advert

http://

Wednesday 22 May 2013

Wengi wafariki kufuatia Kimbunga, Oklahoma


Kimbunga kikubwa kimepiga Jimbo la Oklahoma, nchini Marekani na kuharibu kabisa mitaa.
Maafisa wanasema zaidi ya watu tisini wamefariki, wakiwemo takriban wanafunzi ishirini ambao shule yao ya msingi iliporomoka.
watoto wakipata tabu
ana
Wanafunzi wengine wanahofiwa kufunikwa na vifusi.
Kimbunga hicho kilipiga mji wa Moore kwa takriban dakika arobaine, na kurusha magari katika vifusi vya nyumba na maduka.
Rais Obama ametangaza hali ya mkasa mkubwa na kuahidi usaidizi wa serikali kwa utawala wa jimbo hilo.
Takriban watu 120 wanaendelea kupokea matibabu hospitalini
Masaa kadhaa baada ya Kimbunga hicho kupiga, shughuli za kuwatafuta manusura ingali inaendelea.
Wanatumia mashine kubwa kujaribu kuwatafuta waliokwama chini ya kifusi ili kuwaokoa.
Mji wa Moore ulipigwa na kimbunga kikubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa kwa muda wa miaka 14 wakati kimbunga kingine kikubwa kilipopiga eneo hilo.
Watu wengine zaidi wanajulikana kuuawa katika Kimbunga hicho.
Hospitali zimekuwa zikiwapokea majeruhi , wengine wakiwa katika hali mbaya zaidi na maafisa wa utawala wanaonya kuwa idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka.
Maafisa wakuu wa serikali ya jimbo walitakiwa kuungana katika juhudi za kuwasaka manusura usiku kucha.
Kwa mujibu wa afisaa mkuu wa afya, angalau watoto 20 walikuwa miongoni mwa wale waliofariki.
Shule ya msingi ya Plaza Towers ndiyo iliyoathirika zaidi kuliko sehemu zingine , kimbunga kiliharibu paa ya shule na kuangusha kuta zake zote.
Shule nyingine moja pia ilipigwa na kimbunga hicho lakini walimu walifanikiwa kuwaokoa wanafunzi.

No comments: