advert

http://

Tuesday 25 June 2013





Mtangazaji maarufu wa kipindi cha michezo na taarifa ya habari ITV na 
Radio One, Kitenge Maulid Kitenge kwa kupitia mtandao wa Instagram na 
Twitter ametangaza kugombea ubunge jimbo la Ubungo kwa tiketi ya CCM.




Kitenge anakuwa miongoni mwa watu maarufu na wasanii waliotangaza nia 
hiyo kama Soggy Dogg Hunter (CHADEMA, Segerea) na Afande Sele (CUF, 
Morogoro).
Aidha, kuna tetesi kuwa huenda wasanii MwanaFA (CCM) na Prof Jay 
(CHADEMA) wakatangaza nia bila kumsahau msanii wa Bongo movie Ray 
Kigosi.


Eddymolaze blog

imageWaziri mkuu wa zamani wa Italia ambaye pia ni mmiliki wa klabu ya Ac Milan Silvio Berlusconi amehukumiwa kifungo cha miaka 7 gerezani baada ya kukutwa na hatia ya kujihusisha kwenye ngono na mabinti walio chini ya umri wa miaka 18.
Zaidi ya hapo Berlusconi ambaye amewahi kuiongoza Italia kama waziri mkuu kwa vipindi vitatu tofauti amefungiwa kutojihusisha na siasa kwa maisha yake yote kufuatia kashfa hiyo .
Hukumu hii ni ya tatu kwa Silvio ndani ya kipindi cha miezi tisa iliyopita ambapo mwezi oktoba mwaka 2012 alihukumiwa miaka minne gerezani kwa kukutwa na hatia ya ukwepaji wa kodi na miezi miwili baada ya hapo alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela kwa kosa la kutumia ushahidi wa kunasa mazungumzo ya simu kinyume cha sheria .
Berlusconi anatarajiwa kukata rufaa juu ya hukumu ambayo hata hivyo haina nafasi kubwa ya kufanikiwa kutokana na kashfa zinazomzunguka ambazo zinafanya iwe vigumu kwake kusafishika .
The TZA

Shirika la viwango Tanzania -TBS limepiga marufuku biashara ya uuzwaji wa nguo
za ndani za mitumba zinazoingizwa kwenye soko la hapa nchini.


Msemaji wa shirika la viwango TBS Bi. Rhoida Andusamile amesema hatua
hiyo ni utekelezaji wa matakwa ya agizo la sheria ya 2009 inayozuia
matumizi ya nguo za ndani zilizokwisha tumika
Lakini licha ya unafuu wa gharama za upatikanaji wa nguo za mitumba Nchini,
Serikali kupitia TBS imepiga marufuku biashara ya uuzwaji wa nguo hizo
ikiwemo soksi na nguo za kulalia zoezi linalohusisha Nchi nzima.
Mara nyingi nguo za ndani za mitumba zimekuwa zikitumiwa na jinsia zote 
mbili lakini wanawake ndiyo wameonekana kuwa wateja wakubwa wa nguo hizo. 
Hii ni mara ya pili kwa Shirika la viwango Tanzania - TBS kupiga 
marufuku biashara ya uuzwaji wa nguo za ndani za mitumba, lakini bado
biashara hiyo imekuwa ikishamiri kwa kasi.

Mimi i always assumed MONEY IS THE ANSWER TO ALL PROBLEMS!!!! Yaani its something i believed totally n completely! I believe it to the extent i feel like im starting to turn it to faith!!!!!!!! Bt today i was like WHAAAAAAAAAT!!!!!!! You gotta be kidding me!!!!!!!!! 

Leo katika kupitisha Ze Weekend nikakutana na mashosti long time no seee! Ushosti nao ni full time job hapa mjini! Kama huna roho lazima unawe! Tukaona tukaonje kuku za KFC ndani ya bongo! Chezeya! Bongo kama ulaya! Kweli kuku ni tamu sema calories nazo si mchezo!
 
Sasa katika kurecoup nani uko wapi na nini ndo kupeana update inakuwaje no pete vidoleni?????? WHY???? 

Basi bwana kuna Engine ya Jiji moja (She ain't called engine ya jiji,for nothing! she is way too loaded! Loaded like really loaded!) akawa ana yuko kwenye panic! She is 25, no ring and so desperate!!!!!!!! Karudi toka Obamaaaa Land na Masters yake mkononi, chuo cha ukwee manake alishinda Full Bright Scholarship ya US Embassy! She is way too bright! Kushinda hio makitu you need to be brightest of the brightest!!!!!!
 
Basi ndo karudi, amepewa u manager sehemu flani, na appartment na gari!!! The only thing missing is jst 1, only 1 out of millions nice man to call hubby! Sasa the challange anayokutana nayo she doesnt know where to meet nice men! Alikuwa ana hang hang maneo ya Manhattan ya Bongo, Hyatt huko, na golden tulip sijui wapi wapi akawa anakutana na waume za watu tu, na wale vijana WANNA BEssss!!!!!!! Siku mbili wanamkopa! While all she needs a nice dude to love her as she is!
 
Basii bwana ndo kwenda bank, disco, kanisani, kusocialize holaaaaaaaaaa! Anadai akiwa na mtu akijua tu yuko uzuri basi anaanza kumkopa na kutangaa njaa namna gani, afu mtu mwenyewe Mpare afu na ki exposure cha US na uzungu mchungu kupita maelezo, hatoi hela bila sababu! Na haiingii akili mwake even if she has excess kwanini akupe wewe?
 
Akahisi cause she is driving maybe ndinga ndo linamnyima exposure ikabidi awe anapanda vidala! Wapiiiiiiiii! Hakutani na yoyote! Sasa finally she is breaking up! The pressure is too high! Ndo akawa anatupasha NO LUCK AT ALL!!!!!!!!
 
For me who i thought MONEY IS THE ANSWER TO ALL MY ISSUES it came as a shocker! Sasa kama yeye mzuriiii, show stopper, fashion yoyote za madesigner kina Zara hadi CL ana rock ana mihela n yet she cant make things happen for herself!!!!!!!!! Some simple things arent simple after all!!!!!! Je mie nikijikuna natoka unga!!!!!? Kumb even with the money i might be dooooomed!!!!!!!!!!! Yani im so disappointed with this city!!!!!!!!!!
 
Nimejisalimisha kwa Oga on top! Hizi ni nyakati za mwisho! Nimeona nianze tu  manake the future is so very uncertain!!!!!!!!!!! Mmmmmmmmh! Nimeona bila kuomba external forces watu wanapaki ndinga kuzama kwenye dala waonekane, mie ninae panda dala itanilazimu kutembea na vigoko a.k.a TZ 11 ili nionekane, na jua lilivo kali hapa jijini!!!!!!!!!! Mmmmmmmh!


Source: Mdau 

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inawajulisha wadau wake wote kuwa Ofisi yake ya Makao Makuu inahama kutoka Jengo la TIRDO, Barabara ya Kimweri, Msasani kwenda Kiwanja Na.. 8, Kitalu Na. 46, Barabara ya Sam Nujoma, Mwenge, Dar es Salaam kufikia Juni 30, 2013.

Katika kipindi cha kuhama, Bodi itahakikisha huduma zinarejea katika hali ya kawaida ndani ya siku chache.

Aidha uombaji wa mikopo kwa njia ta mtandao upo kama kawaida, na hivyo waombaji wa mikopo wanaweza kuendelea na utaratibu wa kuomba mikopo. Hata hivyo, huduma ya simu kwa waombaji wa mikopo imesitishwa kwa muda wakati mitambo ikifungwa na huduma itaendelea kama kawaida kuanzia Jumanne Juni 25, 2013.

Bodi inaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaotokea wakati ikijiweka sawa katika makazi mapya.Imetolewa na:

Mkurugenzi Mtendaji,

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu,

Kiwanja Na.. 8, Kitalu Na.. 46, Barabara ya Sam

Nujoma, Mwenge

S.L.P. 76068, Dar es Salaam, Tanzania.

Simu: +255 22 2669036/2669037 Faksi: +255 22 2669039

Barua pepe: info@heslb.go.tz

Tovuti : www.heslb.go.tz

WABUNGE wanachama wa Chama cha Kupambana na Ukimwi (TAPAC), wiki iliyopita walikutana na kujadiliana mambo mbalimbali na mashoga katika mkutano wa mwaka wa chama hicho uliofanyika kwa muda wa siku tatu mjini  Dodoma. Katika mkutano huo, baadhi ya wabunge walionyesha wasiwasi wa taifa kupata rais shoga katika miaka ijayo kutokana na ongezeko la mashoga hapa nchini.

Mbali na wasiwasi ulioonyeshwa na wabunge, mashoga waliokuwa wakihudhuria mkutano huo, walilalamikia vitendo vya unyanyasaji wanavyofanyiwa na wanajamii wenzao na kudai watambulike na wapatiwe huduma za msingi za kibinadamu.

Akizungumza katika mkutano huo uliomalizika jana, Mbunge wa Nkasi, Ally Kessy (CCM), alitahadharisha uwezekano wa nchi kupata rais shoga katika miaka ijayo, iwapo hatua za makusudi za kudhibiti hali hiyo hazitachukuliwa.

“Tabia ya kuwapeleka watoto kwenye shule za mabweni wangali wadogo wa umri wa miaka hadi miwili, itatuletea matatizo baadaye.

“Katika shule nyingi za bweni vitendo vichafu vinafanyika, vikiwamo vya ushoga. Katika vyuo vikuu hivi sasa kuna mashoga wasiopungua 40,000. Hii ni hatari, tusipojihadhari tutakuwa na rais shoga katika miaka ijayo,” alisema Kessy huku akishangiliwa na wabunge.

Mbunge huyo alitaka elimu dhidi ya ushoga na athari zake ienezwe nchini kupitia vyombo vya habari na nyumba za ibada.

Naye, mmoja wa mashoga waliohudhuria mkutano huo aliyejitambulisha kwa jina la Abdilah Ally, alieleza kuwa yeye ni shoga mwenye wanaume watatu lakini amekuwa akikutana na vitendo vya unyanyasaji kutoka ndani ya jamii inayomzunguka.

“Tunataka haki zetu. Tunanyanyaswa katika jamii hasa na polisi. Na sisi tunastahili huduma bora za afya na nyingine tuweze kujikinga na Ukimwi,” 
alisema Ally, mkazi wa Dar es Salaam.

Wakati huo huo, taarifa iliyotolewa na Mshauri wa Masuala ya Ufundi wa Kampuni ya Jhpiego, Dk. Augustine Hellar, ilieleza kuwa kuna wanaume 397,458 waliotahiriwa nchini hadi Mei, mwaka huu katika mpango maalumu wa tohara kwa ajili ya kupambana na maradhi ya Ukimwi.

Dk. Hellar alitoa takwimu hizo alipowasilisha mada kuhusu tohara ya hiari kwa wanaume katika kukabili maambukizi ya Ukimwi nchini.

Alisema lengo la mpango huo ulioanza kutekelezwa Oktoba, 2011 katika baadhi ya mikoa nchini ni kutoa tohara kwa wanaume milioni 2.8 kila mwaka mmoja.

Alisema mpango huo umekabiliwa na changamoto mbalimbali, ikiwamo ya watu wazima ambao ndiyo walengwa kutojitokeza kwa wingi na baadhi ya watu kuhusisha hatua hiyo na upotevu wa nguvu za kiume.


Mtanzania 

imageimageSiku chache baada ya mchezaji Mrisho Khalfan Ngasa kusajiliwa na klabu ya Yanga akitokea klabu ya Simba ambako alikuwa anacheza kwa mkopo toka klabu ya Azam fc shirikisho la soka Tanzania limeubatilisha mkataba uliopo baina ya Ngassa na Yanga ikisema kuwa haujasajiliwa kwenye ofisi zake .

Shirikisho limezungumza hayo mwishoni mwa wiki hii kupitia kwa msemaji wake ambaye ni Afisa habari wa TFF Boniface Wambura ambaye alisema kuwa TFF inautambua mkataba uliopo baina ya Simba na Ngassa na si wa Ngassa na Yanga kwa kuwa haujasajiliwa na uliosajiliwa TFF ni mkataba wa Simba unaoonyesha kuwa Ngassa ataitumikia Simba msimu ujao kwa muda wa mwaka mmoja .
Ngassa amekuwa akizua gumzo kwenye masuala ya usajili tangu aliposajiliwa toka Yanga kwenda klabu ya Azam na baada ya hapo akahamia Simba kwa mkopo kabla ya kurudi Yanga . Viongozi wa Simba awali walisikika wakisema kuwa Ngassa ni mchezaji wao halali na sheria za usajili za TFF zitachukua mkondo wake jambo ambalo linaonekana kudhihirika .
Kanuni za TFF kuhusiana na masuala ya usajili wa wachezaji zinasema kuwa lazima mkataba wa mchezaji husika usajiliwe kwenye ofisi za TFF . Ofisa habari wa TFF Boniface Wambura alisema kuwa mkataba wa Ngassa na Yanga haujafika TFF na ndio maana hata kwenye timu ya Taifa , Taifa Stars ameorodheshwa kama mchezaji wa Simba.
Bado viongozi wa Yanga na Simba pamoja na mhusika mkuu kwenye sakata hili Mchezaji mwenyewe hawajatoa tamko lolote juu ya taarifa hii ya Tff kutotambua mkataba wa Ngassa na Yanga.
The TZA







Huyu ni mhadhiri wa chuo kikuu cha mzumbe na pia ndio yule mwl wa chuo kikuu anayefanya bongo fleva.Ukitaka kumjua vizuri bofya hapa 


Yeye kama Msomi mzuri na mwalimu wa wasomi wa chuo kikuu,ameona kabisa Ommy Dimpoz hana makosa kabisa na amewaomba watanzania wamuelewe Ommy Dimpoz na kumsamehe.

Haya ndio maneno ya huyu mhadhiri wa chuo kikuu Issaya Lupogo jina la kisanii Lupojizo.

''Binafsi nasikitishwa sana na mashabiki kumfanyia Ommy Dimpoz mambo haya mabaya. Nilimsikiliza sana Ommy Dimpoz siku ya KTMA, hakumaanisha kama watu suku hizi wanavyotafsiri. 
Alichikisema Ommy kwa namna nyingine kinaweza kutafsiriwa kama wadau na serikali zitoe kipaumbele na kuthamini kazi za wasanii wa nyumbani ili wasanii wanufaike zaidi na siku ya mwisho wasife masikini. Huu ni ukweli kabisa kuhusu hali iliyopo kwa wasanii sasa. Wasanii wananyonywa na kudhulumiwa, mwisho wa siku msanii anaishia kupata umaarufu tu usio na kitu chochote.
Kingine nilichokiona ni Ommy D kutotetea hoja yake pindi alivyohojiwa na waandishi wa habari, badala ya kueleza hoja hiyo kiumakini alijikuta aikbabaika na kukumbilia kuomba msamaha.

Jambo alilolisema Ommy D lilisemwa pia na Afande Selle na Mr. Sugu siku ya kuaga mwili wa Ngwair uwanja wa Jamhuri morogoro, kama ni hvo basi mbona hao hawakuandamwa kama Ommy D?

Watanzania tuwe waelewa,wasanii wengi wa Tanzania bado ni masikini, kipatao wanachokipata hakiendani na kazi wanayoifanya na umaarufu walionao, hii sio kwa Ngwear tu bali kwa wasanii wengi wa Bongo. Sababu ni unyonyaji na udhulumaji uliopo wa kazi za wasanii, na serikali kutoweka mkazo juu ya kuangalia maslahi ya wasanii nchini.
Nawaomba watanzania tusiendelee kumsakama Ommy D, na Ommy D naomba uwe unajaribu kujenga hoja vizuri kwa kile unachokisema na sio kukimbilia kuomba msamaha bila hata ya kutenda kosa lolote.''
https://www.facebook.com/groups/457838860975599/?ref=ts&fref=ts


Ni hakika ‘mtaa wa ngono’ umefumuliwa! Sakata hilo lilijiri saa tisa usiku, Ijumaa iliyopita, Barabara ya Shekilango, kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori jijini Dar eneo ambalo makahaba wameligeuza chumbani
Kwa mujibu wa takwimu za kiserikali, eneo hilo
(kuanzia Bamaga hadi Sinza Mori) limekubuhu kwa wasichana kujiuza nyakati za usiku huku makao yao makuu yakiwa eneo la Afrika Sana hasa pembezoni mwa Corner Bar.
 

Mmoja wa viongozi wa serikali ya mtaa ya eneo hilo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe , alisema:
 

“Tumejitahidi sana kushirikiana na polisi ili kutokomeza ukahaba eneo hilo lakini wapi! Hawa mabinti ni wabishi, mbaya zaidi wamelifanya eneo hili kuwa la ngono.“Watoto wetu wanapita usiku pale wanawaona wanavyofanya, wanatuharibia kizazi kijacho, kama wao wamejishindwa wasiwaambukize wengine.”
Siku ya tukio, saa tisa usiku,  askari wa ulinzi shirikishi walijipanga kwa ajili ya kuufumua mtaa huo huku wakiwa na tahadhari kufuatia habari za kiintelijensia kudai kuwa, makahaba hao walipanga kuua mtu punde watakapovamiwa.
 

Askari hao wakiwa kwenye doria ya kila usiku, waliwavamia makahaba hao eneo lenye majani madogo katikati ya Afrika Sana na Mapambano upande wa yadi ya Mwanamboka wakiwa na wateja wao wakifanya ngono hadharani.


Katika hali iliyoonesha makahaba wamejiimarisha kwa ulinzi siku hizi, wakati wa zoezi hilo, machangu hao sanjari na vibaka  wanaowaunga mkono wakisemekana ni ‘walinzi’ wao, waliokota mawe na kuwarushia askari hao hali iliyozua tafrani zaidi.



Ndipo piga nikupige ilipozuka ambapo askari walionesha umahiri wao wa kupambana na wahalifu kwa kuwadhibiti kwa vichapo vya hapa na pale na kufanikiwa kuwaweka wengi chini ya ulinzi.


Kuona hivyo, baadhi ya makahaba na wateja wao walifanikiwa kuwachoropoka askari bila nguo na kutokomea gizani hivyo kulifanya eneo hilo kuwa jeupe.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, baadhi ya makahaba waliokimbia walijikuta wakiacha kwenye majani nguo zao za ndani na kuzua maswali kwamba ni kwa nini hawakuwa wamezivaa!


“Jamani hizi si nguo zao za ndani? Ina maana wakiwa kazini hawavai siyo? Wanakuwa tayaritayari kwa kazi? Jamani!” alisema kwa mshangao mkubwa mmoja wa askari hao.

Licha ya kuwa chini ya ulinzi mkali, baadhi ya makahaba walionaswa walikuwa wakiwalalamikia askari hao kwamba wanawafuatafuata wakati kila mtu siku hizi anaangalia atakulaje!
 

“Mnatuonea bure, nyie mnakula kivyenu na sisi mngetuacha tule kivyetu, hao watoto wenu mnaosema tunawaharibu usiku huu wao wanatokea wapi na wanakwenda wapi?” alisikika akisema kahaba mmoja aliyekuwa mtata kuwekwa chini ya ulinzi.


Mwingine akadakia: "Kama mnataka tuwape uroda si mseme, mnatukamata kila siku kwani tunawatibulia nini majumbani mwenu? Lini tumekuja kuwaghasi wakati mmelala na wake zenu?”
 

Uchunguzi wa kawaida ulibaini kuwa muda rasmi wa 
makahaba hao kuwasili eneo la Corner Bar ili kuanza ‘kazi’ ni saa mbili usiku japokuwa wapo wanaoripoti mapema na kufanya biashara hiyo kwa wizi kulingana na wateja wenye ‘kiu’ nyakati hizo. 

Licha ya kuwa chini ya ulinzi, makahaba hao waliahidi endapo watapelekwa polisi na kutoka watarejea eneo hilo kujiuza kwani ndiyo ajira inayowafanya waendelee kuishi katika Jiji la Dar es Salaam, kusomesha watoto vijijini kwao na kuwasaidia wazazi wao mahitaji mbalimbali.
 

“Hata kama mtatupeleka polisi, tutarudi tu hapa, sisi tunasomesha watoto, tunasaidia wazazi wetu vijijini, pia tunaishi Dar kwa sababu ya kipato hiki cha kuuza miili yetu, acheni hizo,” mmoja wa makahaba hao alisema bila kumung’unya maneno.


Source:GPL

BAADA ya hivi karibuni mchumba wake anayejulikana kwa jina la Dickson ‘Dick’ kuukacha uchumba, msanii wa filamu za Kibongo, Shamsa Ford ameibuka na kusema anaogopa sana ndoa.


Akistorisha na paparazi wetu, Shamsa alisema japokuwa mwanamke yeyote anahitaji kuolewa lakini yeye anaogopa kuingia kwenye ndoa kwani wanaume ni watu wa kubadilikabadilika kama kinyonga ambapo huwanyima uhuru wake zao kwa kuwawekea sheria kali.
“Naogopa ndoa mwenzenu, wanaume ni watu wa kubadilikabadilika. Nasubiri ahadi ya Mungu kama ni mapenzi yake nifunge ndoa na Dick basi itakuwa kama siyo siwezi kulazimisha kwani hapendi niigize kitu ambacho siwezi kukiacha,” alisema Shamsa.



Ni vigumu sana kumdhania mtu maarufu na aliyefanikiwa kwa
kiasi kikubwa katika kazi zake kama Beyonce Knowlence eti anaweza kuwa mvivu au
mzembe katika kazi, lakini swaiba wake Kelly Rowland aliyefanya nae kazi kwa
muda mrefu yeye anamjua vyema kuwa alikuwa mvivu/mzembe. 

Kelly Rowland ambae yuko kundi moja na Beyonce ‘Destiny’s
Child’ amefunguka katika interview aliyofanya katika kipindi cha ‘Watch what
Happens Live’ baada ya mtangazaji Andy Cohen kumuuliza ni kitu gani ambacho
kinamkera/kumkasirisha kinachomhusu Beyonce, ndipo alipofunguka kuwa mama Blue
Ivy alikuwa mvivu/mzembe na kwamba afadhali sasa hivi amekuwa mama..lakini ana
mambo mengi kwenye ubongo wake na mengi yanaendelea. 
“She would tell you this. She was a slob, If you walk
in..may be she’s gotten better since becoming a mother…but she’s got a lot on
her brain. You can tell she’s got a lot going on.”

Alichokisema Kelly Rowland kinaweza kuwa kweli kiasi flani
kwa kuwa hakiko mbali sana na sentensi alizowahi kuzisema Beyonce mwenyewe
mwaka 2009 kuwa alikuwa anamuudhi kimtindo mumewe Jay Z ambae ni mchapakazi na
amejipanga muda wote, sasa yeye alipokuwa anatoka katika mishemishe za muziki
akirudi nyumbani hataki kufanya kazi yoyote kwa kuwa anakua amechoka.

“I’m a little messy…when I get home, I don’t want to take
care of anything. I drop it…I work so much that when I get home I don’t want to
thing about anything.”
Kelly Rowland anaendelea kupromote album yake ‘Take a Good
Game’ na tayari ameshaachia wimbo mmoja ‘Dirty Laundry’ ambao amesema umemaliza
kinyongo alichokuwa kuwa nacho juu ya mafanikio ya Queen Bey.

WAKATI vifo vikizidi kuwatafuna wasanii, staa wa sinema za Kibongo,

 Aunt Ezekiel amefunguka kuwa hawezi kuishi miaka mingi, atakufa mapema.

Aunt Ezekiel alifunguka hayo juzikati jijini Dar ambapo alibainisha kuwa

akijitazama mustakabali wa maisha yake basi anaona kabisa hawezi kufikisha
 miaka 40.
“Daah! Sijielewi kabisa yaani kwa jinsi ambavyo 
najiona, nikifikisha miaka 40 ni bahati aisee, dunia sasa imebadilika 
sana,” alisema Aunt.

 Na Imelda Mtema

STAA wa filamu na muziki Bongo, Miriam Jolwa ‘Jini Kabula’ amekiri kuwa katika wakati mgumu kutokana na kukabwa na mashetani usiku na kumsababishia maumivu makali ya mwili hadi kuhisi kufa.


Hivi karibuni Jini Kabula alipotea kwenye ulimwengu wa mastaa jijini Dar hivyo Ijumaa Wikienda likaamua kumtafuta, alipopatikana ndipo likabaini hali yake ni tete kiafya.
Akizungumza na mwanahabari wetu wikiendi iliyopita, Jini Kabula alisema kwa muda mrefu sasa amekuwa mtu wa kuumwaumwa na mwili kukosa nguvu ambapo alishapima vipimo vyote lakini aligundulika kuwa na malaria, akatumia dozi na kuimaliza lakini hali bado siyo nzuri.
Huku akiwa amedhoofu mwili, Jini Kabula alisema kila ikifika usiku wa manane akiwa amelala huwa anakabwa na mtu ambaye hamuoni, hali inayomfanya ashindwe kupumua huku mwili ukikosa nguvu na kuuma kupindukia.

“Nahisi kabisa nakufa kwa jinsi ninavyojisikia mwilini, natamani hata usiku usiingie kwa sababu mateso ninayopata ya kukabwa ni makubwa, wakati mwingine nakesha nikiangalia muvi kwa kuhofia nikilala tu lazima nikabwe.
“Hata rafiki zangu nimeshawaaga na kuwaambia kuwa muda wowote wakisikia nimekufa wasishangae kwa sababu naumwa ila ninayemhurumia ni mwanangu, jamani nitamuacha bado mdogo maskini wa Mungu sijui ni shetani gani ametukumba wasanii,” alisema Jini Kabula kwa masikitiko.

source:ijumaa wikiend



Nguli wa muziki wa kizazi kipya Soggy Doggy Anter aka Anselm Tryphone Ngaiza leo ametangaza nia ya kugombea Ubunge wa jimbo la Segerea, Dar es Salaam kupitia tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, MWAKA 2015.
Msanii huyo ametiririka katika ukurasa wake wa facebook, na hapa nanukuu "Shikamoo Mbunge wa Segerea, Makongoro Mahanga, imetosha sasa nadhani ni zamu yangu kuwatumikia wana-segerea 2015 kupitia CHADEMA" mwisho wa kunukuu. Pia kwenye ukurasa wake wa twitter imesomeka ivyo ivyo.
Nilipoongea na Msanii huyu aliniambia ameamua kufanya ivi ili kuwasaidia na kuwaletea maendeleo wana-segerea na watanzania kiujumla.
Pia aliniambia ameamua kugombea kupitia CHADEMA, kwasababu ndo chama kinachoweza kufanya mabadiliko kwenye jamii kwasasa.
Nikamuuliza je amemfuata rafiki yake Joseph Mbilinyi aka "SUGU" katika chama icho, akasema hapana, hawajawahi kupewa ushawishi wowote wa kisiasa na Nguli huyo wa muziki wa Hip Hop.
Wana-Segerea kazi kwenu kijana ameamua na amedhamiria.

Chanzo:Udakuspecially.






Habari
mi ni kijana mwenye mke na mtoto mmoja, nina mpz nje ya ndoa yangu ambaye anakaa kwao. nimekuwa na uhusiano nae kwa kipindi cha zaidi ya miaka miwili sasa; sijawahi kwenda nae kupima licha ya yeye kudai mara ya mwisho alipima mwaka 2007 na alikuwa safi lakini mimi huwa napima mara kwa mara.
hivi karibuni alikuwa mbali nami kwa masomo ingawa mawasiliano yalikuwepo kama kawaida na nilikuwa namtania kuwa hata kama naibiwa basi tumieni kondom, utani huo ulionekana kumkera hata kufikia kusema akiridi kabla ya kukutana tupime kwanza nikamkubalia.
amerudi na jana tukaenda kupima alikuwa ananipigia mara kwa mara kuniuliza tunaenda saa ngapi?

tulipofika eneo la tukio kama kawaida tulipewa ushauri nasaa na kuulizwa maswali kama kwa nin mriamua kuonana kimwili kabla ya kupimwa binafsi nilijibu kutokana na afya yake niliamini hana maambukizi (ni binti mnzuri kwa muonekano, hips za kuvutia na ---- lakutosha ni raha hata kuongozana nae) na yeye alisema aliniamini.

tukatolewa damu ingawa ilikuwa tofauti kidogo na nivyowahi kupima kabla, kabla walikuwa wanatoa damu kidoleni kama wanavyopima malaria ila sasa walinitoa hapo wanapotoa damu kama unataka kumuongezea damu mtu.

baada ya muda tuliitwa kupewa majibu na mambo yalikuwa hivi
baada ya maneno ya daktari aliendelea kutuuliza maswali kama itaonekana mwenzako ameathirika (nilimtambulisha kama mke wangu) utafanyaje nikajibu nitaendelea kuwa nae na nitatumia kondomu kwake ila yeye alijibu ana uhakika yupo vizuri; mi nikadakia nakumwambia usimchagulie docta jibu.
baadae daktari akaniambia nipo vizuri nakumwambia mwenzangu samahani kwa majibu hayo nitakoyokupa vipimo vinaonesha umeathirika. sikuamini na bado siamini
daktari alienda mbali zaidi kwa kutuonesha kuwa baada ya kumpima kwa kipimo cha kwanza akampima kwa mara ya pili, tatu na baadae akaamua kubadilisha kipimo akatumie kingine (alituonesha) lakini majibu bado ni yale yale.
Mapokea ya majibu ya mwenzangu
hakushtuka sana kitu kilichonishangaza alianza kulia baada ya dk 20 kupita
haamini matokeo ana taka kurudia kupima, aliendelea na kulia huku majuto ya kiwa kwa kiasi kidogo ila alikuwa mara kwa mara akiomba nisimuache na mimi nirimhaidi kuto muacha.
nilitumia muda mwingi kumnyamazisha ingawa hakutulia kwa asilimia mia, na baadae nilimpeleka kwao ambapo wazazi wake walikuwa wameondoka na yeye alibaki na wadogo zake, tulipofika kwao aliendelea kulia waliniuliza analia nini nikawajibu tumekorofishana lkn namwambia yameisha hataki kuelewa akawa anajibu kuwa mi mwongo na alitaka kusema ukweli nikamkataza na mara akawasha simu yake akitaka kumpigia simu mamake nikamnyang'anya.
alikuwa na kadi ya harusi ya mamake aliniambia ataenda kwenye sherehe na baadae alienda (mambo haya yote yalianza saa kumi na mbili jioni) alikuwa huko nilikuwa namfuatilia kwa kumpigia simu alikuwa haoneshi kuwa na wasi wasi sana ila aliomba nisimuache, na asubuhi ya leo ameenda kunisani kama kawaida.

NinachohisiAidha alikuwa anajua ameathirika au alikuwa anajua ametembea na mtu aliyeathirika hivyo alikuwa na uhakika wa zaidi ya asilimia 50 kuwa ameathirika kwa sababu.

  1. Alitaka kumlazimisha daktari kutoa majibu kama haja athirika (rule out the doctor)
  2. hakupokea majibu kwa mshtuko sana.
  3. anaomba kuto achana na mimi badala ya kufikiria zaidi kuathirika kwake
  4. ameweza kwenda kwenye sherehe ya harusi just after an hour (nilipenda aende kwa ajili ya kupoteza mawazo) lakini sikutegemea akubali au iwe rahisi kwake
  5. ameweza kwenda kanisani leo


Nataka

  1. Nimpeleke hospitali nyingine akapime tena na hata kama majibu yataendelea kuwa kama yalivyo sasa basi apewe ushauri nasaha ili aondokane na mawazo ya kuathirika ni mwisho wa maisha na kuwa huru kimawazo.
  2. niendelee kuwa nae karibu kwa muda fulani then nitampotezea (ushauri unahitajika kutoka kwako msomaji)


Naomba ushauri kuhusu hali hiyo ikiwemo uhusiano wetu wa kimapenz.i ili kumuondoa mawazo nilimwambia nitaendelea kufanya mapenzi nae ila kwa kondomu sio kama ilipokuwa kuwa awali ambapo kondomu ilikuwa haitumiki.

ndigu zangu ukimwi upo tuwe makini na wapenzi wetu tusipime kwa macho huyo ambaye namzungumzia ukimwona alivyoshiba huwezi amini kuwa ameathirika.

naomba kama huna cha kuchangia pita tu utani singefurahia sana

POLISI mjini Mombasa wamemkata raia wa Uingereza akiwa na wasichana wawili wa shule ya upili.Mkuu wa Polisi wilayani Kisauni Julius Wanjohi alisema wasichana wote ni wanafunzi wa kidato cha nne katika shule moja mjini Mombasa na eneo la Yatta mkoani Mashariki.

Kulingana na Bwan Wanjohi, Bwana Henson Nigel Grahan, 50, anayezuiliwa katika kituo cha polisi cha Nyali alipatikana na wasichana hao usiku wa Ijumaa katika 

eneo la Nyali Cinemax kabla ya kutiwa mbaroni na polisi.
“Mshitakiwa alipatikana na wasichana hao wawili ambao kwa umri wanaonekana ni wachanga lakini wao walisema wana umri wa zaidi ya miaka 18,” akaeleza Bw Wanjohi.
Mwingereza huyo ambaye aliwaelezea polisi kwamba yeye ni mhasibu, amekuwa nchini kinyume cha sheria na kwa mujibu wa Bwana Wanjohi alipaswa kurudi kwao
mnamo Januari mwaka huu pale muda wa vyeti vya kuwa nchini ulipokwisha.
Alisema polisi wanapeleleza kubaini iwapo mshukiwa ni miongoni mwa wageni
wanaohusika na uhalifu wa usafirishaji hila wa watoto kwa ajili ya
kuwashirikisha ngono.“Tutamuhoji na kumfikisha mahakama hapo Jumatatu,”akasema Bw Wanjohi.

Aidha wasichana hao wawili walihojiwa na kuzuiliwa katika kituo hicho cha 

polisi cha Nyali huku polisi wakitafuta mbinu za kuwapata wazazi wao.
Hapo Ijumaa polisi walimtia nguvu mwanamume anayefahamika kama Spider Man ambaye alitajwa na wasichana tisa waliopatikana mapema mwezi huu kucheza uchi katika klabu moja huko Mtwapa.
Mshukiwa ambaye alitajwa kwa jina la Ibrahim Wafula anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Mtwapa akisubiri kufikishwa kortini mnamo siku ya Jumatatu.
Kulingana na polisi mshukiwa ndiye mwendesha biashara ya wasichana wachanga kucheza ngono katika vilabu kadha vya usiku mji Mtwapa, Mombasa miongoni mwa miji mingine ya utalii mkoani Pwani.
Alikamatwa majuma kadha baada ya kukwepa polisi kwenye msako uliopelekea raia wa Uingereza Bw Ian Huthson anayemiliki Klabu ya Bahnhof club mjini  Mtwapa
kutiwa nguvuni pamoja na wasichana tisa waliopatikana wakicheza uchi

Upepo unaendelea kutuendea vyema
 ndani ya jumba la BBA baada ya Nando mshiriki wa Tanzania aliyeingia
 kikaangaoni week iliyopita

kupigiwa
 kura nyingi za kubaki mjengoni,inanavyoonekana
washiriki wanaoiwakilisha Tanzania wanawashabiki
 wengi toka nchi tofauti Afrika kwani kwa chati
 inayoonesha jinsi kura zilivyopigwa inaonesha Nando
 kapigiwa kura za kubaki kutoka nchi ya Tanzania,Uganda ,Nigeria kenya na
 Namibia..ikumbukwe mwakilishi mwingine toka Tanzania,Feza kessy nae alipigiwa
 kura nyingi za kubaki kutoka nchi tofaut
 tofauti zikiwemo Sierra leon na Ghana..kuendelea kubaki 
kwa watanzania hao kunazidi kutoa matumain ya huenda 
mwaka huu ukawa nin wetu..who knows??pengine 
historia ya Tanzania kufanya vizuri on BBA ikajirudia kikubwa
 tuendelee kutoa sapoti kwa wawakilishi wetu kwa kupiga kura mara
 tu waingiapo kikaangaoni..Mungu ibariki Tanzania..

No comments: