kwamba magazeti yetu ipo siku yatakuwa na gut ya kuandika uongo wa namna hii. Just because nakaaga kimya ndo muone kwamba mnaweza nionea all da time, roho inaniuma sana, naumia kwasababu nimechoka kuchafuliwa jina bila sababu.

Nimesema nitoke zangu kimya kimya kuja huku kujihangaikia zangu kuhusu kazi zangu ila nimeonekana nimekuja kuuza unga na nitanyongwa soon. Wen are you guys gon leave me in peace..sidhani kama nishawahi kumkosea mtu yeyote kati yenu. Maskini ya Mungu naishi maisha yangu mwenyewe sina habari na mtu. Sijawahi hata kufikiria kufanya those stuff. Nimeumia sana. Da last time I cried was wen nilipoambiwa nina pepo la ngono…leo ninalia ten aim jus so so hurt… God help me please.

Wema siku za karibuni amekuwa aki post picha mbalimbali zinazoashiria yuko nje ya nchi.

Tunasikitika kuwaarifu kuwa kutokana na sababu zisizozuilika, tutashindwa kuendelea kuwaletea habari mpya kupitia tovuti yetu (www.mwananchi.co.tz) na mitandao ya kijamii ya Mwananchi kwa wakati wote ambapo uzalishaji wa gazeti la Mwananchi utakuwa umesitishwa.


Tunasikitika kwa usumbufu wowote utakaosababishwa na hali hii na tunatumaini mtaendelea kuwa nasi wakati wa kipindi  
 hiki kigumu cha mpito. Tunatarajia kurejea rasmi hewani na habari moto moto wiki ijayo, Ijumaa, tarehe 11 October.

Tunawakaribisha muendelee kusoma habari zetu za zamani (archives) kwenye tovuti ya Mwananchi na kurasa zetu za Facebook na Twitter ili mzidi kuhabarika.

Pia tunawakaribisha mtembelee tovuti zetu za www.thecitizen.co.tz na www.mwanaspoti.co.tz ambazo zitaendelea kufanya kazi kwa ufanisi, zikiwaletea habari za uhakika na kuaminika kipindi hiki ambapo Mwananchi imefungiwa.

Ahsanteni,

Wahariri.

Mbunge wa viti maalum kupitia kundi la vijana toka chama cha mapinduzi akiwakilisha mkoa wa Mara wilaya ya Bunda alikuwa akifanyiwa mahojiano katika kipindi cha ''hot mix'' kinachorushwa kupitia kituo cha television cha EATV - Chanel 5!


Akaulizwa swali kuwa nje ya siasa anapenda kufanya shughuli gani?mojawapo ya shughuli aliyoitaja kwamba huifanya ni pamoja na kusoma vitabu na kusikiliza hotuba za wanaharakati kama Martin Luther King Jr., Mwalimu Nyerere na Mandela! 


Katika kukoleza maelezo yake akasema anapenda sana kusoma kitabu kinachoitwa ''How to be a Good Political Leader''. Mtangazaji akamuuliza jina la Author wa hicho kitabu lakini mheshimiwa mbunge akashindwa kumtaja kwakuwa alikuwa hamkumbuki pamoja na kuomba apewe muda ili amkumbuke!!

MY TAKE:
Kwa mtazamo wangu si rahisi mtu kusahau jina la author wa kitabu unachokipenda kukisoma mara kwa mara! Pengine Mh.Esther alikuwa anatafuta mileage kwamba ni msomaji mzuri wa vitabu lakini kachemka kwa kutomjua author wa kitabu akipendacho!


source-JF.



leo tarehe 2 October ni siku ya kuzaliwa kwa Diamond Platnum na katika siku hii maalum amepewa zawadi ya Wimbo na Dogo aitwaye Dogo S.Kide anayedai Diamond ni nduguye wa Damu na amemtenga wala hakumbuki alipotoka.

Wimbo huu kiukweli inamwelezea Diamond Kabla hajatoka Kimuziki.Dogo kaua balaa.Kama hujapata bahati ya kuisikiliza basi isikilize hapa Chini na kuidownload.Ni Bonge 1 la Ngoma.Happy birthday Diamond Platnum.

 Rihanna's New Look iliyoteka headlines kwenye blogs na website tofauti Duniani. Hapa alikuwa akifanya shooting ya video yake mpya ya Pour It Up.

 




 Alicia Keys amefanya kazi kubwa ya kurudisha 
umbo lake baada ya kujifungua. 
Hii Ndio Moja ya show zake za kwanza alizo 
fanya baada ya kurudisha Shapu yake. 








Msanii MAC 2 B amezikwa  leo katika makaburi ya YOMBO MAKANGALAWE  wasanii waliojitokeza kumzika ni wachache sana tofauti na misiba mingine ya wasanii inavyokuwa, ''hii kitu yakuchagua watu wakuwazika sio nzuri kabisa alisikika mdau mmoja akisema'' wasanii wana ubakuzi na hawana ushirikiano.ukiangalia hapa kuna wasanii wachache sana waliojitokeza kumzika mac 2 b. Na hawa ndio wasanii niliowaona leo na watu maalufu katika msiba wa mac 2 b. CRAYZE BUFA,PROD LAMAR,MABAGA FRESH,MOX,KIMALIO,HK,RICH ONE na DAZ BABA .

wasanii wengine mko wapi jaman sio vizuri kabisa.

Mwigizaji Irene Uwoya ambae alipata tuzo ya Steps kama mwigizaji bora kike 2012/2013 amethibitisha kuacha kuigiza movie kwa sasa ili kufanya kazi ambayo ameianza hivi karibuni.


Namkariri akisema: “Nimeamua kuacha mambo ya movie na kuwaachia wengine, haya maamuzi nimeyafanya kama miezi sita iliyopita… Mara ya mwisho kuigiza ni zaidi ya miezi sita iliyopita pia.”

Irene ambae ni mama wa mtoto mmoja kwa sasa anafanya show ya TV ya kusaidia Watanzania wanaoishi kwenye nyumba ambazo ni mbovu au hazina mahitaji muhimu yanayotakiwa kwenye nyumba.

Ni show ambayo haitahusika kujenga nyumba bali kuzirekebisha kwa gharama za mamilioni kwa kutegemea ubovu wa nyumba yenyewe, ambapo Irene amethibitisha hakuna kiwango cha mwisho cha pesa kama bajeti ya kutengeneza nyumba moja bali lengo ni kukarabati nyumba ikamilike.

Movie alizocheza mpaka sasa zinafika 40 lakini za kwake ni nne tu na amekiri kwamba kuacha kwake kuigiza hakuta mshushia kipato chake cha siku zote ambapo kwa movie moja ya kwake mwenyewe alikua anaiuza mpaka kwa milioni 35.

Show yake ya TV imeshaanza kuonekana Tanzania pamoja na kupata wadhamini ambao watamuwezesha kwenye kazi hii kubwa ya kupokea maombi ya Watanzania mbalimbali ambao wanahitaji nyumba zao zirekebishwe bure, kupitia kipindi hicho cha TV.


Mama  mmoja  nchini  Kenya  amejifungua  mtoto  wa  ajabu  ambaye  anafanana  na  viumbe  wawili  wa  dunia  hii.


Sehemu  ya  juu ya  mtoto  huyo  inafana  na  chura  huku  sehemu  ya  chini  ikifanana  na  binadamu  wa  kawaida....

Mtoto  huyo  ambaye  alizaliwa  wikiendi iliyopita  anaonekana  kutokuwa  na  shingo  huku  macho  yake  yakiwa  kama  ya  chura.

Ripoti  ya  kitaalamu  toka  hospitali  ya  Gaurishnkar  ambako  mtoto  huyo  alizaliwa  imeeleza  kuwa  mama  huyo  aliingiliwa  na  mbegu  za  uzazi  wa  chura wakati  akioga  katika  bwawa  la  maji..

"Tulifanya  mazungungumzo  na  huyu  mama  na  akatueleza  kuwa  alikuwa  na  mazoea  ya  kuoga  katika  bwawa.Tunaamini  kwamba  mbegu  za  chura  zitakuwa  zilimwingia  wakati  akiwa  katika  siku  hatari"..Alisema  dakatari  mmoja.


Godzilla akiwa katika studio za R NAME

    R Name na Suma Ryder katika pozz.
   Producer R NAME

Anaitwa Tonya na timu yake ni Mashujaa ya Vingunguti.Amekuwa Bingwa wa Pool Table Mwaka huu.

Mashindano hayo yalifanyika huko Morogoro ambapo Timu yake imeambulia nafasi ya 4 huku Top Land ya Kinondoni ikiibuka Clab Bingwa Mwaka huu.Nafasi ya pili Mpo Afrika na ya Tatu ni Timu kutoka Mkoa wa Manyara.