advert

http://

Thursday, 16 January 2014

B12, ADAM MCHOMVU NA DIVA WAMEPIGWA CHINI CLOUDS FM.



Stori:  MUSA MATEJA
WATANGAZAJI maarufu Bongo wa Redio Clouds Fm ya jijini Dar es Salaam, Hamis Mandi ‘B 12’, Adam Mchomvu na Loveness Malinzi ‘Diva’, wamepigwa chini na kituo hicho, Risasi Mchanganyiko linakupa zaidi.


Habari za chini kwa chini kutoka kwa chanzo chetu zinasema kuwa uongozi wa Clouds umefikia hatua hiyo baada ya kuchoshwa na tabia ya utovu wa nidhamu wa watangazaji hao.

Hata hivyo, madai ya mitaani yanasema kwamba watangazaji hao wamepigwa chini kwa kosa la kukacha sherehe za maadhimisho ya miaka 14 ya Clouds FM,yaliyofanyika hivi karibuni katika Viwanja vya Mwembeyanga, Temeke, Dar.

Risasi Mchanganyiko lilimvutia waya Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba na kumwuliza juu ya ishu hiyo ambapo alikiri.


“Ni kweli tumefikia uamuzi wa kuwasimamisha B 12, Diva na Mchomvu baada ya kukiuka baadhi ya makubaliano baina yao na ofisi hivyo kusababisha usumbufu mkubwa ambao ulitulazimu kuingia gharama ambazo hazikutarajiwa.

“Hatutakuwa nao kwa muda usiojulikana ingawa watu wengi wamekuwa wakinihoji juu ya hilo lakini watachotakiwa kuelewa ni kwamba hakuna ofisi isiyokuwa na sheria na taratibu za kuongoza watu wake, sasa hao wamevunja taratibu zetu,” alisema Ruge bila kufafanua zaidi.

Alipoulizwa ni taratibu zipi watangazaji hao walizovunja alisema: “Nashindwa kueleza kosa la kila mmoja ila naomba nieleweke kuwa hao watangazaji kwa sasa tumewasimamisha kwa muda usiojulikana wakati tukifikiria cha kufanya. Muhimu hapo ni kwamba wamekwenda kinyume na tulivyokubaliana.”


Credit:GPL


Utata umeibuka kuhusu alipo mfanyabiashara maarufu nchini, Alex Masawe baada ya kuwepo kwa tetesi kuwa ameachiwa huru huko Dubai, Falme za Kiarabu (UAE) alikokuwa akishikiliwa.


Masawe ambaye alikamatwa katika uwanja wa ndege huko UAE akitokea Afrika Kusini, kati ya Juni 20 na 25, mwaka jana, anatuhumiwa kwa makosa mbalimbali yakiwamo ya mauaji.

Mkuu wa Shirika la Polisi la Kimataifa (Interpol) - Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile alikiri kuwapo kwa taarifa kwamba Masawe ameachiwa huru na hayupo Dubai ingawa bado tawi la Interpol katika nchi hiyo halijatoa taarifa yoyote.

“Tumejaribu kuwasiliana nao mara kwa mara kuhusu kumrudisha nchini lakini hawajajibu lolote. Hivi karibuni tuliwasiliana nao lakini hawajatujibu, kwa hiyo tumebaki na maswali. Kwa kifupi hatujui alipo hadi sasa,” alisema Kamishna Babile.

Alisema awali, baada ya kukamatwa huko Dubai, Tawi la Interpol Tanzania lilikuwa linafanya mchakato wa kumrudisha nchini ikiwamo kutuma ombi la kumrejesha mhalifu nchini, lakini ghafla mawasiliano yakakatika.

“Taarifa zilizopo ni kuwa Masawe ameachiwa huru, kwa vigezo gani hatuelewei,” alisema Babile.

Babile alisema iwapo atakuwa ameachiwa na polisi wa UAE, basi itakuwa ameachiwa kutokana na sheria za nchi hiyo ingawa bado Tanzania itaendelea kumsaka kwa udi na uvumba.

“Sisi tutaendelea kumsaka kama kawaida, iwapo atakamatwa nchi nyingine au ikitokea akaonekana hapa nchini, tutaendelea na mchakato wa kumfungulia kesi kwa sababu sisi tunajua kuwa ana makosa,” alisema Babile.

Massawe alitajwa mahakamani Aprili 4, mwaka jana katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara, Onesphory Kituly ambaye aliuawa katika mazingira ya kutatanisha Novemba 6, 2011 nyumbani kwake Magomeni, Dar es Salaam.

Katika kesi hiyo, mshtakiwa wa kwanza ni mfanyabiashara Abubakar Marijani, maarufu kama ‘Papaa Msofe’ na mshtakiwa mwingine ni Makongoro Joseph Nyerere.

Nyerere aliwahi kulalamika mbele ya Hakimu Mkazi, Agnes Mchome anayesikiliza kesi hiyo, akidai kwamba kumekuwa na ucheleweshaji wa shauri hilo kutokana na ndugu wa marehemu Kituly kutaka Massawe akamatwe ili ajumuishwe.

Mtuhumiwa huyo aliomba jalada la kesi yao lipelekwe mahakamani hapo kwa ajili ya kulifanyia kazi. Alitoa malalamiko hayo baada ya Wakili wa Serikali, Mwanaisha Kombo kudai upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuomba tarehe mpya ya kutajwa kwake.


Rosemary Namubiru, 64, was produced before Buganda Road Court to answer to charges of 
attempted murder. She denied the charges


Chief Magistrate Olive Kazaarwe sent her to Luzira prison until January 31 following her failure to apply for bail. She also never had a legal representative in court.

Over the weekend, the country was thrown into dismay after Namubiru was arrested by Wandegeya police for maliciously infecting her patients mainly the children with her HIV positive blood.

Prosecution led by Martin Rukundo, alleges that on January 7, 2014 at Victoria Medical Centre, along Lumumba Avenue in Kampala, Namubiru with intent to unlawfully cause the death of two year-old Mathew Mushabe, pricked her finger and used the same syringe to inject the same child well knowing that she was HIV/Aids positive.

According to police records, on the fateful day the child was showing signs of tonsillitis, an inflammation of the tonsils.

The mother of the victim decided to take her sick son to Victoria Medical Centre, one of the health centers on the family’s health insurance scheme.

Unfortunately on her arrival, she found that the doctor who normally attends to her family was absent before the medical facility assigned nurse Namubiru.

But to the mother’s surprise, the nurse got hold of a syringe, first pierced one of her fingers, drew out some blood, and then injected the baby.

The terrified mother shouted at the nurse to stop injecting her child before reporting the matter to the in-charge of the facility leading to her arrest.

Later the victim’s family demanded to know Namubiru’s HIV status and upon testing, she was found to be positive.

Immediately, the child was transferred to another health centre and put on PEP treatment for the next 30 days with the aim of avoiding the contraction of the deadly virus.

Source: Redpepper


Waumini wa Mchungaji Daniel walijikuta wakianza kuumwa mara baada ya Mchungaji huyo kuwafanya wale wale majani.

Picha zinazofuata zinaonyesha watu tofauti wakiwa wagonjwa kwenye vyoo -  picha za vyooni zinawaonyesha wanawake wakishikilia matumbo yao, huku wanaume wakiwa wanatapika kwenye masinki.

Japokuwa Mchungaji huyo bado hajasema lolote juu ya tukio hilo ila kupitia ukurasa wake wa Facebook hapo jana aliandika: 'Mungu yupo kazini na watu wake wanatoa ushuhuda sasa'

Taarifa za kuibuka kwa kainsa hilo zilianza kusamba katika mitandao mbalimbali ya kijamii ambayo kwa nyakati tofauti iliripoti kuwepo kwa kanisa linaloimiza waumini wake kula nyasi kama ishara ya kutangaza miujiza ya Mungu.

Uchunguzi uliofanywa na Wadadisi wa Habari, ulibaini uwepo wa kanisa wa aina hiyo maeneo ya Upanga jijini Dar es salaam na huduma yao inafanywa kwa kutumia jina la Rabboni Centre Ministries yenye makao yake makuu jijini Pretoria, Afrika Kusini.

Waandishi wa Habari hizi, walifika Upanga, kwenye nyumba inayodaiwa kuwa ndilo kanisa hilo lakini hakuna mtu aliyekutwa hapo.

Hata hivyo, baadhi ya majirani walisema huwa wanawaona watu wakiingia katika nyumba hiyo lakini ajabu kunakuwa hakuna kelele zozote.

Chanzo chetu cha habari kimesema kuwa waumini wa kanisa hilo hula nyasi na baadaye kutapika, hali inayowafanya waamini kuwa kwa kufanya hivyo, wametakasika kiroho kwa kujazwa Roho Mtakatifu.

“Mchungaji wao huwakusanya waumini wake wanaopandisha mashetani wakiwa kanisani, hiyo hufanya shetani kumtoka mtu haraka,” kilisema chanzo.

Habari zinasema huduma hiyo ilianzishwa Afrika Kusini na Mtu anayejiita kuwa ni Mchungaji na Nabii Daniel Lesego mwaka 2002.

Imedaiwa kuwa kwa sasa waumini hao wapo kwenye mfungo ambao watu hufika kanisani na baadaye kula majani yaliyopo nje ya kanisa hilo wakisema kwamba Roho Mtakatifu huongoza mtu kula chochote huku ikidaiwa kuwa manyasi hayo ni chakula kutoka mbinguni

Monday, 16 December 2013

MWALIMU AFA KIMIUJIZA.



Mwalimu Gloria Tarimo ‘Ticha Gloria’ (29) aliyekuwa akifundisha katika Shule ya Mbezi High School ya jijini Dar, amefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha
huku baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wakidai kifo chake ni cha kimiujiza.
Ticha Gloria ambaye alikuwa akikaimu nafasi ya mwalimu mkuu wa shule hiyo, alifariki dunia Desemba 6, mwaka huu katika Hospitali ya Muhimbili jijini Dar huku wengi wakihisi kuna mkono wa mtu nyuma ya kifo hicho.
                                                      Marehemu Glory A Tarimo enzi za uhai wake.
USHIRIKINA WAHUSISHWA
Akizungumza na gazeti hili, mmoja wa ndugu wa marehemu aliyeomba hifadhi ya jina lake kwa kuwa si msemaji wa familia alisema, kifo cha Ticha Gloria kinahusishwa na ushirikina kwa kuwa kabla ya mauti kumfika alikumbana na mambo mengi ya ajabu.
“Ni kifo cha ajabu kwa kweli na kimemshangaza kila mmoja wetu. Nakumbuka ilikuwa Juni, mwaka huu ambapo alienda kazini na alipofika kwenye mlango wa ofisi yake alikuta nazi imevunjwa.
“Licha ya kushangazwa na uwepo wa nazi hiyo, aliiruka kisha akaingia ofisini kwake. Kuanzia hapo alianza kuumwa mguu, kuna wakati akawa anahisi unawaka moto. Tulimpeleka Hospitali ya Muhimbili, akapatiwa matibabu na akapata nafuu,” alisema ndugu huyo.

AKUTA NJIWA KWENYE KITI OFISINI
Ndugu huyo alizidi kueleza kwa masikitiko kuwa, baada ya tukio hilo la kukuta nazi imevunjwa kwenye mlango wa ofisi yake, mambo hayakuishia hapo kwani hivi karibuni alipoingia ofisini kwake alikuta Njiwa kwenye kiti chake.
“Alipiga kelele sana, walimu na wanafunzi wake wakaja  kushuhudia huku kila mmoja akishangaa na kuogopa kumtoa njiwa yule kwenye kiti.
“Mwalimu mmoja aliyefahamikwa kwa jina la Fadhili ndiye aliyemuondoa njiwa yule. Bila kujua kuwa roho yake inasakwa, Gloria akakaa kwenye kile kiti na kuendelea na shughuli zake,” alisema ndugu huyo na kuongeza:
“Haikuchukua muda mrefu akahisi kama anachomwa na kitu chenye ncha kali kwenye makalio yake huku kichwa kikimuuma sana. Walimu wenzake walimchukua na kumrudisha hospitalini.”

AANZA KUZIONA SIKU ZAKE MFULULIZO
 Ilielezwa kuwa, baada ya mwalimu Gloria kufikishwa hospitalini, hali ilizidi kuwa mbaya na akaanza kutokwa na damu ya hedhi mabongemabonge huku damu nyingine ikitokea puani.
Ndugu wa Marehemu.
“Hali ilikuwa hivyo, akawa anateseka sana huku wakati mwingine akilalamikia baadhi ya walimu wenzake kuwa ndiyo wanaotaka kumtoa roho.
“Kuna siku alimuita daktari aliyekuwa akimhudumia na kumwambia anamshukuru kwa kujitahidi kuokoa uhai wake lakini anaamini hatapona kwani anajua kuna walimu wamedhamiria kumuua ili wakalie kiti cha ualimu mkuu, baada ya hapo alikata roho,” alisema ndugu huyo ambaye ndiye aliyekuwa akiwasiliana na marehemu mara kwa mara.

WALIMU WANASEMAJE?
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, baadhi ya walimu wa shule hiyo walisema wamesikitishwa sana na kifo cha Ticha Gloria, wakasema licha ya kwamba kila kifo kinapangwa na Mungu lakini hiki cha mwenzao kimeacha utata.
“Kwa kweli kifo cha Gloria kimenifanya niamini kuwa Mungu yupo lakini pia ushirikina upo. Amekufa kifo cha kimiujiza sana, mambo yaliyomtokea kabla ya kufariki dunia yanaashiria kabisa kuna mkono wa mtu,” alisema mwalimu mmoja wa kike aliyeomba hifadhi ya jina lake.
MSIKIE MWENYE SHULE
Mkurugenzi wa shule hiyo aliyefahamika kwa jina la Said Mgude alielezea masikitiko yake juu ya kifo cha mwalimu Gloria kwa kuwa alikuwa mchapakazi sana ila akataka watu wasihusishe kifo hicho na mambo ya kishirikina.
“Kila mmoja lazima aumie kwa kifo cha Gloria, lakini nawasihi watu wamuamini Mungu na waachane na dhana za kishirikina. Shule yangu ni taasisi kubwa sana, minazi ipo mingi hivyo kama alikuta nazi imevujwa mlangoni inawezekana ilianguka tu na kupasuka.
“Kuhusu Njiwa hapa Dar es Salaam siyo jambo la ajabu kwa sababu wapo wengi sana, mimi siwezi kukubaliana na mambo hayo ya kishirikina na hakuna kitu kama hicho,” alisema.
Mwili  wa mwalimu Gloria uliagwa Desemba 10, mwaka huu katika Kanisa Katoliki Mbezi Mwisho jijini Dar na baadaye ulisafirishwa kwenda  Moshi Rombo mkoani Kilimanjaro na kuzikwa siku iliyofuata ya Desemba 11.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi-Amin.

Stori: Gladness Mallya, Nyemo Chilongani na Haruni Sanchawa.

Stori: Mayasa Mariwata na Chande Abdallah

JAMANI jamani! Dunia imefika pabaya zaidi, Mungu asaidie. Mwanamke mkazi wa Chalinze,
Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga, inauma sana kwa kweli!
  Mwanamke mkazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga.

Tukio hilo la kutisha lilijiri usiku wa Desemba 7, mwaka huu…
Stori: Mayasa Mariwata na Chande Abdallah
JAMANI jamani! Dunia imefika pabaya zaidi, Mungu asaidie. Mwanamke mkazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga, inauma sana kwa kweli!
  Mwanamke mkazi wa Chalinze, Mkoa wa Pwani, Moshi Rashid (43) amefanyiwa unyama uliopitiliza na watu wasiojulikana baada ya kumbaka na kumnyonga.
Tukio hilo la kutisha lilijiri usiku wa Desemba 7, mwaka huu Chalinze Kwamwarabu ambapo mwanamke huyo alikwenda kujumuika na ndugu na majirani katika mkesha wa ngoma ya kuwatoa wari siku ya Jumapili.
                                                              Eneo la tukio Chalinze Kwamwarabu.
Mkasa huu unasimuliwa kwa majonzi mazito na mdogo wa marehemu ambaye alikuwa mshehereshaji wa shughuli hiyo ‘MC’, Siwema Rashid.
Alisema: “Mpaka sasa tunashindwa kuelewa kilichotokea maana siku ya tukio tulikuwa naye kwenye ngoma usiku. Alikuwa mchangamfu sana, aliifanya shughuli ipendeze.
“Ilipofika saa nane usiku baadhi ya watu walianza kulala, sasa sijui yeye ilikuwaje mpaka hali hiyo ikamfika maana hao watu walichomfanyia wametuachia historia kubwa sana.
“Walimbaka wakaona haitoshi wakamwingiza chupa ya soda sehemu ya siri ya mbele halafu wakamwingiza chupa ya bia sehemu ya siri ya nyuma.
“Ili kuzidi kutimiza unyama wao, waliondoka na kumwacha kama alivyozaliwa, inauma sana halafu matukio ya hivyo yamekithiri sana.”
Aliongeza: “Marehemu ametuachia jukumu la malezi kwa watoto wake wawili, Sikudhani Juma (18) na Ally Juma (12).”
Naye mtoto mkubwa wa marehemu, Sikudhani akisimulia kifo cha mama yake, alisema: “Nasikitika sikuweza kuuona mwili wa mama hata pale watu walipojazana na kumshangaa.

“Hata polisi na mganga mkuu wa mkoa walipofika kumchomoa zile chupa sikutaka kusogea kabisa, naamini Mungu atawaonesha jambo hao watu hapahapa duniani.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Yurichi Mtei akizungumzia ukatili huo alisema: “Taarifa za tukio hilo bado hazijafika kwangu kutokana na majukumu mengine ya kikazi, isipokuwa nalifanyia kazi kuhakikisha watuhumiwa wanakamatwa.”
Tukio hilo lilifunguliwa jalada kwenye Kituo cha Polisi Chalinze kwa nambaCH/RB/3767/2013 MAUAJI.
Mpaka kifo chake, mwanamke huyo alikuwa akiishi na mwanaume mmoja (jina halikupatikana mara moja lakini si aliyezaa naye watoto hao wawili). Alizikwa Jumapili iliyofuata, Chalinze.
Mungu ailaze pema peponi roho yake. Amina.

source:GPL

Sunday, 15 December 2013

Mama Mlemavu Akionyesha UPENDO kwa Mwanae.


Upendo wa Mama.

Wakazi wa eneo la Likoni, Mombasa nchini Kenya walipatwa na mshangao mkubwa mara baada ya mbuzi mmoja kujifungua mtoto mwenye sura inayofanana na binadamu.

Tukio hilo lilifanya shughuli mbalimbali kwenye kijiji hicho kusimama huku wakazi wa eneo hilo wakiwa wanastaajabu juu ya tukio hilo la ajabu.
 
Tazama video ya tukio hilo hapo chini....
 

Lulu
Muigizaji wa filamu nchini Elizabeth Michael aka Lulu, amesema kuwa hatamani tena kutumia simu ya mkononi kwakuwa anasumbuliwa mno na watu wasiokuwa na mambo ya msingi huku akitamani irudi enzi ya kutumiana barua.


Akiongea na paparazi wetu jana,Lulu alisema kuwa kero hiyo humfanya atamani kurudi katika enzi za kale za kuwasilia kwa kutumiana barua kwa njia ya posta.

“Nadhani sihitaji simu ya mkononi kwa sasa, mwenye shida na mimi atanitumia barua. Sijui, hata sijielewi nikasimame wapi, maana hata nikibadili nambari ya simu inasambaa kwa kasi sana,”alisema.

Lulu alibainisha kuwa kwa siku hupigiwa simu zisizokuwa na idadi na zisizo na faida kwake, lakini akakiri kwamba idadi kubwa ya watu wanaompigia simu ni mashabiki wake.

“Ninapigiwa simu nyingi kwa siku ambazo ni kero kwangu, nafurahi sana ninapopigiwa simu na shabiki wangu, lakini wapo wanaopiga simu kutaka mambo ya ajabu. 

Sawa ni wengi wao ni mashabiki wangu, lakini simu kwangu ni kero kubwa ingawa ni msaada mkubwa pia kwangu ni sehemu ya kitendea kazi.”
Posted: 14 Dec 2013 04:07 PM PST
http://www.theclicktz.com/
Mwanafunzi wa chuo kimoja alimwagiwa mafuta ya moto na rafiki yake kipenzi baada ya kumkuta na boyfriend wake wakifanya mapenzi.


Ilikuwa ni siku ya ijumaa Nasra alipokuwa akitoka darasani na kurejea hostel alipokea sms ikisema "Nenda kwa Rafiki yako kipenzi Naima kuna Bonge la Surprize, tafadhali usikose nenda sasa hivi" Nasra aliamua kuchukua pikipiki hadi kwa rafiki yake alipofika tu alikuta viatu vya boyfriend yake nje, akashtuka kwanza kwani sio kawaida ya jamaa huyo kwenda kwa Naima bila ya kuwa na Nasra, Nasra alijaribu sana kugonga lakini hakufunguliwa, na baadae aliamua kupiga simu zote mbili ya rafiki yake na ya boyfriend wake pia zote zikaita tu bila kupokelewa, Alikaa pale nje hadi majira ya saa sita usiku, ambapo alishajua kunakitu kinaendelea. Muda ulivyozidi kwenda  Nasra alitoka na kwenda kuchukua marafiki zake wengine wawili, aliporudi alikuta bado hawajatoka ndani.

Mpaka majira ya saa saba hivi usiku, Nasra akiwa amebeba mafuta ya moto kwenye chupa ya chai yeye na marafiki zake walivunja mlango na kuwakuta wawili hao ndani wakiwa katika hali ya uoga jamaa alifanikiwa kukimbia na kumuacha Naima chumbani ambapo Nasra alifungua chupa ya chai na kumwagia mafuta hayo ya moto rafiki yake huyo msaliti.
Nasra alikamatwa baadae na kufikishwa kituo cha polisi ambayo alihojiwa na kusema kwamba, alikuwa akipata tetesi na uvumi kwamba mchumba ake anatembea na rafiki yake kwa siku nyingi hivyo alikuwa anatafuta tu uthibitisho, na ameupata baada ya kuatilia kwa muda mrefu. 

 Exclusive: Mkuu wa Wilaya ya Musoma Mjini, Jackson Msome aelezea mapokezi ya Mshindi wa EBSS 2013 na washiriki waliofika top 5 Musoma, yanatarajiwa kuweka historia (Audio)

Mshindi wa EBSS 2013 Emmanuel Msuya ameandaliwa mapokezi ya kiserikali leo, Musoma mjini ambapo ndipo makazi yake.

Mkuu wa wilaya ya Musoma Mjini, mheshimiwa Jackson Msome amesema wamemuandalia mapokezi mazuri kwa kuwa ushindi wake umeleta heshima kubwa katika mji huo.
“Kwanza ni mkazi wetu, ni mkazi wa mji wa Musoma. Sisi tukiwa kama wenzie na viongozi wake, kwanza tunayo fahari kwa ushindi wake. Lakini la pili tulimsapoti sana na tulimuomba sana Mungu amsaidie katika jitihada zake hizo. Ushindi wake huo unaleta heshima kwake, kwa wilaya yetu, kwa mkoa wetu, kwa kanda yetu na Tanzania kwa ujumla. Kwa hiyo tuna kila sababu ya kufurahi pamoja naye.” Mheshimiwa Msome aliiambia tovuti ya Times Fm.
Mheshimiwa Msome, ameelezea pia faida/changamoto waliyoipata vijana wa Musoma wenye vipaji kutokana na ushindi wa Emmanuel Msuya.
“Hii ni changamoto kwa vijana, kwamba vijana wapo na wana vipaji mbalimbali. Kinachotakiwa ni kutambua fursa zilizopo na hivyo kuzitumia kujitokeza kukuza vipaji vyao, na kwa kweli ni sehemu ya ajira kwa vijana wetu.”
Naye mratibu wa mapokezi hayo ambaye ni mdau wa muziki mjini musoma maarufu kwa jina la Kayombo, amesema kuwa mapokezi hayo yatakuwa ya kihistoria kwa mtu wa kawaida ambaye sio kiongozi wa nchi, na kwamba kutakuwa na misafara ya pikipiki na magari. Ameongeza kuwa kesho (December 15) washiriki waliombatana na Msuya watatumbuiza katika ukumbi wa Bwalo la Polisi.
Akiongea na Times Fm wakati akiwa uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam, Emmanuel Msuya amesema yuko na timu ya washiriki waliofika Top 5 ya shindano hilo pamoja na mama yake mzazi na wanaelekea Mwanza.
Amesema wanategemea kuingia Musoma majira ya saa kumi na moja jioni.
Emmanuel Msuya alitangazwa kuwa mshindi wa EBSS 2013, November 30 na kuwa mmiliki wa shilingi Million 50 zilizokuwa zinashindaniwa. 

MWANAMKE MMOJA AMWAGIWA MAJI YA MOTO NA MWANAMKE MWENZIE KISA WIVU WA KIMAPENZI.


Bi. Neema Teti aliyemwagiwa maji ya moto mwili mzima, kwa kudaiwa kuwa na uhusiano na mume wa mtu. 


Muuguzi wa zamu Bi. Neema Bayo akimfunika majeruhi Bi. Neema Teti aliyemwagiwa maji ya moto mwili mzima, kwa kudaiwa kuwa na uhusiano na mume wa mtu.  

Bi. Neema Teti aliyemwagiwa maji ya moto mwili mzima, kwa kudaiwa kuwa na uhusiano na mume wa mtu.

Na Gadiola Emanuel -Arusha

Mwanamke mmoja mkazi wa Mbuguni Arusha,Bi. Neema Teti amejeruhiwa vibaya kwa kumwagiwa maji ya moto katika sehemu mbalimbali za mwili wake katika kisa kinachodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi. Tukio hilo limetokea baada ya mtekelezaji wa kitendo hicho Mama Tatu Msuya ambaye ni jirani yake akidaiwa kumtuhumu majeruhi huyo kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mume wake.
Katika wodi ya wagonjwa majeruhi hosipitali ya Mkoa wa Arusha Mount Meru alikolazwa,Neema ameelezea tukio hilo kuwa limetokea juma lililopita baada ya kuitikia mwito wa jirani yake Tatu Msuya uliomtaka afike nyumbani kwake kwaajili ya kumsaidia uangalizi wa familia yake kutokana na kuhitajika msibani na ndipo alipomjeruhi vibaya kwa kumwagia maji ya moto.Neema Teti-Majeruhi
Muuguzi wa zamu katika hospitali ya Mount Meru,Neema Bayo amesema majeruhi huyo aliletwa hospitalini hapo akiwa katika hali mbaya lakini hali yake imezidi kuimarika baada ya kupatiwa matibabu na jopo la madaktari hospitalini hapo. Nae Muuguzi wa wodi ya majeruhi mount Meru Hospitali Bi.Neema Bayo amesema matukio kama hayo yakizidi kushamiri katika maeneo mbalimbali
nchini,bado inaelezwa kuwako kwa ugumu wa kutoa taarifa katika vyombo vya sheria kutokana na wahusika kuwaficha wahalifu mara wanapotoka hospitalini
Afisa wa dawati la jinsia mkoa wa Arusha Maria Maswa akizungumza wakati alipotembelea waathirika wa matukio ya unyanyasaji wa kijinsia katika hospitali ya mount Meru,amesema yanapotokea matukio hayo,walengwa wamekuwa wagumu kutoa ushirikiano kwa madai ya kumaliza swala hilo kinyumbani hatua inayochochea ukuaji wa matatizo hayo.Maria Maswa-Afisa Dawati la Jinsia Mkoa wa Arusha Bi. Maria Maswa alisema "Kufuatia tukio hilo Jeshi la Polisi Mkoani Arusha limeeleza kuwa linaendelea na msako dhidi ya Mama Tatu Msuya anayedaiwa kutekeleza kitendo hicho; pia aliongeza kuwa jumla ya kesi 507 zimeripotiwa kati kipindi cha mwezi november 2012 mpaka sasa. 
Picha zote na Gadiola Emanuel wa Wazalendo 25 Blog.

Rihanna aandika historia nyingine kubwa kimuzikiRihanna amefanikiwa kuandika historia nyingine kimuziki kufuatia wimbo alioshirikishwa Eminem, Monster kuwa wimbo wake 13 kukamata nafasi ya kwanza kwenye chart za Billboard.
Akiwa na nyimbo 13 zilizokamata nafasi ya kwanza, amewazidi Madonna, Stevie Wonder na Whitney Houston na amefungana na hayati Michael Jackson.
Wanaoongoza kwa kuwa na nyimbo nyingi zilizoshika nafasi ya kwanza ni the Beatles walioingiza nyimbo 20 na kufuatiwa na Mariah Carey mwenye nyimbo 18.

Video: Mkalimani feki wa viziwi kwenye kumbukumbu ya Mandela ajitetea, asema aliona malaika wakiingia uwanjani akachanganyikiwaMkalimani anayeshutumiwa kwa kudanganya alama za viziwi wakati akitafsiri hotuba za viongozi mbalimbali wa dunia akiwemo Rais Barack Obama wa Marekani kwenye hafla ya kumbukumbu ya Nelson Mandela, Alhamis hii amesema alikuwa akiona malaika wakiingia kwenye uwanja huo wa mpira wa FNB na kwamba amekuwa akisumbuliwa na tatizo la akili.
Thamsanqa Jantjie amehojiwa na shirika la habari la The Associated Press aliloliambia kwamba mauzauza hayo yalianza alipokuwa akitafsiri na kwamba alijaribu kutopanic kwasababu polisi wenye silaha walikuwa karibu yake.
“Kilichotokea siku hiyo, niliona malaika wakiingia uwanjani. Nilianza kugundua kuwa tatizo lilikuwa hapa. Na tatizo, sijui shambulio la tatizo hili, litakujaje. Wakati mwingine huwa nakua katili sehemu hizo. Huwa naona vitu vinavyonifukuza,” alisema Jantjie.
“Nilikuwa kwenye wakati mgumu sana,” aliongeza. Na kumbuka watu hao, Rais na kila mtu, walikuwa na silaha, kulikuwa na polisi wenye silaha pembeni yangu. Ningeanza kupanick ningezusha tatizo. Nilitakiwa kukabiliana nalo ili nisiiabishe nchi yangu.”
Aliongeza kuwa aliwahi kulazwa hospitali ya wagonjwa wa akili kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Serikali ya Afrika Kusini imekiri kuwa kulifanyika makosa katika kumchukua Jantjie kwa kazi hiyo.
Naibu waziri wa Wanawake, Watoto na Walemavu, Hendrietta Bogopane-Zulu alisema maafisa wa serikali wamejaribu kufuatilia kampuni iliyompa kazi Thamsanqa Jantjie lakini wamiliki wa kampuni hiyo wameingia mitini.
Aliwaomba radhi watu wote wenye ulemavu wa kusikia na kusema kuwa uchunguzi unafanyika kubaini ni vipi Jantjie alikuwa amechukuliwa kufanya kazi hiyo.
Aliongeza kuwa kampuni hiyo ilitoa huduma chini ya kiwango na kwamba ujira waliomlipa mkalimani huyo kilikuwa kidogo mno. Mkalimani huyo alilipwa dola 85 tu.
AP waliomuonesha Jantjie video inayomuonesha akitafsiri kwenye hafla hiyo na kusema hakumbuki  chochote.
“I don't remember any of this at all.

Surprise: Beyonce aachia album mpya kwa kushtukizaWeekend hii, Beyonce ameachia album yake ya 5, iliyopewa jina lake mwenyewe na inapatikana itunes pekee yake.

Katika album hiyo, Beyonce amewashirikisha wakali akiwemo mumewe, Jay Z, Drake, Frank Ocean na mwanae Blue Ivy.
Hiyo ni album yake ya kwanza tangu mwaka 2011 alioachia albam yake ya nne, "4".
Beyonce ina jumla ya nyimbo 14. Cha kuvutia ni kuwa kila wimbo kwenye albam hiyo ina video yake ambayo nayo inapatikana iTunes.
Hizi ni nyimbo zilizopo kwenye "Beyonce":
1. Pretty Hurts
2. Haunted
3. Drunk In Love (feat. Jay Z)
4. Blow
5. No Angel
6. Partition
7. Jealous
8. Rocket
9. Mine (feat. Drake)
10. XO
11. Flawless (feat. Chimamanda Ngozi Adiche)
12. Superpower (feat. Frank Ocean)
13. Heaven
14. Blue (feat. Blue Ivy) 

Label ya Baby Madaha, Candy n Candy yakumbwa na mgogoro, polisi waingilia katiMigogoro kwenye label ya Kenya inayomsimamia Baby Madaha imeonesha kutengeneza makazi ya milele kila anaposainishwa msanii mpya. Ikumbukwe kuwa wasanii wa zamani wa label hiyo walianza kulalamika kuwa CEO wa label hiyo, Joe Kariuki alikuwa akimpendelea mno Baby Madaha na kuwaacha wao wakisaga miguu tu.
Na sasa baada ya kusainishwa msanii mpya wa Nigeria, Lil Gee na kuachia wimbo mpya na kisha kutaka afanyiwe video, vijana wa zamani wameanza kulalamika tena.
Mmoja wao ni Dazlah Kiduche, aka ‘Dazlah’ ambaye hiyo haijamuingia kichwani kwakuwa anashangaa iweje mgeni apate video wakati yeye aliyeanza kuachia wimbo wake “Bangereba” akiwa hana video bado. Wasanii hao walijikuta wakiingia kwenye ugomvi mkubwa uliofanya hadi polisi waitwe kwenye ofisi hizo kusuluhisha mambo.
Chanzo kilichoongoea na mtandao wa Niaje wa Kenya kimesema kuwa CEO Joe Kariuki bado hajaamua video ya nani ianze kutoka.

Rich Mavoko atolewa machozi na Mama Sharo anayedai kudhulumiwa haki za mwanaeMuimbaji wa Roho Yangu, Rich Mavoko amemtembelea mama mzazi wa marehemu Sharo Milionea huko wilayani Muheza Tanga.

Mavoko ameshare picha akiwa na mama mzazi wa msanii huyo aliyefariki November mwaka jana inayoonesha akiwa kwenye simanzi zito kutokana na alichokuwa akisimuliwa na mama huyo.
"Muda mwingine wasanii tunahitaji tukumbuke wenzetu walio tangulia tena kwa kuwa enzi ata kwa kuwatembelea ndugu zake coz kuna vitu vinauma sana ukielezewa hapa alikuwa ana nielezea sharo baada ya kufa haki zake nyingi hajui zipo zinaenda wapi na mambo mengi yanayo muhusu marehem sharo kiukweli ili niuma... pole sana mama angu binadamu ndivyo walivyo,” ameandika Mavoko.

Watu 41 akiwemo waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa wanusurika kifo baada ya ndege waliyopanda kupasuka matairi
Abiria 37 na wafanyakazi 4 wa ndege ya Precision Air wamenusurika kifo baada ya ndege waliyokuwa wamepanda kupasuka matairi wakati ikitua katika uwanja wa ndege wa Arusha leo majira ya mchana.

Waziri mkuu mstaafu ambaye ni mbunge wa Monduli, Edward Lowassa alikuwa miongoni mwa abiria wa ndege hiyo waliokuwa wakisafiri kutoka Dar es Salaam kwenda Arusha.  
Shirika la ndege la Precision Air limetoa tamko rasmi kwa umma, ambapo limeeleza kuwa watu wote waliokuwa kwenye ndege hiyo wako salama.

Ivo Mapunda kuichezea rasmi Klabu ya Simba

Baada ya uongozi wa Klabu ya Gor Mahia ya Kenya kuweka wazi mpango wa kumuongeza mkataba mlinda mlango wao shujaa wa kupangua michomo ya penalti, Ivo Mapunda, uongozi wa klabu ya Simba nao umesema umeshafanya mipango ya kumsainisha mkataba nyota huyo.

Uongozi wa mabingwa wa Ligi Ku ya Kenya -- Gor Mahia ulikaririwa juzi ukieleza kuwa utambakisha kipa Mapunda kwa gharama yoyote.

Hata hivyo, Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, ambaye alikuwa nchini Kenya juzi, ameiambia NIPASHE kuwa Mapunda alitarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili kuwatumikia 'Wanamsimbazi', na kwamba tayari ameshatanguliziwa shilingi million 15.

"Tayari tulishamkabidhi mke wake shilingi milioni 15 jijini Dar es Salaam jana (Jumatano) kabla ya kuja huku (Nairobi)," alisema Mtawala.

Katibu Mkuu huyo alisema wamelazimika kuja jijini hapa kumsajili baada ya kusikia kuwa klabu yake ya Gor Mahia ina mpango wa kumwongeza mkataba mpya.

Kipa huyo amejipatia umaarufu nchini hapa kwa ushujaa wake wa kupangua mikwaju ya penalti. Katika mchezo wa jana wa Kombe la Chalenji kutafuta mshindi wa tatu kati ya Zambia (Chipolopolo) na Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars), Mapunda alidaka penalti mbili kati ya nane ambazo mabingwa hao wa zamani wa Afrika -- Chipolopolo walipiga.

Kutua kwa Mapunda Simba kutaisaidia timu hiyo iliyopo katika mgogoro mkali wa uongozi kwani kuanzia msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, hakuna timu itakayoruhusiwa kuwa na kipa wa kigeni ili kukidhi matakwa ya Azimio la Bagamoyo.
Source:Nipashe